Hata mimi nilikua na mawazo ya kuhama kama wewe wakati nipo kijijini.
Baadae nilingundua mawazo ya kuhama yananizuia kujiendeleza na kuwekeza, na pia yanazuia kuziona fursa na kuzitumia.
Mm nilianzia wilayani nikaomba niende kijijini. Huko kwa kweli nilifanikiwa kibiashara kiasi, familia ilinipatia mtaji, na nilibahatika kufanya biashara kutoka Malawi miaka hiyo hasa mbuzi na karanga. Na locally nilikua nanua mpunga kipindi cha mavuno na kuuweka hadi mwisho wa mwaka.
Nilipoondoka, alienipokea alikuja kwa program ya Mkapa foundation, hakuwa na uhakika wa ajira ya kudumu, alikua Msukuma, alianzisha mradi wa ng'ombe wa maziwa, ufugaji kuku, na akatafuta location akaweka pool table. Aliwahi kuniambia hata akikosa ajira, hatohama hapo kijijini.
Kwa sasa nimesikia amewekeza ziwani (ziwa Nyasa) na ana bodaboda kampa kijana, still anapambana, na kwa ujumla anaendelea vyema.
Sometimes it is all about mindsets and priorities.