Kurekebisha mkataba wa DP World, hongera Rais Samia

Imagine China na Oman investment ya $10 billion, Bagamoyo port; serikali ilipiga hesabu za ROI on investment. Based on potential future income the ‘optimistic return on investment’ was 15 years and worst case scenario miaka 25.

Serikali ikataka kuwapa mkataba wa 33 years only, hiyo waliamini inatosha kurudisha hela yao na kuvuna faida.

Leo mnaenda wapa watu port kwa miaka 30 kwa uwekezaji usiofika hata $1 billioni moja.

Shamba la bibi.

Shida aikuwa kwenye IGA watu mmeelezwa wee kile ni kitu gani; amtaki kuelewa mnajazana ujinga.

It’s from those false premises zenu za IGA ndio mwarabu kawatandika kumbe mnafikiria miaka 100 wakati angepewa miaka 20 sehemu nyingine kwa hela hiyo bahati.

Kumbe mnafikiria kuchukua ubia wakati bandari yenu wenyewe yeye alikuwa apewe lease tu; kwenye mapato nyie mnauwezo wa kumpangia achukue kiasi gani kwenye kurudisha hela yake.

Sijawahi ona nchi ya ovyo kama Tanzania.

Shida aikuwa kwenye IGA, shida ilikuwa inakuja kwenye lease agreements na nyie mlishawatengenezea waarabu bargaining chip kwa kutumia uongo (ujinga wenu wenyewe) ndio wameingia nao mezani na kuwatandika.

What a pity
 
HONGERA MWABUKUSI,TEC NA WOTE WALIOBWEKEA WAOVU
 
Mwabukusi bado yupo
 
Mfano wa kuigwa na marais wajao.
Sikilizeni hoja za wananchi.
 
Mkuu Jidu, Jidu La Mabambasi , sisi ma Tomaso tupo tunasubiri kuona huo mkataba ili kujiridhisha madudu yote yameondolewa, kwa sababu kuna madudu mengine yalikuwa hayaondosheki unless kama ile IGA ilifanyiwa marekebisho kuondoa illegality.

P.
 
Mkuu Jidu, Jidu La Mabambasi , sisi ma Tomaso tupo tunasubiri kuona huo mkataba ili kujiridhisha madudu yote yameondolewa, kwa sababu kuna madudu mengine yalikuwa hayaondosheki unless kama ile IGA ilifanyiwa marekebisho kuondoa illegality.

P.
Ni vema mkataba ukawa tested mahakamani kama vigezo vyote vimezingatiwa.
 
Limeibuka kundi la watu wanaotaka kujipatia sifa katika masuala ambayo jamii yetu haiyafahamu vyema.

IGA ni kanuni tu ndio maana baada ya kuvuja mitandaoni DP World hawakujihangaisha na nani amevujisha, ingevuja mikataba hii iliyosainiwa Jumapili Asubuhi pale Dodoma ndio tungeweza kushtakiwa kwa kuuza siri za mwekezaji.

IGA imeshikiwa bango kwa sababu uelewa wetu wa kijamii ni mdogo, ni mkataba usio na uzito sana kulinganisha na ile ya kibiashara iliyoisainiwa.

Kwanini biashara hii haikutangazwa tender yake kama zilivyotangazwa tender nyingine kuhusu uendeshaji wa bandari?. Ni kwa sababu ya ukubwa wa mradi wenyewe haswa hizo mali zilizopo huko DRC na Rwanda, kutangaza tender kwa taratibu za kimanunuzi ingekuwa ni sawa na kumpoteza mwekezaji mwenyewe.

Kuna ukubwa na unyeti wa uwekezaji unaotofautiana kati ya kampuni moja hadi nyingine, huwa ni kigezo cha taratibu za kimanunuzi kutofuatwa.

Uwekezaji wa DP World pale bandarini huwezi kuulinganisha na ule wa mwendeshaji mwingine atakayepatikana kupitia tender zilizotangazwa.

DP World anafanya end to end logistics kwa maana ya kuchukua mzigo kule DRC kuuleta bandarini na kuupeleka kwenye bandari za ughaibuni. Huo ni uwekezaji mkubwa tofauti na hao waendeshaji wengine wanaotafutwa.
 
Unajikosha tu. Mkataba na vipengele vyake ni uleule na wala haujabadilishwa. Mliamua kuupinga kwa sababu zenu binafsi na mafisadi wa bandari. Sasa mmeona Serikali imewakazia eti mnajidai vipengele vimebadilishwa.
 
Ni kweli kabisa, kuyaweka mambo peupe imesaidia sana kurekebisha kasoro.

..yale madudu yaliyopitishwa bungeni yakatenguliwe na kufutwa.

..kinyume cha hapa kuna ulazima wa wanaharakati kuendeleza mapambano mahakamani.

..pia mkataba mpya ulisainiwa uweke wazi wananchi wajue vipengele vyake vyote.

..utamaduni wa kusomewa na kusimuliwa mikataba na watu wa serikali imetugharimu pakubwa Watanzania.

..jambo hili lisifanywe kienyeji-enyeji, au kwa mtindo wa funika kombe...
 
Unajikosha tu. Mkataba na vipengele vyake ni uleule na wala haujabadilishwa. Mliamua kuupinga kwa sababu zenu binafsi na mafisadi wa bandari. Sasa mmeona Serikali imewakazia eti mnajidai vipengele vimebadilishwa.
Kwa hiyo kipengele cha muda indefinately hakijaondolewa?
Au tuseme kipengele cha muda wa miaka 30 kilichowekwa sasa ni uongo mtupu?
 
Sema umependa kurudi kwa Makonda. Acha kuzunguka. Ukabila tu.
 
Hapa naona kama kuna watu wanajitekenya na kujichekesha wenyewe.

Sijaona mkataba uliorekebishwa hata mmoja. IGA ni ile ile, mikataba iliyosainiwa, mmmoja ni HGA amao IGA ilisema ndiyo inabidi iwepo, nini kilichobadilika hapo?

Mikataba wili ni "concession Agreements', ambao mmoja ni wa utendaji kazi wakishirikiana na TPA, kwenye IGA ipo hiyo, kilichobadilika ni nini? Wa pili ni ukodishwaji wa eneo la bandari. Nini kilichobadilika hapo?

Mikataba iliyosainiwa yote mitatu ni mipya kabisa, haijawahi kuonekana wala haijawahi kuwepo na hatuna haki ya kuiona kabisa tusiohusika nayo. labda ivujishwe, nalo ni kosa la jinai kisheria, linaweza kuwa uhujumu uchumi au hata usaliti. Uhalali wa kuiona tutaupata ifike bungeni kwanza. Na si rahisi, hususan ile ya "concession agrreements", hiyo ni ngumu sana kuwekwa "public. Hata mlie machozi ya damu.

Hii mikataba ilielezwa tokea awali na Mbarawa na watu wengine kibao, mpaka hapa JF tumejadili sana, kuwa itakuja.

Tusidanganyane, IGA haaijabadilishwa na wala haikufanyiwa marekebisho yoyote. Labda bunge lingetaka hivyo, lakini bunge liliipitisha IGA kama ilivyo.

Pia niwakumbushe, hata hii mikataba mipya imesainiwa ndani ya muda ulioainishwa kwenye IGA.

Kuna watu walikuwa walikuwa na hamu kubwa muda huu upite, waliwachwa wanaishi kwa matumaini. Mama Samia anajuwa kutengeza movie za "syuspense". Tumpe mauwa yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…