Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

Kwa tuliosoma shule za serikali enzi za mwingereza chini ya silabasi ya Cambridge hatuwezi kukubaliana na kiwango duni cha elimu iliyopo hivi sasa. Shule za kati (middle school) zilifundisha stadi za maisha zikiwemo ufundi na kilimo jambo ambalo hivi sasa halipo na elimu ni duni sana sana.

Kumbuka hata huo mfumo wa elimu ya aina hiyo ni wao walituletea, mababu zetu walikua na namna yao ya kuandaa vijana namna ya kukabiliana na majukum yao. Bado tunarudi pale pale elimu ile ilitakiwa imsaidie mhusika kuwa mtumishi mzuri kwa hao hao wakoloni. Hatusemi yote yaliyofanywa hayakuwanufaisha waafrika la hasha, mambo mengi yalikua na maslahi mapana kwao.
 
RWEGOSHORA FROLIAN,
Nani asiekumbuka matendo maovu ya Karl peters(mkono wa chuma),nakukumbusha wapo viongozi wengi waafrika wenzetu walitawala nchi zao kwa Mkono wa Chuma na hata leo wapo wanaoendelea kufanya hivyo,umezungumzia kutujengea miundombinu ambayo haikuwa na lengo la kumfurahisha mtu mweusi lakini ukiangalia mpaka leo ipo miundombinu mingi iliyofanywa na hao wakoloni ambayo bado inatunufaisha kuliko iliyoanzishwa na waafrika wenzetu baada ya kujitawala.

umezungumzia suala la kuchukua ardhi kwa mabavu nataka nikukukumbushe hata kabla wakoloni hawajaja zilikuwepo WATEMI,WAFALME na viongozi wa koo waliokuwa wanaenda kuvamia koo zingine na kuteka ardhi na watuwake na kuwa chini ya himaya yao na wanakuwa kama watumwa tu kwenye himaya mpya.

kuhusu utitiri wa kodi hata sasa bado tunalalamikia utitiri wa kodi,sidhani kama ingekuwa ni hiyari kulipa kodi unadhani watu wangelipa kodi?
kutumikisha watu bila malipo hata sasa wapo watu wengi wanatumikishwa bila malipo au kwa malipo kiduchu.

mifupa ya mijusi mikubwa hata wangetuachia tungeifanyia nini kwa kipindi hicho?hata sasa inatusaidia nini zaidi ya kuiweka tukitegemea hao hao wakoloni waje kuitizama kwa kulipia pesa kuna faida yoyote nyingine tunaweza kuipata?

Hii mada aliyoileta mtoa mada ni ya kufikirisha sana,Tujiulize tu Je?kama wakoloni wasingekuja kututawala waafrika tungekuwa tunaishi maisha ya namna gani leo hii?maendeleo yetu tungeyapimaje?maana mpaka leo yapo maeneo hapa hapa Afrika watu wake wanaishi maisha yaleyale waliokuwa wanaishi waafrika kabla ya kuja mkoloni je?hizo madini pembe za ndovu na ngozi za wanyama zingekusaidiaje?

kwa mfano tuchukue kabila kama WAMANG'ATI,tungekuwa tunaishi hivyo maana wao wanaishi maisha waliyoishi kabla wakoloni hawajaja je?hayo madini yangewasaidiaje?
yapo maendeleo ambayo tungekuwa nayo kama waafrika lakini usifananishe na maendeleo haya tunayoyaishi ambayo yametokea kwa wakoloni.
Nun
miaka 50 iliyopita,bado tu hatujaweza kufanya vitu bila wao?na si mpaka leo kuna makabila yanaishi kama vile tulivyoishi kabla ya wakoloni?vipi maendeleo yao sasahivi yanazuiliwa na kina nani?au bado wakoloni wanawazuia?wapo wamang'ati,wamasai,na wengine wengi vipi maendeleo yao?
Dreamlinerz nadhani hukuwahi kusoma vizuri historia ulikuwa bize na hisabati au physics, hz jamii unazozitolea mifano za kimang'ati hata kabla ya ukoloni hazikuwa na mwamko wa kimaendeleo yaani ni decentralized societies hazikuwa na strong political organization. Kwa hyo zingeendelea kuwa hvhv lkn jamii zingine ambazo zilikua na mifumo mizuri ya kichumi na kitawala zingekua mbali Sana hapo tunazungumzia himaya kama Songhai, ghana, mwenemtepe, mali, karagwe, bunyoro, buganda, nk zilikua na viwanda na uchumi wake imara na biashara kubwa.
Sasa kama hoja yako ni kwa nn wamasai, wamang'ati sijui wahadzabe hawajaendelea wakati wanaishi primitive life kama zamani hilo ni suala la kihistoria kutokana na mfumo wao lkn wasingezuia jamii zingine zisipige hatua kwasababu hata ulaya, America, Brazil, India na maeneo mengine yaliyoendelea bado wana jamii primitive kama wahadzabe lkn nchi zao ziko mbali kutokana na uwepo wa jamii zingine zinazopiga hatua. Lazima ktk jamii kuwe na diversity of people hatuwezi kuwa sawa lkn siyo kigezo kwamba tusingeendelea. Hata ww mwenyewe kwenye familia au ukoo wenu wapo ndugu zenu wana mali lkn wengine ni kapuku, hvo umaskini wa baadhi ya ndugu zako haufanyi wengine kwenye familia au ukoo wasitajirike.
Utajiri na stock kubwa za dhahabu walizo nazo mabepari hadi leo ni akiba ya mzigo waliopiga Africa na bado wanaendelea kupiga kupitia watu wanaowasapot kama ww. Fuatilia vizuri stages of capitalism from mercantilism (primitive accumulation of capital i.e. plundering, rooting and piracy), competitive capitalism & Monopoly capitalism)
 
Kumbuka hata huo mfumo wa elimu ya aina hiyo ni wao walituletea, mababu zetu walikua na namna yao ya kuandaa vijana namna ya kukabiliana na majukum yao. Bado tunarudi pale pale elimu ile ilitakiwa imsaidie mhusika kuwa mtumishi mzuri kwa hao hao wakoloni. Hatusemi yote yaliyofanywa hayakuwanufaisha waafrika la hasha, mambo mengi yalikua na maslahi mapana kwao.
Mkumbushe kuwa hzo stadi za maisha kama kilimo waliwaandaa kuwatumikia ktk mashamba ya kikoloni wakiwa kama mabwana shamba. Kwa hyo kama walinufaika halikuwa lengo la mkoloni hapo ni malengo kupitiliza na kuwanufaisha indirect
 
Kumbuka hata huo mfumo wa elimu ya aina hiyo ni wao walituletea, mababu zetu walikua na namna yao ya kuandaa vijana namna ya kukabiliana na majukum yao. Bado tunarudi pale pale elimu ile ilitakiwa imsaidie mhusika kuwa mtumishi mzuri kwa hao hao wakoloni. Hatusemi yote yaliyofanywa hayakuwanufaisha waafrika la hasha, mambo mengi yalikua na maslahi mapana kwao.
Silabasi moja na mtihani mmoja nchi zote zilizokuwa chini ya uingereza, shule za kati tulifundishwa useremala, ujenzi, kilimo na wasichana domestic, needlework na mengineyo yanayohusu mazingira ya kwenu, sasa sijui mwingereza alifaidika nini zaidi ya porojo za wanasiasa wa hovyo, nasema wahovyo kwani jambo linapokuwa bovu kisingizio lilijengwa enzi za mkoloni halifai! Ikulu ilijengwa na mkoloni na magereza nyingi ni za enzi za mkoloni. Ukweli utabaki palepale mwingereza alituachia elimu bora na ndiyo ilimwezesha mwanafunzi wa darasa la NNE kuwa na uwezo wa kuajiriwa umesenja ofisini na wa darasa la nane ukarani ofisini; Miaka 58 ni mingi sana tumefanya nini kwenye elimu na uchumi zaidi ya kusherehekea kupokea ndege tuliyoinunua badala ya tuliyoitengeneza. Alama yetu kama viumbe wenye akili ni ipi zaidi ya kuzaa watoto.
 
Silabasi moja na mtihani mmoja nchi zote zilizokuwa chini ya uingereza, shule za kati tulifundishwa useremala, ujenzi, kilimo na wasichana domestic, needlework na mengineyo yanayohusu mazingira ya kwenu, sasa sijui mwingereza alifaidika nini zaidi ya porojo za wanasiasa wa hovyo, nasema wahovyo kwani jambo linapokuwa bovu kisingizio lilijengwa enzi za mkoloni halifai! Ikulu ilijengwa na mkoloni na magereza nyingi ni za enzi za mkoloni. Ukweli utabaki palepale mwingereza alituachia elimu bora na ndiyo ilimwezesha mwanafunzi wa darasa la NNE kuwa na uwezo wa kuajiriwa umesenja ofisini na wa darasa la nane ukarani ofisini; Miaka 58 ni mingi sana tumefanya nini kwenye elimu na uchumi zaidi ya kusherehekea kupokea ndege tuliyoinunua badala ya tuliyoitengeneza. Alama yetu kama viumbe wenye akili ni ipi zaidi ya kuzaa watoto.


Hoja kwenye huu uzi ni wizi au uporaji uliofanywa na wakoloni. Mleta uzi anasema hawakuiba au kuchukua chochote, akatolea mfano miundo mbinu na vitu walivyofanya wakoloni.

Kuanzia jibu langu la mwanzo kwenye huu uzi, nimesisitiza kwamba chochote walichofanya hawa jamaa tunaowaita wakoloni, kiliwanufaisha zaidi wao.

Walihitaji makarani na vibarua ili kazi zao ziende. Hiyo elimu iliwasaidia waafrika kuwa na uwezo wa kutumika vizuri zaidi kwenye hizo kazi zao.
 
Wewe unayejua tueleze tuelewe na tutoe hoja zetu, hii ni JF of GT si ukumbi wa kuunga mkono hoja.
Wengi wa watoa hoja nimewaona hawajui historia ya Tanganyika wakati wa mwingereza. Hawajui Tanganyika ilikuwa nchini ya nani na nani alimuweka mwingereza kuiongoza! (siyo kuitawala) na kwanini tulikwenda UNO kutaka tujiongoze wenyewe. Bahati mbaya historia halisi ya Tanganyika ilivyurugwa ili ifanane na ya Kenya ambayo ilikuwa koloni la mwingereza. Mada hii under 60 hawataielewa zaidi ya kutoa hoja za kufikirika za chini ya CCM.
Mkuu MABABU zetu walivyocharazwa bakora na kuuzwa utumwani kama mifugo huo sio ubaya ??? Walifanyishwa kazi kama watumwa kweny Mashamba yote ya wazungu,walibebeshwa mizigo Punda cha mtoto,ubaguzi wa rangi ulitamalaki,waliwaua wote waliokataa kutumwa nk
 
Back
Top Bottom