Kusafirisha wanafunzi ni kazi ya nani?

Kusafirisha wanafunzi ni kazi ya nani?

Mkuu hao wanafunzi wenyewe unaowajungua humu mbona kwenye hizo daladala hawakalii siti zako...wanajisimamia zao na ndio maana wanalipa 200.
 
Sasa mkuu kwanini watoto tuwafanye wawe ni wakuwaonea huruma ndoo wafike shule? Je kama wote madereva wakiona na makonda wakiona hakuna haja ya kuwaonea huruma kwa kuwa wanapata hasara watoto wataendaje shule?

Mtoa mada yupo sahihi kabisaa,serikali hilo ni jukumu lao kwa kushirikiana na wazazi.Mbona kila huduma wanayoitaka popote hakuna punguzo wala huruma ya mtoa service mpaka kwa mwenye daladala ndoo limuangukie yeye wakati nae anafanya biashara kama wengne.

hata hakuna hasara

ndio maana wanasafirishwa kila siku

hoja hapa siyo hasara,ni kutaka kutumia wanafunzi kama kigezo cha kuvunja sheria za barabarani
 
hii 200 siyo sheria,na wamiliki wa daladala walishaurina wakakubaliana hivi,ndio maana waliambiwa wawe na ile siti yao ya moto juu ya engine...halafu hata ukigoma kuwapakia siyo umevunja sheria,hakuna kesi hapo ni uungwana wako mwenyewe kama hutaki kuwapakia wewe acha...ila kama ukiamua kuwapakia usiwatumie kama excuse ya wewe kuvunja sheria za barabarani

ile ajali ya lucky vicent dereva akijitetea kwamba alikua anawahisha wanafunzi wanakoenda nao utamuelewa?!
Unataka kusema mwanafunzi anapoingia kwenye mgahawa atengewe sahani, viti, meza na chakula chao kwa bai pungufu?

Bro, daladala hawana jukumu la kisheria la kugharamia Usafiri wa wanafunzi, walimu na Askari. Bila kupepesa macho Wala kumung'unya maneno Huku ni kuwakandamiza Hawa wafanyabiashara, hii ndio inayosababisha madaladala wavunje sheria ili kufidia hasara za aina hii.
 
Mkuu hao wanafunzi wenyewe unaowajungua humu mbona kwenye hizo daladala hawakalii siti zako...wanajisimamia zao na ndio maana wanalipa 200.
Kwani mtu akikosa siti huwa analipa nauli pungufu? Mbona hapo aliposimama mtoto wa shule angepata 600 Kama angesimama mtu mzima? Kwahiyo ukienda bar ukakosa kiti Cha kukaa na ukasimama Bei ya bia inapungua?
 
hata hakuna hasara

ndio maana wanasafirishwa kila siku

hoja hapa siyo hasara,ni kutaka kutumia wanafunzi kama kigezo cha kuvunja sheria za barabarani
Usibadilishe mada Mkuu, hoja hapa Ni Nani awasafirishe wanafunzi kwenda shuleni?.

Wapo wazazi wenye uwezo wa kunywa bia kila siku, kuendesha magari, kuhonga wanawake na kujenga majumba, lakini na wao wanataka daladala isafirishe watoto wao kwa 200
 
Back
Top Bottom