Kurudisha mabinti waliopata mimba shuleni ni kunyoosha mikono juu na kulikabidhi taifa letu kwa wakoloni mambo leo kwa ajili ya mkopo wa bil 600

Hao washenzi ndio wameharibu watoto wa kike ulaya wamekuwa na viburi hata kuolewa hawawezi sababu ya kuwakumbatia kwenye kila upumbavu wanaoufanya!
 
Nakubaliana nawewe Mkuu..

Hawa waschana wadogo, wanapeana mimba na Wanafunzi wenzao .


Mabazazi yasokua na akili pia huchangia.
 
Hivi unadhani kipimo cha zinaa ni mimba peke yake? Unadhani hao ambao hawapati mimba hawatumii njia mbadala kujamiana na boifrendi zao? Unadhani huko kulawitiana watoto wa kuume na mabinti kusagana na kujiingiza vitu vya ajabu vimeanza leo? Hayo mambo yako miaka yote.
Hayo mafunzo kuhusu ngono za utotoni na unataka wapewe wale tu walioisha "haribika" lakini sio wale unaoamini bado ni mabikira? Kama watu wazima wanakaa nyumbani miezi mitatu tu na baada ya hapo wanarudi kazini, kwa nini mabinti waliojifungua wasitendewe hivyo hivyo? Ni ujinga kuamini kuwa ukiwaondoa wenye uja uzito basi waliobaki wataacha kudadisi mambo ya "kiutu uzima" wakiwa na rafiki zao shuleni na nje ya shule. Hasa hii enzi ya WhatsApp.
Experience inaonyesha kuwa nchi zote ambazo zimeruhusu hali hii ( Msumbiji n.k.) uzazi wa utotoni umepungua. Badala ya kuwanyanyapa inabidi jamii nzima ( sio kuwaachia walimu peke yao) inatakiwa kutoa elimu ya mambo ya uzazi kwa watoto wao wote bila kujali jinsia. Wavulana wanatakiwa wafunzwe kuheshimu wasichana na kuachana na dhana kuwa ujanja ni kutembea na visichana vingi iwezekanavyo. Wasichana nao hivyo hivyo na wapewe uwezo wa kuwashtaki wale wote wanaowatendea vitendo hivyo bila wao kuathirika.
Tuache unafiki. Hatuwezi kuwazuia watoto wetu kufanya vitendo hivi kwa vitisho na adhabu peke yake. Tuwapende watoto wetu pamoja na mapungufu yao yote.

Amandla...
 
Kabisa. Wenye kujali maisha yao tuna kazi ya ziada kwa kweli. Mungu azidi kututia nguvu.
Tuendelee kuwafunza, kuwapigania, na kuwatetea kwa nguvu zote.


Na unajua kwann hilo rika ndo linaongoza maambukiz ukiachana na mimba??


KWA SABABU KUNA MIBAZAZI MIGONJWA, ISHAJICHOKEA, SASA INADEAL NA VITOTO .
 
Tuendelee kuwafunza, kuwapigania, na kuwatetea kwa nguvu zote.


Na unajua kwann hilo rika ndo linaongoza maambukiz ukiachana na mimba??


KWA SABABU KUNA MIBAZAZI MIGONJWA, ISHAJICHOKEA, SASA INADEAL NA VITOTO .
Aisee sikujua hili. So sad!
 
Hiyo mikopo hiyo ndio imefanya uganda wakaachia uwanja wa ndege kwa wachina. Yajayo yanafurahisha sana sijui kama tuko tayar
 
Jambo lolote lina matokeo chanya na hasi. Unachojarib kutetea ni eneo lenye hasi kubwa sn,aidha imekutokea kwa bahat mbaya au umetii maksud ulonayo na pengne yenye mlengo wa kupingana na msimamo wa serikali.
Hapa umetaja ujauzito na uvutaji wa bangi pekee. Lakin umejisahaulisha km sabb za kukatiza masomo zipo nying tu. Nadhan nchi hii tumewah kuwa na kiongoz mkuu kinchi ambaye alipata tatzo na kufukuzwa shule aliyoanzia sekondar,mzazi wake akatumia nafuu hii iliyotangazwa wakt huu kumpeleka shule nyingne na akaendelea na masomo kwa mafanikio na hatmaye kuja kuwa mkuu wa inchi yetu. Kwa uelewa na mtazamo wako huyo kiongoz alikuwa mvuta bangi🤣🤣🤣
Au bas ni kwel (kwa mtazamo wako) kuwa nchi hii imepata kuptia mikonon mwa mvuta bangi?? Mwanadamu yeyte huptia kipind cha kuteleza na kufanya makosa na baada ya hapo majuto anayopitia huwa ni msaada wake! Na hivyo kuhtaji nafas ya pili ili arekebishe makosa yake.
"Ndugu,ikiwa hatuwez kuwazuia msiwarubuni hao mabinti (nawe ukiwemo),Basi ni sahh tuwape fursa ya pili ya kurekebisha makosa yao!
 
