kundi kutajwa katika katiba haitoi haki kama katiba haina mfumo wa kutoa haki

kundi kutajwa katika katiba haitoi haki kama katiba haina mfumo wa kutoa haki

Hivi mwakaboko nani aliyekuloga?ukianza tu kuchangia mada unaharibu,utoke humu jf kama hupawezi
 
sijui nikuiteje maana nikikueleza ukweli utasema nimekutukana.

bado narudia kilichotajwa katika kifungu kimoja cha katiba kama muundo wa katiba yenyewe hauwezeshi kilichotajwa katika kifungu hicho kimoja kupatikana on ground ni kama kifungu hicho hakipo.

kama katiba imetaja haki fulani lakini haiweki mifumo ya kuwezesha haki hizo zipatikane, katiba hiyo haiweki mifumo ya kusimamia ili wenye dhamana kutimiza wajibu wao, kama katiba haiweki mifumo ya kuhakikisha kuwa pale wenye dhamana wanapokiuka ni lazima haki itendeke, katiba hiyo yaweza kufanana na kitabu cha hadithi ambacho msomaji ana hiari ya kuyakubali au kuyakataa yale yaliyoandikwa.

tumefika hapa tulipo kutokana na wale wanaojidhani ni wataalamu wa uandishi wa katiba kumbe sometimes they can be ignorant katika mada hiyo.

nani ni mtaalamu inahukumiwa na kile kilichoandikwa kukidhi mahitaji ya kilichokusudiwa.

kama huwezi kutambua ukweli kuwa jambo lolote linalotajwa katika katiba, ndani ya katiba hiyo hiyo kuna mamlaka inatakiwa kutekeleza jambo hilo, kuna mamlaka inatakiwa kusimamia utekelezaji wake, kuna mamlaka ambayo ukiona hujatendewa haki unatakiwa unaweza kwenda kuidai huko.

kimsingi nilichokisema ni kuwa katiba ni sawa na treni. kwa kawaida treni ina kichwa ambacho huvuta mabewa. haki za makundi ni sawa na mabehewa ambapo kundi linakimbilia kuangalia sisi behewa letu lipo? lakini hapa tukumbuke kuwa mabehewa yetu yanaweza kuwepo lakini kichwa cha kubeba mabehewa haya je kipo?

hapa tunachokifanya watanzania ni kuunda treni yetu, hivyo ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa tunatengeneza kichwa cha kuvuta mabehewa yote na tukisha maliza kutengeneza kichwa ndio sasa makundi yaanagalie mabehewa yao.

kichwa ni mihimili mitatu kuhakikisha inakuwepo.

kuwepo kwa mihimili mitatu sio kuitaja tu katika vifungu bali ni kuhakikisha mihimili hii kila mmoja haumezwi na mhimili mwingine na hakuna mhimili unaoweza kuwa na nguvu zaidi ya mingine.

lengo hapa ni kutokana na rasilimali za jamii kutowezekana kwa jamii kuzisimamia yenyewe moja kwa moja hivyo jamii inalazimika kutengengeneza vyombo ambavyo vitafanya kazi ya jamii kwa kusimamiana vyombo vyenyewe.

ukiwa na chombo kimoja au chombo kimoja chenye nguvu au vikaungana na kuwa chombo kimoja matokeo yake ni uwezekano wa chombo hiki kimoja au chombo chenye nguvu kupora madaraka ya wananchi.

mtaalamu wa uandishi wa katiba anayeweza kujigamba ni si yule wa kuangalia kifungu kimoja kimoja kinasemaje bali ni yule anayeweza kutengeneza "checks and balansi " katika mtiririko mzima wa katiba na kujumuisha mambo muhimu yote.

katiba sio tu kile kilichotajwa bali katiba nzima inasimamiaje yale yalitotajwa.

naendelea kuamini unaandika bila kufanya rejea na ulichoambiwa kuwa na utaratibu wa kusoma sio kubwabwaja tu...umeandika weee lakin hamna kitu vyote ulivyoviandika ukirejea kweny kifungu nilichokwambia utapata jibu....umezungumzia haki na utekelezaji wake umejibiwa accordingly......sasa unavyotaka mtu afanye rejea kwenye katiba nzima utakuwa huelewi zaidi ya kupotosha....
 
naendelea kuamini unaandika bila kufanya rejea na ulichoambiwa kuwa na utaratibu wa kusoma sio kubwabwaja tu...umeandika weee lakin hamna kitu vyote ulivyoviandika ukirejea kweny kifungu nilichokwambia utapata jibu....umezungumzia haki na utekelezaji wake umejibiwa accordingly......sasa unavyotaka mtu afanye rejea kwenye katiba nzima utakuwa huelewi zaidi ya kupotosha....
huyo anabisha tu lkn ukweli anaujua
 
mimi sina terms of reference wala master behind my contribution.

binafsi naamini ni vigumu jamii kubadili but when they are informed slowly jamii itabadilika na siku moja juhudi hizi zitazaa matunda.

yawezekana ikawa vigumu kwa kizazi hiki kwa maana wengi ni samaki waliokauka lakini naamaini if not now in future vizazi vyetu vitatoka katika utumwa huu tuliomo wa kutumikishwa na ujinga ambao ndio mwanzo wa everything bad kwenye jamii yetu.

