Kurasa tatu za Tamko rasmi la Kanisa Katoliki kuhusu kuruhusu ubatizo kwa wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja

Nimeandika kichokozi tu. Siamini kwenye kutenga mashoga. Hawachagui kua hivyo.
 
Sisi sote tunaoishi wakati wa sheria ya Kristo; Kristo Yesu ametufundisha jinsi mambo yalivyo na yanavyotakiwa kuwa. Ametufundisha vilevile tunavyotakiwa kutenda na kuwatendea ndugu zetu. Kwa sababu hii, Kanisa ni kwa ajili ya watu wote: wenye dhambi na wasio na dhambi.

Kwetu sisi, ambao bado tupo duniani, Kanisa ni mahali pa kujitakasa au kuongoka. Ni mahali pa kujifunza ili kubadilika tabia kuwa watu wema, watakatifu - mpango wa Mungu.

Kristo hakuweka Kanisa ili liwe kwa ajili ya watu wema, wasio na dhambi. Kwa kweli lengo la Kanisa ni kuongoa na kutakasa. Kwa hiyo ni kwa ajili ya watu wote.

Kristo aliwaagiza aliowaachia mamlaka kuwafundishe watu wote duniani. Hii maana yake Kanisa linawakaribisha na ni kwa ajili ya watu wote na hali zao zote.

Kanisa kwa lenyewe halitendi dhambi, ni takatifu. Watu ndio wanaotenda dhambi. Mungu kupitia Mwanae wa pekee Yesu Kristo anawaalika watu wote na kipee kabisa wadhambi. Mungu mwenyewe anasema, katika biblia kwamba, "hakuja dunia kwa ajili ya watu wema bali wakosefu. Anaendelea anasema, wenye afya hawahitaji daktari ila wagonjwa".

Tunaweza kutokukubaliana kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwa na elimu ya vitu na uelewa wa mambo.

Kanisa kwa kuwapokea wadhambi halihalalishi uovu. Yesu aliwaeleza wayahudi wa nyakati zake waliotaka kumpiga mawe na kumwua mwanamke mzinzi; "asiye na dhambi na awe kwanza kurusha jiwe juu mwanamke huyu".
 
mimi kitambo sana nishakimbia sitaki hata kuwasikia
 
Mungu ni wetu sote.

Katoliki ingeruhusu hayo, kesho tu hapo ungeona picha za transgenders waliosimamia ndoa, ubatizo na vyote vilivyoainishwa hapo.
Na huu uzi ungesindikizwa na picha murua kabisa ya vidume vikiwa pamoja vimesimamia ndoa/ubatizo..

KANISA MOJA, TAKATIFU, LA MITUME.

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.

TUMSIFU YESU KRISTO.....
MILELE, AMINA.
 
Kwa hiyo mungu ndiye anayepanga huo ujinga wa mashoga lol
 
Endeleeni kusali ili mje muende mbinguni,mimi huo upuuzi uitwao dini ni mbali kabisa na mimi.......eti Mungu akuumbe na akuchome moto tena
Utahukumiwa kutokana na makosa yako mfano wewe mwenyewe hivi mzazi aliyekuzaa hawezi kukuadhibu hata kama unafanya makosa au wewe mwenyewe kama mzazi mwanao akikosea utamwacha tu bila kumuadhibu eti kwa sababu umemzaa?
 

Sasa hapo mgalatia unazidi kupuyanga,waachane na dini wamfuate yesu?kwani yesu anahubiri dini Gani?

Usitafute kichaka Cha kujifichia, mambo yameshaharibika Huko
 
Mmewakataza hao maaskofu kuoa na hao masister kuolewa,ambao ni viongozi wenu,mnategemea nini?? kwanin wasiwe machoko??na haapo baado,yaani mpaka msemeeee....
 
Wewe utakubali mwanaume aliyemuoa mwanaume mwenzie awe baba wa ubatizo wa watoto wako?

Kama hilo huwezi na moyo unagoma, basi jua kuna tatizo kwenye maamuzi ya sasa ya kanisa!
 
Sasa hapo mgalatia unazidi kupuyanga,waachane na dini wamfuate yesu?kwani yesu anahubiri dini Gani?

Usitafute kichaka Cha kujifichia, mambo yameshaharibika Huko
Yesu hahubiri dini. Yesu anajihubiri mwenyewe. Yesu anahubiri uzima wa milele unaopatikana ndani yake, full stop.
 
Hayo ni mawazo yako na hiyo rc yenu, walicho kipigania rc ni hiki wanacho kifanya leo ambacho ni mbali kabisa na ukristo, Zima fegi ukae kwa kutulia

Yesu kristo alikula na kunywa pamoja na makahaba unazungumziaje hili?
 
Hayo ni mawazo yako na hiyo rc yenu, walicho kipigania rc ni hiki wanacho kifanya leo ambacho ni mbali kabisa na ukristo, Zima fegi ukae kwa kutulia

Rc itabaki kuwa kanisa mama la ukristo duniani,hii ibaki kuwa heshima yake kuu. Kanisa limeulinda na kuupigania ukristo hadi leo hii wewe umezaliwa ukawa mkristo,hakuna uchafu wowote ni vile kanisa limeamua kufungua mikono kupokea wenye dhambi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…