Kusitishwa Mradi wa Bagamoyo SEZ kumedhihirisha udhaifu wa Rais Magufuli kwenye Uchumi na Diplomasia

Kusitishwa Mradi wa Bagamoyo SEZ kumedhihirisha udhaifu wa Rais Magufuli kwenye Uchumi na Diplomasia

Twende Mbele turudi Nyuma, hili ni kosa kubwa serikali ya awamu hii ya tano imefanya, Tanzania ambayo inataka kukua kiuchumi Zaidi haiwezi kuwa inaogopa ushindani, hoja ya kusema china itataifisha bandari tukishindwa kulipa ni hoja totally mfu, mfu kabisa,mawazo ya kimasikini kabisa, sisi tumetoa eneo la uwekezaji tu, mtaji unatoka china/Oman,hata kama china/oman wataendesha hiyo bandari kwa muda ya miaka kadhaa ni sawa, serikali wao watakuwa wanapata mapato, ajira zitaongezeka kwa vijana, bagamoyo ingekuwa na kuwa center ya usafirishaji wa bidhaa katika ukanda huu wa EAC nad nchi nyingi za kusini,ukisimamisha mradi huu kwa woga wako kuwa eti bandati yetu ya Dar itakufa au kukosa mizigo huwakomoi wachina, unakomoa wananchi wako, unajikomoa wewe mweyewe na serikali yako kwa kukosa mapato, unajirudisha nyuma wewe mwenyewe katika dhamira ya Tanzania ya viwanda,tuacheni kuogopa kwa kila jambo, nature ya Zambia na srilanka ni tofauti na Tanzania, kwa hili Zitto Kabwe yuko sahihi Zaidi 100%, Magufuli aangalia upya maamuzi yake, ni bora aangalie jinsi ya kukutana na Rais mwenzake wa china kwa majadiliano Zaidi.
Aisee! Akili kama hizi zako hazina tofauti na zile za kina Mangungo wa kipindi kile cha utumwa
 
Hoja yako ina mashiko kiasi kikubwa, nimeipenda.

Nimeipenda zaidi sababu inaturejesha kwa swali la miaka yote "kati ya kuku na yai kipi ni cha kwanza?" au "fedha na elimu nini kitangulie?".

Hoja ya SGR kuwa huduma badala ya biashara kama bandari isipokuwa fanisi (mizigo michache) hili ni kweli.
Lakini kama hatuwezi kujenga vyote kwa pamoja ni lazima tuchague kimoja, nafikiri SGR ni cha kuanza nacho sababu tayari tunayo bandari inayo fanywa upanuzi, SGR itakuwa inatoa huduma kama ulivyosema wakati tunasubiri mradi wa Bagamoyo ESZ.

Tukiangalia suala la umeme ni kweli itakuwa huduma na biashara lakini uangalie umeme kama kichocheo cha ujenzi wa viwanda vingi vitakavyo hitaji malighafi mengine toka nje hivyo zitapitia bandari na kuingiza pesa, hivyo viwanda pia vingi vitajengwa na wawekezaji toka nje ambao wataleta fedha za kigeni.

Usisahu uzalishaji wetu viwandani ukiwa mkubwa tutahitaji kuunza nje bidhaa zetu, tutahitaji bandari kubwa.

Kwa mtindo kama wa mikataba yetu ya madini, gesi na hoteli tulizo karibisha wawekezaji utaona heri umeme au SGR itakayo kuwa chini ya usimamizi wetu vitaleta pesa kuliko mradi wa wawekezaji tunaosubiria mrahaba sijui mrabaha. Hakuna kitu kabisa tubaishia na vurugu kama za makinikia n.k.
Tuko pamoja mpaka hapo,nakukumbusha tena mkuu,kusema kwamba kusimamia wenyewe ndio tutapata faida kidogo kuna ukakasi japo nakubaliana nawewe mirabaha nayo ina changamoto kikubwa ni majadiliano,mfano sasa hivi makusanyo ya taasisi nyingi ikiwemo bandari yanaenda hazina,mfano mda huu bandari wawe na changamoto ya vitendea kazi mlolongo wa kupata hiyo pesa ili wakanunue vifaa ili waboreshe utendaji utakuwa mrefu na pengine wasifanikiwe huku utendaji ukiendelea kuzorota wewe mwenyewe utakuwa unajua milolongo ya mambo ya serikalini ni tofauti na kwa wawekezaji.mfano mzuri ni mwendokasi wameagiza magari karibia 100 lkn bado hayajaingia barabarani pamoja na uhitaji mkubwa wa magari hayo sasahivi yote hii kwasababu taratibu gani dijui za manunuzi wabia hawakuelewana yani serikali na mwekezaji.
 
amekiri kuwa ni kweli mradi una masharti magumu, hajayasema hayo masharti. viongozi wa namna hii ni hatari kwa nchi, serikali yenye akili timamu ikakatae mradi wa trilion 23 hivi hivi? wasomi wa tanzania wana bei, wanaweza kulipwa kitu kidogo waje wapige kelele humu mitandaoni
 
kichwa maji kweli wewe unasoma kwa kuruka ruka kukimbilia dirashani kupanga foleni kwa ajili ya buku saba. Huo mradi wa bagamoyo ni uwekezaji sio kwamba nchi inatoa kila kitu toka mfukoni mwake zaid ni hao wachina ndo wanahusika kurun hiyo project
Mkuu, kichwa sio pambo! Kitumie kufikiri!
 
jamaa kahis akijenga Kikwete atafaidi sana kaamua kusitisha ili ajenge uwanja chattle mambo yanayofanywa awamu hii ni ya hovyo toka dunia iumbwe
 
Ni maamuzi ambayo watakuja kuyajutia in 10-15 years time, bandari ya Dar as a center of gravity kwa uchukuzi wa Tanzania na nchi za jirani aiwezi mudu volumes kadri uchumi wa Tanzania, Uganda,Burundi, Zambia na nchi zingine zinavyokuwa na logistic zake zitaongeza kero zaidi kwenye jiji. Kwa ivyo expansion of transportation infrastructure is bound to occur which is a future expensive undertaking.