UOTE=claudiaeliakimu;12365862]Ego mie nakusoma sana afu we mbishi kinoma sikuwa hewani kitambo lakini nimekusoma hapa naona unapoteza muda sababu kibao za kuunga mkono Katiba Inayopendekezwa wamezitoa afu wewe huzielewi unakomaa ili iweje nakumbuka ulianza komaa kwenye utoaji haki ukaambiwa kasome Sura ya Tano kuanzia Ibara ya 32 mpaka 59 hukusoma na bado ulikua unauliza tu.? Kama sio kupotezea muda ni nini acha hizo bhana!!![/QUOTE]
 
wakati mwingine yawezekana uwezo wako wa kuelewa ni mdogo na au ubongo wako unafanya kazi kama komputa zile za kizamani ambazo ukifungua faili unachukua nusu saa faili halijafunguka.

hivyo take time kusoma ninachokisema najua baadae utaelewa au kama text ziko beyond your inteligence capacity jaribu kujadiliana na ambaye ubongo wake uko update kidogo.

ninachokisema kuhusu imani ni hatuhitaji kutoa uhuru wa imani kwa sasa ni lazima tutaje ni imani za aina gani zinaruhusiwa.

only outdated mind anaweza kusema mtu akija kwako anakuambia nikuombee utapata mali, mtoto wako ugonjwa unaomsumbua amerogwa na bibi yake, tatizo ulilo nalo ukipata kitu fulani haijalishi ni kuua mtu au kufanya nini na akasema kila mtu achague kinachomfaa.

watu hawa wanaoshauriwa au kupotoshwa wanakuwa katika state gani?

kwa nini bangi na madawa ya kulevya tusiseme tuache tu na mtu akiona kinamfaa afuate akiona bangi haimfai aache kuvuta.

najua kwa uwezo mdogo wako wa akili utasema bangi na imani wapi na wapi lakini wanaofikiri mbali watakuuliza anayevuta bangi akafarakana na wazazi watu wanaomzunguka na anatabiriwa uchawi akafarakana na ndugu zake wanatofauti gani? yupi mwenye nafuu muuza bangi au muuza kikombe cha loliondo?

nimekuambia mimi si mtumwa wa terms of reference au master yeyote hivyo ninaandika kwa staili yangu ambayo wenye kufikiri wanaona ninachokisema lakini wanaokalili wanataka reference ya vifungu.

naendelea kuamini unaandika bila kufanya rejea na ulichoambiwa kuwa na utaratibu wa kusoma sio kubwabwaja tu...umeandika weee lakin hamna kitu vyote ulivyoviandika ukirejea kweny kifungu nilichokwambia utapata jibu....umezungumzia haki na utekelezaji wake umejibiwa accordingly......sasa unavyotaka mtu afanye rejea kwenye katiba nzima utakuwa huelewi zaidi ya kupotosha....
 
ningekujibu kwa lugha uliyotumia lakini nitakuwa najishusha, kwangu mimi naamini kundi kutajwa katika katiba ni useless kama hakuna mfumo wa kulinda haki hiyo iliyotajwa.

mimi sisomi katiba kwa kuangalia ibara fulani inasema nini bali naenda mbali zaidi kuangalia baada ya katiba kusema nini kinafuata na ni nani atatekeleza na je yule anayetakiwa kutekeleza nani atahoji au mhusika ataenda wapi na kuna mfumo unaofanya haki itendeke.

katiba haisomwi kwa kifungu kimoja kwani huwezi kupata kitu chochote katika maisha kwa kutumia kifungu kimoja tu cha katiba na hilo ndilo tatizo la wengi.


Mjibu tu kwani shida iko wapi?acha uoga wewe!
 
mimi sina terms of reference wala master behind my contribution.

binafsi naamini ni vigumu jamii kubadili but when they are informed slowly jamii itabadilika na siku moja juhudi hizi zitazaa matunda.

yawezekana ikawa vigumu kwa kizazi hiki kwa maana wengi ni samaki waliokauka lakini naamaini if not now in future vizazi vyetu vitatoka katika utumwa huu tuliomo wa kutumikishwa na ujinga ambao ndio mwanzo wa everything bad kwenye jamii yetu.

UOTE=claudiaeliakimu;12365862]Ego mie nakusoma sana afu we mbishi kinoma sikuwa hewani kitambo lakini nimekusoma hapa naona unapoteza muda sababu kibao za kuunga mkono Katiba Inayopendekezwa wamezitoa afu wewe huzielewi unakomaa ili iweje nakumbuka ulianza komaa kwenye utoaji haki ukaambiwa kasome Sura ya Tano kuanzia Ibara ya 32 mpaka 59 hukusoma na bado ulikua unauliza tu.? Kama sio kupotezea muda ni nini acha hizo bhana!!!
[/QUOTE]

Huwezi kufananisha watu na samaki waliokauka huko ni kukosa heshima,jenga hoja yako ueleweke sio ukalia mi maneno kibao afu hakuna point yoyote, tuliza akili.
 
makundi mbalimbali yamekuwa yakipigania kutajwa katika katiba na hata wengine kudiriki kutaka mambo ambayo kimsingi si ya kuingia katika katiba.

hapa tumejisahau kuwa kinachotusumbua si kutotajwa katika katiba ndio maana hatukuridhika huko nyuma bali kutokuwepo kwa misingi ya kutoa haki pengine katika katiba ndio tatizo kubwa.

jambo la kwanza kwetu sote iwe ni kupigania misingi ya kutoa haki kwa wote ijengwe katika katiba na hapo kila mmoja katika kundi lake dogo haki yake ataipata.
Wewe unaonekan ni mvivu wa kusoma katiba maana mambo uloyazungumzia hapo juu kuhusu misingi ya kutoa haki imewekwa vema ktk hiyo katiba epuka kupotosha umma humu ndani.
 
