Kuporomoka Kwa Maadili, Kushamiri Kwa Ushoga Na Ukahaba

Kuporomoka Kwa Maadili, Kushamiri Kwa Ushoga Na Ukahaba

Jamani jamani muogopeni Mwenyezi Mungu;
Hili suala la uasherati, ushoga ni baya sana na dini zote mbili (uislamu & Ukristo) zinalipiga marufuku,

Rejeeni maandiko hapa chini;
MOSI:
“ Au, je, hamjui kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msijidanganye! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wafiraji au walawiti, wanyang’anyi, wachoyo, walevi, wenye kusengenya, walaghai, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu” (1Wakorinto 1:9)

PILI:
“ Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo. Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale; sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uwongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.” (1 Timoteo 1:8-10).

Msijesema kuwa hamjui kiswahili, hii hapa kwa kiingereza;
8 Now we know that the law is good, if one uses it legitimately. [SUP]9[/SUP]This means understanding that the law is laid down not for the innocent but for the lawless and disobedient, for the godless and sinful, for the unholy and profane, for those who kill their father or mother, for murderers, [SUP]10[/SUP]fornicators, sodomites, slave-traders, liars, perjurers, and whatever else is contrary to the sound teaching.(1 Timothy 1:8-10).

Kila mtu ana jukumu la kukeme hili suala kwa nguvu zote..

@Mr.Toyo, Nakubaliana na wewe kuwa uislam na ukristo unakataza ushoga kwa maana hiyo ni mungu anakataza ushoga. Kama ndivyo vipi wale wasio na dini au hawaamini kama mungu yupo (atheisits) wahukumiwe kwa dini ambazo haziwahusu? Pili, tunaambiwa kuwa kwa mungu kila jambo linawezekana, je ilikuwaje huyu mungu mwenye uwezo wa ajabu akaumba mashoga? uwezo wake ulikuwa likizo wakati mashoga wanazaliwa? Why didn't god stop the recreation process in the first place? Na kama basis ya argument ni maandiko yatokayo kwa mungu tumepata wapi mamlaka ya kuhukumu? (i.e biblia inakataza kuhukumu).

Lakini kuna hili, vitabu vya dini hizi mbili (Uislam &Ukristo) vinonekana kukataza ushoga. Ina maana ushoga umekuwepo tangu miaka hiyo (2000 yrs)? Kama ndivyo Tanzania mbona tunashtuka kama ndio kwanza tumeuskia kumbe ni mambo yako kwa miaka na miaka? Hivi ni kweli hakuna mashoga Tanzania? Na kuna sheria Tanzania inayokataza mtu kuwa ushoga? Ya ndoa ipo (watu wa jinsia tofauti i.e mke mume) lakini ni sheria ipi inayosema mtu haruhusiwi kuwa shoga?

Nimalizie, kuna mahali umenukuu maandiko ya biblia :"Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wafiraji au walawiti, wanyang’anyi, wachoyo, walevi, wenye kusengenya, walaghai, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu" Nikiangalia hapa napata maswali mengi. Hivi wale wakwepaji wa EPA, 'walaghai wa Richmond watakuwa na hatia mbele ya mungu kwa kutumia hayo maandiko? Viongozi wetu serikalini (past & present) wanaweza kuwa wametenda/wanatenda moja ya hayo makosa? Sasa inakuwaje viongozi wa dini wanapiga makelele saaana kuhusu ushoga lakini wanapokea pesa za walaghai na wanyang'anyi? Ni mara ngapi tunaona kwenye TV maaskofu, masheikh wanapokea pesa toka kwa watu walioiba/wanaoiba hela za umma? Kuna exemption kwenye haya masharti ya kupata uzima wa milele?

Hivi inakuwaje mtu anayeiba hela zilizokusudiwa kulipia huduma za afya na hivyo kusababisha wagonjwa kulala chini na wengine kufa kwa kukosa dawa ananyamiziwa lakini mtu anayeingia chumbani kwake kwa hiari na kujifurahisha kwa namna atakavyo ndiye anayehukimiwa?double standard?

