Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

mkuu ile ulaya unayoiona inangaa vile lile ni jasho letu.
 
Mkoloni hasa Mjerumani aliondoka Tanganyika akiwa ameijenga vizuri mzizima (Baadae ilikuja kuwa Dar es Salaam). Majengo yote mazuri ikiwemo Ikulu na majengo ya serikali yote alijenga. Alipanga miji karibia yote na kutengeneza master plan akielekeza watu wajenge na kuishi kwa ustaarabu.

Alijenga pia reli na kuhamasisha kilimo cha Mazao ya biashara. Alijenga viwanda vya kuprocess law materials kwa ajili ya usafirishaji.

Kulikuwa na shule za wamissionary aliowaruhusu kuja kujenga. Kulikuwa na wafanyabiashara sliowaruhusu kuja kuwekeza na kufanya biashara.

Ufike muda tuseme ukweli. Mkoloni alikuwa anafanya maendeleo makubwa sana Tanganyika na Tanganyika ingekuwa nzuri, iliyojengeka vizuri na tena kimpangilio chini ya mkoloni.

Tanganyika ilikuja kuharibika baada ya Mzee Nyerere kuanza kuweka vitu vyake hasa ujamaa n.k.

Mengi anayoyafanya Mh Magufuli leo na tunamsifia sana Mkoloni aliyafanya kwa kiwango kikubwa sana hasa ujenzi wa miundombinu
 
Nimesikitika sana na watu wanaomuunga mkono mleta mada. Ama kweli kutokujua ulipotoka ni hatari. Mkoloni alifanya mambo yote kwa manufaa yake na aliua wengi sana. Hatuna cha kumshukuru mkoloni zaidi ya kumtupia lawama kwa uovu wake. Na kwa nyakati hizi mkoloni bado yupo akiwa kavaa koti la IMF na WB. Ni unyonyaji mtupu.
Acha kupotosha. Kwani machief tuliokuwa nao hawakuua watu? Serikali zilizoundwa baada ya uhuru hazikuua watu?? Kwenye ukweli tuseme ukweli. Hao IMF na World Bank unaowasema ndo wanaofadhili miradi mingi nchini kwako ikiwamo ya utafiti wa madawa , ujenzi wa miundombinu Mf barabara unazoona zinajengwa kwenye miji na majiji mbalimbali sasaivi.

Sie tumeshindwa hata kutenga fedha tu kufufua utalii wa kusini mwa Tanzania mpaka World Bank ndo wametoa pesa zinafanya kazi kule.

Bora kukaa kimya ndugu
 
Tutafakari kwa hoja. Je, hali ya mwafrika kabla ya wazungu kuja afrika na baada ya kututawala akaondoka, ilizidi kuwa mbaya au iliboreka?

Je kama wazungu wasingewahi kukanyaga afrika kabisa mpk leo hii 2019, Afrika tungekuwa wapi? Tungekuwa na maendeleo ya teknolojia kiasi gani? Tungepiga hatua kiasi gani kupambana na magonjwa na maradhi, tungekuwa na mataifa?

Hata China, Singapore, Malaysia walikuwa makoloni. Ukoloni ulitunyonya ndio lakin kupitia maumivu hayo tulipiga hatua nyingi tu za kimaendeleo kama binadamu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni ujinga kuaminishwa kuwa wakoloni ‘wazungu’ walikuja kunyonya malighafi Africa kwa sababu kwao hakukuwa na nazo za kutosha, eti walitulimisha mfano mahindi na mkonge kisha wakasomba vyote kupelekea ndugu zao huku sisi tukifa njaa.... kama hilo ni kweli je siku hizi mashamba yameongezeka huko Ulaya kiasi kwamba hawahitaji tena kuja kulima huku..?
 
Nyerere alitaka sifa za kipuuzi, sasa amepelekea taifa kuwa na umaskini.

Kila siku nalisema hili na nitazidi kusema. Hakukuwa na maana ya kutufukuza wazungu. Labda kwa nchi nyingine lakini Tanzania hapana.
 
