kundi kutajwa katika katiba haitoi haki kama katiba haina mfumo wa kutoa haki

kundi kutajwa katika katiba haitoi haki kama katiba haina mfumo wa kutoa haki

tatizo lako unadhani amani inakuja yenyewe tu!

nimekueleza angalia nchi yoyote yenye amani tazama nyuma kabla kulikuwa na mambo gani na tazama nchi yoyote yenye vurugu tazama nyuma kulikuwa na nini.

amani au vurugu haviji kama mvua kuwa vinakuja vyenyewe bali vinatokana na maisha ya wananchi.

ukiangalia maisha yetu ya sasa unaweza kujua tunaelekea wapi.

kusema amani amani haisadii kwa kuwa huko nyuma hatukuijenga kwa kuhubiri maneno hayo bali yanayotendeka katika maisha ya watu.


matendo yetu sote ndio yatakayotupeleka ama kwenye amani au kinyume.


Wewe unajifanya unajua sana theories za kuvuruga amani basi nenda Field work Somalia ukajiunge na Elshabab. Tanzania ninayoijua mimi imejengwa kwenye msingi imara Mvua zinakuja, Mafuriko yanakuja na Pepo zinakuja zinaipiga lakini haianguki ng'ooo kwa kuwa imejengwa juu ya Mwamba! mawazo uliyonayo hayako applicable in Tanzania nakuonea huruma mtoto!Na Katiba inayopendekezwa inakuja mwendo mswano ucpime!
 
kwanza nakushangaa na kukudharau kama haya ninayoyasema unaona yanaendana na elshabab.

inanisikitisha sana!

lakini unanisikitisha pale ambapo pengine ulikuwa hujui kwa nini tumekuwa na amani na kwa nini wengine wamekuwa na vurugu.

vurugu au amani ni sawa na kilimo kwa maana unaadaa shamba, unapanda, unapalilia, unaweka mbolea na mwisho unavuna.

sasa amani au vurugu ni mavuno ambayo yapo matendo ambayo yakifanyika kwenye jamii basi inakuwa ni kama unalima shamba la hayo.

yapo mambo ambayo yakifanyika ni kama unapanda mbegu za kutoa vurugu au amani.

yapo mambo ambayo yakifanyika ni kama unaweka mbolea katika mazao yako haya ambayo yanakuja kutoa vurugu au amani.

na mwisho ni kufaidi matunda ya kile mlichokipanda.

elishabab, boko haramu, isil, LRA na mengine haya ni makundi ambayo yanaweka mbolea tu kwenye mazao ambayo jamii inakuwa tayari imekwisha yapanda na kuvuna mazao hayo ya wanajamii.

nadhani utakumbuka kuwa matatizo ya somalia hayajaanzia kwa elshabab wala matatizo ya nigeria hayajaanzia kwa boko haramu wala matatizo ya uganda hayajaanzia kwa LRA.

ni vigumu kwa makundi haya kuweka kujitokeza katika jamii iliyojenga usawa na haki na kila mwananchi anaridhika.

lakini jamii yoyote inayojenga manunguniko, inayojenga chuki, inayojenga malalamiko katika jamii yake ni mambo ambayo baadhi ya wanajamii wanayafanya ambayo yanapelekea baadhi ya watu kuwa na mioyo ya hivyo. na wapuudhi hawa wanapopata nafasi wanakaribishwa na watu hawa ambao hawajui cha kufanya juu ya manunguniko yao ingawa mwisho inakuwa ni kuangamia zaidi.

Wewe unajifanya unajua sana theories za kuvuruga amani basi nenda Field work Somalia ukajiunge na Elshabab. Tanzania ninayoijua mimi imejengwa kwenye msingi imara Mvua zinakuja, Mafuriko yanakuja na Pepo zinakuja zinaipiga lakini haianguki ng'ooo kwa kuwa imejengwa juu ya Mwamba! mawazo uliyonayo hayako applicable in Tanzania nakuonea huruma mtoto!Na Katiba inayopendekezwa inakuja mwendo mswano ucpime!
 
kutafuta chanzo cha migogoro ya jamii usiishie kwenye swali moja au mawili tu na ukafikia muafaka.

jiulize jamii kabla ya kuingia katika migogoro ilikuwa inaishi vipi? jiulize waliingiaje katika migogoro, jiulize migogoro yao kama imekuwa ikibadilika au ni ya aina moja, jiulize mambo mengi sana.

lakini katika yote hayo utagundua kuwa jamii zinaanzia katika kutokuwa na usawa, zinafuata propaganda za kueneza chuki na baadae jamii inaingia katika vurugu na vurugu hizi zinakuwa wakati mwingine zinabadilika au zinakuja na sababu tofauti tofauti.