nakushangaa sana pale unaponukuu misemo au methali na kuvichukua kama vilivyo bila kutafuta maana ya msemo husika.

na hilo ni tatizo letu kubwa hata katika kutunga katiba na kusoma katiba kwamba hatutafsiri kile kilichoandikwa kina maana gani kwenye jamii yetu na je kinachofanyika ni kitu gani na kama tunataka mabadiliko katika utekelezaji tufanyeje.

mfano katiba inayopendekezwa inatamka wazi kuwa malengo makuu ya katiba ni pamoja na usawa, haki, udugu, amani nk.


ukizungumza na mtanzania yeyote yule unayemkuta mfano mitaani akiwa na shida watanzania hawa wanalaumu sana.

watanzania walio wengi wanalaumu kuwa kwa sasa kuna tatizo kubwa la ajira hasa katika nyanja ya ajira kutolewa kwa kujuana (hakuna mtanzania mlalahoi anaweza kupata nafasi nzuri ya utendaji wa serikalini kama hamjui mtu yeyote wa kumsimamia) au kutoa rushwa iwe ya starehe kwa watu kuwapa kazi mahawara wao au ya mali.

sasa usawa unaozungumzwa katika katiba uko wapi?

bora tatizo liwe linaishia hapo lakini tatizo hili limekuwa likileta mlolongo wa matatizo kibao. kwanza katika utoaji wa ajira au security ya mtu katika kazi inapohama kutoka katika utendaji wa kazi wa mfanyakazi na kuwa katika unamjua nani au uko tayari kutoa nini kunasababisha kujazana maofisini watu kwanza wasio na ujuzi, watu wasiojali kazi bali kujali mahusiano na biashara binafsi maofisini, molari ya kufanya kazi inaondoka na kujenga morali ya kuwanyenyekea mabosi.

hili linatupeleka kwenye utendaji mbovu wa serikali kwa kuwa na watumishi wanaojaza kalenda ya mahudhurio lakini utendaji hakuna.

hili litasababisha corruption kuwa juu kwa maana hakuna supervision, hili litasababisha kazi zinazoendeshwa na serikali kuwa duni kwa maana watumishi hawajali, pengine hawana utaalamu, viongozi makazini wapo lakini hawana madaraka kwa maana huwezi kumkemea mtoto wa kigogo fulani, huwezi kumkemea hawara wa kigogo fulani na ukifanya hivyo hata kama kafanya kosa unaonywa.

hili linasababisha gharama za uendeshaji serikali kuwa kubwa kwa maana mtu asiyejua kazi na asiyesimamiwa anatazama katika kazi yake anaweza kufanya ujanja gani kutengeneza fedha haramu hivyo wananunua vitu feki ili bajeti walizonazo wapate chenji za kuweka mifukoni mwao, wanafoji risiti ili wapate hati safi ingawa utendaji ni mbovu, wanatumia fedha za maendeleo kwa starehe na mambo mengine.

hivyo matatizo yanaanza yakiwa madogo lakini yanatafuna nchi.

ni wakati wa kujiuliza sasa hivi matatizo haya tuliyonayo yanaanzia wapi?

cha kusikitisha ni pale tunaposikia baadhi ya watanzania wakitoa kauli kuwa raisi anachapa kazi lakini watendaji wake ndio wanamuangusha! hakuna mtu anayefahamu menejimenti anayeweza kumsifia meneja na kuwapona watendaji waliochini ya meneja.

raisi kazi yake ni kuwaelekeza watendaji wa chini na kuwasimamia sasa kama chini ni kubovu basi ubovu huo ni wa raisi kwa maana kazi yake ya kwanza ni kutengeneza timu iliyo bora na kuisimamia.

wengine wakati mawaziri wakuu wanapotaka kuwajibishwa unashangaa taifa linaendesha mijadala na kudai waziri mkuu hakuhusishwa hivyo yeye hahusiki! unashangaa hivi tuko vipofu kiasi hicho? kwa maana jambo lolote lililo katika dhamana yako likifanya vibaya kama hujachukua hatua na likaenda ngazi ya juu basi ngazi hiyo inashughulika na wewe ukiwa namba moja ama kwa uzembe au kwa utendaji mbovu.

lakini mifumo tuliyoijenga ndio mibovu inayosababisha haya mambo ya kipuudhi yanayotupeleka katika umasikini ambao unatengenezwa na minyororo ya matatizo yanayotokana na uzembe fulani ulio sehemu.

sasa katika katiba ni wakati wa kuangalia ni wapi ambapo ndio kiini cha matatizo haya yote.

bila kumumunya maneno matatizo yaliyo katika mihimili mitatu ya juu ndio chimbuko la haya yote.

hii inatokana na mfanyakazi yeyote kabla ya kufanya jambo lolote anafanya risk analysis isiyo rasmi.

kila mwanadamu anatawaliwa na ubifasi na nafsi ya kwanza ndio inaongoza hivyo kwa jambo lolote analolifanya hujitazama yeye kwanza. lakini usimamiaji umewekwa ili kumfanya mwanadamu asitumikie nafsi yake bali atimize wajibu wake.

mwenye kupewa dhamana ya kuajiri anajiuliza hivi nikitumia nafasi hizi kujinufaisha mfumo wa usimamiaji kuanzia kwenye mifumo iliyo kwa mwajiri wake mpaka mifumo iliyo nje ya mwajiri wake mfano kama ni mtumishi wa serikali atajiuliza mwajiri wangu serikali atanifanya nini? lakini atajiuliza mahakama na bunge vinaweza kumfanya nini ? akiona anachoweza kufanywa ni kidogo au uwezekano wa kushughulikiwa kama atajinufaisha ni mdogo basi mtu huyo anaamua kutumia nafasi aliyopata kujinufaisha mwenyewe.

