Kupinga Serikali Tatu; Natofautiana Na Profesa Issa Shivji...

Kupinga Serikali Tatu; Natofautiana Na Profesa Issa Shivji...

maggid

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2006
Posts
1,084
Reaction score
1,246
Ndugu zangu,


Mimi naamini, kuwa Mfumo wa Serikali Tatu hautavunja Muungano, yumkini utauimarisha. Kama kweli tuna dhamira ya dhati ya kutoka kwenye tope la kero za Muungano tulilonasa, basi, Serikali Tatu haziepukiki.


Juzi hapa Profesa Issa Shivji, mbali ya mambo mengine yaliyomo kwenye rasimu ya Katiba, ameonyesha wasiwasi wake kuwa Serikali Tatu zitapelekea kuuvunja Muungano.


Naheshimu sana mawazo ya Profesa Shivji, lakini, katika hili la Serikali Tatu nahofia ametanguliza hofu isiyo lazima.


Uhalisia tulio nao sasa ni kuwa hali ya Muungano wetu inadhohofika kila kukicha. Wengi walio upande wa visiwani wanataka mamlaka kamili ya kidola. Na sauti za wabara wenye kuhoji muungano zinaongezeka kila kukicha. Hivyo, kero za Muungano zingalipo na zitaongezeka. Ili walau tuwe na nafasi ya kuunusuru Muungano, mimi naikubali kwa dhati kabisa ' Njia ya Jaji Warioba'.


Naamini pia, kuwa Serikali Tatu zinaweza pia kupelekea wananchi wa nchi husika kufanya kazi zaidi kwa ajili ya nchi zao. Hivyo basi, kuongeza zaidi bidii ya kuzalisha na kugharamia Serikali ya Muungano bila matatizo makubwa. Serikali Tatu zitaongeza pia hali ya kujitambua na kuheshimiana kama ndugu. Demokrasia ina gharama. Hivyo basi, hatuwezi kuchagua mfumo dhaifu kwa kuogopa gharama za demokrasia.


Na Mwanadiplomasia mahiri wa Kitanzania alipata kuliweka hili vizuri kabisa. Ni Balozi Augustine Mahiga. Alisema, kuwa ingawa Serikali Tatu zina gharama zake, lakini, kisiasa ina manufaa yake kutokana na mijadala ya muda mrefu kuhusiana na muundo wa Muungano.

Balozi Mahiga anazidi kunukuliwa akisema, kuwa iwapo Rasimu hiyo itapitishwa na Watanzania, ni wazi kwamba Tanzania itakuwa imerekebisha kasoro za Muungano unaotimiza miaka 50 mwakani, kwa njia ya mazungumzo. ( Mwananchi, Jumapili, Juni 9, 2013, Uk 2)

Ndugu zangu,

MUUNGANO wa nchi MBILI unapaswa uzae nchi MOJA. Hivyo, Serikali MOJA pia. Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Hata hivyo, Zanzibar kuna Serikali ya Mapinduzi tangu mwaka 1964. Tanganyika hakuna, na jina pia halitumiki.


Tuukubali ukweli, kuwa katika kilichoanishwa hapo juu, ni vigumu kuzungumzia Muungano wa Serikali MBILI badala ya MOJA au TATU.


Naam, umefika wakati wa kuukubali ukweli, kuwa kwa muundo huu wa Muungano tulio nao sasa, siku zote kutakuwa na manung'uniko. Kuukataa ukweli huu ni sawa na kufagilia takataka chini ya jamvi. Iko siku jamvi lazima liinuliwe, na uchafu huo utaonekana tu.


Maggid Mjengwa,

Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio
 
Pungufu ya mamlaka kamili ya zanzibr muungano bye bye!
 
Well said mjengwa....!!

Walioanza kupinga kipengele cha serikali tatu ni chama tawala-ccm....nahisi kama kuna dalili za wao kuwatumia watu maarufu kama akina shivji kuwachanganya watoa maoni/wananchi ili nao pia wakatae then baadaye waje waseme wengi wamekataa kuwa na serikali tatu....!!

