Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

hawakuiba sawa, lakini walitutawala bila ridhaa yetu, ubaguzi wa elimu, dini, kabila, walitugawa sana ili watutawale vizuri
Hizo story za viongozi wetu tuwaone wa maana mbona wanatubagua kiitikadi, ukiwa chadema humo makazini au sehemu za biashara viongozi wa serikali wanakuona adui wa nchi hata kama unachapa kazi kwa mjibu wa sheria, taratibu na miongozo. Hiyo inatofauti gani na mkoloni. Katiba yetu inaruhusu vyama vingi lkn uonezi ni mkubwa sana kwa wapinzani. Hayo ndo aliokuwa anafanya mkoloni.
 
Mtoa mada hana elimu ya historia.

Hapo alipo hata hajui maana ya Ukoloni.
Angejua maana hata ya neno hilo asingeandika mada hii ya kipuuzi ambayo hata mtoto wa kidato cha pili hawezi kuelezea kama yeye.

Mtoa mada sijui kama unajua hata ukoloni mamboleo jinsi unavyonyonya nchi za dunia ya tatu.


Mtoa mada apuuzwe kwa kuwa anaupungufu wa Elimu ya Historia.
 
Jokajeusi,
Jokajeusi hivi unajua maana ya neno Dunia ya tatu? Je hiyo ya kwanza na ya pili ni ipi? Hiyo ndo divide and rule do not depend on it.
 
Jokajeusi hivi unajua maana ya neno Dunia ya tatu? Je hiyo ya kwanza na ya pili ni ipi? Hiyo ndo divide and rule do not depend on it.


Dunia ya tatu ndio yetu hii ya watu masikini.
Dunia ya pili ni vile vinchi kama India, Brazil, Nchi za mongolizi, N.k

Dunia ya kwanza ni zile nchi babalao. G8
 
Mada fikirishi. Tusiishi kwa kuaminishwa ati umaskini wetu kwa kuwa tumeibiwa mali zetu na wakolonI. Tumeibiwa nini, wapi, kiasi gani na kwa namna gani. Na je, ni kwa namna gani tunafanya tofauti kulinganisha na huyo mkoloni?
 
Nani huyu asiyekumbuka matendo maovu ya Karl Peters(mkono wa chuma), biashara ya watumwa iliyochagizwa na wazungu, wizi wa mali mf: ngozi za wanyama, pembe za ndovu, madini mbalimbali, kutujengea miundo mbinu ambayo haikuwa na lengo la kimnufaisha mtu mweusi, elimu yenye ubaguzi na utabaka, kutuhubiria dini zenye kutusahaulisha asili yetu, utitiri wa kodi, ukiukwaji wa haki za mtu mweusi kama vile kuchukua ardhi kwa mabavu, kutumikisha watu bila malipo au kwa ujira kiduchu na kwa muda mrefu bila kupumzika, kuibwa kwa masalia ya mifupa yaani skeleton ya mijusi wakubwa yaani (dinosaurs), kuharibu viwanda vyetu asili vya kipindi kile ambavyo ndio ungekua msingi wa ubunifu wa leo, kutujengea viwanda vidogo visivyo na tija yaani (processing industries) siyo heavy industries, kuwafanya baadhi ya makabila kuwa vibarua wa kidumu hadi leo.

Kiujumla nakishangaa kutetea wakoloni, yaani hata kina Kinjekitile Ngwale na Mkwawa walipambana na huu udhalimu bado wewe msomi wa Leo unatetea! Dah

Wakoloni ni wabaya zaidi ya wabaya hasa kupitia matendo yao makuu matatu yaani Creation, Destruction & Preservation.
Si kwamba nawatetea waarabu la hasha! Naongelea upande wa wazungu kuanzia kwa wareno, wajerumani na waingereza. Waarabu nao wana shida zao pia
 
Mwanzi1, Wakati wa mkoloni watu walikufa kwa njaa,na sasa watu wanakufa kwa njaa,kuna tofauti gani?
Wakati wa mkoloni watu waliuawa kwenye mapambano ya kukataa kutawaliwa na wakoloni,leo huko Z'bar watu wengi waliuawa kwa kudai haki yao kwenye uchaguzi,maiti zinaokotwa ufukweni, na watu wengi wanapotea na hakuna hata uchunguzi,kuna tofauti gani?

