Kutoka kwa Mtanzania mwenzetu Twahir Abbas

Kutoka kwa Mtanzania mwenzetu Twahir Abbas

Lakini watawala wengi huacha legacy na kukubukwa kwa MAWAZO mazuri yanayoishi, yenye manufaa ENDELEVU na UJENZI wa MIFUMO mizuri yenye tija kwa kizazi kimoja hadi kingine katika kupambana na UMASIKINI, UJINGA, MARADHI na DHULUMA.

Shukrani, mataga wasome bandiko lote hili murua kabisa hapa JamiiForums tukielekea 40 ya mwendazake.
 
Sasa mtoto wa Tunguu huko Zanzibari angejuaje habari za Abrahamu kama amejenga barabara wakati alitoshelezwa na kuambiwa habari za maana ya Demokrasia kisha jambo likaishia hapo,ila huko kwao watoto wa huko huenda hata hawajui habari za maana ya Demokrasia aliyoitoa Ahrahamu ila wanajua kuhusu ujenzi wa barabara.

nyumbu wana tabu mkuu,yaani bora uchunge mbuzi 10 kuliko kumwelewesha nyumbu mmoja.
 
[emoji38][emoji38]anasema hivyo si vitu vya kuacha legacy.

wakati asipotuma pesa ya matumizi nyumbani kwao kwa mwezi,roho yake haitulii.
Diaspora ni mafundi wa kukosoa. Ni burudani ya kipekee ukiwa nao katika group moja la whatsapp, huwa na maoni fulani ya ajabu.
 
Bibi yangu nilidhani alikuwa akithamini sana vitu....nilikosea sana, nilikuja kugundua.. yeye akithamini zaidi tendo la kupewa au kupata. Vitu vilimkumbusha tu watu, na matokeo ya jitihada na upendo wao kwake.

Vitu kwake vilikuwa alama tu ya jambo la muhimu zaidi (uhusiano) lilikokuwa likigusa moyo wake. Maneno matupu hayajengi... Mawazo mazuri ila matupu yasiyo na vitendo vya kuyadhihirisha ni ubatili.

Legacy au urithi wakati mwingine si wathamani kubwa.. ila moyo na jitihada za upendo za mtoaji huishi ndani ya zawadi hizi ndogo. Na wapokeaji wenye hekima hupokea hata ikiwa si cha thamani na watakitunza na kukithamini.



Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Kalamu,
Shilingi ina sura mbili na kampuni ina assets na liabilities. Kwa ni wema upo kwa JPM mimi nimejikita kwenye mazuri aliyofanya, simzuii mtu anaeona upande wa pili wa shilingi.

Hata JK ambae watu tulidhani tuko huru sana, Kibanda na Dr. Ulimboka walikutana na maswahibu na sote tunamshukuru Mungu walipona japo kuna muandishi wa Channel 10, David Mwangosi aliuwawa mbele ya polisi ambao wanadhamana ya kulinda amani.

Juzi UN wametoa tribute ya JPM, sio kwamba hawajui au hawakumbuki ni yapi alifanya hayakurandana na matarajio ya UN, yet wali-embrace mazuri aliyofanya na yanaweza kuigwa na waliopo kwenye utawala na wale watakaokuja kutawala mbele ya safari.

Tofauti za kifikra ni ubinadamu na ni afya kwenye jamii kutofautina ila sio kwa extent ya matusi. Staha ni utu
Kwa mantiki hiyo, tuihimize UNO hiyo pia imusifu Idd Amin na watu wa namna hiyo!

Kiongozi anapokanyaga haki za raia zake hayo mengine anayofanya hayana maana yoyote.

Watumwa waliochukuliwa hapa, hao waliofanya hivyo nao tuwashukuru kwa vile baadhi ya hao watumwa walipewa maisha mazuri?

Kuna mambo ya msingi yasiyotakiwa kwa kiongozi yeyote kuyakanyaga. Akifanya hivyo anaharibu kila kitu.

Kiongozi akanyage Katiba, aliyoapa kuilinda, halafu leo tuseme shilingi ina pande mbili?
 