Mkoloni hasa Mjerumani aliondoka Tanganyika akiwa ameijenga vizuri mzizima (Baadae ilikuja kuwa Dar es Salaam). Majengo yote mazuri ikiwemo Ikulu na majengo ya serikali yote alijenga. Alipanga miji karibia yote na kutengeneza master plan akielekeza watu wajenge na kuishi kwa ustaarabu.

Alijenga pia reli na kuhamasisha kilimo cha Mazao ya biashara. Alijenga viwanda vya kuprocess law materials kwa ajili ya usafirishaji.

Kulikuwa na shule za wamissionary aliowaruhusu kuja kujenga. Kulikuwa na wafanyabiashara sliowaruhusu kuja kuwekeza na kufanya biashara.

Ufike muda tuseme ukweli. Mkoloni alikuwa anafanya maendeleo makubwa sana Tanganyika na Tanganyika ingekuwa nzuri, iliyojengeka vizuri na tena kimpangilio chini ya mkoloni.

Tanganyika ilikuja kuharibika baada ya Mzee Nyerere kuanza kuweka vitu vyake hasa ujamaa n.k.

Mengi anayoyafanya Mh Magufuli leo na tunamsifia sana Mkoloni aliyafanya kwa kiwango kikubwa sana hasa ujenzi wa miundombinu

Kosa kubwa Sana la nyerere ni kutuletea ujamaa ukatufukarisha
 
Ni ujinga kuaminishwa kuwa wakoloni ‘wazungu’ walikuja kunyonya malighafi Africa kwa sababu kwao hakukuwa na nazo za kutosha, eti walitulimisha mfano mahindi na mkonge kisha wakasomba vyote kupelekea ndugu zao huku sisi tukifa njaa.... kama hilo ni kweli je siku hizi mashamba yameongezeka huko Ulaya kiasi kwamba hawahitaji tena kuja kulima huku..?

Waliojiita wapigania uhuru walipigania maslai yao kwa kuwaminisha wengi,ndio hao hao waliotufikisha kwenye ufukara huu.
 
Nyerere alitaka sifa za kipuuzi, sasa amepelekea taifa kuwa na umaskini.

Kila siku nalisema hili na nitazidi kusema. Hakukuwa na maana ya kutufukuza wazungu. Labda kwa nchi nyingine lakini Tanzania hapana.

Unawafukuza wakoloni kisha unaanza kusafiri kwenda kwao kila wakati ili kujipatia mahitaji yako, hapo ni kujiongezea gharama zisizo na tija.... Canada hadi leo bado ni koloni je wanakosa nini..?
 
Mimi ninaimani 100% mkoloni angeendelea kutawala africa, tz ingekuwa zaidi ya china kwa viwanda.

Wakoloni waliokuwa wabaya ni waarabu. Hwa jamaa biashara zao za utumwa ndyo zilikuwa tatizo africa.

Ni mara 100000000 mkoloni mzungu kuliko mkoloni CCm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unawafukuza wakoloni kisha unaanza kusafiri kwenda kwao kila wakati ili kujipatia mahitaji yako, hapo ni kujiongezea gharama zisizo na tija.... Canada hadi leo bado ni koloni je wanakosa nini..?
Nilishindwa kuelewa mantiki yake, ni mtu wa ajabu sana.

Australia, Canada , Indonesia wanaendelea kwa sababu wanasupport kutoka kwa wengine. Imagine Indonesia hawa tuliokuwa nao sawa enzi za uhuru sasa hivi wamepiga hatua kubwa.

Hata Colombia inayojinasibisha na US angalia hatua iliyofikia.

"Africa it's gonna be Africa" nimewahi kuambiwa na Mjerumani hii kauli.
 
Wakoloni ni kweli walitufanyia maovu mengi. Lakini hadi ipite miaka mingapi tutaacha kuwalalamikia? Kwanini tusidai fidia basi.

Ni kupoteza muda kila siku kulialia kuhusu ukoloni.

