Nani anayechukia Uislamu? I am sure unajua kuwa uwepo wa Al Shabaab, Al Qaeda, Islamic State, Boko Haram, Hamas, Hezbollah, etc ni kwa ajili ya kujaribu kuuangamiza Ukristo! Hebu chukua ushauri huu ambao Mwalimu wa Torati aliutoa wakati Wakristo walipotaka kuangamizwa na Wayahudi:
Matendo ya Mitume 5
"34 Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo,
35 akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa.
36 Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu.
37 Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika.
38 Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa,
39 lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu."
Kuna vitabu viwili vilivyoandikwa na Wakristo wenyewe vinavyothibitisha kuwa Wakristo wametumia nyadhifa zao katika serikali kuuhujumu Uislamu na Waislamu.
Jan P van Bergen katika kitabu chake,
Development and Religion in Tanzania, (1981) ametoboa siri kuhusu uadui aliokuwa nao Nyerere dhidi ya Uislamu na Waislamu.
Kitabu kinaeleza kwa ufasaha jinsi Nyerere wakati alipokuwa madarakani alivyokuwa akifanya mikutano ya siri na viongozi wa Kanisa kuweka mikakati ya kuupa nguvu Ukristo. Katika mikutano hiyo Nyerere aliwahakikishia viongozi wa Kanisa kuwa anaaunga mkono Ukristo.
Kitabu hicho kinaeleza jinsi Nyerere alivyotimiza ahadi yake hiyo kwa Kanisa kwa kuhakikisha kuwa anawapa Wakristo nafasi za juu katika serikali na chama.
Kitabu hiki kilikuwa kikiuzwa
Catholic Bookshop, Dar es Salaam. Lakini ilipokuja kudhihirikia Kanisa kuwa kitabu hiki kilikuwa kinatoa habari nyeti na siri za Kanisa kuhusu njama dhidi ya Waislam, kwa haraka sana kikaacha kuuzwa. Hadi hivi sasa kitabu hicho ni marufuku kuletwa tena Tanzania.
Kitabu hiki kilikuwa kikiuzwa
Catholic Bookshop, Dar es Salaam. Lakini ilipokuja kudhihirikia Kanisa kuwa kitabu hiki kilikuwa kinatoa habari nyeti na siri za Kanisa kuhusu njama dhidi ya Waislam, kwa haraka sana kikaacha kuuzwa. Hadi hivi sasa kitabu hicho ni marufuku kuletwa tena Tanzania.
Kitabu cha pili ni cha Dr John C. Sivalon,
Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985 (1992).
Kitabu hiki kinaeleza njama ndani ya serikali kuuhujumu Uislam.
Sivalon anafichua kuwa kuanzia mwaka 1961 baada ya Tanganyika kupata uhuru, Kanisa lilikuwa na hofu mbili. Hofu ya kwanza ilikuwa umoja wa madhehebu za Kiislamu kati ya Sunni, Bohora, Ismailia na Ithnasheri.
Hofu ya pili ilikuwa kuhamishwa kwa makao makuu ya EAMWS kutoka Mombasa kuja Dar es Salaam. Kanisa lilikuwa linahofu kuwa mali walizokuwanazo Waasia Waislamu zikitiwa katika shughuli za Waislamu ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uwanja wa siasa zitaathiri maslahi ya Ukatoliki katika Afrika ya Mashariki. Kwa ajili hii Kanisa likatanganza kuwa Uislamu ni adui wake na ikaanza mikakati ya hujma dhidi ya Uislamu ili kuudhoofisha.
Kuna kazi mbili zilizoandikwa na Waislamu kuhusu uhusiano baina ya serikali na Waislamu. Kazi ya kwanza ni tasnifu ya Kiwanuka,
'The Politics of Islam in Bukoba District' (1973); kazi ya pili ni makala ya utafiti 'Islam and Politics in Tanzania' (1989)
Ilikuwa baada ya kusoma tasnifu ya Kiwanuka na kuona jinsi ukweli wa kuvunjwa kwa EAMWS kulivyopoteshwa ndipo kama Muislamu na kama ada ya Uislamu inavyodai kuwa pande mbili za mgogoro zote lazima zisikilizwe, ndipo nilipoamua kufanya utafiti na kuandika tatizo lile kwa mtazamo wa Waislamu. Ukweli ambao kwa miongo miwili ulizuiwa usifahamike kwa Waislamu.
Kiwanuka anadai na kuafiki kuwa Nyerere alikuwa na haki ya kutumia vyombo vya dola dhidi ya Waislam kwa kuwa kama asingefanya hivyo nchi ingekuwa na mamlaka mbili, yaani ya Waislam na ya serikali. Kwa ajili hii aliamua kuivunja EAMWS ili 'kulinda umoja wa kitaifa'.
Halikadhalika ipo 'Kwikima Report' (1968) ambayo imeeleza kwa ufasaha tatizo la EAMWS, chanzo chake na mchango wa serikali katika kuhujumu umoja wa Waislamu. Taarifa hii inafaa kutumika leo kama dira ya kuelewa tatizo la Waislamu wa Tanzania kama ilivyokuwa wakati ule ilipotolewa kwa mara ya kwanza.
Taarifa ya Kwikima inaeleza jinsi TANU, serikali na Waislam wachache katika TANU walivyodanganyika kudhani kuwa katika kuisaidia serikali kuivunja nguvu EAMWS walikuwa wanatimiza uzalendo na maslahi ya taifa.
Rejea hizi tano ni muhimu kwa wanafunzi wa historia ya siasa Tanzania; na kwa mtafiti yeyote anaetaka kujua chanzo cha chuki baina ya Waislam na serikali na chanzo cha hisia kali za kidini zinazoikumba nchi yetu kuanzia miaka ya 1980.
Rejea zote hizo za vitabu, makala za utafiti na taarifa mbalimbali, ingawa zimeandikwa na waandishi tofauti na kwa muelekeo tofauti zote hizi zinadhihirisha kitu kimoja kuwepo kwa njama zinazoendelea kwa zaidi ya karne moja dhidi ya Uislamu na Waislamu, kwanza zilikuwa zikifanywa na wakoloni walioitawala Tanganyika na sasa zinafanywa na Wakristo wananchi kuhakikisha kuwa Uislamu haupati nguvu. Kama hali ndiyo hii vipi Uislamu hadi leo bado upo Tanzania na unazidi kupata nguvu kila kuchao?