Anaandika mtanzania mwenzetu Twahir Abasi (kutoka Chuo kikuu cha Sayansi na teknolojia cha Huazhong, huko Wuhan, China).
______
Legacy ya watawala haipo sana kwenye ujenzi wa vitu labda vitu hivyo viwe ni VIKUBWA SANA, vya muhimu sana au vya kipekee sana. Kwa mfano Great wall ya China au Pyramid za Misri.

Lakini watawala wengi huacha legacy na kukubukwa kwa MAWAZO mazuri yanayoishi, yenye manufaa ENDELEVU na UJENZI wa MIFUMO mizuri yenye tija kwa kizazi kimoja hadi kingine katika kupambana na UMASIKINI, UJINGA, MARADHI na DHULUMA.

Thomas Jefferson wa Marekani hakumbukwi kwa visima vya maji alivyochimba, bali anakumbukwa kwa Tamko la Uhuru wa Marekani (Declaration of Independence).

Abraham Lincoln hakumbukwi kwa barabara alizojenga huko New York na Michigan, bali anakumbukwa kwa tamko la kishujaa la kuachia huru watumwa (Emancipation declaration) na Falsafa ya demokrasia (Philosophy of democracy).

Yeye ndiye aliyesema "democracy is a government of the people, by the people, for the people" definition ambayo vizazi na vizazi vimeikariri duniani pote. Mtoto wa form one kule Tunguu (Zbar) au Lutindi (Korogwe) ukimtajia Abraham Lincoln hatakumbuka barabara alizojenga huko Maryland, bali atakumbuka "government of the people, by the people, for the people." Hii ndiyo legacy.

Hata Mwalimu Nyerere hatumkumbuki kwa kujenga viwanda vya nguo vya MWATEX na URAFIKI, au kiwanda cha nyama cha TANGANYIKA PACKERS, bali tunamkumbuka kwa MAWAZO yanayoishi ya kudai UHURU, HAKI, UMOJA na HESHIMA ya MWAFRIKA.

Kizazi kijacho hakitakumbuka Stendi za mabasi, wala madaraja ya juu yaliyojengwa miaka 20 au 50 iliyopita, maana hata chenyewe kitajenga yao. Tena ikibidi hizi flyover za sasa watazivunjilia mbali ili wajenge nyingine zenye ubora zaidi, nyingi zaidi na za kisasa zaidi.

Kizazi kijacho kitaona legacy ya watawala wa sasa kikikuta nchi yenye HAKI na UHURU kama vichocheo vya MAENDELEO YA WATU. Kwa hiyo KATIBA bora ni msingi wa LEGACY imara, Sheria nzuri ni kuta za LEGACY imara, na MIPANGO thabiti ni Paa la Legacy Imara. Legacy sio madaraja au stand za mabasi.

Muhimu zaidi Legacy hailindwi, inajilinda. Legacy haitetewi, inajitetea yenyewe. Asomaye na afahamu.! View attachment 1756583
Toka nimejiunga JF huu ndio uzi 100%
 
Anaandika mtanzania mwenzetu Twahir Abasi (kutoka Chuo kikuu cha Sayansi na teknolojia cha Huazhong, huko Wuhan, China).
______
Legacy ya watawala haipo sana kwenye ujenzi wa vitu labda vitu hivyo viwe ni VIKUBWA SANA, vya muhimu sana au vya kipekee sana. Kwa mfano Great wall ya China au Pyramid za Misri.

Lakini watawala wengi huacha legacy na kukubukwa kwa MAWAZO mazuri yanayoishi, yenye manufaa ENDELEVU na UJENZI wa MIFUMO mizuri yenye tija kwa kizazi kimoja hadi kingine katika kupambana na UMASIKINI, UJINGA, MARADHI na DHULUMA.

Thomas Jefferson wa Marekani hakumbukwi kwa visima vya maji alivyochimba, bali anakumbukwa kwa Tamko la Uhuru wa Marekani (Declaration of Independence).