sio serikalini tu bali hata kwa kwa sekita binafsi kama mwajiri akimuachia mtumishi kufanya anavyotaka bila kumsimamia basi mtumishi anatumia ajira kujinufaisha.

kama mtu amepewa mradi wa maendeleo au dhamana yoyote kutekeleza kama mfumo wa usimamiaji ni mbovu basi hutumia nafasi hiyo kujinufaisha.

wapo ambao kwa jinsi walivyokuzwa wao huanza kwa kutaka kufanya mambo kwa ukweli ambao jamii huwaita wajinga kutokana na kupewa nyadhifa wakabaki masikini bila kujua kuwa umasikini wa hawa watu umetokana na uaminifu wao lakini nao hukata tamaa baada ya kufanya kazi kwa uaminifu kwa mda na kugundua kuwa uaminifu wao hauwalipi na wasiokuwa waaminifu wao wanapata mali haraka sana.

hivyo mifumo yetu inawageuza hata watu waaminifu kuwa waporaji.

kurekebisha mifumo ya usimamiaji ili iwalazimishe watumishi kutumikia jamii na sio kujitumikia wao wenyewe kupitia ofisi za umma ndio jambo la kwanza ambalo tuliliitaji katika katiba.

kwa mambo yalivyo sasa hakuna mtu anaweza kututoa katika umasikini kwa maana mifumo yetu yote imeshakuwa corrupt kiasi cha kuifananisha na tenga kutumika kuteka maji.

kila ofisi mtu yeyote utakayempa dhamana anaajiri ndugu zake, yeyote utakayempa fedha anatafuta kuweka chenji mfukoni.

matatizo haya kwetu sisi yanatokana na kukosa mihimili mitatu inayosimamiana na hivyo mfumo mzima wa usimamiaji haufanyi kazi.

watanzania walio wengi wanashindwa kuhusisha matatizo ya jamii yetu na makaratasi kama katiba na maisha yao lakini kutohusisha huku kumeenda mbali sana.

nyerere aliwahi kusema ni bora mjinga kuliko mpumbavu.

mjinga ni mtu ambaye hajui kitu lakini akielezwa anaelewa na anafuata.

lakini mpumbavu ni mtu ambaye anajua kivingine tofauti na maana halisi na huyu kumtoa kwenye maana aliyonayo kuwa hiyo sio sahihi na kumrudisha kwenye maana halisi ni ngumu na huyu ndiye samaki ambaye amekauka bila kukunjwa sasa kumkunja akiwa amekwisha kauka ni vigumu.

lakini kwa vizazi vijavyo pengine wakifundishwa tangu wakiwa wadogo njia sahihi pengine jamii yetu inaweza kubadilika.


[/QUOTE]Huwezi kufananisha watu na samaki waliokauka huko ni kukosa heshima,jenga hoja yako ueleweke sio ukalia mi maneno kibao afu hakuna point yoyote, tuliza akili.[/QUOTE]
 
nakushangaa sana pale unaponukuu misemo au methali na kuvichukua kama vilivyo bila kutafuta maana ya msemo husika.

na hilo ni tatizo letu kubwa hata katika kutunga katiba na kusoma katiba kwamba hatutafsiri kile kilichoandikwa kina maana gani kwenye jamii yetu na je kinachofanyika ni kitu gani na kama tunataka mabadiliko katika utekelezaji tufanyeje.

mfano katiba inayopendekezwa inatamka wazi kuwa malengo makuu ya katiba ni pamoja na usawa, haki, udugu, amani nk.


ukizungumza na mtanzania yeyote yule unayemkuta mfano mitaani akiwa na shida watanzania hawa wanalaumu sana.

watanzania walio wengi wanalaumu kuwa kwa sasa kuna tatizo kubwa la ajira hasa katika nyanja ya ajira kutolewa kwa kujuana (hakuna mtanzania mlalahoi anaweza kupata nafasi nzuri ya utendaji wa serikalini kama hamjui mtu yeyote wa kumsimamia) au kutoa rushwa iwe ya starehe kwa watu kuwapa kazi mahawara wao au ya mali.

sasa usawa unaozungumzwa katika katiba uko wapi?

bora tatizo liwe linaishia hapo lakini tatizo hili limekuwa likileta mlolongo wa matatizo kibao. kwanza katika utoaji wa ajira au security ya mtu katika kazi inapohama kutoka katika utendaji wa kazi wa mfanyakazi na kuwa katika unamjua nani au uko tayari kutoa nini kunasababisha kujazana maofisini watu kwanza wasio na ujuzi, watu wasiojali kazi bali kujali mahusiano na biashara binafsi maofisini, molari ya kufanya kazi inaondoka na kujenga morali ya kuwanyenyekea mabosi.

hili linatupeleka kwenye utendaji mbovu wa serikali kwa kuwa na watumishi wanaojaza kalenda ya mahudhurio lakini utendaji hakuna.

hili litasababisha corruption kuwa juu kwa maana hakuna supervision, hili litasababisha kazi zinazoendeshwa na serikali kuwa duni kwa maana watumishi hawajali, pengine hawana utaalamu, viongozi makazini wapo lakini hawana madaraka kwa maana huwezi kumkemea mtoto wa kigogo fulani, huwezi kumkemea hawara wa kigogo fulani na ukifanya hivyo hata kama kafanya kosa unaonywa.