Mimi naona wanasiasa wanatupoteza kwa kukuza huu mjadala wa ushoga. Badala ya kujibu kwanini miaka 50 ya uhuru nchi yetu bado ni ombaomba wao wanataka wananchi wajadili nani anatumiaje viungo vyake vya mwili wake chumbani kwake!. Na ili ujue wanasiasa wetu ni wasanii, Malaysia ambayo inafuata misingi ya kiislam hawajasema lolote (Malaysia pia ni mwanacham wa jumuiya ya madola). Na Malaysia walipata uhuru toka kwa Waingereza hawa hawa around the same time na sisi. Utagundua hii kauli ya Cameron imewagusa zaidi Matonya kwa sababu wameambiwa kuanzia sasa huduma za vibakuli zitatolewa kwa vigezo na masharti, kama hutaki uko huru kupeleka bakuli lako unakojuwa.
 
Kwa kweli, Qur'an inasema (Suratul Tin, 95) : Alahi Salah bi Ahkamil Hakimil (Isn't God the greater of all the juges?)
Na Bibilia inasema (Matayo 7: 1-5): Do not judge, or you too will be judged.
Nauliza, hivi kuna big sinners and small sinners? If we are all sinners, who gives you the right to condemn the sins commited by other persons? huyajui maisha yao, na hujui ni wema gani wanafanya. we mwenyewe ulipo huja kamilika.
Naomba tuwe waelewa na kabla ya kuhukumu tuanze kwa ushahuri.
Asanteni.

Whaaaaaaaaaaaatttttt!!! Wema wao watuhusu nini sasa. Khaaa!
 
laana ijuu yao, ni vema kutambua thamani yako kama we ni me au ke, [ personal conscience]
 
Mwenyezi Mungu hakuumumba binadamu halafu akamuachia tu aishi anavvotaka, bila shaka amempangia taratibu na mfumo mzima ambao yeye anatakiwia aishi, ili lengo la yeye kiumbe kuwepo hapa duniani lifikiwe, ndomana akatultea muongozo (wahy) kupitia huo jinsi gani tuishi, napia akatuelezea yale yaliowafika waliopinga na yale waliopata waliofuata ili kuwa ni kigezo kwetu

kwahiyo bila shaka product ya matatizo yote yaliopo leo hii duniani ni kutokana na watu kujitungia mifumo yao wenyewe ya kuishi, kutokana tu na matashi ya nafsi zao.

Mungu anasema katika qur-an " hakika yeye Allah(s.w) hatobadilisha maisha yenu mpaka nyinyi mbadilishe yale yaliomo katika nafsi zenu" hii ina ashiria kuwa mfumo wa maisha ikiwa utaendelea kuwa chini ya mamlaka ya binadamu duniani hali hii itaendelea kuwepo na kuongezeka, na mabalaa zaidi kutokea.

kwahiyo njia kuu ya kuondosha matatizo yaliyopo katika jamii ni kuweka mfumo wa Mwenyezi Mungu juu na binadamu chini.
 
Yote ni malezi tu na Kumsahau Mungu...

Tumrudie Mungu kwa kila jambo...
 
Nakupinga jambo moja la TGNP kusupport mashoga sio kweli. Mi nilikuwepo kwenye matukio yote ya gender festival ambayo yanatumika kama platform ya watu kuongea kuhusiana na theme zinazowekwa. Na TGNP walijibu kuwa wao wanatambua jinsia mbili tu ya mwanamke na mwanaume...na sio mashoga au wasagaji.