hapa unaweza kulinganisha taifa linaloelekea katika vurugu na mwili wa mgonjwa wa ukimwi kwa maana mwili ukishakuwa dhaifu kila ugonjwa ni wake. jamii inapokuwa imekwisha vurugika kila vurugu inawezekana.

lakini kama tunaweza kutambua hayo ni kurekebisha mifumo ili ianze kufanya kazi na kila mwananchi ataridhika na utendaji.

nitakupa mifano.

zipo nchi zimeingia kwenye vurugu kwa sababu ya rasilimali za nchi watu wanaona haziwanufaishi wananchi. leo hii sisi hatutaki kutengeneza mifumo ili isimamie, unapokuwa huna mifumo ya kusimamia ukimpa mmoja wenu dhamana ya kuongea na wawekezaji basi anachukua rushwa anasaini mikataba ya kipuuzi maana mtoa rushwa anatoa ili apore apatiwe mkataba wa kumpa faida.

sasa anayepinga kuweka mifumo ya kusimamia katika nchi hii hivi kweli anajua anachokifanya

kama anajua je analitakia nini taifa hili kiuchumi, je analitakia nini taifa hili kiamani?

leo hii mnaleta wawekezaji mnalegeza masharti ili waje kuwekeza kwenu lakini mkijua baadae mtakuja kuwatoza kodi lakini kutokana na kutokuwepo kwa mifumo ya usimamiaji mnayemkabidhi ofisi ya kusimamia haya mda ukibaki mchache katika mkataba basi anachukua rushwa anaongeza mda wa mwekezaji huyu kutolipa kodi na mwisho ni nchi kutopata faida iliyolengwa.

hivi anayegangania nchi kutokuwa na mifumo ya usimamiaji anajua analolifanya au ni mbambaishaji tu, hivi analitakia nini taifa hili kiuchumi? hivi analitakia nini taifa hili kiamani?

leo hii taifa linakaa linabuni mashirika au taasisi na inaonekana wazi kuwa mashirika haya yataleta faida na tija kwa taifa. lakini kutokana na kutokuwepo kwa mifumo ya kusimaia na kudhibiti basi mnayemkabidhi ofisi kazi yake ni kuandaa miradi ya kutafuta mianya ya kujinufaisha, wanaandaa mipango ya kuibia ofisi zao.

katika mazingira kama haya nani anaweza kutuletea maendeleo?

katika mfumo kama huu hakuna mtu mmoja anaweza kudhibiti taifa hili bali ni kila mmoja wetu kuwa polisi kutokomeza haya.

kila mmoja wetu kuwa polisi ni kwa kufanya mifumo ya kitaifa ya usimamiaji ifanye kazi kwa maana raisi anasimamia walio chini yake ambao ni mawaziri, mawaziri wanasimamia walio chini yao, bodi, wakurugenzi wanasimamia walio chini yao. bunge linafanya kazi yake, mahakama inafanya kazi yake.

kila anayezembea hatua ya kwanza ni kumwajibisha mzembe na sio kumuunga mkono ili aendelee kuwa mzembe kwa kuwajibisha walio chini yake na yeye akabaki salama.

hapo kila mtu mwenye dhamana atawajibika kutekeleza majukumu yao.

katiba ndio sehemu pekee ya kufanya mifumo ifanye kazi.

wapo wababaishaji wachache ambao ndio wanatufanya tupotee lakini wapo watanzania makini wengi tu ambao mifumo ikifanya kazi watatuletea maendeleo kwa haraka sana.

Wewe unajifanya unajua sana theories za kuvuruga amani basi nenda Field work Somalia ukajiunge na Elshabab. Tanzania ninayoijua mimi imejengwa kwenye msingi imara Mvua zinakuja, Mafuriko yanakuja na Pepo zinakuja zinaipiga lakini haianguki ng'ooo kwa kuwa imejengwa juu ya Mwamba! mawazo uliyonayo hayako applicable in Tanzania nakuonea huruma mtoto!Na Katiba inayopendekezwa inakuja mwendo mswano ucpime!
 
kutafuta chanzo cha migogoro ya jamii usiishie kwenye swali moja au mawili tu na ukafikia muafaka.

jiulize jamii kabla ya kuingia katika migogoro ilikuwa inaishi vipi? jiulize waliingiaje katika migogoro, jiulize migogoro yao kama imekuwa ikibadilika au ni ya aina moja, jiulize mambo mengi sana.

lakini katika yote hayo utagundua kuwa jamii zinaanzia katika kutokuwa na usawa, zinafuata propaganda za kueneza chuki na baadae jamii inaingia katika vurugu na vurugu hizi zinakuwa wakati mwingine zinabadilika au zinakuja na sababu tofauti tofauti.

