Kuna wadada wema tu ila wanauza Baa, shida hizi

Acha Wenge,

Analysisi ya siku 1 au 2 au wiki haitoshi kujustify kuwa flani ni Mke mwema

Aliyokuambia yote umeyaamini? Kama ana mtoto alimuacha kwao utajuaje?

Amewaambia Washkaji wangapi? Mbona hawajamchukua?

Btw, nitumie namba yake nithibitishe uyasemayo

Dunia hadaa
 
Tena mwenye matokeo mazuri kuanzia O-Level mpk GPA ya Hatari

Chai hii
 
H
Hauko sahihi na hujui shida. Kuna msemo mwenye shida ni hanithi hata kama rijali.

Ikiwa na shida kazi ya baa utafanya na sio hiyo tu hata zingine zisizofaa kama kazi za ndani ( house girl). Huyo binti kufanya kazi baa haimaanishi hafai anaweza kufaa muhimu endelea kumchunguza.

Na nikuambie kitu kama ingekuwa sio shida za kiuchumi au tamaa za vitu wanawake ingekuwa nguma sana kuwapata.
 
U
Una utibitisho kuwa huyo dada ni Nungaembe?? Wanaume wengi ni women abusers , sishangai kuona single and divorced mothers , ata wewe inaonekana unaweza kukontrol ndugu/mtoto wako aoe nani😭upo una taka dunia yote ifuate unavyotaka wewe! Kuuza bar sio Umalaya na wala sio kuwa kila muza bar yupo anajiuza. Mimi ni kaka na mzazi sijawia ingilia mausiano ya ndugu wala mtoto wangu na sintopoteza muda katika hilo wapo free kuoa au kuolewa na wamatakae. Na iwapo wataachana na wenziwao nawapa ushauri na kuwatuliza.kuna watu nawajua mama zao walikuwa wauza bar wakaolewa wakazaliwa na sasa ni watu mashuhuli na wema kabisa hapa Tanzania. One of the biggest person na maharufu na ameliletea taifa la TZ sifa kubwa kwa utendaji wake wa kazi hapa TZ ameo former bar maid na wapo mpaka leo. Kama mke na mume na wana wajukuu. Wewe ishi kwa kukariri
 
Kuna watu wana mahose girls majumbani mwao na wanawachia nyumba zao na vitu vya thamani na pia wanaamini 90% kama walezi wa watoto wao na pia wanaamini chakula wanachopikiwa na hawa madada lakini wanawadharua.Wajinga sana na wanajifanya smart mbele ya wengine wakati ni wapumbavu tu kama wapumbavu wengine.... chakula kapika yeye wakati wa kula mnamtenga ale peke ake🤣🤣
 
Kujuana labda kwa majina.

Lakini rangi halisi ya mtu huonekana baada ya kufunga ndoa.

Haya ya kujuana hayana uhalisia wenye manufaa.

Ndiyo maana vijana wengi wanaofeli kwenye ndoa, walikaririshwa hili.

Maana kujuana wengine wanachukulia kama kuishi na msichana ili kumuelewa background zake, ama 'kuonja mapishi' nk nk.

Kumbe hayo yote hupelekea saazingine kufubaza muhu wa kijana kuendeleza mchakato wake wa kufunga ndoa na msichana huyo na kuendelea kuangalia pengine.

Na 'kujuana' huko unakokusema kumebeba mambo mengi sana ambayo mengine hata wewe uliyelisema hili neno huyajui.

Kuna mila moja ya kwetu ambayo ikitumiwa kama shamba darasa itawavusha vijana wengi.

Ni kwamba: ukishamtamani msichana, ukamtongoza kwa nia ya kumuoa, akakukubalia na kisha ukaenda kwao kueleza nia yako kwa wazazi wake.

Wazazi watafanya utafiti kuhusu nasaba yako, kisha wakiridhia utaenda kupata jibu la go ahead na kutoa kishika uchumba.

Baada ya hapo ni mshenga pekee atakayewasiliana juu ya mahari na mipango ya ndoa na tarehe ya harusi.

Ni mwiko kijana kumzoea ama kulala na mchumba'ake kabla ya ndoa.

Haya yote yakizingatiwa yanalinda sana hadhi za wasichana.

Ndiyo maana nimetoa hoja kwamba kufahamiana ama kujuana saana kabla ya ndoa hakuleti afya.
 
Mkuu samahani wewe ni msabato?
 
Mk
Mkuu umetetea kwa nguvu kubwa sana kulikoni?

Swali langu lipo pale pale.

Ukiwa kama mzazi na kaka wa kijana anayetaka kuingia kwenye ndoa utashauri nini?

Je utashauri kama uliyoyaandika hapa kwamba wewe upo free kufuata mawazo ayatakayo yeye?

Mi ninachojua, kushauri ni kutoa hints juu ya uzoefu wa jambo unalolishauri.

Naomba na mimi sasa nibakie na msimamo huu nilioshauri linapokuja swala la kushauri vijana wanaotaka kuingia kwenye ndoa.
 
Atutakiwi kuhukumu yeyote yule. Maana Mungu aliyemuumba anaweza mbadilisha either kuwa mtu mwema au kuja kuwa mtu mbaya. Mimi na wewe ni nani ata tuhukumu kuwa huyu dada awezi badilika??Matayo 7:1
 
Mliendelea kuitana KAKA na MAMA baada ya sufuria kuwa nyeupe kama theluji?
 
Haya
 
Ukweli ni kwamba wanawake wengi wanaolewa wakiwa wana mahusiano mengi Sana yaliyopita, Kwa wanawake mahusiano yaliyopita huwa wanapona ngumu sana kuelezea maana inakuwa ni aibu kwao.
Mdau ni muhanga wa kuongea ukweli, kitu ambacho wengi wetu hatupendi na tunapenda kufunika..
 
Ndoa zote ni game of chance, hakuna tofauti kabisa na betting.
Mambo kwenda kombo au kunyooka ni swala la bahati sana halina uhodari!! Ninachojaribu kuelezea hapa ni kwamba Kuna nafasi zinakuja mara moja tu katika maisha usipotumia akili yako haiji tena hiyo nafasi.
Kujuana kwenye mahusiano haina guarantee yoyote kama mtadumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…