Kwani haya maswala ya ndoa, nani alianzisha, kwanini tuoane, kwanini heshima itoke ndani ya ndoa.
Ndoa ni ile iliyoandikwa na sheria au dini, au shuruti baada ya hatia ya kuzini, ndoa sio akiba ni sanaa, hakuna kitu halisi kwenye ndoa zaidi ya watoto.
Ndoa ni upendo unaobakia baada ya kuchoka kingono, ndoa ni kuvumilia maudhi yanayokera, ndoa ni maigizo yasiyo na hela, ndoa ni kama jela, ndoa sio kwa ajili yako ni kwa ajili ya watoto, unaweka ndoto zako kando na unazivaa changamoto, ndoa ni kukumbatia kaa la moto, ndoa ni jua kali, ndoa ni joto, ndoa ni kama kesi ya jinai, wanasema ndoa ni hukumu, NDOA SIO TUNU.
Ndoa ni maisha baada ya harusi.
Ndoa ni fumbo.
"Bora kupoteza hirizi kuliko kufiwa na mganga"
Sent from my SM-A107F using
JamiiForums mobile app