hapa unaweza kulinganisha taifa linaloelekea katika vurugu na mwili wa mgonjwa wa ukimwi kwa maana mwili ukishakuwa dhaifu kila ugonjwa ni wake. jamii inapokuwa imekwisha vurugika kila vurugu inawezekana.

lakini kama tunaweza kutambua hayo ni kurekebisha mifumo ili ianze kufanya kazi na kila mwananchi ataridhika na utendaji.

nitakupa mifano.

zipo nchi zimeingia kwenye vurugu kwa sababu ya rasilimali za nchi watu wanaona haziwanufaishi wananchi. leo hii sisi hatutaki kutengeneza mifumo ili isimamie, unapokuwa huna mifumo ya kusimamia ukimpa mmoja wenu dhamana ya kuongea na wawekezaji basi anachukua rushwa anasaini mikataba ya kipuuzi maana mtoa rushwa anatoa ili apore apatiwe mkataba wa kumpa faida.

sasa anayepinga kuweka mifumo ya kusimamia katika nchi hii hivi kweli anajua anachokifanya

kama anajua je analitakia nini taifa hili kiuchumi, je analitakia nini taifa hili kiamani?

leo hii mnaleta wawekezaji mnalegeza masharti ili waje kuwekeza kwenu lakini mkijua baadae mtakuja kuwatoza kodi lakini kutokana na kutokuwepo kwa mifumo ya usimamiaji mnayemkabidhi ofisi ya kusimamia haya mda ukibaki mchache katika mkataba basi anachukua rushwa anaongeza mda wa mwekezaji huyu kutolipa kodi na mwisho ni nchi kutopata faida iliyolengwa.

hivi anayegangania nchi kutokuwa na mifumo ya usimamiaji anajua analolifanya au ni mbambaishaji tu, hivi analitakia nini taifa hili kiuchumi? hivi analitakia nini taifa hili kiamani?

leo hii taifa linakaa linabuni mashirika au taasisi na inaonekana wazi kuwa mashirika haya yataleta faida na tija kwa taifa. lakini kutokana na kutokuwepo kwa mifumo ya kusimaia na kudhibiti basi mnayemkabidhi ofisi kazi yake ni kuandaa miradi ya kutafuta mianya ya kujinufaisha, wanaandaa mipango ya kuibia ofisi zao.

katika mazingira kama haya nani anaweza kutuletea maendeleo?

katika mfumo kama huu hakuna mtu mmoja anaweza kudhibiti taifa hili bali ni kila mmoja wetu kuwa polisi kutokomeza haya.

kila mmoja wetu kuwa polisi ni kwa kufanya mifumo ya kitaifa ya usimamiaji ifanye kazi kwa maana raisi anasimamia walio chini yake ambao ni mawaziri, mawaziri wanasimamia walio chini yao, bodi, wakurugenzi wanasimamia walio chini yao. bunge linafanya kazi yake, mahakama inafanya kazi yake.

kila anayezembea hatua ya kwanza ni kumwajibisha mzembe na sio kumuunga mkono ili aendelee kuwa mzembe kwa kuwajibisha walio chini yake na yeye akabaki salama.

hapo kila mtu mwenye dhamana atawajibika kutekeleza majukumu yao.

katiba ndio sehemu pekee ya kufanya mifumo ifanye kazi.

wapo wababaishaji wachache ambao ndio wanatufanya tupotee lakini wapo watanzania makini wengi tu ambao mifumo ikifanya kazi watatuletea maendeleo kwa haraka sana.
Acha porojo zako bhana hujielewi wewe!
 
kama nilivyosema hapo mwanzo jamii yoyote inayotegemea mtu mmoja mmoja kubadilika kwa kutumia nafsi yake inajidanganya na jamii hiyo ina mawazo ya fisi.

fisi huwa akimuona mlevi anatembea anarusha mikono huwa anamfuata akitegemea mikono hiyo itadondoka na aokote lakini mpaka mwisho wa safari mikono haidondoki na fisi hukosa.

maisha ya wanadamu yana kitu kinaitwa fursa na hizo fursa za maisha ndizo wananchi hutumia kuendesha maisha.

mfano chukua usafiri wa dar es salaam,

kama unakaa gongo la mboto na kutokana na matatizo ya usafiri watu wanapanda magari kupitia madirishaji na kukimbiza magari unadhani jamii itabadilika kwa watu wenyewe kukataa kupanda kupitia madirishani? ki msingi ni vigumu kwa maana yule mmoja atakayesema siwezi kupanda kupanda kupitia madirishani basi kila siku atafika kazini saa nne. sasa kwa njia hii kweli unadhani jamii inaweza kubadilika? kwa maana hakuna mwajiri atakuelewa kila siku unachelewa kazini na unamuambia mimi siwezi kupanda gari kupitia dirishani au kukimbiza na kwa asubuhi na mapema usafiri hakuna watu wanapanda kupitia madirishani na kukimbilia sasa sisi wastaarabu mpaka saa nne ndio tupande. sijui kama wewe ni mwajiri utamuonaje mfanyakazi wako wa hivyo na hapo ujiulize je jamii kweli inaweza kubadilika kwa mtu mmoja mmoja kufanya maamuzi?

