Kusafirisha wanafunzi ni kazi ya nani?

Kusafirisha wanafunzi ni kazi ya nani?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Wanafunzi wetu nchini ni kundi kubwa la wananchi wenye mahitaji maalumu.

Hapa nchini daladala tu ndizo zilizopewa jukumu la kuwasafirisha kwa bei pungufu ya sh. 200. Hii Ni tofauti na biashara nyingine kama ya stationery, uniforms, bodaboda, chips, soda, nk ambao wao huwa wanawauzia wanafunzi kwa bei kamili. Hawana Bei pungufu kwa wanafunzi.

Daladala zinanunua mafuta, spea na kufanya matengenezo kwa bei kamili. Tena huwa zinalimwa faini kwa makosa ya barabarani kila siku bila huruma Wala kujali kazi wanayofanya ya kuwahudumia wanafunzi kwa bei pungufu.

Je, daladala zinapewa motisha gani ili zipende kuwasafirisha wanafunzi wetu kwa bei hiyo bila kinyongo?

Inauma Sana traffic anakotoza faini ya sh. 30,000 wakati ndani umebeba wanafunzi 10 wanaolipa sh 200. Hivi sh. 30000 za traffic utazipata kwa kubeba wanafunzi wangapi? Labda ndiyo maana makondakta wa madaladala hawataki wanafunzi kwenye magari yao.

Itafutwe motisha kwa madaladala itakayowavutia kuwabeba wanafunzi kwa furaha, la sivyo wanafunzi walipe pia Bei kamili Kama wanavyolipa kwenye stationery, uniforms, chips, bodaboda na kwingineko au watafutiwe namna yao ya kusafiri.
 
Umeongea jambo moja la mafikirio makubwa sana, lakin hawa ni watoto zetu mkuu labda kungefanyika maelewano mengine na serikali juu ya ubebaji wa hawa wanafunzi, lakini sio kupandisha nauli.
 
Faini ya shilingi 30,000, inatozwa tu bila ya sababu?
 
Kuna hawa wengine wanajeshi walimu magereza na hii level seat nao wanagombania siti.
 
Kwa ufikiri wangu mdgo, nafikir wanafunz walitakiwa wawe na bima ya usafiri, yaani wapande kwa hyo 200 lakini pia serikali iwe inatoa fungu kwny magari, fungu fixed
 
Faini ya shilingi 30,000, inatozwa tu bila ya sababu?
Hata ikiwa na sababu lakini Ni lazima ilipwe kutoka kwenye Mapato ya daladala. Je, ukiwa unabeba watoto wa shule wa sh 200 wengi kila siku utaulipaje?
 
Tunawasaidia taifa la kesho, wanafunzi wenyewe wanasimama bila shida.
 
Umeongea jambo moja la mafikirio makubwa sana, lakin hawa ni watoto zetu mkuu labda kungefanyika maelewano mengine na serikali juu ya ubebaji wa hawa wanafunzi, lakini sio kupandisha nauli.
Ni kweli kabisa mkuu Hawa Ni Watoto wetu lakini wafanyabiashara wote wanalijuwa hilo au ni hawa wa daladala tu? Mbona huko kwingine kote hakuna Bei ya wanafunzi? Je, wenye daladala wanapewa nafuu gani ili wapende kuwabeba watoto wetu?
 
Kupakia wanafunzi isiwe sababu ya wewe kuvunja sheria.
Mbona Kuna watu wanapita taa nyekundu, kwenye zebra na kutanua barabara bila
Lakini kubeba wanafunzi siyo kisingizio cha kufanya kosa barabarani.
Kutanua barabarani ili kuwawahisha wanafunzi madarasani Kuna ubaya gani? Mbona Kuna watu wanafanya hivyo kwa kisingizio Cha kuwahi majukumu bila kuchukuliwa hatua?
 
Lakini kubeba wanafunzi siyo kisingizio cha kufanya kosa barabarani.
Je, Ni Nani Wana ruhusa ya kutenda makosa ya barabarani? Maana yako magari yanapita kwa speed jali kwenye zebra cross na taa nyekundu kwa kutumia nyazifa zao, je kuwahisha wanafunzi shukeni sio sababu ya msingi kwa dereva wa daladala aliyebeba wanafunzi kupewa kipaumbele barabarani? Tena wako traffic wanaoanza operation zao za kukamata magari Asubuhi sana wakati watu wanafunzi, walumu, manesi, madaktari na wafanyakazi wengine wanawahi kazini. Hivyo kusababisha watu kuchelewa shukeni na maofisini
 
Je, Ni Nani Wana ruhusa ya kutenda makosa ya barabarani? Maana yako magari yanapita kwa speed jali kwenye zebra cross na taa nyekundu kwa kutumia nyazifa zao, je kuwahisha wanafunzi shukeni sio sababu ya msingi kwa dereva wa daladala aliyebeba wanafunzi kupewa kipaumbele barabarani? Tena wako traffic wanaoanza operation zao za kukamata magari Asubuhi sana wakati watu wanafunzi, walumu, manesi, madaktari na wafanyakazi wengine wanawahi kazini. Hivyo kusababisha watu kuchelewa shukeni na maofisini

kwamba unataka kusema sasa sababu hao wanavunja basi na daladala zivunje sheria

huoni magari ya serikali yanavyowaua kila siku watumishi kisa mwendo?...kama hao wameamua kuvunja sheria acha wavunje,isiwe kigezo cha wewe pia kuvunja

na mfanyabiashara atavuka zebra anasema anawahi fungua duka akalipe kodi,ndio unataka tufike huku?

halafu acha watu wazima watumie utashi wao kuvunja sheria ila siyo kuwatumia watoto uliowabeba kama excuse...zingatia sheria usijilingnishe na mwingine
 
kwamba unataka kusema sasa sababu hao wanavunja basi na daladala zivunje sheria

huoni magari ya serikali yanavyowaua kila siku watumishi kisa mwendo?...kama hao wameamua kuvunja sheria acha wavunje,isiwe kigezo cha wewe pia kuvunja

na mfanyabiashara atavuka zebra anasema anawahi fungua duka akalipe kodi,ndio unataka tufike huku?

halafu acha watu wazima watumie utashi wao kuvunja sheria ila siyo kuwatumia watoto uliowabeba kama excuse...zingatia sheria usijilingnishe na mwingine
Yaishe, Basi kila mzazi agaramie Usafiri wa mtoto wake Kama vile anavyogaramia chips, vitabu, madaftari, uniforms na pen kwa madukani badala ya kumdhulumu mwenye daladala, maana daladala Ni biashara sawa na biashara nyingine zinazolipa Kodi.
 
Yaishe, Basi kila mzazi agaramie Usafiri wa mtoto wake Kama vile anavyogaramia chips, vitabu, madaftari, uniforms na pen kwa madukani badala ya kumdhulumu mwenye daladala, maana daladala Ni biashara sawa na biashara nyingine zinazolipa Kodi.

hii 200 siyo sheria,na wamiliki wa daladala walishaurina wakakubaliana hivi,ndio maana waliambiwa wawe na ile siti yao ya moto juu ya engine...halafu hata ukigoma kuwapakia siyo umevunja sheria,hakuna kesi hapo ni uungwana wako mwenyewe kama hutaki kuwapakia wewe acha...ila kama ukiamua kuwapakia usiwatumie kama excuse ya wewe kuvunja sheria za barabarani

ile ajali ya lucky vicent dereva akijitetea kwamba alikua anawahisha wanafunzi wanakoenda nao utamuelewa?!
 
hii 200 siyo sheria,na wamiliki wa daladala walishaurina wakakubaliana hivi,ndio maana waliambiwa wawe na ile siti yao ya moto juu ya engine...halafu hata ukigoma kuwapakia siyo umevunja sheria,hakuna kesi hapo ni uungwana wako mwenyewe kama hutaki kuwapakia wewe acha...ila kama ukiamua kuwapakia usiwatumie kama excuse ya wewe kuvunja sheria za barabarani

ile ajali ya lucky vicent dereva akijitetea kwamba alikua anawahisha wanafunzi wanakoenda nao utamuelewa?!
Sasa mkuu kwanini watoto tuwafanye wawe ni wakuwaonea huruma ndoo wafike shule? Je kama wote madereva wakiona na makonda wakiona hakuna haja ya kuwaonea huruma kwa kuwa wanapata hasara watoto wataendaje shule?

Mtoa mada yupo sahihi kabisaa,serikali hilo ni jukumu lao kwa kushirikiana na wazazi.Mbona kila huduma wanayoitaka popote hakuna punguzo wala huruma ya mtoa service mpaka kwa mwenye daladala ndoo limuangukie yeye wakati nae anafanya biashara kama wengne.
 
Back
Top Bottom