Watanzania ni watu wa ajabu sana. Wanawashupalia wanafunzi wa kike kupata uja uzito wakati wengi wameoa wasio na bikira. Na wengi wameolewa wakiwa hawana bikira.

Zamani siku ya harusi ilikuwa kitanda cha maharisi kinatandikwa shaka nyeupe na baada ya shughuli inaonyeshwa kwa jamii ikiwa na damu. Huo mchezo umeisha kimya kimya.

Basi na nyie ulizaneni hizo bikira zilipotea lini ndio mtajua kuwa wanaopata uja uzito ni wachache sana ukilinganisha na wanaojihusisha na haya mambo. Acheni kuwatilia kiwingu watoto wa kike.

Amandla...
 
Obama amesema wazi kuwa alipokuwa shule alikuwa mvuta bangi mzuri. Clinton amevuta bangi. Kamala Harris hivyo hivyo.
Wangapi wanaweza kujilinganisha mafanikio na hawa wavuta bangi?

Amandla...
 
Obama amesema wazi kuwa alipokuwa shule alikuwa mvuta bangi mzuri. Clinton amevuta bangi. Kamala Harris hivyo hivyo.
Wangapi wanaweza kujilinganisha mafanikio na hawa wavuta bangi?

Amandla...
Kuna watu ukisikia kauli zao juu ya jambo hili unabaki na butwaa tu!
Hivi mtu mwenye akili timamu unaweza ushangae watoto kupewa nafas ya kuendelea na masomo kweli jaman🤭🤭🤭🤭
Kama ni chuki zao za kisiasa,watafute nyuz za kuchafuana lkn siyo hili,unless uwe ni mwanaume maksai.
Yaan Mama kadhihirisha uchungu wa mwana anaujua zaidi ni mama.
 
Ukifanya ngono na binti wa chini ya miaka 18 unakuwa umebaka (statutory rape) kf 130-131 kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya 2019.

Hivyo hawa watoto wanaokuwa wamebakwa wanahitaji kupewa haki ya elimu kwa gharama yeyote.



YESU NI MWOKOZI
 
rasilimali gani? magufuli mwenyewe alijaribu, akaishia kuvamia account za watu benki.
 
kwani watu wa dizain hiyo mbona unaishi nao wengi mitaani, na huja vuta bangi wala mimba hujapewa,

kama toto lako ni malaya litafanya umalaya tu, na kama ni kibaka ukibaka litaufanya tuu hata ulipe malezi gani, hata asipoishi na vibaka.

Mambo mengine ni asili na laana tuuu, hakuna jipya.
 
Hapo ndo sheria zinakinzana, labda imefutwa au atafukuzwa wa kiume peke yake.

Nimeuliza hivyo makusudi kwa sababu ujauzito ni kiashiria tosha kwamba umetafuna tunda dhahiri pasi shaka. Na kama sheria hazijabadilishwa, inamaana tayari mjamzito anapoteza sifa ya kuwa mwanafunzi. Ukimfukuza wa kiume haitakua kummnyima haki yake ya msingi kupata elimu pia?
 

..tunatumia trillion of shillings za walipakodi kununua midege toka kwa mabeberu.

..halafu tunarudi kuomba mikopo yenye masharti ya kidhalilishaji toka kwa haohao mabeberu kwa ajili ya elimu.

..tatizo sio mabeberu, tatizo ni viongozi wetu.
 
Una fikra za kichawi chawi. Mbona makosa mengine kama wizi, bange, ubakaji, wanaendelea na masomo?. Mbona huwazii wanaopata mimba kwa kubakwa au kulazimishwa na mazingira kama sextortion. Mbona hugusii wanaowapa mimba kwanin huendelea kusoma!
Kubeba mimba hakuui akili ndugu.
Nilitegemea ulete mtiririko wa hoja za namna gan wapate elimu kama haki yao. Mfano binafs nashaur serkali iwape madarasa yao. Walim wale wale. Shule ile ile. Mtaala ule ule. Mkazo uwekwe kwenye kukinga zaid watoto wa kike, kuwadhibiti, ikizingatiwa kwa sasa wao ndo wanajichochelea matatizo had vijana wanawakimbia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…