Kupotea taratibu kwa alama ya Kanisa Katoliki katika kupinga dhuluma

Katika Kanisa Katoliki kuna kitu kinaitwa Hirakia. Hao Walei hawana maamuzi yoyote. Wao hushauri tu. Maamuzi yooote katika Kanisa hufanywa na Hirakia....
Amepeleke maoni yake yapokelewe kama ushauri?
 
Makanisa yapo mengi, sio lazima uende RC
 
RC limekuwa ovyo kabisa..
Mimi ni muumini wake lakini lazima niseme ukweli RC limepotea kabisa na Viongozi wetu wa Kanisa hapa Tz wamekuwa ovyo kabisa.

Mkuu wewe sio RC. Wewe Ni CHadema. RC kadi hasomi barua za kiuchungaji za kanisa lake. Wewe utakuwa ushatapikwa. Vuguvugu. RC sio chama cha Siasa. Wasomi wenye akili na busara zao. Wewe nenda kwa Bagonza. Anakufaa kwa aina ya ukristu wako.
 
Mkuu pole kama una undugu na Pengo lakini ukweli lazima usemwe

Mkuu Wewe Ni MPUMBAVU. Anakuelimisha unazidi tu. Hakuna Siri katika majukumu ya watumishi wa kanisa. Go and read and stop advertising your stupidity and nonsenses.
 
Labda wamenunuliwa.

Kwa sababu ya ukubwa wake, RC haimo miongoni mwa madhehebu yanayoweza kutishiwa 'kufutwa' na watawala dhalimu wasiotaka kukosolewa.

Ndiyo maana ni vigumu kuelewa sababu ya wao kunyamazia maovu makubwa ya watawala
 
Dawa yao kupunguza sadaka tu
 
Hao 'Maji Maji warriors ndio wanapendwa kweli kweli' nasikia ndio rahisi kuwaburuza achilia mbali kuwatawala.
 
Mleta hoja shida yako kubwa unacho moyoni unachotaka kanisa liseme na unao upande ambao unataka kanisa liuunge mkono.
 
Mimi siyo mweupe kwenye muundo wa Kanisa, majukumu ya Kanisa, imani ya Kikristo na msimamo wa jumla wa Kanisa Katoliki katika masuala mbalimbali.

Dini yangu kubwa, upande wangu mkubwa na chama changu kikubwa ni HAKI.

Rejea hotuba ya Papa Francis alipofanya misa kubwa kule Brazili kwenye viunga vya jiji la Sao Paulo, kwenye mitaa ya watu maskini, "Kanisa ni lazima lisimame na watu maskini na watu wanaoonewa badala ya kujifunga na watawala". Huo ndio ujumbe wa Mama Kanisa. Kanisa Katoliki la Tanzania tunauishi vipi ujumbe huu?

Kanisa halitakiwi kutafuta kumfurahisha mtu bali lisimame katika kweli ya Mungu. Kanisa halitakiwi kusimama na chama chochote wala halitakiwi kutafuta chama rafiki maana kanisa siyo chama, bali lisimame katika ukweli.
 
Umeshawekewa ujumbe wa kanisa Katoliki juu kule ambao umekiri ulikuwa huufahamu, lakini nakushangaa bado unapiga kelele tu, au ndio vile hutaki uzi wako ukose wachangiaji?

Hii tabia mnayoendekeza kulaumu Katoliki kwa kila jambo kama vile nyie hamna midomo ya kujisemea na kuwasemea hao mnaoona wanaonewa itawadumaza akili, haki za watu zitazidi kuporwa huku nyie mmezubaa tu kulisubiri Kanisa Katoliki.

Msipojinasua kwenye hili tope la fikra mlilokwama, huku mkijiita GT, CCM itatawala milele, amka badala ya kulaumu kila siku anzeni kudai haki zenu privately, au kwa makundi, mjue namna mtakavyo organise ili mfikie malengo, sio kulia lia kila siku kwa Katoliki, lisingekuwepo mngefanyaje?
 
Wote hawa hakuna mwenye nafuu, ukiona wamekuwa wakali jua maslahi yao yameguswa
Kweli, mfano Askofu shoo kawa mkali Sana baada ya mfadhili wake mtoa sadaka nyingi kuwekwa mahabusu.
 
Ila kwa sasa sababu ya Rais wa Nchi hii ni Muislam utalisikia kanisa likikemea na kutoa waraka kama upendavyo
Kwanini waislam wanategemea kanisa kutoa waraka? Ina maana rais akiwa muislam jukumu la kutoa nyaraka haliwahusu? Ni jukumu la Nani maana kanisa mnataka wahusika Mara TEC, Pengo nk. Kwenye uislam Ni jukumu la Nani?
 
Fafanua unamaana gani ya majimaji fighters? Waliishia wapi hao katoliki na corona yao? Askofu wa Rulenge ngara bado kafunga kanisa? Mnafahamu maana Diversity na differences katika kuishi kwetu. Msimamo wa kusimama na Mungu kwenye corona ni kichaa peke yake ndio atanena. Hata Kagame na Museven watashindwa tu na ubabe wa lockdown.
 
Tangu kale, tangu enzi za manabii, Kanisa Katoliki lilisimama katika ukweli, lilifundisha, lilikemea na kuwaonya watawala dhidi ya dhuluma. Mifano ipo mingi.
Kwa mwanzo huu, ni nani ataendea kusoma bandiko lako? Kanisa katoliki halikuwepo enzi za manabii.

Kama unaanza na uongo, basi yote yanayofuata ni uongo na uchochezi.
 
Ingefaa uchungaji wa kondoo uendane na kudai haki zao za kisiasa pia ili wasidhulumiwe.
 
Serikali haina dini.

Serikali inanyonga
Dini inasamehe

Na ikitokea kanisa limekemea hapo misuguano inaanza
 
Amepeleke maoni yake yapokelewe kama ushauri?
Kiukweli, ndani ya kanisa katoliki kuna misigano. Ndio maana hata kipindi ule waraka maarufu wa "Ujumbe wa Kwaresima" ambao Kanisa Katoliki lilitoa makaripio kwa serikali katika maeneo ya Demokrasia, uhuru wa kujieleza na utawala bora, Kardinali Pengo, wakati huo akiwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, alitangaza kujiweka kando na waraka huo. Tunakumbuka kwamba matokeo mojawapo ni kutimuliwa kwa Katibu Mkuu wa TEC wakati huo, Raymond Sabas, na kutangazwa siyo raia.

Ni kweli kwamba, kama asemavyo Tundu Lissu, Makanisa ya Tanzania kwa ujumla yamejitenga na mapambano ya kudai haki na Uhuru wa kujieleza. Mara chache Kanisa Katoliki lilipojikakamua, KKKT nao wamewaunga mkono, hasa kupitia Askofu wao mkuu Shoo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…