Kuna yeyote aliyewahi kufanikiwa kupata simu yake iliyoibiwa kupitia Cyber Crime Unit?

Kuna yeyote aliyewahi kufanikiwa kupata simu yake iliyoibiwa kupitia Cyber Crime Unit?

Zamazamani

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2008
Posts
1,869
Reaction score
787
Wanajamvi,

Nipo hapa kutaka kujua nakosea wapi.

Mpaka sasa ndani ya miezi sita nimeibiwa /poteza simu tatu- smart phones. Simu ya kwanza nikairipoti polisi, Central Police, Dodoma kwa taratibu za kawaida za kipolisi pale Cyber Crime Unit lakini nikawa sina IMEI number hivyo nikaambiwa ndiyo sababu ya kuwa ngumu kuipata, ikapotea.

Simu ya pili ikaibiwa Dar es Salaam, nikaripoti polisi Oysterbay. Pamoja na kuwapa IMEI number, na kuahidi kwamba nipo tayari kuongeza 'nguvu'- lakini nayo nikaishia kuzungushwa - ikapotea.

Simu ya tatu mwezi January mwanzoni ikiaibiwa Dar es Salaam, nikafuata taratibu za kipolisi - Cyber Crime Unit - nimefuatilia wee mpaka sasa nimekaribia kukata tamaa, naambulia stori na kuzungushwa tu, nayo pia inaelekea itapotea.

Sasa najiuliza: Nakosea wapi wakuu? Kama kutoa cha mboga ili kutia nguvu mbona siyo kesi na sijabisha wakuu? Najiuliza kwanini inakuwa ishu kubwa kupata huduma hii wakati ndiyo kazi yao kitaalam?

Naomba ushauri nini cha kufanya au wapi pa kwenda sababu simu zinaibiwa kila siku na hasara yake siyo ya kitoto, vinginevyo nikomae na vitochi tu.

PS. Najua kuna njia za ku-block isitumike au kui-trace simu ilipo pia ikawa mbinde -- njia pekee iliyoonekana itafaa ilikuwa ni kutumia chombo cha dola, lakini mpaka sasa bila bila.
 
Mkuu ulijaribu kwenda TCRA? Labda wangekupa mwangaza na pia ungejaribu kwenda pale sayansi kwa madogo wa UD-CICT (University Of Dar es Salaam College Of Information and Communication Technology) wangeweza kukushauri utumie manoeuvre gani maana hayo ndio mambo yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polisi ni janga sana kwenye hili, gharama utakazoombwa ili simu yako irudishwe zinalingana na ununuzi wa simu mpya hivyo wengi hukata tamaa. Polisi imekosa weledi kwenye Kitengo cha Cyber kwa kweli ni holela holela tu vijana wanatafuta namna ya kutoka na kupush vyombo
 
Polisi ni janga sana kwenye hili, gharama utakazoombwa ili simu yako irudishwe zinalingana na ununuzi wa simu mpya hivyo wengi hukata tamaa. Polisi imekosa weledi kwenye Kitengo cha Cyber kwakweli ni holela holela tu vijana wanatafuta namna ya kupush vyombo.
Ni kweli naona wamejaa vijana wenye uchu wa kutoboa fasta fasta kweli kweli
 
Hapo unatafuta kupigwa pesa yako kisha simu hupati, hapo kwenye chamboga
 
Unakosea kitu kimoja, Kama unatumia Android, Kuna sehemu ya kuset kwamba iwapo simu itapotea Google watakuwezesha kuiona mtaa ilipo kupitia Google map.

Kuripot cyber crime sio uhakika kuwa utaipata, kutrace mtu kunahitaji resources, watu, magari, helicopters etc,
 
Mei nilikaribu kuitrack nikaiona kwenye map iko Sinza karibia na Shule ya Mugabe nilivuotoka tu mtandaoni nirudi tena sikuiona Tena nilikutana na mjanja sema mungu atamlaani[emoji24][emoji24] afe kifo cha Moto niliibiwa na mtu kwenye pikipiki kwenye gari aliingiza mkono gari ikiwa kwenye mwendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupata simu iliyoibiwa ni kazi ngumu Sana... Kama alivyotanguliza kusema mdau hapo juu kuwa mwizi anahonga hata akikamatwa!
 
2016 niliibiwa simu yangu Dodoma Uhindini (iPhone 6s+) karibia na car wash mida ya saa 2 usiku, within a two days nikaipata na cover lake tatizo system charge tu ndio walikua wameiharibu

Niliipata Msalato mbele kabisa ndani ndani kuna sehemu wanauza matofali ndio huko waliko kuwepo, na bahati nzuri ile tunafika tumewakuta nayo simu red handed kabisa wenyewe wamekaa nje wanapiga story[emoji16][emoji16] kwa msaada wa central police (nililipia kiasi) na Internet cafe kuna mkaka mtundu wa simu (nako nililipia)

Ilikua wanazima na kuwasha huku icloud inasoma, police wakafatilia kupitia imei jioni nikapigiwa simu niende na hela ya tax twende hiyo sehem (walichezea makofi hadi nikawaonea huruma) na simu yenyewe nikaiuza wiki hiyohiyo
 
Back
Top Bottom