Abraham Lincoln hakumbukwi kwa barabara alizojenga huko New York na Michigan, bali anakumbukwa kwa tamko la kishujaa la kuachia huru watumwa (Emancipation declaration) na Falsafa ya demokrasia (Philosophy of democracy).

Yeye ndiye aliyesema "democracy is a government of the people, by the people, for the people" definition ambayo vizazi na vizazi vimeikariri duniani pote. Mtoto wa form one kule Tunguu (Zbar) au Lutindi (Korogwe) ukimtajia Abraham Lincoln hatakumbuka barabara alizojenga huko Maryland, bali atakumbuka "government of the people, by the people, for the people." Hii ndiyo legacy.

Hata Mwalimu Nyerere hatumkumbuki kwa kujenga viwanda vya nguo vya MWATEX na URAFIKI, au kiwanda cha nyama cha TANGANYIKA PACKERS, bali tunamkumbuka kwa MAWAZO yanayoishi ya kudai UHURU, HAKI, UMOJA na HESHIMA ya MWAFRIKA.

Kizazi kijacho hakitakumbuka Stendi za mabasi, wala madaraja ya juu yaliyojengwa miaka 20 au 50 iliyopita, maana hata chenyewe kitajenga yao. Tena ikibidi hizi flyover za sasa watazivunjilia mbali ili wajenge nyingine zenye ubora zaidi, nyingi zaidi na za kisasa zaidi.

Kizazi kijacho kitaona legacy ya watawala wa sasa kikikuta nchi yenye HAKI na UHURU kama vichocheo vya MAENDELEO YA WATU. Kwa hiyo KATIBA bora ni msingi wa LEGACY imara, Sheria nzuri ni kuta za LEGACY imara, na MIPANGO thabiti ni Paa la Legacy Imara. Legacy sio madaraja au stand za mabasi.

Muhimu zaidi Legacy hailindwi, inajilinda. Legacy haitetewi, inajitetea yenyewe. Asomaye na afahamu.! View attachment 1756583
Busara tupu hizi. Mawazo huishi milele bali majengo ni ya muda.
 
Kwa mantiki hiyo, tuihimize UNO hiyo pia imusifu Idd Amin na watu wa namna hiyo!

Kiongozi anapokanyaga haki za raia zake hayo mengine anayofanya hayana maana yoyote.

Watumwa waliochukuliwa hapa, hao waliofanya hivyo nao tuwashukuru kwa vile baadhi ya hao watumwa walipewa maisha mazuri?

Kuna mambo ya msingi yasiyotakiwa kwa kiongozi yeyote kuyakanyaga. Akifanya hivyo anaharibu kila kitu.

Kiongozi akanyage Katiba, aliyoapa kuilinda, halafu leo tuseme shilingi ina pande mbili?
Soma kitabu kinaitwa; War in Uganda and legacy of IDD Amin.
"By Tony Avirgan and Martha Honey."
Kiliandikwa na waandishi wamarekani walioshiriki kwenye vita ya Kagera mwanzo mppaka mwisho
 
Asante mtoa mada kwa maelezo yaliyonyooka. Sisi Watanzania hatukuwa na Rais bali kutokana na ajali ya kisiasa ya mwaka 2015 tulipata Shetani aliyejifanya anajuwa kila kitu.

Bado kuna Watanzania wapumbavu wengi tu ambao wanamsifia na ndiyo hao wanalazimisha hiyo legacy. Legacy haijadiliwi inakuja yenyewe.

Kwa kweli sioni cha kukaa na kumsifia Magufuli ambaye ameturudisha nyuma miaka 20 kiuchumi.

Lakini tumshukuru Mungu analioenda Taifa letu, alipomuona anapata kiburi na kutaka kubadili ukomo wa utawala alamtupilia Jehanam.
Magufuli hata yale mazuri aliyofanya yaliharibiwa na mambo mabaya kupita kiasi aliyofanya. Kila nikikumbuka watu walivyofariki kwa corona kwa kukosa miongozo sahihi ya serikali huku yeye anakataza watu kuongelea kabisa hilo suala huwa naona akili zake zilikuwa zina hitilafu. Watu wanakufa kwa mateso makali na rais anajua lakini anajifanya hakuna shida yoyote?
 
