Kuongezeka kwa Ujenzi wa Vituo vya Mafuta kwenye makazi ya watu Serikali inasubiri ya Morogoro yatokee ndio ichukue hatua?


Wafanya maamuzi(viongozi) wanapojihusisha na biashara, usitegemee utaratibu, tegemea kuona utaratibu ukiwekwa kando kabisa.

Kama mnakumbuka ile kampuni ya Elon ilikutana na vitimbi gani, mara wafungue ofisi Tanzania, ujinga mtupu.

Nchi ya kitu kidogo.
 
Mtu amepiga 10% yake ya mradi wa wa bilion 100 aipeleke wapi kama sio kuhonga maafisa ardhi ewura
 
Kuna kijana wangu mmoja anaishi Tandale, ghetto lake kwa nyuma limeunganishwa na fence la walipojenga kitu cha mafuta ina maana yeye yuko nyuma

Ova
 
Wewe shida Yako ni nini, tra hawachukua Kodi huko!? Acha wivu na biashara za Watu
Usalama wa raia na jambo la muhim sana mm sio mtaalam sana ila hata kwa akili tu unajua hii ni hatari siku likitokea la kutokea
 
Maringo pale kona vp hakuna kituo kinachojengwa pale
Ila pale jkt majirani walitaka kuanza kupinga uwepo wa kituo hicho anyway
Sjui walimalizana vp

Ova
JKT pale majirani ni nani zaidi ya Jeshi?
 
Hivyo vituo ndio vinaongozwa na energy cartels ambao ndio viongozi wanawaongoza na ndio wanahusika na matatizo makubwa (mgao, upandaji nauli, upandaji bei za bidhaa)

Ni njia nzuri ya viongozi majizi /wafanyabishara wakwepa kodi kuchepusha pesa haramu (kutakatisha fedha)

Hizo ndio sababu mbili kuu za utitiri wa hivyo vituo na CCM inanufaika sana na biashara hiyo na wanajizolea makusanyo ya kampeni 2025.
 
Huu ni wivu TU, watuambie ni
JKT pale majirani ni nani zaidi ya Jeshi?
Vituo vingapi vimeshaleta madhara tangia uwepo wake!? Anyway uwepo WA majenzi holela ndio nilitegemea liwe priority ya waziri na Sio hizi cheap politics kuumiza wengine
 
JKT pale majirani ni nani zaidi ya Jeshi?
Kuna wakina mzee mgm na wenzake walijaribu
Ku complain kuhusu kituo hicho
Lakini waliangukia pua naona labda
Kwa sababu kina milikiwa na watu fulani
Kuna mtu hapo nyumba yake alipangisha ubalozi fulani,baada ya kituo cha mafuta kuwepo walisepa

Ova
 
Kwamba unataka mpaka uone ndiyo uone ni hatar? Mbona pale unapoenda kwenye kituo cha mafuta unakuta alama mpaka za kuzima simu, shusha abiria, zima gari etc? Kwamba huhisi tu kuwa eneo ilo linaweza tokea mlipuko?
 
Hivi vituo vilitakiwa vijengwe nje ya mji vijitenge na makazi ya watu. Kuna mji mmoja barabara kuu vituo vya mafuta vimejengwa vinakaribiana mita chachache kutoka kimoja hadi kingina na vyote vipo kwenye makazi ya watu
Mkuu vijengwe nje ya mji wapi? Hapo nje ya mji hakuna watu? Kwani hao wakaazi wanaolindwa hawahitaji huduma ya mafuta, upepo na gesi?

Mkuu cha msingi elimu na mafunzo ya usalama wa kuzuiwa na kujikinga na hatari ya moto ufanyike mara kwa mara kwenye vituo na kwa wakaazi majirani na vituo.

Mpaka sasa vituo vya mafuta Dar es salaam takriban asilimia 99% vipo kwenye makazi ya watu. Vifutiwe leseni?

Kwa vituo vya mafuta ambavyo vipo ndani ya makazi ya watu Dar es salaam, je **** matukio yoyote ya hatari kwa wakaazi yatokanayo na vituo hivyo yametokea?

Tuache fikra za kijima na kijamaa, tukubaliane na nguvu ya soko. Hawa ndio wawekezaji wazawa, wanalipa kodi, wanaajiri watanzania na wanaleta huduma karibu na wananchi!

Na jambo lingine na muhimu wamiliki wa vituo hawajengi bila kufuata sheria, Anapata vibali halali kutoka serikalini na wanajenga mchana kweupe.

Mkuu kama sheria zimepitwa na na wakati zibadilishwe kuendana na wakati uliopo, kuliko kuleta mkanganyiko na taharuki kwenye jamii.

Tusikatishana tamaa! enzi za giza za kufilisiana zimepita!
 
Duh nimeangalia hiyo picha ya mji wa kawe, inasikitisha sana hivi sisi ujinga tutaacha lini? Tunajenga hovyo hivyo mpaka tuna udhi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…