Bila shaka waafrika wangetangulia kufika ulaya wangewatawala wazungu maana ni asili ya binadamu kupenda kumtawala mnyonge.

Hata kama wote tungekuwa wazungu bado wazungu wajanja wa sehemu moja wangewatawala wazungu mapopoma wa sehemu nyingine.

Tujikite kupambana na hali zetu za sasa na wakati ujao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hujui ubaya wa wakoloni mpaka umri huo basi bora unyamaze
Wewe unayejua tueleze tuelewe na tutoe hoja zetu, hii ni JF of GT si ukumbi wa kuunga mkono hoja.
Wengi wa watoa hoja nimewaona hawajui historia ya Tanganyika wakati wa mwingereza. Hawajui Tanganyika ilikuwa nchini ya nani na nani alimuweka mwingereza kuiongoza! (siyo kuitawala) na kwanini tulikwenda UNO kutaka tujiongoze wenyewe. Bahati mbaya historia halisi ya Tanganyika ilivyurugwa ili ifanane na ya Kenya ambayo ilikuwa koloni la mwingereza. Mada hii under 60 hawataielewa zaidi ya kutoa hoja za kufikirika za chini ya CCM.
 
Chochote walichokifanya wakoloni, walifanya kwa manufaa yao mapana.

Hata sasa bado sie ndio soko la bidhaa zao, chanzo cha mali ghafi za viwanda vyao n.k.

Tukiwa na dunia yenye amani na utulivu, watauza wapi silaha zao ikiwa wao ndio wazalishaji wa silaha?

Walijenga reli na barabara wakati uke zirahisishe usafirishaji wa bidhaa ziende kwao, hapo bidhaa inajumuisha watumwa, mafini, mazao n.k.

Tafiti walizofanya kuhusu maeneo yenye madini na miundo mbinu nayo ilikua kwa kusudi lilelile, kuwanufaisha wao.

Kusingekua ni kwa ajili ya maslahi yao kwanini waligombania maeneo ya Afika hadi kufikia kufanya mkutano wa kugawana bara letu?

Maovu na uzembe wa viongozi wetu baada ya uhuru umekithiri kiasi cha kufanya tuwakumbuke wakoloni, lakini haiondoi ukweli kwamba mkoloni hakufanya chochote kisicho na faida kwake.

Barbarosa pole sana, mbaya zaidi umesahau kusema kuna jamaa sasa hivi ametuletea lugha ya kuwaita wazungu mabeberu huku akiendelea kuwaomba watusaidie na kuwasifia kila wanapofanya hivyo.

Wakoloni hawa kama kweli wana kusudi na nia njema, UN wapo kuhakikisha dunia inakua salama na hatuna migogoro kati ya nchi na nchi huku haki za binadam zikipewa kipaumbele, lakini hilo halijawahi kufikiwa.

Mashirika yake ya maendeleo yamekuwepo zaidi ya miaka 70 wakijinasib kusaidia nchi kupambana na umaskini, kuimarisha utawala bora, kueneza demokrasia n.k lakini hakuna nchi hata moja wanaweza kuitolea mfano kwamba waliikuta na hali mbaya, wameisaidia na sasa imefikia pazuri wanaweza kuiacha ikajiendesha yenyewe, haipo.

Nabaki na msimamo wangu kwamba mkoloni alifanya yote kwa maslahi yake binafsi.
Kwa tuliosoma shule za serikali enzi za mwingereza chini ya silabasi ya Cambridge hatuwezi kukubaliana na kiwango duni cha elimu iliyopo hivi sasa. Shule za kati (middle school) zilifundisha stadi za maisha zikiwemo ufundi na kilimo jambo ambalo hivi sasa halipo na elimu ni duni sana sana.
 
Kuna ramani zingine walikimbia nazo wamezificha Ulaya. Kuna wawekezaji wanakuja kuwekeza leo ila target yao ni maeneo yenye Mali zao walikohifadhi. Mfano Mbeya Gereza la Songwe na Madini yA Nobium

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom