Kushabikia Soka la Ulaya hakutusaidii

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,319
Makala hii ilichapishwa katika gazeti la Mwananchi toleo la Jumatatu, 12 Mei 2014.
 
...

....Mwenye historia ya mashabiki wa soka katika Taifa letu since huko nyuma Piter Tino ,Sembuli, Jela Mtagwa watupie kidogo
 
Timu za nyumbani zinawakatisha moyo mashabiki,na siasa imeingia kwenye soka letu, kumekuwa na maneno mengi ambayo hayaleti matunda tofauti na soka la huko nje amabalo pamoja na uwekezaji bado tuaona matunda watu wanaona bora kushabikia timu za nje kuliko za ndani ambazo kimsingi haziwafurahishi wapenzi wa mpira

hata kama hakuna faida tunayopata kwa kushabikia timu hizo angalau tunapata faraja na raha ya kimchezo
 

Kucheza waende tu wakacheze ili walete fedha nyumbani. Mahaba yabaki kwa timu zetu za nyumbani kama vile mimi ninavyoipenda Yanga hadi kufa.
 
Mimi sitaki kuchaguliwa timu ya kushabikia. Ni kama tu leo mtu aniambie nisinunue kahawa ya nestle, badala yake ninunue africafe ya hapa hapa. Dunia ya sasa ni network. Napata kitu roho inapenda.

Wakati nikiwa shule ya msingi nilikuwa shabiki wa yanga. Nikiwa sekondari nikaanza kupoteza interest ya mpira wa bongo. Hiyo ilikuwa miaka ya mwanzo ya 80. Maisha yangu ya ughaibuni ya zaidi ya muongo mmoja yakanifanya nipende na kulielewa soka la huko. Kinachonivutia hasa ni kitu kinachoitwa sports (football) management.

Nilivyorudi Bongo, nimeona Azam wana mwelekeo wenye matumaini. Kwa hivi sasa kwa bongo nashabikia azam. Lakini timu za ughaibuni siachi.
 
Makala hii ilichapishwa katika gazeti la Mwananchi toleo la Jumatatu, 12 Mei 2014.

Tatizo la mpira wa Tanzania unavutia kuusoma kwenye magazeti lakini uwanjani magumashi kibao. Viongozi wanaoongoza mpira wababishaji tu kuanzia vyama hadi vilabu.
 
Binafsi nimepoteza interest sana na soka la Tanzania, lipo stagnant kwa miaka mingi, hamna maendeleo zaidi ya siasa na USHIRIKINA. Timu ya Taifa na vilabu vimekuwa vichwa vya mwendawazimu, viongozi wamekuwa wababaishaji sana.

Katika kushabikia kwangu mpira wa miguu hapa nchini, nimeona napoteza nguvu nyingi, uyanga na usimba vimeathiri mpira wetu sana. Uwepo wa sponsorship toka kwa azam kunaonyesha jinsi gani mpira wetu unaweza wetu unaweza kubadilika.
 
Babu zetu walijitahidi kujituma tena bila malipo ya maana lakini bado hatujafika popote,sasa wachezaji wanalipwa mamilioni lakini ndo tunazidi kudidia afadhali ya zamani..kwa sababu hizo, ndo tunatafuta timu kama LIVERPOOL ili kupata faraja..
 
Madhara ya utumwa na kutawaliwa yanajionyesha.mataifa yote yaliyotawaliwa na wazungu yana kasumba ya kushabikia vilabu vya ulaya.kaulimbukeni hako nakachukia sana.mimi nabaki na simba yangu
 
Kwenye soka tunafuata burudani, soka la bongo ni stress tupu, mipango ya kipwagu, siasa za kina rage na malinzi mpaka mpirani, wacha tulowee ulaya
 
Shabikia azam basi au mbeya city,
Wanajitahidi wana mfumo kama hao unaowapenda
 
Mimi oljoro jkt kashuka daraja, sasa nipo mbeya city
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…