Na kuhusu maadili ni kweli yanamong'onyoka kwa sababu ya utandawazi. Media inapositive na negative side...na negative side ndo hiyo so serikali inabidi iwe makini na media

Nehondo unanisikitisha kaka serikali itakuwaje makini wakati yenyewe ndiyo imahalalisha mambo haya tena kwa gharama kubwa za walipa kodi wa nchi hii kwa kuweka redioni kipindi cha kufundisha watu kufanya mapenzi (KUMBWAYA) bila kujali nani anasikiliza na manufaa yake kwa jamii hivi mapenzi yanafundishwa darasani? Mimi ninachoamini na kuelewa mapenzi ni asili na sehemu ya maisha ya mwanadamu(Nature) hivyo hakuna lecture inayotakiwa hapo bali kilichofanyika hapo na huyo mwendawazimu anayeitwa serikali ni ulimbukeni na ujinga wa kunakiri kila ujinga unaofanyika Ulaya. Kwa hiyo naomba uelewe serikali haina msaada juu ya hilo.
 
Whaaaaaaaaaaaatttttt!!! Wema wao watuhusu nini sasa. Khaaa!
Na dhambi zao zinakuhusu nini? si wanafanya wenyewe kwa wenyewe? Kahaba anajilipa mwenyewe? si analipiwa na mtu kama wewe na mimi? Kama unataka tabia hii ikome condemn the buyers, condemn the sellers too. Homosexuals ndio kabisa sioni kwa nini watu wanawasema. they do it among themselves. if you are not gay/lesbian hakuna risk ya kukutana nao kimwili. So what's the hate about?
Bibilia na Qur'an vimesema msihukumu watu. Acheni Mungu mwenyewe awahukumu. Just don't do what they do.
 
Na dhambi zao zinakuhusu nini? si wanafanya wenyewe kwa wenyewe? Kahaba anajilipa mwenyewe? si analipiwa na mtu kama wewe na mimi? Kama unataka tabia hii ikome condemn the buyers, condemn the sellers too. Homosexuals ndio kabisa sioni kwa nini watu wanawasema. they do it among themselves. if you are not gay/lesbian hakuna risk ya kukutana nao kimwili. So what's the hate about?
Bibilia na Qur'an vimesema msihukumu watu. Acheni Mungu mwenyewe awahukumu. Just don't do what they do.



dah haya!
 
Na dhambi zao zinakuhusu nini? si wanafanya wenyewe kwa wenyewe? Kahaba anajilipa mwenyewe? si analipiwa na mtu kama wewe na mimi? Kama unataka tabia hii ikome condemn the buyers, condemn the sellers too. Homosexuals ndio kabisa sioni kwa nini watu wanawasema. they do it among themselves. if you are not gay/lesbian hakuna risk ya kukutana nao kimwili. So what's the hate about?
Bibilia na Qur'an vimesema msihukumu watu. Acheni Mungu mwenyewe awahukumu. Just don't do what they do.
Tukiwaachia hao, basi itabidi tuwaachie na wauza unga maana wanauziana wenyewe kwa wenyewe, halazimishwi mtu, vile vle na wale ambao wameamua kutembea na watoto zao wa kuwazaa au dada/kaka zao, na hata wale ambao wameamua kufanya mapenzi na wanyama... Tusiwahukumu pia, maana ni maamuzi yao binafsi.

Na hata likitokea kundi ambalo lenyewe limeamua kufanya uharifu ndani ya jamii yao yaani wenyewe kwa wenyewe (kama vile wauza madawa wanavyopigania masoko) haina haja kwa jamii kulalamika pia.... Maana tukilalamika tutakuwa tunawahumu.

Ila kumbuka kuwa vitabu vya dini havijakataza kuhukumiana, ni sisi binadamu ndio tunatafuta upenyo wa kufanya maasia na si kweli kwamba vitabu vimekataza... si kweli.
 
Nimekusoma mkuu.
Tukiwaachia hao, basi itabidi tuwaachie na wauza unga maana wanauziana wenyewe kwa wenyewe, halazimishwi mtu, vile vle na wale ambao wameamua kutembea na watoto zao wa kuwazaa au dada/kaka zao, na hata wale ambao wameamua kufanya mapenzi na wanyama... Tusiwahukumu pia, maana ni maamuzi yao binafsi.

Na hata likitokea kundi ambalo lenyewe limeamua kufanya uharifu ndani ya jamii yao yaani wenyewe kwa wenyewe (kama vile wauza madawa wanavyopigania masoko) haina haja kwa jamii kulalamika pia.... Maana tukilalamika tutakuwa tunawahumu.

Ila kumbuka kuwa vitabu vya dini havijakataza kuhukumiana, ni sisi binadamu ndio tunatafuta upenyo wa kufanya maasia na si kweli kwamba vitabu vimekataza... si kweli.
 
Kwa kweli, Qur'an inasema (Suratul Tin, 95) : Alahi Salah bi Ahkamil Hakimil (Isn't God the greater of all the juges?)
Na Bibilia inasema (Matayo 7: 1-5): Do not judge, or you too will be judged.
Nauliza, hivi kuna big sinners and small sinners? If we are all sinners, who gives you the right to condemn the sins commited by other persons? huyajui maisha yao, na hujui ni wema gani wanafanya. we mwenyewe ulipo huja kamilika.
Naomba tuwe waelewa na kabla ya kuhukumu tuanze kwa ushahuri.
Asanteni.

Pal!! I dint get you!!? ... am sure you wont mind to come again!!

Hivi how do you distinguish Mwizi na Homosexual arnt both of them committing mistakes?
 
Tukiwaachia hao, basi itabidi tuwaachie na wauza unga maana wanauziana wenyewe kwa wenyewe, halazimishwi mtu, vile vle na wale ambao wameamua kutembea na watoto zao wa kuwazaa au dada/kaka zao, na hata wale ambao wameamua kufanya mapenzi na wanyama... Tusiwahukumu pia, maana ni maamuzi yao binafsi.Na hata likitokea kundi ambalo lenyewe limeamua kufanya uharifu ndani ya jamii yao yaani wenyewe kwa wenyewe (kama vile wauza madawa wanavyopigania masoko) haina haja kwa jamii kulalamika pia.... Maana tukilalamika tutakuwa tunawahumu.Ila kumbuka kuwa vitabu vya dini havijakataza kuhukumiana, ni sisi binadamu ndio tunatafuta upenyo wa kufanya maasia na si kweli kwamba vitabu vimekataza... si kweli.
Nafikiri huu mtizamo ni wa kuzingatiwa!! NA Je kama ni mwanao would you still stand on don't judge? Kwa kuwa mzazi hauko kwneye mambo hayo mwnanao aachiwe kutekeleza uhuru wake ? Naona kuna jambo halijakaa vema!!
 
Pal!! I dint get you!!? ... am sure you wont mind to come again!!

Hivi how do you distinguish Mwizi na Homosexual arnt both of them committing mistakes?
Kwenye vitabu vya dini walawiti Mwenyezi Mungu aliwaangamiza walawiti na wazinifu... Watenda dhambi wengine walipata hukumu tufauti.

Alafu ni vipi mtu aseme kuwa tusihukumu, nashindwa kuelewa hapa, mtu kama anafanya liwati (ushoga) asiambie eti tu anasaidia jamii yake kwa pesa zake...?

Mbona hatuwaachi ndugu zetu wanao tuhusu wakaharibika kwa kuchaguwa kuwa Walevi wa unga... Kiufupi kilicho katazwa kina madhara... si kwa mtu binafsi tu, bali kwa jamii nzima.
 
Kwenye vitabu vya dini walawiti Mwenyezi Mungu aliwaangamiza walawiti na wazinifu... Watenda dhambi wengine walipata hukumu tufauti.

Alafu ni vipi mtu aseme kuwa tusihukumu, nashindwa kuelewa hapa, mtu kama anafanya liwati (ushoga) asiambie eti tu anasaidia jamii yake kwa pesa zake...?

Mbona hatuwaachi ndugu zetu wanao tuhusu wakaharibika kwa kuchaguwa kuwa Walevi wa unga... Kiufupi kilicho katazwa kina madhara... si kwa mtu binafsi tu, bali kwa jamii nzima.