chukua mfano mwingine wa rushwa katika sekita ya afya. ukiwa na mgonjwa anaumwa na umefika hospitali na mgonjwa hali yake ni mbaya lakini mara ukipeleka faili kwa daktari hauitwi kuingia ndani kumuona daktari, watumishi wanakuambia habari ambazo ukiwasikiliza kwa juu wanaonekana wako sahihi lakini mtu akitoa kitu kidogo mazingira yanabadilika. sasa utajiangalia mfukoni kuna nini na kutoa ili mgonjwa wako apone au utaanza kubadilika kwa kusema mimi siwezi kutoa rushwa hata kama mgonjwa anakufa, na kama wamezembea kwa mgonjwa kukaa mda mrefu bila kuhudiwa au mpaka mgonjwa akafa hakuna mamlaka inayokusaidia kuangalia kama kuna uzembe na kuwajibisha bali mgonjwa akifa unaenda kuzika. je unafikiri jamii inaweza kumaliza rushwa hii katika sekita ya afya kwa watu kukataa kutoa rushwa kwa njia hii?

ki msingi hakuna jamii inaondoa maovu au kuweka utaratibu mzuri kwa kutegemea watu wenyewe kubadili tabia.

bali jamii inabadilishwa kwa kuweka sheria na kanuni na kusimamia kanuni hizo.

kama mamlaka husika zitaweka utaratibu wa kupanda kwenye mabasi na zikasimamia kuwajibisha anayekiuka bila shaka watu watafuata. lakini kama hakuna utaratibu wenye usimamiaji anayejifanya kuleta utaratibu anageuka mjinga.

kama huduma za afya zitawekewa taratibu na kanuni na zikasimamiwa bila shaka yeyote anayekuja na mgonjwa na akazungushwa ana pa kukimbilia kutafuta msaada na hatatoa rushwa lakini kama taratibu na kanuni hakuna kila atakayejifanya kuleta kanuni atageka mjinga.

hivyo tusitegemee jamii yoyote kubadilika kwa kutegemea maamuzi ya mtu mmoja mmoja kwa maana kama maisha yana mifumo ya kipuuzi ndiyo inatumika kuendesha maisha kila mtu atajaribu kujiweka katika mifumo hiyo ya kipuuzi ili awini maisha.

lakini watu hawa wanakuwa wanatambua kuwa njia za kistaarabu ni bora zaidi na jamii inatakiwa kubadili mifumo kwa jamii nzima.

hapa ndipo linapokuja swala la kusema kama tunataka mabadiliko ni swala la kujitazama na kuangalia kama taifa tatizo letu liko wapi? na sote tuweke mifumo ya kutufanya kuenenda katika mifumo hiyo.

Huko kujielewa ndo kuanze na wewe maana hujielewi kila wakati sa cjui unaota nini mchana mchana.
 
kwanza nakushangaa na kukudharau kama haya ninayoyasema unaona yanaendana na elshabab.

inanisikitisha sana!

lakini unanisikitisha pale ambapo pengine ulikuwa hujui kwa nini tumekuwa na amani na kwa nini wengine wamekuwa na vurugu.

vurugu au amani ni sawa na kilimo kwa maana unaadaa shamba, unapanda, unapalilia, unaweka mbolea na mwisho unavuna.

sasa amani au vurugu ni mavuno ambayo yapo matendo ambayo yakifanyika kwenye jamii basi inakuwa ni kama unalima shamba la hayo.

yapo mambo ambayo yakifanyika ni kama unapanda mbegu za kutoa vurugu au amani.





yapo mambo ambayo yakifanyika ni kama unaweka mbolea katika mazao yako haya ambayo yanakuja kutoa vurugu au amani.

na mwisho ni kufaidi matunda ya kile mlichokipanda.

elishabab, boko haramu, isil, LRA na mengine haya ni makundi ambayo yanaweka mbolea tu kwenye mazao ambayo jamii inakuwa tayari imekwisha yapanda na kuvuna mazao hayo ya wanajamii.

nadhani utakumbuka kuwa matatizo ya somalia hayajaanzia kwa elshabab wala matatizo ya nigeria hayajaanzia kwa boko haramu wala matatizo ya uganda hayajaanzia kwa LRA.

ni vigumu kwa makundi haya kuweka kujitokeza katika jamii iliyojenga usawa na haki na kila mwananchi anaridhika.

lakini jamii yoyote inayojenga manunguniko, inayojenga chuki, inayojenga malalamiko katika jamii yake ni mambo ambayo baadhi ya wanajamii wanayafanya ambayo yanapelekea baadhi ya watu kuwa na mioyo ya hivyo. na wapuudhi hawa wanapopata nafasi wanakaribishwa na watu hawa ambao hawajui cha kufanya juu ya manunguniko yao ingawa mwisho inakuwa ni kuangamia zaidi.