hili linasababisha gharama za uendeshaji serikali kuwa kubwa kwa maana mtu asiyejua kazi na asiyesimamiwa anatazama katika kazi yake anaweza kufanya ujanja gani kutengeneza fedha haramu hivyo wananunua vitu feki ili bajeti walizonazo wapate chenji za kuweka mifukoni mwao, wanafoji risiti ili wapate hati safi ingawa utendaji ni mbovu, wanatumia fedha za maendeleo kwa starehe na mambo mengine.

hivyo matatizo yanaanza yakiwa madogo lakini yanatafuna nchi.

ni wakati wa kujiuliza sasa hivi matatizo haya tuliyonayo yanaanzia wapi?

cha kusikitisha ni pale tunaposikia baadhi ya watanzania wakitoa kauli kuwa raisi anachapa kazi lakini watendaji wake ndio wanamuangusha! hakuna mtu anayefahamu menejimenti anayeweza kumsifia meneja na kuwapona watendaji waliochini ya meneja.

raisi kazi yake ni kuwaelekeza watendaji wa chini na kuwasimamia sasa kama chini ni kubovu basi ubovu huo ni wa raisi kwa maana kazi yake ya kwanza ni kutengeneza timu iliyo bora na kuisimamia.

wengine wakati mawaziri wakuu wanapotaka kuwajibishwa unashangaa taifa linaendesha mijadala na kudai waziri mkuu hakuhusishwa hivyo yeye hahusiki! unashangaa hivi tuko vipofu kiasi hicho? kwa maana jambo lolote lililo katika dhamana yako likifanya vibaya kama hujachukua hatua na likaenda ngazi ya juu basi ngazi hiyo inashughulika na wewe ukiwa namba moja ama kwa uzembe au kwa utendaji mbovu.

lakini mifumo tuliyoijenga ndio mibovu inayosababisha haya mambo ya kipuudhi yanayotupeleka katika umasikini ambao unatengenezwa na minyororo ya matatizo yanayotokana na uzembe fulani ulio sehemu.

sasa katika katiba ni wakati wa kuangalia ni wapi ambapo ndio kiini cha matatizo haya yote.

bila kumumunya maneno matatizo yaliyo katika mihimili mitatu ya juu ndio chimbuko la haya yote.

hii inatokana na mfanyakazi yeyote kabla ya kufanya jambo lolote anafanya risk analysis isiyo rasmi.

kila mwanadamu anatawaliwa na ubifasi na nafsi ya kwanza ndio inaongoza hivyo kwa jambo lolote analolifanya hujitazama yeye kwanza. lakini usimamiaji umewekwa ili kumfanya mwanadamu asitumikie nafsi yake bali atimize wajibu wake.

mwenye kupewa dhamana ya kuajiri anajiuliza hivi nikitumia nafasi hizi kujinufaisha mfumo wa usimamiaji kuanzia kwenye mifumo iliyo kwa mwajiri wake mpaka mifumo iliyo nje ya mwajiri wake mfano kama ni mtumishi wa serikali atajiuliza mwajiri wangu serikali atanifanya nini? lakini atajiuliza mahakama na bunge vinaweza kumfanya nini ? akiona anachoweza kufanywa ni kidogo au uwezekano wa kushughulikiwa kama atajinufaisha ni mdogo basi mtu huyo anaamua kutumia nafasi aliyopata kujinufaisha mwenyewe.

sio serikalini tu bali hata kwa kwa sekita binafsi kama mwajiri akimuachia mtumishi kufanya anavyotaka bila kumsimamia basi mtumishi anatumia ajira kujinufaisha.

kama mtu amepewa mradi wa maendeleo au dhamana yoyote kutekeleza kama mfumo wa usimamiaji ni mbovu basi hutumia nafasi hiyo kujinufaisha.

wapo ambao kwa jinsi walivyokuzwa wao huanza kwa kutaka kufanya mambo kwa ukweli ambao jamii huwaita wajinga kutokana na kupewa nyadhifa wakabaki masikini bila kujua kuwa umasikini wa hawa watu umetokana na uaminifu wao lakini nao hukata tamaa baada ya kufanya kazi kwa uaminifu kwa mda na kugundua kuwa uaminifu wao hauwalipi na wasiokuwa waaminifu wao wanapata mali haraka sana.

hivyo mifumo yetu inawageuza hata watu waaminifu kuwa waporaji.

kurekebisha mifumo ya usimamiaji ili iwalazimishe watumishi kutumikia jamii na sio kujitumikia wao wenyewe kupitia ofisi za umma ndio jambo la kwanza ambalo tuliliitaji katika katiba.

kwa mambo yalivyo sasa hakuna mtu anaweza kututoa katika umasikini kwa maana mifumo yetu yote imeshakuwa corrupt kiasi cha kuifananisha na tenga kutumika kuteka maji.

kila ofisi mtu yeyote utakayempa dhamana anaajiri ndugu zake, yeyote utakayempa fedha anatafuta kuweka chenji mfukoni.

matatizo haya kwetu sisi yanatokana na kukosa mihimili mitatu inayosimamiana na hivyo mfumo mzima wa usimamiaji haufanyi kazi.

watanzania walio wengi wanashindwa kuhusisha matatizo ya jamii yetu na makaratasi kama katiba na maisha yao lakini kutohusisha huku kumeenda mbali sana.

nyerere aliwahi kusema ni bora mjinga kuliko mpumbavu.

mjinga ni mtu ambaye hajui kitu lakini akielezwa anaelewa na anafuata.

lakini mpumbavu ni mtu ambaye anajua kivingine tofauti na maana halisi na huyu kumtoa kwenye maana aliyonayo kuwa hiyo sio sahihi na kumrudisha kwenye maana halisi ni ngumu na huyu ndiye samaki ambaye amekauka bila kukunjwa sasa kumkunja akiwa amekwisha kauka ni vigumu.

lakini kwa vizazi vijavyo pengine wakifundishwa tangu wakiwa wadogo njia sahihi pengine jamii yetu inaweza kubadilika.