Hata mimi naona suluhisho la manung'uniko ya muundo wa muungano tulio nao ni kuwa na serikali moja ya tanzania ua serikali tatu....kwani serikali mbili, ya mapinduzi zanzibar inasimama kwa tanzania visiwani ya muungano mambo ya muungano iko wapi inayosimamia mambo ya tz bara....?
 
serikali tatu ndio njia bora ya kuvunja muungano bila kelele, wengi tunapenda muungano ufe asubuhi na mapema
 
Wengi wanaotaka mfumo wa Muungano wa Serikali mbili ni WAHIFADHINA(CONSERVATIVES) kwa asili.Wahifadhina siku zote ni waoga wa MABADILIKO because they are not sure what those changes will hold for them in the future.pamoja na uoga wao tutawalazimisha tu waingie katika Meli ya MV MABADILIKO,Naamini mabadiliko yatawabadilisha tu watake wasitake.
 
Well said mjengwa....!!

Walioanza kupinga kipengele cha serikali tatu ni chama tawala-ccm....nahisi kama kuna dalili za wao kuwatumia watu maarufu kama akina shivji kuwachanganya watoa maoni/wananchi ili nao pia wakatae then baadaye waje waseme wengi wamekataa kuwa na serikali tatu....!!

Hata mimi naona suluhisho la manung'uniko ya muundo wa muungano tulio nao ni kuwa na serikali moja ya tanzania ua serikali tatu....kwani serikali mbili, ya mapinduzi zanzibar inasimama kwa tanzania visiwani ya muungano mambo ya muungano iko wapi inayosimamia mambo ya tz bara....?

Kwa maneno yako haya unakosea.....Shivji huwa hapelekeshwi na huongea kile anachoamini yeye na haya ni mawazo yake siku zote...
Fuatilia kongamano la Kwanza akitoa hotuba kuhusu Katiba mpya na kwa nini katiba mpya.....maoni yake kuhusu muungano yalikuwa ni hayo hayo....
Tunaweza kumpinga sio kosa....ila kuwa na serikali tatu ni ngumu kiutendaji kwa serikali ya muungano!
 
Shivji anatumika kwa matakwa ya magamba.
 
Skiliza mzalendo.

Kwani shivji yeye kama nani hapa ? Kwani nchi yake ? Hakuna mtu yoyote anae weza kuwasemea wananchi zaidi ya wananchi wenyewe, sio warioba wala kikwete wala shein wala mpumbavu yyote, suala la muungano nani alie pendekeza serikali tatu ? Kwanza tuangalie maoni, ccm wamependekeza serikali mbili, jamuhuri ya muungano na zanzibar, ccm wa zanzibar wamependekeza hivyo hivyo ila zanzibar yenye mamlaka kamili, cuf imependekeza mkataba kwa upande wa zanzibar, kwa bara siwezi kujua, ukija kwa wananchi wa zanzibar walio wengi wengi walipendekeza muuungano wa mkataba zanzibar yenye mamlaka kamili, walio pendekeza mfumo huu uliopo ila zanzibar yenye mamlaka kamili asilimia kama 13, asilimia 66 mkataba, ni wazi kwamba wananchi ni ndio wanao guswa na muungano hakuna mwengine.

Sasa hizi serikali tatu kazitoa wapi ? Kwa chadema ? Kama kwa chadema basi ccm imekufa, inamana chadema inakauli kuliko ccm ?

Sisi wanzanizbari tunataka mkataba , au tuvunje kabisaa, hatutaki kusemewa tunataka maoni yetu yatekelzwe
Ndugu zangu,


Mimi naamini, kuwa Mfumo wa Serikali Tatu hautavunja Muungano, yumkini utauimarisha. Kama kweli tuna dhamira ya dhati ya kutoka kwenye tope la kero za Muungano tulilonasa, basi, Serikali Tatu haziepukiki.


Juzi hapa Profesa Issa Shivji, mbali ya mambo mengine yaliyomo kwenye rasimu ya Katiba, ameonyesha wasiwasi wake kuwa Serikali Tatu zitapelekea kuuvunja Muungano.


Naheshimu sana mawazo ya Profesa Shivji, lakini, katika hili la Serikali Tatu nahofia ametanguliza hofu isiyo lazima.


Uhalisia tulio nao sasa ni kuwa hali ya Muungano wetu inadhohofika kila kukicha. Wengi walio upande wa visiwani wanataka mamlaka kamili ya kidola. Na sauti za wabara wenye kuhoji muungano zinaongezeka kila kukicha. Hivyo, kero za Muungano zingalipo na zitaongezeka. Ili walau tuwe na nafasi ya kuunusuru Muungano, mimi naikubali kwa dhati kabisa ' Njia ya Jaji Warioba'.


Naamini pia, kuwa Serikali Tatu zinaweza pia kupelekea wananchi wa nchi husika kufanya kazi zaidi kwa ajili ya nchi zao. Hivyo basi, kuongeza zaidi bidii ya kuzalisha na kugharamia Serikali ya Muungano bila matatizo makubwa. Serikali Tatu zitaongeza pia hali ya kujitambua na kuheshimiana kama ndugu. Demokrasia ina gharama. Hivyo basi, hatuwezi kuchagua mfumo dhaifu kwa kuogopa gharama za demokrasia.


Na Mwanadiplomasia mahiri wa Kitanzania alipata kuliweka hili vizuri kabisa. Ni Balozi Augustine Mahiga. Alisema, kuwa ingawa Serikali Tatu zina gharama zake, lakini, kisiasa ina manufaa yake kutokana na mijadala ya muda mrefu kuhusiana na muundo wa Muungano.

Balozi Mahiga anazidi kunukuliwa akisema, kuwa iwapo Rasimu hiyo itapitishwa na Watanzania, ni wazi kwamba Tanzania itakuwa imerekebisha kasoro za Muungano unaotimiza miaka 50 mwakani, kwa njia ya mazungumzo. ( Mwananchi, Jumapili, Juni 9, 2013, Uk 2)

Ndugu zangu,

MUUNGANO wa nchi MBILI unapaswa uzae nchi MOJA. Hivyo, Serikali MOJA pia. Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Hata hivyo, Zanzibar kuna Serikali ya Mapinduzi tangu mwaka 1964. Tanganyika hakuna, na jina pia halitumiki.


Tuukubali ukweli, kuwa katika kilichoanishwa hapo juu, ni vigumu kuzungumzia Muungano wa Serikali MBILI badala ya MOJA au TATU.


Naam, umefika wakati wa kuukubali ukweli, kuwa kwa muundo huu wa Muungano tulio nao sasa, siku zote kutakuwa na manung'uniko. Kuukataa ukweli huu ni sawa na kufagilia takataka chini ya jamvi. Iko siku jamvi lazima liinuliwe, na uchafu huo utaonekana tu.


Maggid Mjengwa,

Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio
 
Shivji anatumika kwa matakwa ya magamba.

Ndugu Ndoa,

Profesa Shivji ametoa maoni yake. Tuamini hivyo na tuheshimu fikra zake hata kama kuna kutofautiana kimitazamo. Ndio demokrasia.
Maggid,
Iringa.
 
njia sahihi yani ama kuwa na serikali moja au kuvunja muungano kila bajeti watu wanalalamika pesa za maendeleo kidogo,kodi imepanda serikali ina wizara nyingi hizo gharama za serikali kuendesha serikali tatu nani abebe kama sio mwananchi wa kawaida kama tumeona hatuna haja ya muungano ni bora tuuvunje kila mtu awe kivyake
 
watanganyika na wazanzibar wameulalamikia huu muundo wa mungano tangu ulipoasisiwa na Karume na Nyerere,kama watu walo wengi wana lalamika kuhusu huu mungano hii ina maana kuwa mungano hauna faida kwa walalamikaji labda inawezekana una faida kwa watu wachache

Ushauri wangu kama kitu kimelalamikiwa na wengi kwa muda mwingi bora kiondolewe, yaani bora mungano uvunjwe kiundwe chombo chengine ambacho kitasimamamia hizi nchi kwa ridhaa ya watu wa pande zote mbili za Tanganyika na zanzibar