Ego unatumia nguvu kubwa sana kutetea uhalifu, mie sikubaliani na wewe hata kidogo, huo upatikanaji wa Haki unaousema wa kumridhisha kila mtu umeuona wapi dunia hii labda ahela peke yake!wanadamu hawaridhiki wewe usipende kuongea tu bila kufikiri, unaweza kupewa kila kitu ukaanza kulia kuwa umepewa vingi wakupunguzie, wakipunguza unaanza kulia tena waongeze!!! huyu ndio mwanadamu wewe!!!

Hiyo mifano unayoitoa ni ya huko huko sio Tz wewe sie tunajielewa and we know how to handle our difference, I tell you Uganda have been under military rule several times so far Nigeria and Somalia your case study, mazingira yao ya freedom fighting ni tofauti na yetu, hili hivi hulioni usitake turudishane darasani hapa!Kikubwa uelewe kuwa Tanzania iko stable na iko timamu kuhandle mambo yake! Watanzania tuko makini na tunamaamuzi makini katika mambo yanayohusu mustakabali wetu!Usikubali kudanganywa!!!!

Pia kumbuka hili sehemu unayoona wewe ni haki yako mwenzio anaona ni kero kwake, wewe unapoona kuna kero kwako yeye kwake anaona ni haki huyo ndiye mwanadamu sio mkamilifu ndio maana Katiba inayopendekezwa imeweka wazi HAKI ZA BINADAMU SURA YA 5 Kuanzia Ibara ya 32 hadi 59 hapa ukisoma kwa makini utayaona makundi kibao yameainishwa hapo na haki zao ndio maana kila mara nakushauri acha kukimbiza upepo piga kura yako ya ndiyo ili haki hizo zilindwe kwa mujibu wa sheria.
 
kuna mambo yako wazi jamani

mfano hebu angalia swala la ardhi

huko nyuma sekita ya ardhi ilikuwaje? na ujiulize ni kwa vipi sekita ya ardhi ingeweza kuleta migogoro huko tulikotoka?
kimsingi mambo sio lazima yawe parfect 100 % lakini ili kuweza kuleta vurugu kuna limit ya matatizo.

leo hii angalia sekita yetu ya ardhi, leo hii tunakarikisha wawekezaji na tunawapa baadhi yetu dhamana ya kufanya maamuzi katika swala hili la ardhi.

angalia yanayofanyika, yapo maeneo mengi mfano kisarawe kule tumewahamisha wanavijiji katika maeneo yao na kumpa eti mwekezaji kulima mbono (jatropha), kule rukwa tumechukua mashamba tukampa mwekezaji kwa milioni 600 na serikali inatafuta bilioni 3 kukomboa mashamba hayohayo ili kuwapa wakulima ambao iliwanyima mwanzoni. mijini leo hii kuna maeneo madalali wanatapeli watu viwanja, madalali wanapandisha bei za viwanja kiasi mabacho watanzania hawawezi kumudu na hatuna udhibiti wa biashara hizi hivyo uwezekano wa mgeni kuja na kuingia katika biashara hii na kununua kwa bei ndogo kwa wazalendo na kuyapandisha maeneo haya bei na kuyauza kwa bei za juu kwa wageni inawezekana na fedha zinazopatikana zisije kwetu zirudi huko huko nje.

tunacreate nini katika sekita hii ya radhi?

hivi tunajua kitu gani kinaleta vurugu zimbabwe? je hicho kilichosababisha zimbabwe kuwa na vurugu kilianzaje? na kama hakikuanza kama mazingira haya yetu je matokeo ambayo yaliwapeleka kwenye vurugu tunaelekea kutengeneza hayo? na je tuko salama huko tunakokwenda tutakuwa salama kupitia sekita hii ya ardhi?

je tatizo liko wapi?

tatizo ni pale tunapoona serikalini kuna watendaji ambao wanaweza kufanya maamuzi ya kuipeleka taifa kwenye matatizo baadae kwa mwajiriwa mmoja wa serikali kuidhinisha wanakijiji kuhamishwa kumpisha mwekezaji. sekita binafsi inapotoka katika biashara ya nyumba na viwanja mijini ambapo baadae miji yetu inaweza kumulikiwa na wageni na kuwapangangisha wenyeji kwa gharama wanazotaka kuchukua mapato hayo kwao daima. hivi hili linatupeleka wapi pale wananchi watakapobaini baadae kuwa wageni pengine wanawanyanyasa katika sekita ya ardhi au watanzania wanaoneana kupitia sekita ya ardhi.