Si bora hata mkoloni kuliko huu upumbavu wa kutekana hovyo na maneno ya hovyo ya mkoloni mweusi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waliokwiba ni Hao jamaa wa kijani

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
(1) Awamu ya kwanza ilizalisha wajamaa uchwara
(2) Awamu ya pili yakazuka makupe
(3) Awamu ya tatu ikakaliwa na mabwanyenye
(4) Awamu ya nne mafisi yakasogea
(5) Awamu hii naona makabaila yanakaba kila yanaemuona mwenye simu haya ! Mwenye heleni ya dhahabu yatakutoa hata sikio ili yapate yenyewe
Mimi najua mkoloni alituletea hadi kabichi mapera Leo tumwite beberu sio haki kabisa
 
Unafahamu nyerere alikuwa na maana gani kuzuia shughuli za uchimbaji wa madini Tanganyika Na Akasema tutakuja kuchimba wenyewe Siku tukiwa tumeendelea??????
Nyerere alikuwa na mawazo mazuri kuhusu uchimbaji wa madini.

Baadae alituachia watu wasiojielewa ambao waliwazika wakaazi wa Bulyanhulu wakiwa wazima wazima na kutoa maeneo yao kwa watu waliowaita wawwkezaji kwa malipo kiduuchu sana, mpaka sasa nchi haifaidiki na uchimbaji ule kutokana na maamuzi ya mkoloni halisi,yaani ccm mpya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Ngoja nikuulize swali simpo sana, kama leo hii Meli ikipaki bandari zetu Dar, Tanga au Mtwara na kusema wanaotaka kwenda Ulaya au Uarabuni kuwa Watumwa wapande, unafikiri Meli zitaondoka tupu?
Isitoshe usisahahu utumwa una pande mbili, hata sisi tulikamata na kuuza ndugu zetu pia, hao waliuza babu zetu kwa Mkoloni utawadai fidia pia?
Aliyeongelea habari ya utumwa wala hajui historia ya nchi yetu kwa sababu wazungu mwishowe hawakutaka biashara ya utumwa wakati walipokuja huku Afrika Mashariki.

Waliofanya biashara ile walikuwa ni waarabu wakishirikiana na machifu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui kwa watu wa mwambao unamaanisha nini, lkn kama ni Waarabu walijenga pia tena sana tu mfano Stone town Zanzibar, Miji mashuhuri na ya kihistoria kama Kilwa, Bandari Mikindani, hata ramani ya reli treni kutoka Kigoma - Dar ilifuata Karavani, Wajerumani hawakubadilisha kitu waliweka mataruma tu kwa ramani ambayo tayari ilikuwepo.

Lkn Mada haihusu Waarabu vs Muzungu.
WAHARABU---ni jamii ya wanyama wakatili sana. wamewatesa na kuwauwa babu zetu. Nikiwaangalia kwakweli mwili unasisimuka hatale
 
Sijui kwa watu wa mwambao unamaanisha nini, lkn kama ni Waarabu walijenga pia tena sana tu mfano Stone town Zanzibar, Miji mashuhuri na ya kihistoria kama Kilwa, Bandari Mikindani, hata ramani ya reli treni kutoka Kigoma - Dar ilifuata Karavani, Wajerumani hawakubadilisha kitu waliweka mataruma tu kwa ramani ambayo tayari ilikuwepo.

Lkn Mada haihusu Waarabu vs Muzungu.
Ikulu yenyewe imejengwa na mwarabu na majengo mengi tu ya miji mikongwe Mjerumani aliipora kutoka kwa mwarabu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RWEGOSHORA FROLIAN, Bajeti ya kuendesha nchi yako inachangiwa na hao unaowaita wakoloni mpaka sasa.

Miradi mingi ya huduma za kijamii kama shule,hospitali,miradi ya maji na umeme ni kwa hisani ya nchi zao.

Hata chakula,na madawa wanatusaidia,leo tunawananga kuwa ni wakoloni,wezi wa raslimali zetu,mabeberu na kadhalika.

Nadhani ni vizuri na inafaa kuwashukuru kuliko tunavyowalaumu.

Hizo lawama zenu zingekuwa za kweli kama tungekuwa tunajitegemea kibajeti,tungekuwa na demokrasi ya kweli na kuacha kubaguana kwa misingi ya kabila,chama,nk mngeweza kuaminika.

Miaka 58 ya uhuru bado hatuoni sababu ya kumuondosha mkoloni,hatuoni hata kidogo,bora mkoloni angeendelea kuwepo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hawakuiba sawa, lakini walitutawala bila ridhaa yetu, ubaguzi wa elimu, dini, kabila, walitugawa sana ili watutawale vizuri
Waliiba, wanaiba na wataiba....
Vijana hatuna budi kutoka nje ya Dar kuona mikoa mingine mambo yapoje,
Nakumbuka pale Ndanda kipindi nipo kidato cha 5 kuna baadhi ya sehemu huwezi kufika yaan, kila siku walikua wanapasua miamba tuu,
Watu walishaingia mikataba siku nyingi, wana maeneo yao hata ndege ndogo zinaweza kutua na kuondoka na mzigo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom