Kuna wengine hatujui tulipokosea

Kuna wengine hatujui tulipokosea

Pole sana sana

Ila mama yako aseeh....... Utafkr mtoto wa mke mwenza!

Hapo kwenye fanta orange daah... Lkn kila mtu ana namna ya kutoa kitu fulani ambacho hausiani nacho
 
EP 15

Baada ya kufika pale duka la dawa sijataka kukaa namuaga auntie na kwenda nyumbani. Auntie ananiambia nimsubiri afunge tuondoke wote lakini namkatalia nachukua bodaboda na kurudi nyumbani. Nyumbani namkuta mdogo wangu, dada wa kazi wapo sebuleni nawasalimia na kwenda chumbani kwangu sina mudi kabisa ya kuongea na mtu yeyote.

Auntie anarudi ananigongea namfungulia anakaa kitandani na kunilaza miguuni kwake na kuniuliza kwa upole mbona umekuja umebadilika Lisa kwani Dav amekufanya nini? Namwambia Aunt wewe si ulikuwa unamsifia Dav wewe yaani hapo tena sijisikii kumuita kaka kama mwanzo. Unaweza kuamini kuwa ananinataka kimapenzi, mwanamke wake namjua, mama yake ananichukulia kama bint yake, marafiki zake wanajua kuwa mimi ni mdogo wake baadhi ya marafiki zangu wanajua sisi ni ndugu inakuwaje ananitaka kimapenzi. Simpendi Dav aunt naanza kumchukia.

Auntie huku akinichezea nywele zangu. Lisa mwanangu sikia Dav hajakukosea kukueleza hisia zake. Kumbuka mna historia wewe na Dav hamjafahamiana leo au jana angekuwa na nia mbaya na wewe angelishakwambia maneno hayo zamani tu. Lakini kumbuka amevumilia muda gani. Pili alikupambania na bado atakupambania. Angekuwa na nia mbaya asingeniambia na mimi. Namuuliza auntie kwani na wewe ulikuwa unalijua hili?

Akanijibu ndio sio mimi tu hata mama yake Dav anajua angekuwa na nia mbaya kabisa asingetushirikisha na sisi. Dav anakupenda tena sana alafu ni kijana mzuri tu. Au una mahusiano mengine huko Dar na kama unayo yakoje mimi ni rafiki yako unaweza kunambia.?

Kama mnavyojua Lisa sio mtu wa kujichanganya nikitoka kazini nipo kwangu siku za kuwa nyumbani nitafanya usafi labda na kwenda kanisani. Sio mtu wa kwenda club, sijui beach sijui wapi, kwa ujumla sio mzururaji. Mimi ni kazini, kanisani, na kuwatembelea ndugu na penyewe mara moja moja ndio Maisha yangu.

Hapana auntie sina mahusiano husiano kwa sasa.

Basi mwanangu jaribu kumpa nafasi Dav japo kidogo najua hawezi kukuumiza wala kukudhuru kumbuka mimi na mama yake Dav tupo upande wako. Auntie ananibembeleza mpaka nalala huyu mwanamke (auntie) alikuwa na upendo sijawahi kuona

Kumekucha!

Nimekubalia Dav ombi lake, tunapendana sana yaani mapenzi ni matamu yaani ukinichanja damu inatoka jina Dav. Maisha yanaendelea vizuri kabisa na Dav ndo alikuwa mwanaume wangu wa kwanza katika Maisha yangu nampenda sana. Maisha yangu hayaishi safari ni Dar – Morogoro, Morogoro – Dar na Dav hivyo hivyo asipokuja yeye nitaenda mimi Morogoro na kuna kipindi naweza kwenda kwa Dav nikaishia kwake hata kwetu nisifike.

Nipo Dar kazini napokea simu namba ngeni. Halo Lisa mambo, namwitikia na kumuuliza nani mwenzangu anajibu kuwa yeye ni Omary (Omary huyu tulikutana naye ep 4) tumesalimiana akanambia kuwa anategemea kuja Dar wiki moja mbele nikamjibu karibu.

Wiki imepita kweli Omary ananipigia simu na kuomba kuonana na mimi. Sijamkatalia ila nikamwambia kuwa tuonane Jumamosi sababu ni siku ambayo nakuwa sipo kazini.

Jumamosi imefika Omary akanitumia location. Waswahili wanasema kubali wito kubali wito kataa neno. Nikaenda kuonana nae nina shahuku kujua anataka kunambia nini.

Nimefika pale alipo tumekumbatiana nimekaa nikaagiza juice ya matunda huku nina hamu sana ya kujua Omary anataka kunambia nini.

Lisa umependeza sana na unaonekana mkubwa tofauti na kipindi kile.

Hahaa ni kweli nimekua ila sijabadilika bado lakini miaka imeenda lazima nibadilike kidogo.

Lisa naomba unisamehe sana najua kipindi kile nilikuumiza bila sababu.

Unaongelea nini tena.

Lisa bado nakupenda sana nahitaji nikuoe wewe ni mwanamke wa ndoto zangu naomba unisamehe. Huu mguu ni wako nimetoka kanda ya ziwa mpaka dar kwa ajili yako.

Omary kwani mke wako Hawa si yupo sasa inakuwaje unaangaika tena.

Omary huku akitokwa na machozi. Hii ilikuwa mara ya kwanza kumuona mwanaume anatokwa na machozi. Akaanza kunambia “kwani Lisa hujui kilichotokea kati yangu na Hawa hata dada yako hajakwambia?”

Kumetokea nini kati yenu? Mimi sijui chochote nikiongea na dada ni salamu tu hakuna zaidi ya salamu labda na mambo ya familia. Hivyo sijui kitu.

Hawa alinidanganya kumbe yule mimba ambayo ndo ulimwacha nayo haikuwa yangu. Nimelea mtoto ambaye sio wa kwangu yule mwanamke ni msaliti na muuaji. Alinidanganya. Kipindi kile nataka kuanzisha mahusiano na wewe alinionyesha msg ulizokuwa unachati nae ukimweleza unavyompenda supervisor na anavyokununulia vitu. Basi mimi nikamwamini nikajua kweli unatoka na supervisor. Na nilipokuwa naona supervisor mara kwa mara akikuuliza kama unataka soda tunakunywa staff nzima na ukikataa hanunui, na yule dada alivyokuwa amedaivet simu yako nikaamini kweli utakuwa unatoka nae.

Nikaamua kuwa na yeye kumbe alikuwa mjamzito tayari na mhusika alikuwa nje ya nchi kimasomo. Nilitaka kufunga nae ndoa ya kanisani (naomba nieleweke omary sio jina lake nimetumia tu omary kwahiyo msishangae ) alikataa tukaishia kufunga ndoa ya serikali kumbe alikuwa anajua anachokifanya. Jamaa yake alipomaliza masomo amekuja kumchukua yeye na mtoto na ninavyoongea na wewe walishafunga ndoa ya kanisani na sasa wanatarajia mtoto mwingine (kumbe Hawa ni mjamzito)

Omary ilinihukumu pasipo kufuatilia sikutoka na mwanaume yeyote pale kazini kwenu. Pili unafikiri hiyo miaka yote mi ningekaa nakusubiri wewe ili ujue ukweli? Asingekuacha je ingekuwaje. Mimi nipo na mahusiano yangu tena yapo imara siwezi kumsaliti mpenzi wangu wala kuwaza kumuacha. Ila pole kwa yalokukuta. Alinibembeleza sana lakini nikamkatalia nawezaje kumkubalia wakati mimi na Dav tuko sawa.

Tuliachana hapo akiwa mnyonge sana. Toka siku hiyo sina taarifa zake. Ila asikwambie mtu, ukisikia aliyekuumiza bila sababu naye kaumizwa moyo wako unafurahi sana. Kwakweli moyoni nilifurahia anguko la omary. Mchana mwema.
 
EP 15

Baada ya kufika pale duka la dawa sijataka kukaa namuaga auntie na kwenda nyumbani. Auntie ananiambia nimsubiri afunge tuondoke wote lakini namkatalia nachukua bodaboda na kurudi nyumbani. Nyumbani namkuta mdogo wangu, dada wa kazi wapo sebuleni nawasalimia na kwenda chumbani kwangu sina mudi kabisa ya kuongea na mtu yeyote.

Auntie anarudi ananigongea namfungulia anakaa kitandani na kunilaza miguuni kwake na kuniuliza kwa upole mbona umekuja umebadilika Lisa kwani Dav amekufanya nini? Namwambia Aunt wewe si ulikuwa unamsifia Dav wewe yaani hapo tena sijisikii kumuita kaka kama mwanzo. Unaweza kuamini kuwa ananinataka kimapenzi, mwanamke wake namjua, mama yake ananichukulia kama bint yake, marafiki zake wanajua kuwa mimi ni mdogo wake baadhi ya marafiki zangu wanajua sisi ni ndugu inakuwaje ananitaka kimapenzi. Simpendi Dav aunt naanza kumchukia.

Auntie huku akinichezea nywele zangu. Lisa mwanangu sikia Dav hajakukosea kukueleza hisia zake. Kumbuka mna historia wewe na Dav hamjafahamiana leo au jana angekuwa na nia mbaya na wewe angelishakwambia maneno hayo zamani tu. Lakini kumbuka amevumilia muda gani. Pili alikupambania na bado atakupambania. Angekuwa na nia mbaya asingeniambia na mimi. Namuuliza auntie kwani na wewe ulikuwa unalijua hili?

Akanijibu ndio sio mimi tu hata mama yake Dav anajua angekuwa na nia mbaya kabisa asingetushirikisha na sisi. Dav anakupenda tena sana alafu ni kijana mzuri tu. Au una mahusiano mengine huko Dar na kama unayo yakoje mimi ni rafiki yako unaweza kunambia.?

Kama mnavyojua Lisa sio mtu wa kujichanganya nikitoka kazini nipo kwangu siku za kuwa nyumbani nitafanya usafi labda na kwenda kanisani. Sio mtu wa kwenda club, sijui beach sijui wapi, kwa ujumla sio mzururaji. Mimi ni kazini, kanisani, na kuwatembelea ndugu na penyewe mara moja moja ndio Maisha yangu.

Hapana auntie sina mahusiano husiano kwa sasa.

Basi mwanangu jaribu kumpa nafasi Dav japo kidogo najua hawezi kukuumiza wala kukudhuru kumbuka mimi na mama yake Dav tupo upande wako. Auntie ananibembeleza mpaka nalala huyu mwanamke (auntie) alikuwa na upendo sijawahi kuona

Kumekucha!

Nimekubalia Dav ombi lake, tunapendana sana yaani mapenzi ni matamu yaani ukinichanja damu inatoka jina Dav. Maisha yanaendelea vizuri kabisa na Dav ndo alikuwa mwanaume wangu wa kwanza katika Maisha yangu nampenda sana. Maisha yangu hayaishi safari ni Dar – Morogoro, Morogoro – Dar na Dav hivyo hivyo asipokuja yeye nitaenda mimi Morogoro na kuna kipindi naweza kwenda kwa Dav nikaishia kwake hata kwetu nisifike.

Nipo Dar kazini napokea simu namba ngeni. Halo Lisa mambo, namwitikia na kumuuliza nani mwenzangu anajibu kuwa yeye ni Omary (Omary huyu tulikutana naye ep 4) tumesalimiana akanambia kuwa anategemea kuja Dar wiki moja mbele nikamjibu karibu.

Wiki imepita kweli Omary ananipigia simu na kuomba kuonana na mimi. Sijamkatalia ila nikamwambia kuwa tuonane Jumamosi sababu ni siku ambayo nakuwa sipo kazini.

Jumamosi imefika Omary akanitumia location. Waswahili wanasema kubali wito kubali wito kataa neno. Nikaenda kuonana nae nina shahuku kujua anataka kunambia nini.

Nimefika pale alipo tumekumbatiana nimekaa nikaagiza juice ya matunda huku nina hamu sana ya kujua Omary anataka kunambia nini.

Lisa umependeza sana na unaonekana mkubwa tofauti na kipindi kile.

Hahaa ni kweli nimekua ila sijabadilika bado lakini miaka imeenda lazima nibadilike kidogo.

Lisa naomba unisamehe sana najua kipindi kile nilikuumiza bila sababu.

Unaongelea nini tena.

Lisa bado nakupenda sana nahitaji nikuoe wewe ni mwanamke wa ndoto zangu naomba unisamehe. Huu mguu ni wako nimetoka kanda ya ziwa mpaka dar kwa ajili yako.

Omary kwani mke wako Hawa si yupo sasa inakuwaje unaangaika tena.

Omary huku akitokwa na machozi. Hii ilikuwa mara ya kwanza kumuona mwanaume anatokwa na machozi. Akaanza kunambia “kwani Lisa hujui kilichotokea kati yangu na Hawa hata dada yako hajakwambia?”

Kumetokea nini kati yenu? Mimi sijui chochote nikiongea na dada ni salamu tu hakuna zaidi ya salamu labda na mambo ya familia. Hivyo sijui kitu.

Hawa alinidanganya kumbe yule mimba ambayo ndo ulimwacha nayo haikuwa yangu. Nimelea mtoto ambaye sio wa kwangu yule mwanamke ni msaliti na muuaji. Alinidanganya. Kipindi kile nataka kuanzisha mahusiano na wewe alinionyesha msg ulizokuwa unachati nae ukimweleza unavyompenda supervisor na anavyokununulia vitu. Basi mimi nikamwamini nikajua kweli unatoka na supervisor. Na nilipokuwa naona supervisor mara kwa mara akikuuliza kama unataka soda tunakunywa staff nzima na ukikataa hanunui, na yule dada alivyokuwa amedaivet simu yako nikaamini kweli utakuwa unatoka nae.

Nikaamua kuwa na yeye kumbe alikuwa mjamzito tayari na mhusika alikuwa nje ya nchi kimasomo. Nilitaka kufunga nae ndoa ya kanisani (naomba nieleweke omary sio jina lake nimetumia tu omary kwahiyo msishangae ) alikataa tukaishia kufunga ndoa ya serikali kumbe alikuwa anajua anachokifanya. Jamaa yake alipomaliza masomo amekuja kumchukua yeye na mtoto na ninavyoongea na wewe walishafunga ndoa ya kanisani na sasa wanatarajia mtoto mwingine (kumbe Hawa ni mjamzito)

Omary ilinihukumu pasipo kufuatilia sikutoka na mwanaume yeyote pale kazini kwenu. Pili unafikiri hiyo miaka yote mi ningekaa nakusubiri wewe ili ujue ukweli? Asingekuacha je ingekuwaje. Mimi nipo na mahusiano yangu tena yapo imara siwezi kumsaliti mpenzi wangu wala kuwaza kumuacha. Ila pole kwa yalokukuta. Alinibembeleza sana lakini nikamkatalia nawezaje kumkubalia wakati mimi na Dav tuko sawa.

Tuliachana hapo akiwa mnyonge sana. Toka siku hiyo sina taarifa zake. Ila asikwambie mtu, ukisikia aliyekuumiza bila sababu moyo wako unafurahi sana. Kwakweli moyoni nilifurahia anguko la omary. Mchana mwema.
Mchana mwema pia Dadakidoti
 
Ep 16

Mapenzi yetu na Dav yanaendelea vizuri yapo imara kabisa. Viugomvi vidogo vidogo vipo lakini tuko sawa kikubwa tunapendana.

Mke wa baba yangu mdogo anaumwa amelazwa hospitali, baba mdogo amesafiri hana msaada wowote. Watoto wake wapo shule za bweni. Mimi inabidi nichukue jukumu la kumuguza. Kumpelekea chai, mchana na jioni mpaka anavyoruhusiwa sina kabisa kinyongo nae. Tena siku hizi mimi na familia ya bamdogo ni marafiki tupo poa kabisa.

Bibi yangu mzaa baba anafariki tunaenda kijijini kanda ya ziwa. Baba anaenda na mke wake yaani auntie na mdogo wetu ambaye mama yake yupo Arusha anafanya kazi bar. Na mimi natokea dar naenda msibani. Dav naye siku ya mazishi alikuwepo alikuja ndege pesa kwake sio tatizo. Baada ya mazishi namtambulisha Dav kama mchumba wangu kwenye familia. Dav anaondoka anatuacha sisi tukiendelea na msiba.

Baada ya wiki mimi na aunt tunarudi, tunamwacha baba Kanda ya ziwa. Nimepita Morogoro kama kawaida yangu. Familia ya Dav akiwepo mama yake wanakuja kutupa pole. Baada ya siku chache ninakuja dar kuendelea na Maisha yangu kama kawaida, mdogo wangu anang’ang’ana kuja na mimi Dar namkubalia tunamwacha aunt na msichana wa kazi.

Untie yetu anatokomea kusikojulikana.

Kama siku mbili tupo dar mdogo wangu napokea simu kutoka kwa dada wa kazi wa untie anaongea huku analia namuliza kuna nini anambia mama toka ameondoka juzi leo siku ya pili hajarudi simu yake haipatikani. Baada ya kumaliza kuongea na dada najaribu kumpigia auntie simu lakini simpati.

Nampigia simu baba na kumweleza kila kitu. Nafunga safari narudi Morogoro nampigia simu Dav nakumwambia kilichotokea tunaanza kumtafuta auntie pasipo mafanikio. Tumetoa taaarifa polisi, tumeangalia hospitali hamna kitu auntie yetu alipotea hivyo katika Maisha yetu baba naye amerudi lakini ajabu haonyeshi jitihada yoyote ya kumtafuta auntie.

Maisha lazima yaendelee narudi zangu kuendelea na majukumu yangu sina furaha ya kumpoteza auntie.

