we kenge acha kutisha watuwewe unayejificha kwenye keyboard kwa kusema kitu ambcho huna ushahidi nacho, siyo Muoga! hebu fanya ujasiri uende hadharani utaje huyo unayemtuhumu kwa jina lake halisi kuwa ndo kahusika ili tukuone we ni jasiri zaidi yake!
Assume wewe ndio askari ... ungefanyaje ikiwa muathirika amekimbia nchi na mwingine amefichwaKwa hiyo kwa kuwa Lissu yupo Ubelgiji haiwezekani kufanyika uchunguzi ?
Acha kutetea ujinga mzee
Kazi interpol ni ipi ?Assume wewe ndio askari ... ungefanyaje ikiwa muathirika amekimbia nchi na mwingine amefichwa
Chakushangaza wabunge umeshawapa airtime kuzungumza against Mbowe hukohuko ambako wewe ni kiongozi" Sasa jambo lenyewe (Mbowe kuvamiwa) lina hadithi nyingi ya jinsi lilivyotokea maanake inasemekana jana mpaka saa sita usiku alikuwa mahali, inaniwia ugumu kusema chochote kwa hatua hii lakini...eeh! niseme tu kwamba msichukulie kama watu wanavyoongea, watakaosema hali halisi ni vyombo vya usalama na niwaombe vyombo hivyo vitoe taarifa mapema iwezekanavyo, waeleze ilitokea nini isiwe ni kazi yangu...wanavyozidi kuchelewa hadithi zinakuwa nyingi "-Spika Job Ndugai.
Siku zote Mwizi huwa na Kiherehere kingi tu cha Kujitetea na Unafiki uliokomaa kwa waliomshtukia au wale ambao wanataka Kumuadhibu akome.
Acha ukichaa ndugu yangu Interpol wadili na kesi za kuku kweli?Kazi interpol ni ipi ?
Dawa yenu inachemkaMbona mimi sijaona tatizo hapo
Jiwe linakamatika?Cha msingi watihumiwa wakamatwe.
Hakuna taarifa nimeisoma nikiumia Kama hii ya Mbowe leo, kuna jitu lioga Kama jiwe ?
Walinzi binafsi ni wazo zuri ila kila mtu akiwa na ulinzi- huko ndiko tumefikia watanzania?Kwa jinsi hali ilivyo Hakuna namna tena viongozi ambao usalama Upo mashakan kuna haja ya kuwa na walinzo binafsi
viongozi ambao usalama Upo mashakan kuna haja ya kuwa na walinzo binafsi
Huo ni USHUHUDA kuwa matakataka yao yameshindwa kumchafua Mbowe wala kuiua CHADEMA.Chadema lazima wahakikishe Mbowe anatibiwa kwa gharama yoyote, hata kama ni kukausha account za Chama. Haiwezekani Bungeni zitolewe taarifa za eti "alianguka akitoka kulewa" mara "aliendaje kituo cha afya badala ya Hospitali" aaah, wanaongea sana hawa watu!!
Wewe kama siyo kiwele invata wa facebook ni kundi moja lake wanaotafuta teuzi achana na ukada kwenye maisha ya mtuHuu mpango utakuwa umesukwa ndani ya Chadema,kutafta sympathy kwenye uchaguzi,ila wajinga utasikia wanaropoka tu.
Mi sikuwepo wakati wa Ben kama ilikua hivyo kwanini hawajamkamata kubenea? ndo maana nimesema waanze na huyoo mashimoMbona kwenye inshu ya Ben Saa8 hamkusema Kubenea akamatwe ilihali mlimsikia mwenyewe kwa maandishi yake, akikiri kujua mahali Ben aliko na sababu ya kujificha?
Mashimo ni Nabii na unabii hauna ushahidi katika ulimwengu wa mwili labda wote wawe kwenye ulimwengu wa Roho.
Hii ni kazi ya wahuni ambao wanadhani wanaihami serikali ya awamu ya tano kwa maslahi yao binafsi, kumbe wanaichafua na kuibomoa vibaya sana. Serikali hii ni ya ccm; siyo ya mtu mmoja wala kikundi cha watu. Hiki ni chama ambacho Watanzania wengi wanajua siyo cha kihuni. Ila tusubiri kuona kama ccm ya sasa imeharibikiwa kiasi hiki.Kwani Ndugai alikuwa kaombwa kutoa maelezo kwenye swala hili?
Mbona anazidi kujishusha daraja?
Inasikitisha sanaKamanda wa Polisi Mkoani Dodoma, Gilles Muroto amesema leo alfajiri walipokea taarifa kutoka kwa Mbunge wa Viti Maaalum, akiwa na Dereva wa Mbowe, Wilhad Urassa (34) kuwa Mwenyekiti huyo wa CHADEMA wakati akipandisha ngazi kuelekea ndani kwake inadaiwa alishambuliwa na watu 3
Kamanda Muroto amesema “Inadaiwa watu hao 3 waliokuwa wamevaa jackets (makoti) walimshambulia kwa kumkanyaga na kumpiga mateke hasa mguu wake wa kulia. Kutokana na taarifa hizo majeruhi alipelekwa katika Hospitali ya Ntyuka anakopatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri.”
Ameeleza, “Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi bila kuacha chochote ili kupata ukweli na usahihi wa tukio hilo. Tukio hili lisitumike kisiasa au kwa njia yoyote ya kujiongezea umaarufu kwa mtu au watu na ni marufuku kuingilia uchunguzi huo.”
Amesisitiza kuwa eneo lile lina Walinzi na Majirani watafanya uchunguzi kujua ukweli wa tukio. Pia, amewaonya Wafuasi wa CHADEMA wanaohamasishana kukutana kwani Jeshi la Polisi lipo macho na yeyote anayefanya mikusanyiko isiyo halali atashungulikiwa kweli kweli
Aidha, Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amesema Polisi wanapofanya Uchunguzi hawapaswi kufunga milango ya uchunguzi na kuliita hili ni tukio la kawaida kwasababu viashiria vinaonesha tukio hili lina muelekeo wa kisiasa
Mnyika amesema kati ya watu waliokuwa wanamshambulia Mbowe wapo waliosikika wakisema “Wewe unaisumbua sana Serikali, tunakushughulikia tuone kampeni utafanyaje.” Ametoa wito kwa Polisi na vyombo vya Usalama kuchunguza tukio hilo kwa mapana ili waliohusika wachukuliwe hatua
Amesema siku chache kabla ya Mbowe kushambuliwa, katika mitandao ya Kijamii kulisambaa video ya mtu anayejiita Mchungaji wa Kitaifa, Mchungaji Mashimo akisema “Kuna tukio litatokea mbele kwa Kiongozi wa Upinzani kushambuliwa” na kati ya majina aliyoyataja, jina Freeman Mbowe lilikuwepo. Ametoa wito kwa Polisi wamkamate ili aleeze hizo kauli zake.