Huwezi kufananisha watu na samaki waliokauka huko ni kukosa heshima,jenga hoja yako ueleweke sio ukalia mi maneno kibao afu hakuna point yoyote, tuliza akili.
[/QUOTE]

Hayo uloandika yoote takataka tupu kama ulivyo we mwenyewe.
 
kumbuka mchango wako ndio unatumika kukubainisha wewe uko kundi gani na makundi ya wanadamu katika uelewa yako matatu tu.

1. kundi la wajinga - hawa hawajui kitu wanasubiri wakielezwa wanafuata.
2. kundi la wapumbavu - hawa wamepotoka kabisa hawaambiliki, misimamo yao iko kwenye ujinga tu na hawawezi kutoka huko.
3. kundi la wanaojua - hawa wanajua.

taifa linapokuwa na watu wengi walio katika kundi la kwanza na la pili matokeo yake ni umasikini. yaani nchi ikiwa na wajinga wengi basi ujinga ndio unatawala kwa maana mawazo ya wengi ndio hutawala nchi. nchi ikiwa na wapumbavu wengi upumbavu ndio utawala kwa maana mawazo ya wengi ndio hutawala nchi.

na siku zote upumbavu na ujinga ukitawala nchi matokeo yake ni umasikini.

lakini nchi ikiwa na watu wengi walio katika kundi la tatu ambalo ni watu wanaoelewa nchi hupiga hatua kuelekea katika utajiri kwa maana dereva wa utajiri ni werevu.

hapa imewekwa mada ili tujadili kila mtu ajadili mada ili tutoke kwenye ujinga na upumbavu tuingie kwenye werevu ambao una faida kwetu sote.

lakini nimejaribu kuangalia michango yako hapa ni pointi gani umewahi kuzichangia kwenye mada hii? kimsingi unajijua wewe uko kundi gani kati ya hayo matatu.

akili yako ni kama ya mtungi kwa maana mtungi huwa unavujisha maji palepale ulipokaa ukidhani unamkomoa mwenye nyumba kumbe wenyewe ndio unakaa sehemu iliyolowana.

[/QUOTE]Hayo uloandika yoote takataka tupu kama ulivyo we mwenyewe.[/QUOTE]
 
leo hii watanzania wanalalamika kuwa kwenye mahakama zetu haki inatolewa kwa mwenye fedha sasa usawa unaozungumzwa kwenye katiba uko wapi?

na swala tunalolizungumza hapa ni je kuna tatizo gani linalofanya haki iliyozungumzwa katika katiba isipatikane katika kila ofisi inayostahili kutoa huduma kwa watanzania wote kwa haki na usawa.

sasa kama tunakimbilia kuongeza vifungu vya haki bila kuhakikisha yale tuliyoyataja yanatekelezeka hivi kweli tutakuwa tunafanya nini?
 
lengo la mada hii si kuwakatisha tamaa wale wanaodhani kuwa ni muhimu kwao kutajwa pengine ndio watapata haki bali kuwauliza kama kinachowanyima haki wamekitafakari kwa makini na kubaini ni kitu gani?

kuwakumbusha kuwa siku zote mtafuta nyoka huanzia miguuni mwake lakini wao wanaonekana kumulika mbali kutafuta nyoka kumbe nyoka yuko miguuni mwao.

ikijengwa mifumo ya kutoa haki na uwajibikaji ikaanza kufanya kazi, zipo haki nyingi ambazo haijalishi zimetajwa au hazikutajwa zitapatikana tu

lakini kama mifumo ya utoaji haki na uwajibikaji haifanyi kazi basi hata kama haki hizo zimetajwa haziwezi kupatikana kwa maana hakuna mifumo ya kuzitoa.

na njia pekee ya kuweka mifumo ni
1 kuweka cheksi na balansi katika mihimili mitatu ya utawala ili kila mmoja uwe huru bila kuingiliana na mhimili mwingine na mihimili yote mitatu kubalansi nguvu ili kusiwe na mhimili wenye nguvu kuliko mhimili mwingine.
2 kuweka mifumo mathubuti katika kila mhimili ili kila mhimili ufanye kazi kwa kutumia utaalamu na sio propaganda
 
lengo la mada hii si kuwakatisha tamaa wale wanaodhani kuwa ni muhimu kwao kutajwa pengine ndio watapata haki bali kuwauliza kama kinachowanyima haki wamekitafakari kwa makini na kubaini ni kitu gani?

kuwakumbusha kuwa siku zote mtafuta nyoka huanzia miguuni mwake lakini wao wanaonekana kumulika mbali kutafuta nyoka kumbe nyoka yuko miguuni mwao.

ikijengwa mifumo ya kutoa haki na uwajibikaji ikaanza kufanya kazi, zipo haki nyingi ambazo haijalishi zimetajwa au hazikutajwa zitapatikana tu

lakini kama mifumo ya utoaji haki na uwajibikaji haifanyi kazi basi hata kama haki hizo zimetajwa haziwezi kupatikana kwa maana hakuna mifumo ya kuzitoa.

na njia pekee ya kuweka mifumo ni
1 kuweka cheksi na balansi katika mihimili mitatu ya utawala ili kila mmoja uwe huru bila kuingiliana na mhimili mwingine na mihimili yote mitatu kubalansi nguvu ili kusiwe na mhimili wenye nguvu kuliko mhimili mwingine.
2 kuweka mifumo mathubuti katika kila mhimili ili kila mhimili ufanye kazi kwa kutumia utaalamu na sio propaganda

Wewe uko kwenye makundi yote hayo, umejichimbia kaburi.
 