haya ni mambo ambayo yana possibility ya kutokea iwapo wageni wanaweza kuona fursa hizi za kuteka maeneo yetu na kutumia mianya ya corruption iliyoko katika jamii zetu kuzichukua kwa gharama za kutupa.

lakini mambo haya kama serikali inakuwa imeshindwa kutimiza wajibu wake kufanya kazi yake ni kazi ya bunge kubaini mapungufu haya na kutoa maagizo.

sasa angalia mahusiano yaliyopo baina ya bunge na serikali ambayo yanaathiri utendaji wa bunge kwa maana hawasiamimii bali wanapiga porojo tu za utendaji wa serikali.

hebu angalia udhaifu wa bunge kwa maana bunge linaendeshwa kwa porojo tu na hakuja uwezo wa kitaalamu wa kuchambua utendaji wa serikali katika sekita hii na kuchanganua sekita hii ili waweze kuisimamia serikali.

hapa ndipo tusema hiki kinachotendeka si sahihi lakini kutokuwepo kwa usimamiaji wa bunge ni tatizo kubwa kwa maana kama serikali inajisahau bunge linaikumbusha au kuwajibisha wazembe.

na hapo ndipo unapoweza kubaini umuhimu wa kurekebisha muundo wa mihimili ya juu na kule kukikaa sawa na kuweka kanuni bora za kutelemka chini, yaani nakuambia tutaendesha nchii kwa amani na maendeleo makubwa.

sio kweli kuwa wanadamu hawaridhiki kwa maana wanaolaumu hawawwezi kukosekana ila wanaolaumu kwa sababu zao hawawezi kupata sapoti na watakaa isolated ambao hawawezi kuleta vurugu.

lakini ukiwa na watu wanaolalamika kutoka na mambo yakweli na huku wengine hawalalamiki lakini hawaridhiki, basi hawa wakipata mtu wa kuwachochea kidogo tu katika jambo lolote ili walete vurugu moto wake hauzimiki.

chukua katika mfano wa familia. familia baba na mama wanaweza kuanza kutofautiana taratibu na kuweka hasira zao ndani na siku moja mmoja anaweza kufanya jambo dogo lakini kutokana na yale yaliyojengeka moyoni kwa mda wakafikia mahali mbapo mtu akiangalia kosa na matokeo anashangaa kumbe it was accumulation ya matatizo.



Ego unatumia nguvu kubwa sana kutetea uhalifu, mie sikubaliani na wewe hata kidogo, huo upatikanaji wa Haki unaousema wa kumridhisha kila mtu umeuona wapi dunia hii labda ahela peke yake!wanadamu hawaridhiki wewe usipende kuongea tu bila kufikiri, unaweza kupewa kila kitu ukaanza kulia kuwa umepewa vingi wakupunguzie, wakipunguza unaanza kulia tena waongeze!!! huyu ndio mwanadamu wewe!!!

Hiyo mifano unayoitoa ni ya huko huko sio Tz wewe sie tunajielewa and we know how to handle our difference, I tell you Uganda have been under military rule several times so far Nigeria and Somalia your case study, mazingira yao ya freedom fighting ni tofauti na yetu, hili hivi hulioni usitake turudishane darasani hapa!Kikubwa uelewe kuwa Tanzania iko stable na iko timamu kuhandle mambo yake! Watanzania tuko makini na tunamaamuzi makini katika mambo yanayohusu mustakabali wetu!Usikubali kudanganywa!!!!

Pia kumbuka hili sehemu unayoona wewe ni haki yako mwenzio anaona ni kero kwake, wewe unapoona kuna kero kwako yeye kwake anaona ni haki huyo ndiye mwanadamu sio mkamilifu ndio maana Katiba inayopendekezwa imeweka wazi HAKI ZA BINADAMU SURA YA 5 Kuanzia Ibara ya 32 hadi 59 hapa ukisoma kwa makini utayaona makundi kibao yameainishwa hapo na haki zao ndio maana kila mara nakushauri acha kukimbiza upepo piga kura yako ya ndiyo ili haki hizo zilindwe kwa mujibu wa sheria.
 
katiba ya 1977 haina hilo la mamlaka ya wananchi? je hawakupewa mamlaka mwanzo wa kitabu (katiba) na kunyang'anywa katikati na mwisho wa kitabu?
 
lipo tatizo kubwa katika kuelewa maana ya "mamlaka ya wananchi".