Soma kitabu kinaitwa; War in Uganda and legacy of IDD Amin.
"By Tony Avirgan and Martha Honey."
Kiliandikwa na waandishi wamarekani walioshiriki kwenye vita ya Kagera mwanzo mppaka mwisho
"---waandishi wamarekani walioshiriki kwenye vita ya Kagera"? Kulikuwepo na 'mercenary' katika vita hivyo?

Siwezi kwenda kusoma kitabu kwa jambo kama hili.

Kwa hiyo waliandika nini, jinsi Idd Amin alivyoitumikia Uganda kwa uaminifu mkubwa na jinsi waganda walivyompenda kiongozi wao?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Anaandika mtanzania mwenzetu Twahir Abasi (kutoka Chuo kikuu cha Sayansi na teknolojia cha Huazhong, huko Wuhan, China).
______
Legacy ya watawala haipo sana kwenye ujenzi wa vitu labda vitu hivyo viwe ni VIKUBWA SANA, vya muhimu sana au vya kipekee sana. Kwa mfano Great wall ya China au Pyramid za Misri.

Lakini watawala wengi huacha legacy na kukubukwa kwa MAWAZO mazuri yanayoishi, yenye manufaa ENDELEVU na UJENZI wa MIFUMO mizuri yenye tija kwa kizazi kimoja hadi kingine katika kupambana na UMASIKINI, UJINGA, MARADHI na DHULUMA.

Thomas Jefferson wa Marekani hakumbukwi kwa visima vya maji alivyochimba, bali anakumbukwa kwa Tamko la Uhuru wa Marekani (Declaration of Independence).

Abraham Lincoln hakumbukwi kwa barabara alizojenga huko New York na Michigan, bali anakumbukwa kwa tamko la kishujaa la kuachia huru watumwa (Emancipation declaration) na Falsafa ya demokrasia (Philosophy of democracy).

Yeye ndiye aliyesema "democracy is a government of the people, by the people, for the people" definition ambayo vizazi na vizazi vimeikariri duniani pote. Mtoto wa form one kule Tunguu (Zbar) au Lutindi (Korogwe) ukimtajia Abraham Lincoln hatakumbuka barabara alizojenga huko Maryland, bali atakumbuka "government of the people, by the people, for the people." Hii ndiyo legacy.

Hata Mwalimu Nyerere hatumkumbuki kwa kujenga viwanda vya nguo vya MWATEX na URAFIKI, au kiwanda cha nyama cha TANGANYIKA PACKERS, bali tunamkumbuka kwa MAWAZO yanayoishi ya kudai UHURU, HAKI, UMOJA na HESHIMA ya MWAFRIKA.

Kizazi kijacho hakitakumbuka Stendi za mabasi, wala madaraja ya juu yaliyojengwa miaka 20 au 50 iliyopita, maana hata chenyewe kitajenga yao. Tena ikibidi hizi flyover za sasa watazivunjilia mbali ili wajenge nyingine zenye ubora zaidi, nyingi zaidi na za kisasa zaidi.

Kizazi kijacho kitaona legacy ya watawala wa sasa kikikuta nchi yenye HAKI na UHURU kama vichocheo vya MAENDELEO YA WATU. Kwa hiyo KATIBA bora ni msingi wa LEGACY imara, Sheria nzuri ni kuta za LEGACY imara, na MIPANGO thabiti ni Paa la Legacy Imara. Legacy sio madaraja au stand za mabasi.

