GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Wala simlaumu Kipa Ali Salim kwa Kufungwa Goli zile Mbili ( hasa lile la Pili ) kama ambavyo Wengi wenu mnamlaumu ila GENTAMYCINE nalia na Beki wetu Henock Inonga ambaye zaidi ya mara Mbili hapa hapa JamiiForums nimeshamuanzishia Threads kuelezea Madhaifu yake na kwamba yasiporekebishwa ipo Siku atakuja Kutugharimu na kweli Jana Katugharimu.
Sina shaka na Uwezo wake mkubwa wa Mpira ( Kipaji alichonacho ) na ni Mchezaji aliyekamilika Maeneo mengi isipokuwa attitude yake na Pungufu moja la Kiufundi ndilo linalomgharimu na litaendelea Kumgharimu kama hatojirekebisha.
Beki Henock Inonga ana Sifa za Kijinga ambazo zinakera, anapenda mno Kucheza na Jukwaa na Ukabaji wake ( Marking yake ) hasa katika Sita ( 6 ) ni wa hovyo na wa Chini mno na kama Makocha hawatomrekebisha katika hili tutafungwa sana Magoli na kukimbilia Kuwalaumu Makipa wetu wakati kumbe wenye shida ni Mabeki wetu.
Kama ulitulia na kuangalia vyema yale Magoli ya Al Ahly FC jana utakubaliana nami GENTAMYCINE tena 100% kuwa yote yamefungwa mbele ya Beki Henock Inonga na kama angekuwa na Umakini ( Concetration ) ya hali ya Juu yale Magoli yasingefungwa.
Beki Henock Inonga ni Mdhaifu mno katika kufanya Anticipation kwa Mpira Wenyewe unakoelekea au kwa Mikimbio ya Washambuliaji na hii ni katika Sita ( 6 ) ya Goli la Simba SC.
Kwa mfano lile Goli la Kwanza la Al Ahly FC Beki Henock Inonga angelala Yombo ( angefanya Slide tackling ambayo anajmudu vyema ) Yule Mshambuliaji angefunga lile Goli?
Kwa Goli la Pili la Al Ahly FC hivi Beki Henock Inonga angekuwa na Anticipation Ability baada ya kuona Mchezaji wa Al Ahly FC aliyeko Winga ya Kushoto anataka kupiga Majalo ( Krosi ) au Kutoa Pasi ya mwisho angekaa nyuma ya Mfungaji wa Goli la Pili au angekaa mbele yake ili kufanya Blocking ( Zuio ) ili Mpira usimfikie Kiurahisi aliyefunga Goli na Kuutoa kabisa Mpira nje iwe Kona au Kipa adake na tusalimike?
Henock Inonga ajitathmini abadilike.
Sina shaka na Uwezo wake mkubwa wa Mpira ( Kipaji alichonacho ) na ni Mchezaji aliyekamilika Maeneo mengi isipokuwa attitude yake na Pungufu moja la Kiufundi ndilo linalomgharimu na litaendelea Kumgharimu kama hatojirekebisha.
Beki Henock Inonga ana Sifa za Kijinga ambazo zinakera, anapenda mno Kucheza na Jukwaa na Ukabaji wake ( Marking yake ) hasa katika Sita ( 6 ) ni wa hovyo na wa Chini mno na kama Makocha hawatomrekebisha katika hili tutafungwa sana Magoli na kukimbilia Kuwalaumu Makipa wetu wakati kumbe wenye shida ni Mabeki wetu.
Kama ulitulia na kuangalia vyema yale Magoli ya Al Ahly FC jana utakubaliana nami GENTAMYCINE tena 100% kuwa yote yamefungwa mbele ya Beki Henock Inonga na kama angekuwa na Umakini ( Concetration ) ya hali ya Juu yale Magoli yasingefungwa.
Beki Henock Inonga ni Mdhaifu mno katika kufanya Anticipation kwa Mpira Wenyewe unakoelekea au kwa Mikimbio ya Washambuliaji na hii ni katika Sita ( 6 ) ya Goli la Simba SC.
Kwa mfano lile Goli la Kwanza la Al Ahly FC Beki Henock Inonga angelala Yombo ( angefanya Slide tackling ambayo anajmudu vyema ) Yule Mshambuliaji angefunga lile Goli?
Kwa Goli la Pili la Al Ahly FC hivi Beki Henock Inonga angekuwa na Anticipation Ability baada ya kuona Mchezaji wa Al Ahly FC aliyeko Winga ya Kushoto anataka kupiga Majalo ( Krosi ) au Kutoa Pasi ya mwisho angekaa nyuma ya Mfungaji wa Goli la Pili au angekaa mbele yake ili kufanya Blocking ( Zuio ) ili Mpira usimfikie Kiurahisi aliyefunga Goli na Kuutoa kabisa Mpira nje iwe Kona au Kipa adake na tusalimike?
Henock Inonga ajitathmini abadilike.