Katiba ya chenge na kundi lake waizi wa mali za Umma.wezi wa wamepewa lungu kweli hii katiba lazima hitawafunga raia wasio na hatia na kuwacha waizi wachache wa mali za Mtanzania.


swissme
 
Katiba ya chenge na kundi lake waizi wa mali za Umma.wezi wa wamepewa lungu kweli hii katiba lazima hitawafunga raia wasio na hatia na kuwacha waizi wachache wa mali za Mtanzania.


swissme
Ebu angalia hata hiyo lugha uloandika inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa Mvamizi ama mkimbizi cjui unatokea Rwanda maana kiswahili chako hakipo vizuri, we utakuwa Mcongoman au Mrwanda ndo maan unapinga pinga ovyo. We sio raia hama nchini yetu bhana.
 
kaburi ni hatma ya kila mwanadamu, asiyejichimbia anachimbiwa na wengine.

lakini kama taifa lolote linaweza kubaki kuwaogopa wapumbavu wachache ambao wao hufikiri kutumia upumbavu na ujinga kama njia ya kuwaongoza wengine hakika taifa hilo litaangamia na hakuna anayeweza kuwa salama.

hebu angalia somalia, tangu amepinduliwa Mohamed Siad Barre ambaye alikuwa dictator somalia iko wapi?

angalia nchi zote ambazo mtu mmoja au kundi la watu wanaweza kudhani they can turn others into slavery what happens?

hapa kinachotokea ni jamii nzima kujenga hatred in mind na kufikiria njia za kuondoa such master. lipo tatizo kuwa kuwa kwa jamii yenye watu wengi kila mmoja anawaza la kwake.

wapo ambao hawawazi kabisa, kwao their goal kuover come kile wanachokiona mbele yao, wapo wenye busara wanaolinganisha faida na hasara na kusema not only to over come kilicho mbele yao but ni lazima wazidi kusonga mbele.

pale wanaowaza kufanya mabadiliko ambayo ni positive wanapokuwa wachache basi lipo tatizo kuwa anaweza kujitokeza mtu mmoja tu au kundi la watu ambao wanakuja na suluhisho la kipuuzi la kurudisha jamii nyuma na kwa kuwa walio wengi hawachanganui basi wanatumbukia katika matatizo makubwa zaidi.

yaliyowakuta wasomali si kwa bahati mbaya bali jamii imeelekezwa huko

yanayowakuta sudani ya kusini ni jamii kujengwa kuelekea huko

yanayowakuta irak ni jamii imejengwa kuelekea huko.

amani ya tanzania tuliyo nayo sasa jamii yetu ilijengwa kuelekea huko kwa kila mwana jamii kuridhika na jinsi mwenendo wa utawala ulivyokuwa na hakuna hata mmoja alikuwa anajenga chuki ndani ya nafsi yake.

kama kuna mtu anadhani yeye anaweza kufanya lolote analolitaka na jamii ikaa kimya bila kuangalia tunaelekea wapi na kurekebisha ukweli ni kuwa jamii haiwezi kubaki katika ujinga daima bali chuki zinaanza kujengeka ndani ya watu na hao wanaojenga chuki wanakata tamaa ya kujenga nchi yao. lakini watu hawa wakipata mpuuzi wa kutumia chuki hizi siku moja kama mtaji na akapata mahali pa kuwashia moto na ukawaka ni kwamba tutaelekea kwenye mlengo wa somalia, iraki na mifano ya aina hiyo.

only a stupid minded person can think that wananchi wote ni wajinga na yeye anaweza kuwatwist jinsi anavyotaka.

njia pekee ya kuepuka hayo ni kujenga mifumo ambayo itafanya kazi na kila mwananchi akaridhika.

tukijenga mifumo ikaanza kufanya kazi tutakuwa katika mwelekeo wa kufanya mabadiliko kama ya malasia.

tatizo kubwa wapo wahuni wachache wanaodhani mifumo ikikaa sawa hawajiamini na kudhani wanaweza kuhamia mikiani na kutoka sehemu za mbele ama waliko au wanakotaka kwenda. na hawa wanadhani ni bora ukawa kichwa cha panya anayeishi kwa wasiwasi mda wote akikimbizwa na kila jirani jirani yake kuanzia paka mpaka wanadamu kuliko kuwa mkia wa simba anayeishi kwa amani katika eneo lake ambaye kila mmoja anamuogopa kuingia katika himaya yake.

lakini ujinga wa wananchi ndio hatari kuliko kitu kingine chochote kwa maana mwananchi asiyejua kulinganisha maisha yake na kujua chanzo cha matatizo ni nini ni hatari sana kwani hawa wanasikiliza watu wengine na wako tayari kuingia kwenye vurugu mda wowote wakichochewa. hawana akili za kujiuliza kama vichocheo vinavyoletwa kwao ni vya kweli au la au wanachokifanya ni suluhisho au la. ni hatari sana kujenga jamii ya aina hii.

akija mtu
Wewe uko kwenye makundi yote hayo, umejichimbia kaburi.
 
kaburi ni hatma ya kila mwanadamu, asiyejichimbia anachimbiwa na wengine.

lakini kama taifa lolote linaweza kubaki kuwaogopa wapumbavu wachache ambao wao hufikiri kutumia upumbavu na ujinga kama njia ya kuwaongoza wengine hakika taifa hilo litaangamia na hakuna anayeweza kuwa salama.

hebu angalia somalia, tangu amepinduliwa Mohamed Siad Barre ambaye alikuwa dictator somalia iko wapi?

angalia nchi zote ambazo mtu mmoja au kundi la watu wanaweza kudhani they can turn others into slavery what happens?

hapa kinachotokea ni jamii nzima kujenga hatred in mind na kufikiria njia za kuondoa such master. lipo tatizo kuwa kuwa kwa jamii yenye watu wengi kila mmoja anawaza la kwake.

wapo ambao hawawazi kabisa, kwao their goal kuover come kile wanachokiona mbele yao, wapo wenye busara wanaolinganisha faida na hasara na kusema not only to over come kilicho mbele yao but ni lazima wazidi kusonga mbele.

pale wanaowaza kufanya mabadiliko ambayo ni positive wanapokuwa wachache basi lipo tatizo kuwa anaweza kujitokeza mtu mmoja tu au kundi la watu ambao wanakuja na suluhisho la kipuuzi la kurudisha jamii nyuma na kwa kuwa walio wengi hawachanganui basi wanatumbukia katika matatizo makubwa zaidi.

yaliyowakuta wasomali si kwa bahati mbaya bali jamii imeelekezwa huko

yanayowakuta sudani ya kusini ni jamii kujengwa kuelekea huko

yanayowakuta irak ni jamii imejengwa kuelekea huko.

amani ya tanzania tuliyo nayo sasa jamii yetu ilijengwa kuelekea huko kwa kila mwana jamii kuridhika na jinsi mwenendo wa utawala ulivyokuwa na hakuna hata mmoja alikuwa anajenga chuki ndani ya nafsi yake.

kama kuna mtu anadhani yeye anaweza kufanya lolote analolitaka na jamii ikaa kimya bila kuangalia tunaelekea wapi na kurekebisha ukweli ni kuwa jamii haiwezi kubaki katika ujinga daima bali chuki zinaanza kujengeka ndani ya watu na hao wanaojenga chuki wanakata tamaa ya kujenga nchi yao. lakini watu hawa wakipata mpuuzi wa kutumia chuki hizi siku moja kama mtaji na akapata mahali pa kuwashia moto na ukawaka ni kwamba tutaelekea kwenye mlengo wa somalia, iraki na mifano ya aina hiyo.

only a stupid minded person can think that wananchi wote ni wajinga na yeye anaweza kuwatwist jinsi anavyotaka.

njia pekee ya kuepuka hayo ni kujenga mifumo ambayo itafanya kazi na kila mwananchi akaridhika.

tukijenga mifumo ikaanza kufanya kazi tutakuwa katika mwelekeo wa kufanya mabadiliko kama ya malasia.

tatizo kubwa wapo wahuni wachache wanaodhani mifumo ikikaa sawa hawajiamini na kudhani wanaweza kuhamia mikiani na kutoka sehemu za mbele ama waliko au wanakotaka kwenda. na hawa wanadhani ni bora ukawa kichwa cha panya anayeishi kwa wasiwasi mda wote akikimbizwa na kila jirani jirani yake kuanzia paka mpaka wanadamu kuliko kuwa mkia wa simba anayeishi kwa amani katika eneo lake ambaye kila mmoja anamuogopa kuingia katika himaya yake.

lakini ujinga wa wananchi ndio hatari kuliko kitu kingine chochote kwa maana mwananchi asiyejua kulinganisha maisha yake na kujua chanzo cha matatizo ni nini ni hatari sana kwani hawa wanasikiliza watu wengine na wako tayari kuingia kwenye vurugu mda wowote wakichochewa. hawana akili za kujiuliza kama vichocheo vinavyoletwa kwao ni vya kweli au la au wanachokifanya ni suluhisho au la. ni hatari sana kujenga jamii ya aina hii.

akija mtu
wewe acha kufananisha tanzania na vichaka vingine, hii ni nchi ya amqni amqbyo imedumu kww muda mrefu, nyie mnaoipinga ndo mna nia mbaya na kuvuruga amani ya nchi hii, ushindwe na ulegee, kama hauna kazi endelea kuchapa ucngz acha kudanganya watu humu ndani.
 
mimi nadhani mrwanda au mkongo anayejenga tanzania ni bora kwa tanzania kuliko mtanzania anayebomoa tanzania.

nchi zenye jamii ya watu wanaoelewa kwanza wakigundua mtu anaweza kusaidia nchi yao wanamshawishi kumpa uraia.

lakini nchi za wajinga na wapumabavu hudhani waelewa ni maadui hivyo wako tayari kuwafukuza hata raia wao ambao ni welevu ili wabaki katika ujinga wao.

tusiwe wajinga kwa kutaka watu waseme kile tunachotaka kusikia bali tukubali kusikiliza kila mtu mawazo yake na hapo tutatambua mwelekeo wetu ni upi na tufanye nini.

Ebu angalia hata hiyo lugha uloandika inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa Mvamizi ama mkimbizi cjui unatokea Rwanda maana kiswahili chako hakipo vizuri, we utakuwa Mcongoman au Mrwanda ndo maan unapinga pinga ovyo. We sio raia hama nchini yetu bhana.
 
Back
Top Bottom