kuwa na kifungu kinachotaja mamlaka ya wananchi sio mbaya lakini malaka ya wananchi ni katiba ilivyo kuwafanya wanannchi ndio wenye nchi, ndio wamiliki wa nchi na wao wako juu ya kila kitu. na hapa ni utaalamu katika uandishi unaofanya vyombo vinavyoundwa kuwatumikia wananchi na wananchi kuwa na uwezo wa ku "control" mwenendo wa vyombo hivyo.

uandishi wa katiba ambao unafanya makundi kupora vyombo vya wananchi ndio makosa ambayo yanapora madaraka ya wananchi.

mfano bunge kwa maana ya bunge kimantiki ni kitu gani?

bunge ni chombo cha wananchi ambacho kinatakiwa kufanya kzi ya kusimamia utendaji wa serikali kwa maana kuangalia kama serikali inatimiza majukumu yake ya kutumia rasilimali za wananchi kuwaletea maendeleo wananchi. lakini uandishi wa chombo hiki kifanyeje kazi katika katiba na muundo wake kwenye katiba zetu tulizowahi kuwa nazo na tunayoipendekeza inakifanya chombo hiki kuporwa na makundi ya watu waliounda vyama vya siasa na kuacha majukumu yake ya msingi na kujikita kufanya kazi ya siasa.

badala ya bunge kukaa kusimamia serikali ni mabishano ya itikadi tu na mtu anasapoti hata maovu yaliyotendwa na mwanaitikadi mwenzake au anapinga mazuri yanayopendekezwa na mwenye itikadi tofauti naye.

sasa unapozungumza mamlaka ya wananchi unazungumzia nini kuwepo kifungu kwenye katiba kinachosema serikali itapata madaraka yake kutoka kwa wananchi au unazungumzia bunge ambacho ni chombo ambacho wananchi wanakabidhi madaraka yao ya kusimamia serikali ambacho baada ya kukabidhiwa madaraka chombo hiki kupitia uandishi wa katiba kinatolewa katika kazi yake ya msingi ya kufanya kazi ya wanchi na kufanya kazi ya makundi madogo madogo?

hebu angalia mamlaka ya raisi

unapotunga katiba inayompa raisi mamlaka makubwa ambayo yanamuweka raisi juu ya wananchi kwa raisi kuwa kama mfalme katika nchi yenye demokrasia basi hapo unakuwa umewapora wanananchi madaraka.

wananchi kuwa na madaraka ni pale vyombo vyao vinapowatumikia.

wanaunda serikali alafu serikali inafanya inavyotaka na wao kubaki kulalamika tu alafu useme wananchi wana madaraka?
wanaunda bunge alafu bunge linafanya linavyotaka wanabaki kulalamika tu na hwana la kufanya alafu useme wananachi wana madaraka?
wanaunda mahakama alafu mahakama inashindwa kuwapa haki na hawana la kufanya wanabaki kulalamika alafu useme wananchi wana madaraka?

madaraka ya wananchi yanaanzia kwenye kuibalansi mihimili kwa maana jambo hilo linalenga katika kuvifanya vyombo hivi viwatumikie wananchi.

alafu linakwenda katika miundo na jinsi ya utekelezaji wa shughuli wa vyombo vilivyoundwa kama unavifanya vyombo hivyo kufanya kazi ya wananchi sasa hapo unazungumza madaraka ya wananchi kubaki kwa wananchi.

na mwisho ni wananchi kuwa na udhibiti wa vyombo ili viwatumikie.

hivyo wananchi kupewa mamlaka sio kutajwa vufungu ambavyo havina nguvu yoyote ya kuwawezesha kumiliki mali zao, kukontrol mali zao na kuwadhibiti watumishi wao na ukaita mamlaka ya wananchi.

katiba ya 1977 haina hilo la mamlaka ya wananchi? je hawakupewa mamlaka mwanzo wa kitabu (katiba) na kunyang'anywa katikati na mwisho wa kitabu?
 
lipo tatizo kubwa katika kuelewa maana ya "mamlaka ya wananchi".

kuwa na kifungu kinachotaja mamlaka ya wananchi sio mbaya lakini malaka ya wananchi ni katiba ilivyo kuwafanya wanannchi ndio wenye nchi, ndio wamiliki wa nchi na wao wako juu ya kila kitu. na hapa ni utaalamu katika uandishi unaofanya vyombo vinavyoundwa kuwatumikia wananchi na wananchi kuwa na uwezo wa ku "control" mwenendo wa vyombo hivyo.

uandishi wa katiba ambao unafanya makundi kupora vyombo vya wananchi ndio makosa ambayo yanapora madaraka ya wananchi.

mfano bunge kwa maana ya bunge kimantiki ni kitu gani?