Muhimu zaidi Legacy hailindwi, inajilinda. Legacy haitetewi, inajitetea yenyewe. Asomaye na afahamu.! View attachment 1756583
Yote hii ni kuhangaika na marehemu,hakika wewe ni mwehu,hutoweza kumfuta
 
Hebu acha ujinga wako! Ni wapi ilipopigwa marufuku kumjadili magufuli akiwa hai au mfu!? Mbona yesu anajadiliwa mpaka kesho kutwa? 😳
Yote hii ni kuhangaika na marehemu,hakika wewe ni mwehu,hutoweza kumfuta
 
Hebu nisaidie Kiongozi... Ni kiongozi gani duniani aliwapa urithi taifa lake kutoka mikononi mwake au mfukoni mwake.. na alifanya mambo ambayo wananchi hawakumtuma awafanyie!?

Kama hayupo chukua Rais au Mfalme yeyote ambaye ni relevant kwa maisha yetu leo, unipe mifano ambayo amefanya kwa watu anaowaongoza kwa fedha yake na leo tunai-recognize kama Legacy ya Kiongozi huyo.

I would love to learn, ili wenye nia ya kujifunza tujue zaidi juu ya "Legacy/Urithi" wa viongozi.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
1.Hayati Mwl.J.K.Nyerere alifanikiwa kuwaunganisha watanzania wa makabila yote nchini kwa matumizi ya lugha ya kiswahili. Mtazania anawasiliana na mtanzania mwenzie vizuri popote pale nchini kitu ambacho in adimu kwenye nchi nyingine.

1.Mahtma Gandhi anakumbukwa kwa kudai Uhuru kutoka kwa waingereza kwa kuhamasisha uasi na mapambano ya kudai Uhuru bila kusababisha uharibifu wa mali na watu.(Non violent protracted peoples war) Hatimae akashinda vita na India ikapata Uhuru.

3.Nelson Mandera ;.
Huyu alifungwa miaka 27 na makaburu, alipoachiwa na kuchaguliwa kuwa rais wa Afrka ya kusini, aliunda tume ya ukweli na maridhiano ili kujenga taifa moja llilokuwa limegawanyika kwa misingi ya ubaguzi wa rangi na kutawala muhula mmoja licha ya mateso yote ya miaka 27 gerezani.
Gereza alipokuwa amefungwa, kitanda alichokuwa akilala na vifaa vingine alivyokuwa anatumia ni vivutio vya utalii.

Wapo akina Winston Churchill , Franklin Roosevelt. Jerry Rawlings na wengine,
 
"---waandishi wamarekani walioshiriki kwenye vita ya Kagera"? Kulikuwepo na 'mercenary' katika vita hivyo?

Siwezi kwenda kusoma kitabu kwa jambo kama hili.

Kwa hiyo waliandika nini, jinsi Idd Amin alivyoitumikia Uganda kwa uaminifu mkubwa na jinsi waganda walivyompenda kiongozi wao?
Usiwe mvivu wa kusoma, we soma kitabu utaelewa mkuu.
 
1.Hayati Mwl.J.K.Nyerere alifanikiwa kuwaunganisha watanzania wa makabila yote nchini kwa matumizi ya lugha ya kiswahili. Mtazania anawasiliana na mtanzania mwenzie vizuri popote pale nchini kitu ambacho in adimu kwenye nchi nyingine.

1.Mahtma Gandhi anakumbukwa kwa kudai Uhuru kutoka kwa waingereza kwa kuhamasisha uasi na mapambano ya kudai Uhuru bila kusababisha uharibifu wa mali na watu.(Non violent protracted peoples war) Hatimae akashinda vita na India ikapata Uhuru.

3.Nelson Mandera ;.
Huyu alifungwa miaka 27 na makaburu, alipoachiwa na kuchaguliwa kuwa rais wa Afrka ya kusini, aliunda tume ya ukweli na maridhiano ili kujenga taifa moja llilokuwa limegawanyika kwa misingi ya ubaguzi wa rangi na kutawala muhula mmoja licha ya mateso yote ya miaka 27 gerezani.
Gereza alipokuwa amefungwa, kitanda alichokuwa akilala na vifaa vingine alivyokuwa anatumia ni vivutio vya utalii.

Wapo akina Winston Churchill , Franklin Roosevelt. Jerry Rawlings na wengine,
Mandele hajufungwa miaka 27 ni uongo mkubwa
 
Back
Top Bottom