Auntie hakubeba kitu chochote kinachomhusu nahisi aliondoka na nguo zilizokuwa mwilini mwake tu. Duka lake funguo aliacha na alikuwa hadaiwi hata kodi, nguo zake kabatini. Alikuwa anajenga nyumba yake Kihonda hakubeba hata hati yake ya kiwanja.

Wiki mbili tu toka auntie aondoke napigiwa simu na mama yangu mkubwa mke wa bamkubwa niliyekuwa naishi kwake wakati nasoma baada ya salam ananiambia kuwa ana umbea wa kunipa. Namuuliza umbea gani tena ananiambia mama yenu mdogo amerudi na wana mpango wa kufunga ndoa na baba yako. Nilimjibu mamkubwa asante Mungu amesikia kilio changu. Mamkubwa akasema sio huyo auntie yenu namaanisha yule mama yake mdogo wako (anamtaja jina mdogo wangu tunayekutana kwa baba) nikamuuliza tena nikidhani nitakuwa nimekosea kusikia akarudia majibu yaleyale.

Nikamwambia mamkubwa haiwezekani baba hawezi kumrudia mwanamke yule kumbuka alikuwa ameshaolewa na mwanaume mwingine na ameshazaa mtoto mwingine. Pia isitoshe alikuwa anafanya kazi bar. Baba yangu ninayemjua hawezi kufanya hivyo pia hata msiba wa bibi bado mbichi jamani hawezi.

Mamkubwa akanimbia najua ulikuwa unampenda auntie yako lakini ndo hivyo na huyo mama yenu mdogo na mtoto wake kaja naye wapo wote nyumbani kwenu.

Nampigia simu baba kwa hasira na kumuuliza baba umefanya nini auntie mpaka sasa hatujui kilichompata unawezaje kumfanyia hivi auntie. Baba anmbia auntie yako sijamfukuza ameondoka mwenyewe sasa ulitegemea mimi nitaishije bila mwanamke. Baba sio haki kabisa hii. Baba akaamua kunikatia simu.

Ijumaa nafunga safari kwenda Morogoro bila kumwambia Dav, namwambiaje kitu cha aibu kama hicho. Moja kwa moja nyumbani namkuta mke wa baba amejaa tele tena analalia kitanda alichokuwa analalia auntie yangu. Vitu vya auntie vimetolewa nje. Aisee niliumia sana. Mimi ni mkimya nikakaa kimya kwanza nimsubiri baba. Mke wa yaani mama yetu wa kambo hana kabisa hata habari na yupo bize na Watoto wake mara awakumbatie mara awabusu. Mume wangu haitoki mdomoni.

Baba anarudi nyumbani tunasalimiana mama wa kambo anavyojibebisha sasa kwa baba mara amshike sikio, mara amlalie begani mara sijui afanyeje yaani mimi tamani wote niwafanye nini hata sielewi naenda chumbani kwangu vitu vipo hovyo hovyo kumevurugwa hakufai. Tofauti na auntie akiwepo panakuwa pako poa kabisa.

Tumelala asubuhi namwambia baba mbona vitu vya auntie vimetupwa nje? Vinawakiwa nje na kunyeshewa mvua huku nalia kwa uchungu. Baba ananambia alivyitoa mama yako bado hajapata pa kuviweka. Baba mgeviweka chumbani kwangu au kwa Joy. Baba alipojenga alitupa vyumba vyetu yaani kila mtoto ana chumba chake cha kulala.

Nikamtafuta kijana pale mtaani nikavibeba vitu vya auntie na kuviweka chumbani kwangu na kuangalia vile vitu muhimu na kuvihifadhi. Nachukua funguo wa duka lake naenda dukani yaani huko ndo hapafai dawa zimetupwatupwa, vipodozi vingine vimemwangwa yaani sijui hata cha kufanya naamua kupaacha hivyo.

Baba amefunga ndoa na mke wake kimya kimya si Joy wala mimi alikuwepo wala ndugu zake wakina bamdogo, bamkubwa pia hawakuwepo. Tunasikia kwa watu.

Nampigia simu baba na kumuuliza kwanini amefunga ndoa kimya kimya kama angekuwa mama yetu au auntie asingetwambia? Au ndio tumekwisha kubaguliwa tayari baba anachonieleza hata hakieleweki.

Baada ya miezi kupita ndo tunakuja kusikia kuwa auntie yupo Zanzibar ndo anapoishi hajawahi tena kurudi kwenye Maisha yetu. Nampenda auntie yangu nimejitahidi kumtafuta lakini wapi sina cha kufanya zaidi ya kumwombea Maisha marefu.

Jioni njema tukutane kesho.
 
Back
Top Bottom