Vitu vingine inabidi ufikirie in 20 years time sio leo tu.
 
Huu mradi ungebaki kwenye makaratasi tu as utekelezaji wa mradi wa Trilion 23 kwa usawa huu wa kuchangishana buku buku hautekelezeki Kwa sasa!

ZZK usisahau kuwa jimboni kwako maji tu yanayohitaji bajeti chini ya 20 B yameshindikana kupatikana! Then unatetea 23Trilion ziende Bagamoyo?
Hujasoma na kuelewa kilichoandikwa rudia tena kusoma
 
Courtesy ni muhimu sana katika masuala ya uandishi. Ungekuwa muungwana hasa kama ungetaja jina lake hapa.
 
Hoja yako ina mashiko kiasi kikubwa, nimeipenda.

Nimeipenda zaidi sababu inaturejesha kwa swali la miaka yote "kati ya kuku na yai kipi ni cha kwanza?" au "fedha na elimu nini kitangulie?".

Hoja ya SGR kuwa huduma badala ya biashara kama bandari isipokuwa fanisi (mizigo michache) hili ni kweli.
Lakini kama hatuwezi kujenga vyote kwa pamoja ni lazima tuchague kimoja, nafikiri SGR ni cha kuanza nacho sababu tayari tunayo bandari inayo fanywa upanuzi, SGR itakuwa inatoa huduma kama ulivyosema wakati tunasubiri mradi wa Bagamoyo ESZ.

Tukiangalia suala la umeme ni kweli itakuwa huduma na biashara lakini uangalie umeme kama kichocheo cha ujenzi wa viwanda vingi vitakavyo hitaji malighafi mengine toka nje hivyo zitapitia bandari na kuingiza pesa, hivyo viwanda pia vingi vitajengwa na wawekezaji toka nje ambao wataleta fedha za kigeni.

Usisahu uzalishaji wetu viwandani ukiwa mkubwa tutahitaji kuunza nje bidhaa zetu, tutahitaji bandari kubwa.

Kwa mtindo kama wa mikataba yetu ya madini, gesi na hoteli tulizo karibisha wawekezaji utaona heri umeme au SGR itakayo kuwa chini ya usimamizi wetu vitaleta pesa kuliko mradi wa wawekezaji tunaosubiria mrahaba sijui mrabaha. Hakuna kitu kabisa tubaishia na vurugu kama za makinikia n.k.
Sasa huu si upunguani yaani kuingiza trion of shilingi kwenye miradi ambao ni hasara eti huduma,kwamba watu wa kanda ya ziwa wana haraka sana ya kufika Dar?
Nchi hii ina watu wenye hofu na hawawezi kufikiri,,ingefaa maeneo wanayoyatilia doubt yapelekwe mezani yajadiliwe,impacts ya matrion ya bagamoyo kwenye uchumi ni faida kuliko sgr zisizo na maana,,kwani huko Singapore etc huoni free economic zone zinavyoleta faida? Mfumo wa ppp ndio model nzuri kuliko serikali kukopa na maurasimu juu
 
Sasa huu si upunguani yaani kuingiza trion of shilingi kwenye miradi ambao ni hasara eti huduma,kwamba watu wa kanda ya ziwa wana haraka sana ya kufika Dar?
Nchi hii ina watu wenye hofu na hawawezi kufikiri,,ingefaa maeneo wanayoyatilia doubt yapelekwe mezani yajadiliwe,impacts ya matrion ya bagamoyo kwenye uchumi ni faida kuliko sgr zisizo na maana,,kwani huko Singapore etc huoni free economic zone zinavyoleta faida? Mfumo wa ppp ndio model nzuri kuliko serikali kukopa na maurasimu juu
Tayari umehaharibu mjadala kwa kutumia maneno makali ya kashifa na dharau.
Unge pungukiwa na nini kama usingetumia neno 'upunguani'?

Ni kitu cha ajabu kumuona mwenzio punguani sababu mmetofautiana vipaumbele au misimamo.

Kila la heri kiongozi.
 
Wewe ni mvivu wa kusoma na kufikiri. Tayari hata Ndugai ameshamuelewa ZZK na anaonekana kutomuunga mkono yule mkuu katika hilo. Amka!
Nyinyi ndio wale watz wachache mnaotegemea akili za mtu kuishi.

Yaani kila mtu unataka akubaliane na huyo zitto, kwanini una imani naye kiasi hicho!!!

Kwenye hili swala mnaonyesha upumbavu kiwango sana bila kusita.
 
Nadhani ipo haja ya kujua masharti haya ni yapi, maana hapa maelezo yako ya jumla jumla sana.
IMG_20190513_162314.jpeg
 
Back
Top Bottom