bunge ni chombo cha wananchi ambacho kinatakiwa kufanya kzi ya kusimamia utendaji wa serikali kwa maana kuangalia kama serikali inatimiza majukumu yake ya kutumia rasilimali za wananchi kuwaletea maendeleo wananchi. lakini uandishi wa chombo hiki kifanyeje kazi katika katiba na muundo wake kwenye katiba zetu tulizowahi kuwa nazo na tunayoipendekeza inakifanya chombo hiki kuporwa na makundi ya watu waliounda vyama vya siasa na kuacha majukumu yake ya msingi na kujikita kufanya kazi ya siasa.

badala ya bunge kukaa kusimamia serikali ni mabishano ya itikadi tu na mtu anasapoti hata maovu yaliyotendwa na mwanaitikadi mwenzake au anapinga mazuri yanayopendekezwa na mwenye itikadi tofauti naye.

sasa unapozungumza mamlaka ya wananchi unazungumzia nini kuwepo kifungu kwenye katiba kinachosema serikali itapata madaraka yake kutoka kwa wananchi au unazungumzia bunge ambacho ni chombo ambacho wananchi wanakabidhi madaraka yao ya kusimamia serikali ambacho baada ya kukabidhiwa madaraka chombo hiki kupitia uandishi wa katiba kinatolewa katika kazi yake ya msingi ya kufanya kazi ya wanchi na kufanya kazi ya makundi madogo madogo?

hebu angalia mamlaka ya raisi

unapotunga katiba inayompa raisi mamlaka makubwa ambayo yanamuweka raisi juu ya wananchi kwa raisi kuwa kama mfalme katika nchi yenye demokrasia basi hapo unakuwa umewapora wanananchi madaraka.

wananchi kuwa na madaraka ni pale vyombo vyao vinapowatumikia.

wanaunda serikali alafu serikali inafanya inavyotaka na wao kubaki kulalamika tu alafu useme wananchi wana madaraka?
wanaunda bunge alafu bunge linafanya linavyotaka wanabaki kulalamika tu na hwana la kufanya alafu useme wananachi wana madaraka?
wanaunda mahakama alafu mahakama inashindwa kuwapa haki na hawana la kufanya wanabaki kulalamika alafu useme wananchi wana madaraka?

madaraka ya wananchi yanaanzia kwenye kuibalansi mihimili kwa maana jambo hilo linalenga katika kuvifanya vyombo hivi viwatumikie wananchi.

alafu linakwenda katika miundo na jinsi ya utekelezaji wa shughuli wa vyombo vilivyoundwa kama unavifanya vyombo hivyo kufanya kazi ya wananchi sasa hapo unazungumza madaraka ya wananchi kubaki kwa wananchi.

na mwisho ni wananchi kuwa na udhibiti wa vyombo ili viwatumikie.

hivyo wananchi kupewa mamlaka sio kutajwa vufungu ambavyo havina nguvu yoyote ya kuwawezesha kumiliki mali zao, kukontrol mali zao na kuwadhibiti watumishi wao na ukaita mamlaka ya wananchi.
Naona ndugu unachanganya mambo tu hapo juu, muda mwingine unajiuliza maswali yenye majibu ya waziwazi, muda mwingine husomek, tatizo nimegundua kuwa wewe unaisoma hiyo katiba kama kasuku, huingii deep na ukatuliza akili, acha kuwaza yasiyo ndo utaelewa hiyo katiba maana mambo uloandika hapo yameelezwa vema katikamhiyo katiba pendekezwa.
 
ndio maana nimesema ni vigumu wakati mwingine kuhangaika kukunja samaki waliokauka.

binafsi napata wazo la kuelimisha samaki wabichi ili huko mbeleni wabadili mwenendo wa maisha yao nadhani itakuwa na tija.

Naona ndugu unachanganya mambo tu hapo juu, muda mwingine unajiuliza maswali yenye majibu ya waziwazi, muda mwingine husomek, tatizo nimegundua kuwa wewe unaisoma hiyo katiba kama kasuku, huingii deep na ukatuliza akili, acha kuwaza yasiyo ndo utaelewa hiyo katiba maana mambo uloandika hapo yameelezwa vema katikamhiyo katiba pendekezwa.
 
ndio maana nimesema ni vigumu wakati mwingine kuhangaika kukunja samaki waliokauka.

binafsi napata wazo la kuelimisha samaki wabichi ili huko mbeleni wabadili mwenendo wa maisha yao nadhani itakuwa na tija.
wewe ndo umekauka na unakuwa mbishi kama mbogo, hata ukiwaelimisha mwisho wa siku ni NDIYOOOO! usiendelee kupoteza muda wako kijana.
 
Back
Top Bottom