Binafsi naona huu mungano umeleta chuki baina ya watu wa tanganyika na zanzibar, watu ambao walikuwa wanaishi kwa kuelewana kwa muda mwingi kabla ya mungano wa Nyerere na Karume,huwezi kulazimisha kitu ambacho hakifanyi kazi eti kwasababu nchi za nje wanausifu huu mungano ni waina yake, wakati wa sifa umekwisha sasa wanasiasa watafute njia mbadala ya kunusuru chuki zisiendelee baina yetu
 
Unaposema serikali unamaanisha nini?? Kuna mpaka serikali za mtaa ambazo zina legislature (halmashauri), Executive (mayor) na Judiciary (mahakama za jiji). Hizi nazo ni serikali.

Dola!! .. kutakuwa na dola ngapi? Au nchi ngapi? .. Hapo ndiyo tunapokataa kuwa na nchi mbili zilizoungana, ambapo kila moja ina madaraka kamili.Na serikali ya muungano ambayo madaraka yake kikatiba hayashurutishi nchi shirikishi kuyafuata.\

Yaani ukiangalia mfano, unaweza kuona kuwa Zanzibar ina uwezo wa kufanya gerrymandering na kuanzisha wilaya mpya ishirini, just to balance or to even have more votes thAn Tanganyika.

Ni bora kuwe na federation ya Tanzania ambapo Tanganyika na Zanzibar ni states. Na federal legislature pamoja na Judiciary ziwe independent and above the laws of the states. The legislature needs to be bicameral with the senate evenly distributed among the member states.

Ila hii serikali ya Muungano waliyopendekeza hawa jamaa is Bogus to say the least.
 
Ndugu Maggid na Wengine, Mawazo na Maoni ni jambo moja na uzito wa uchambuzi ni jambo jingine. Mapenzi na matamanio ya kutaka au kutotaka Muungano kwa upande mmoja, na matamanio ya serikali tatu, mbili, moja au sufuri nijambo jingine. Suala la msingi ni kuisoma kwa utulivu hoja ya Prof. shivji na kujua msingi wake ni nini. Mathalani Maggidi anataka na kutamani Serikali Tatu na sababu yake ni kuwa itakuwa imetatua kerro za Muungano. Udhaifu wa hoja ya Maggidi ni kutosema kero hizo ni nini, za nani na zinachukua sura gani? Na pili asili ya kiini cha kero hizo ni nini na namna gani Serikali Tatu zinajibu kero hizo. Mfano, Wazanzibari wengi mafukara (ambao ndio wengi) wanaaminishwa kwamba Zanzibar nje ya Muungano itakuwa na neema na ufukara wao utakoma, kwamba ufukara wao unatokana na Muungano. Je, ni sawa kiini cha ufukra ni Mungano na kwamba siku Zanibar itakapopeperusha Bendera yake UN ndio matatizo ya Wazanzibari yamekwisha? Je, Lakini pia haisemwi ni kwa namna gani Nje ya Muungano ama Serikali Tatu zinavyoweza kushugulikia hali ya migawanyiko ya kisiasa ndani ya Zanzibar yenyewe. Hili sasa halisemwi, Zanzibar inaonekana ni moja - lakini hili si sahihi sana! MUHIMU zaidi ni HATA kwa wanaopenda Serikali Tatu kama Maggidi, anachosema Prof. Shivji ni kuwa kwa namna Katiba ya Warioba ilivyo inaweka misingi na masharti dhaifu (Ya Kikatiba) ya kuulinda Muungano. Sasa mimi ningedhani Maggidi na wengine mungesoma kwa Makini na Utulivu - na sio kwa Kutumia Mioyo Yenu - Bali akili na tafakari huru - kuitazama Hoja na mantiki, ushahidi na uchambuzi wa Prof. Shivji juu ya mengi, lakini hata kwa hilo Mnalilipenda na kutamani!
 
Rejea maoni ya Shivji tena na tena.....halafu leta mawazo yako upya.....uchambuzi wako unapwaya mnooo sikutarajia uchambuzi wa hali ya chini hivi.....
 
Kiufupi,pungufu ya mamlaka kamili ya zanzbr muungano bye bye.
 
Back
Top Bottom