Ndio maana kuna wakati nafikiri labada sijui maana ya kuhukumu au kuitofautisha na kuchukua hatua juu ya jambo la muhimu. Mtu akaniibia na ikawa dhahiri kabisa kaniibia ... nikumabia wewe ni mwizi hivyo hilo ni kosa la kuhukumu? Au ningetakiwa nihusianeje naye ili nisiwe nimehukumu?

Mtu anapokuwa na mahusiano yasiyosahihi kibinaadamu mwizi, muonevu, asiyetenda haki, anayedanganya watoto wadogo na kuwahujumu kingono, asiyeheshimu ndoa za watu wengine, homosexual .. ni kimtamkia kosa lake nimefanya kosa la kuhukumu?
 
Tukiwaachia hao, basi itabidi tuwaachie na wauza unga maana wanauziana wenyewe kwa wenyewe, halazimishwi mtu, vile vle na wale ambao wameamua kutembea na watoto zao wa kuwazaa au dada/kaka zao, na hata wale ambao wameamua kufanya mapenzi na wanyama... Tusiwahukumu pia, maana ni maamuzi yao binafsi.

Na hata likitokea kundi ambalo lenyewe limeamua kufanya uharifu ndani ya jamii yao yaani wenyewe kwa wenyewe (kama vile wauza madawa wanavyopigania masoko) haina haja kwa jamii kulalamika pia.... Maana tukilalamika tutakuwa tunawahumu..
Swadakta Mkuu!
Ila tusiishie hapa tu,maana hili sasa ni janga la kitaifa! tuna "supastaa" anayekuja hadharani na kusema yaye ni shoga, akipiga picha kuthibitisha ushoga wake ilhali ya kuwa kuna watoto wengi tu wa taifa hili wanaomuona kuwa yeye ni role model wao! tena kesho au keshokutwa atashinda tuzo hii na ile, hivi ni picha gani wanayopewa watoto wa Kijamii?!....hii inamuondolea mtoto ile wanayoiita "sense of guilt" na kuona haka kamchezo ni OK tu na kanaweza "kukutoa" vilevile!
Ninaviomba vyombo vya habari, wizara ya ustawi wa jamii (kama ipo na inahusika na haya masuala) wazazi na wanajamii kwa ujumla kuukemea na kufanya kila liwezekanalo kuuzima uovu huu ili watoto wa taifa hili wasalimike na ushari wa hawa watu.
 
Na dhambi zao zinakuhusu nini? si wanafanya wenyewe kwa wenyewe? Kahaba anajilipa mwenyewe? si analipiwa na mtu kama wewe na mimi? Kama unataka tabia hii ikome condemn the buyers, condemn the sellers too. Homosexuals ndio kabisa sioni kwa nini watu wanawasema. they do it among themselves. if you are not gay/lesbian hakuna risk ya kukutana nao kimwili. So what's the hate about?
Bibilia na Qur'an vimesema msihukumu watu. Acheni Mungu mwenyewe awahukumu. Just don't do what they do.
Mwenyezi Mungu ktk Quran anasema Yeye ni Hakimu wa Mahakimu. Uamuzi wake ni bora kabisa. Watu kama hawa waliangamizwa wakati wa Nabii Luth. Hiyo ndo benchmark. Hukumu ya Mwizi ni kukatwa mkono, lakini Mahakimu wanawafunga jela. Kahaba ni kupigwa mawe, lakini wanapewa leseni !
 
Picha hii iko gazeti la Mwananchi, leo tarehe 25.7.2012. Najiluliza ni mmonyoko wa maadili au nidhamu mbovu kuongea wakati ameweka mikono mifukoni. Jadili.
 

Attachments

  • ccccccccccccccccccccccc.jpg
    ccccccccccccccccccccccc.jpg
    152.1 KB · Views: 522
Kizazi kipya, hakuna hatari yoyote, tena amesimama kabisa, inabidi apigiwe na makofi
 
wengine huwa ni moja ya sehemu yao ya kuwin confidence maana akitoa tu hiyo mikono hapo confidence yote kwaheri. ni mtazamo tu
 
Back
Top Bottom