Kutoka kofia ya barghashia ya Nyerere 1964 hadi msalaba wa William Lukuvi 2014

Jana kupitia taarifa ya habari K24 nimesikisia Al shaabab wakiimba "Nairobi tutafikaaaaa Al Shaabab tunasemaaaaa" Wakenya matumbo moto saa hizi! Tuache mawazo ya udini tusivuruge nchi.
 

wewe sasa ndio unataka Wakristo waliokuwa wameanza kuwaunga mkono Ukawa warud nyuma. ndio maana huwa wakat mwingine mnadharaulika hv huwez kukaa nyuma ili Waislam na Wakristo walivyokubaliana watusaidie kuitoa CCM madarakan? tambua kuwa cku Chadema na Cuf kwa nia ya dhat wakiungana kwa jina la Tanzania Ccm inapigwa chin plz ucwe kama ccm uctugawe tena. ficha udin wako
 
wewe acha kujidanganya, wakristo hasa wakatoliki Wwa Tanganyika mna chuki Sana na uislam na waislam, hivi zile pumba aizoomwaga #Lukuvi Ni nini kama SI chuki na uislam??

Mimi mtizamo wangu ni kuwa ccm haipendi wakristo na waislamu wawe na maelewano ili wasije kuioji juu ya maendeleo wameamua kuwagawa. Hakuna mkristo anamchukia muislamu au muislamu anamchukia mkristo isipokuwa wachache wanaotumika kisiasa kwa manufaa yao binafsi
 
wewe acha kujidanganya, wakristo hasa wakatoliki Wwa Tanganyika mna chuki Sana na uislam na waislam, hivi zile pumba aizoomwaga #Lukuvi Ni nini kama SI chuki na uislam??

Acha ku- generalize mambo. Aliyosema Lukiuvi yamepingwa na watu wa dini zote na wala hakuna ushahidi wowote kama alitumwa na wakatoliki. Lazima tumwandame mtu kwa upofu wake binafsi.
 

Mohamed Said ni mwandishi mahiri Afrika na duniani kwa ujumla, wewe unam-blacklist kirahisi rahisi tu? Hebu funguka zaidi mkuu Mag3 tuuone upande wa pili wa MS
 
Last edited by a moderator:
Umesema, nanukuu "Wazanzibari asilimia 99 ni Waislam. Hii asilimia 99 leo inajua kuwa nchi yao imeungana na Tanganyika mbayo viongozi walioshika madaraka ni Wakristo na wana chuki kubwa na Uislam" . Hi statement ni matusi kwa viongozi wa wa nchi yetu waliopo na waliong'atuka. Je Mzee Mwinyi na Kikwete ambao wamekuwa au ni viongozi wakuu wa dola la Tanzania nao wanachuki na wananchi wenzao? Acha kuandaki mambo kwa hisia.
 
wewe acha kujidanganya, wakristo hasa wakatoliki Wwa Tanganyika mna chuki Sana na uislam na waislam, hivi zile pumba aizoomwaga #Lukuvi Ni nini kama SI chuki na uislam??

Wewe ndo hujui unachoongea kwani Lukuvi ni Mkatoliki?
Hebu tupia mfano mmoja unaoonyesha chuki za wakatoliki dhidi ya uislam.
 
Kinachonikere ni "ushujaa" wa Lukuvi.

Kulikuwa na kafir wa Makkah aliyevuka handaki lililochimbwa na Waislamu na kuingia upande wa Waislamu watupu, kitu cha kwanza alichofanya kafiri yule alipoingia upande wa Waislamu ni kumkata miguu ngamia wake ili kufuta fikra yoyote ile ya kukimbia na kurudi nyuma, kwa maana nyingine alikwenda pale kupigania ukafiri wake mpaka afe!

Mpaka siku Lukuvi atakapoamua kwenda Zanzibar na kusema maneno yake yale mbele ya mhadhara wa Waislamu basi hapo ndipo nitakapomuona si mnafiki lakini kusema maneno kama yale katika "kona nne" za bunge na kujiita si mnafiki huo kwangu mimi ni ubabaishaji wa hali ya juu.
 
Amma kwa hakika hakuna kilichonifariji bungen(BMK) kama maneno ya William Lukuvi alipokuja "kupangua" hoja ya Ibrahim Lipumba.

Katika "kupangua" kwake hiyo hoja ameudhihirishia ulimwengu kuwa kilio cha Waislaam wa Tanzania si cha bure.

Cha kushangaza, amerudia zaidi ya mara tano neno "hofu".

Nauliza, ikiwa leo ana "hofu" ya Zanzibar kuwa nchi ya Kiislaam, jee, Waislaam wana haki ya kuwa na hofu kuwa Tanzania inafanywa, kuanzia kwa Nyerere na mpaka leo hii kwa William Lukuvi, kuwa nchi ya Kikristo?

Hivi Nyerere ana heri ipi ya kuwa "mwenye heri" kuelekea "utakatifu" ilhali aliongoza Serikali isiyo na dini?
 
Uislam zanzibar ni 93% ukristo 5% wasio waslam wala wakristo 2%. Twakimu ya mleta mada ya 99% ni uongo
 

William Lukuvi ana "hofu" kuwa Zanzibar itakuwa nchi ya Kiislaam. Jee, wewe huna hiyo "hofu"?
 

Wapuuzi hawa. Kwa muda mrefu, Rais, Makamu wa Rais, Mkuu wa Polisi, Mkuu wa Intelijensia, Mkuu wa Mahakama, Waziri wa Fedha walikuwa waislamu kwa wakati mmoja lakini bado wanawalaumu wakristu kwa matatizo yao! Amekuwepo Rais Mwinyi kwa miaka kumi baada ya Mwalimu na sasa tuna Rais Jakaya Kikwete anayetimiza mwaka wa 9 madarakani lakini bado wanaona kama vile ni makafir wanaombana Jumbe huko Kigamboni. Wanashindwa kukubali kuwa ni chaguo lake kuishi Tanganyika na sio Zanzibar kama vile wanavyofanya viongozi wastaafu lukuki kutoka nchi hiyo iliyoneemeka.

Amandla.....
 
Mzee Mohamed Said ,leo hii wapingaji na wenye kebehi dhidi yako wamekaa kimya. Ukweli unapodhihiri uongo hauna nafasi,wanajitia kibri kukutukana na kukubeza na hali wanatumia 'nondo' zako kama references kwa kazi zao. Kibaya zaidi wanaona haya kuku-acknowledge!

Ninakuonea tamaa na wivu wa elmu yako kwa upande mmoja,na ninaona faraja na fahari kwa upande mwingine kwa namna tu ulivyo mtu muhimu katika historia ya nchi yetu. Furaha yangu inaongezeka pale unapotumia lugha ya kuelimisha zaidi hasa kwa makusudi kabisa mtu anapokutukana. Allah akuongezee hekma zaidi na maisha marefu,na akujaalie mwisho mwema In Shaa Allah.
 
Last edited by a moderator:

Kwa hiyo wewe unataka Tanganyika nayo iwe nchi ya Kiislamu? Una hofu gani na Ukristu?

Amandla.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…