Kupaua nyumba (Makadirio ya gharama)

Kupaua nyumba (Makadirio ya gharama)

nzitunga
Inawezekana bro kwa maana nyumba ya mita 20 kwa 15 si mchezo ni kama darasa hilo
 
Last edited by a moderator:
Kaka hizi bei zako mbona utata. Ukiacha kutojua ukubwa. Bati m5 ni Bundle ngapi? Na ni aina gani? Mbao m3 ni kivipi na ngapi na kila moja sh ngapi hadi ziwe na hiyo gharama? huyo fundi wa kupaua kwa m3 nyumba ya mtanzania!.

Ukiangalia hizo gharama unaweza ukafuta kabisa mawazo ya kujenga
 
Jamani kupaua ni gharama kuna rafiki yangu alitajiwa jumla ya 17M (ufundi, mbao, bati-ALAF, ukubwa around 15x20). Hapahapa DSM, Akaomba apunguziwe walau 14, ikashindikana. Akaahirisha. Kama huyo rafiki yangu akiiona hii post, atampigia huyu jamaa mara moja.

Watu wanafikiri kupaua ni raisi, alafu wakitajiwa gharama za ufundi wanaona ni nyingi kana kwamba yule fundi ile kazi ataifanya peke yake.
 
Sio kwamba nigharama sana sema huwezi piga kench ukae baada ya miezi saba upige bati no unatakiwa uwe nayo kwa mara moja yote pesa ya bati fundi na mbao ndiyo maana kuezeka ni tabu tupu but for 3 M too much may be 4 times that the supposed price

Gharama za ufundi 4 times? Umetumia calculation zipi kupata hiyo bei?

Ushahuri wangu kwa wale mnaotaka kupaua mabati ya migongo mipana (IT5) wajipange, wawatafute mafundi kwanza wawape makadilio.
 
kupaua si gharama kiasi hicho kaka acha tamaa na kutisha watu labda gharama hizo ni kwa site za masaki na maeneo kama hayo au huko ni kutafuta faida za juu kabisa....hizo kazi tunafanya kila siku na bei ni za kawaida kabisa mf.. Nyumba ya vyumba 3 au 4 yenye vipimo standard itachukua mbao treated za hadi sh 1.5m, bati kama ni south around 3.5m na ufundi ni around 1-1.2m na tunafanya daily
 
Transporter
Mkuu kwenye mbao hapo mmmm mbona kama rahisi sana any way mi si mtaalamu sana
 
Last edited by a moderator:
Mi nimemaliza juzi juzi kupaua. Mabati 3.2m, mbao 2m na,Fundi ni kama 1.4m, vyumba vitatu vikubwa sana! Viwili ni master,sebule,jiko na stoo na ni Nyumba yenye coridor ndefu. Fundi na wasaidizi wake walimaliza kazi nda ni ya siku tano na nilisimamia mwenyewe.
Nashangaa watu wanaleta mabei makuubwaaa hapa ya kifisadi,acheni kutisha watu.
 
Mi nimemaliza juzi juzi kupaua. Mabati 3.2m, mbao 2m na,Fundi ni kama 1.4m, vyumba vitatu vikubwa sana! Viwili ni master,sebule,jiko na stoo na ni Nyumba yenye coridor ndefu. Fundi na wasaidizi wake walimaliza kazi nda ni ya siku tano na nilisimamia mwenyewe.
Nashangaa watu wanaleta mabei makuubwaaa hapa ya kifisadi,acheni kutisha watu.

Mimi naanza kupaua na gharama yote ni karibu 7.5ml bati nimepata kwa 2.9 ml mbao around 3 ml na Fundi anakula 1.5
 
kupaua si gharama kiasi hicho kaka acha tamaa na kutisha watu labda gharama hizo ni kwa site za masaki na maeneo kama hayo au huko ni kutafuta faida za juu kabisa....hizo kazi tunafanya kila siku na bei ni za kawaida kabisa mf.. Nyumba ya vyumba 3 au 4 yenye vipimo standard itachukua mbao treated za hadi sh 1.5m, bati kama ni south around 3.5m na ufundi ni around 1-1.2m na tunafanya daily
Unasema kweli hizo Bei? Maana nami nna kibanda changu kimekwama maeno hayo, nimepeleka fundi kanipa estimation za 18M +mbao za ceiling board.
 
According @ ze marcopollo gharama za kupauua inatokana na aina ya paa kuna paa zingine inahitaji vipande vingi kwa hiyo kunakukata kata mabati na anasema fundi akikupa estimation nunua 75 % tu vikipelea utaongeza
 
ARV

Mkuu mbona gharama ya kofia huziweki tupia basi tupate real costs kwa maana kupaua nafikiri ni mpaka fisherboards (sina uhakkika na spelling)
 
Last edited by a moderator:
wakuu sidhani kama mnajua maana ya makadirio, anyway, siwalaumu, ili uweze kukokotoa roofing cost lazima ujue ramani na aina ya paa utakayotumia, mimi nimeweka makadirio hayo kwa bati za Ando za vigae, kwa nyumba ya wastani wa 120sqm to 150sqm, so nimemtaarifu mhusika atenge budget ambayo hatoishia kupiga mbao tu, (roofing=treated timber, fascia boardy, sheets, nails, valleys, caps, labour charge, etc.)
attachment.php
 
wakuu sidhani kama mnajua maana ya makadirio, anyway, siwalaumu, ili uweze kukokotoa roofing cost lazima ujue ramani na aina ya paa utakayotumia, mimi nimeweka makadirio hayo kwa bati za Ando za vigae, kwa nyumba ya wastani wa 120sqm to 150sqm, so nimemtaarifu mhusika atenge budget ambayo hatoishia kupiga mbao tu, (roofing=treated timber, fascia boardy, sheets, nails, valleys, caps, labour charge, etc.)
attachment.php

Mkuu,
Sina shaka sana na bei ya vifaa (bati/vigae na mbao) mi naona hiyo labour charge (3m) ni kubwa sana naamini unaweza pata fundi wa bei nafuu zaidi
 
Mi nimemaliza juzi juzi kupaua. Mabati 3.2m, mbao 2m na,Fundi ni kama 1.4m, vyumba vitatu vikubwa sana! Viwili ni master,sebule,jiko na stoo na ni Nyumba yenye coridor ndefu. Fundi na wasaidizi wake walimaliza kazi nda ni ya siku tano na nilisimamia mwenyewe.
Nashangaa watu wanaleta mabei makuubwaaa hapa ya kifisadi,acheni kutisha watu.
Mkuu umetumia aina gani za bati? Maana zipo za kawaida na zile za migongo mipana, na za kiwanda gani, vipi bei ya kofia, na misumali yake, je hizo bati sh ngapi kwa mita
 
Back
Top Bottom