Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Sehemu ya 5
Watu walilala ila yule muhindi akawa naye hajalala na mimi nilikuwa nimesimama nikijua kazi imeanza, nilisikia sauti ikisema mkate wenge mejaa, ghafla nilishtukizwa na kofi moja matata sana nyuma ya kichogo na kusindikizwa na mtama chini nilianguka mzima mzima mpaka chini na wenge lilikata kweli.

Muhindi yule bwana Bensonii naye hakutaka kukubali hivi hivi ila alitoa pesa haswa wenyewe wakisisitiza na kauli yao usitujazie nzi hapa. Na sisi wateja pia tuliibiwa na watu wakasepa.

Mimi nimeenda kuiba ila nikaibiwa kwa kweli jiji la Arusha nyakati hizo lilikuwa na ubabe sana sio mtoto, sio mwanamke, sio mzee kila mtu ni mbabe na hataki kuonewa. Polisi nao sio haba haswa kipindi hicho tukio likitokea mtakaa hadi nusu saa ndio muwaone. Mi nilitoka na sikuwaona wale jamaa zangu, ikanibidi nipige ngoko mpaka kule kambi niliwakuta na kuwahoji kulikoni?

Wao walisema mpango umefeli kuna watu wameuza ramani yao kwa genge lingine kukawa na mvutano wa hapa na pale kisha tukaachana kwa ahadi tutakutana tena siku nyingine.

Niliondoka Arusha nakwenda Rombo tena nikawakuta wadogo zangu na kuwapa zawadi kidogo kidogo, nakutaka kujua maisha yanaendaje kwa kweli malalamiko yalikuwa ni mengi haswa ukizingatia wabibi wakizeeka wanakuwa na maneno sana.

Niliwaahidi naenda mjini nakirudi basi ntawachukua twende wote mjini nao walifurahi na kuonyesha tabasamu lao ambalo kwangu lilinipa moyo sana na faraja.

Hii ilikuwa ni mwaka 2003 nakumbuka nilikuwa na moto sana wakutoboa kwenye maisha na kuwasaidia wadogo zangu hivyo dili za magendo ndio zilikuwa zina unafuu na chanel nilikuwa nishaanza kuziona.

Nyakati hizi niliungana na Mroso wa Matejoo na Palangyo wa Tengeru tuliungana na kuwa kundi moja hivo lengo letu lilikuwa ni kuendesha matukio ya ujambazi hii njia ya Arusha na Moshi haswa tukiwatarget wafanyabiashara wa madini maana walikuwa na fujo sana mjini kipindi wamepata hela na ilikuwa rahisi kuwagundua.

Tulijua kuwavizia huko Mererani ni risky sana maana nao huwa wako rafu mno katika uendeshaji na wengi wamejipanga hivyo tulibidi tujiongeze kwa kutafta wadada wawili mmoja kwa jina Mankah wa Machame Nronga na mwingine Adela Mrombo wa Mashati wote walikuwa weupe na wanalipa.

Hapa sasa tulimtafuta Kicherema yeye ni Mkenya mtaalam sana wa mambo ya madawa haya kizungu na alitupatia maji ambayo anasema ni kemikali sumu na inaweza kumzimisha mtu. Alitwambia ni nitrous oxide kwahyo hata sisi tuwe nayo makini. Tulianza kuwawinda haswa huko huko Mererani kwenye nyumba za wageni na 🍺🍻. Mara nyingi hawa wakishapiga mishondo wanakuwa na wapambe saivi ndio chawa ila kipindi hicho ni wapambe.

Nakumbuka aliingia Ima akiwa na wapambe wake akamwita meneja wa bar na kumpa hela acheze wimbo mmoja tu aliuchagua mpaka achoke. Kutokana na watoto wale wakichaga nimekaa nao pale wanaita jamaa alituma wapambe wake waje na sisi tulikuwa 5 jumla wanaume 3 na warembo 2. Hivo sisi hatukubana nao wakasema hawana hela hawa miyeyusho hivyo wakatuhama nakuhamia meza kuu ya hela.

Hapo tuliona mambo yanaenda kama tulivyopanga. Sisi tuliondoka na kwenda eneo letu kutulia tukisubiri ishara.

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.


"Mkate wenge mejaa"😂
kumbe akili zenyuu sio kosa lenu ni kawaida huko bange kubeli miraa bado pombe karee😎!!
 
Sehemu ya 5
Watu walilala ila yule muhindi akawa naye hajalala na mimi nilikuwa nimesimama nikijua kazi imeanza, nilisikia sauti ikisema mkate wenge mejaa, ghafla nilishtukizwa na kofi moja matata sana nyuma ya kichogo na kusindikizwa na mtama chini nilianguka mzima mzima mpaka chini na wenge lilikata kweli.

Muhindi yule bwana Bensonii naye hakutaka kukubali hivi hivi ila alitoa pesa haswa wenyewe wakisisitiza na kauli yao usitujazie nzi hapa. Na sisi wateja pia tuliibiwa na watu wakasepa.

Mimi nimeenda kuiba ila nikaibiwa kwa kweli jiji la Arusha nyakati hizo lilikuwa na ubabe sana sio mtoto, sio mwanamke, sio mzee kila mtu ni mbabe na hataki kuonewa. Polisi nao sio haba haswa kipindi hicho tukio likitokea mtakaa hadi nusu saa ndio muwaone. Mi nilitoka na sikuwaona wale jamaa zangu, ikanibidi nipige ngoko mpaka kule kambi niliwakuta na kuwahoji kulikoni?

Wao walisema mpango umefeli kuna watu wameuza ramani yao kwa genge lingine kukawa na mvutano wa hapa na pale kisha tukaachana kwa ahadi tutakutana tena siku nyingine.

Niliondoka Arusha nakwenda Rombo tena nikawakuta wadogo zangu na kuwapa zawadi kidogo kidogo, nakutaka kujua maisha yanaendaje kwa kweli malalamiko yalikuwa ni mengi haswa ukizingatia wabibi wakizeeka wanakuwa na maneno sana.

Niliwaahidi naenda mjini nakirudi basi ntawachukua twende wote mjini nao walifurahi na kuonyesha tabasamu lao ambalo kwangu lilinipa moyo sana na faraja.

Hii ilikuwa ni mwaka 2003 nakumbuka nilikuwa na moto sana wakutoboa kwenye maisha na kuwasaidia wadogo zangu hivyo dili za magendo ndio zilikuwa zina unafuu na chanel nilikuwa nishaanza kuziona.

Nyakati hizi niliungana na Mroso wa Matejoo na Palangyo wa Tengeru tuliungana na kuwa kundi moja hivo lengo letu lilikuwa ni kuendesha matukio ya ujambazi hii njia ya Arusha na Moshi haswa tukiwatarget wafanyabiashara wa madini maana walikuwa na fujo sana mjini kipindi wamepata hela na ilikuwa rahisi kuwagundua.

Tulijua kuwavizia huko Mererani ni risky sana maana nao huwa wako rafu mno katika uendeshaji na wengi wamejipanga hivyo tulibidi tujiongeze kwa kutafta wadada wawili mmoja kwa jina Mankah wa Machame Nronga na mwingine Adela Mrombo wa Mashati wote walikuwa weupe na wanalipa.

Hapa sasa tulimtafuta Kicherema yeye ni Mkenya mtaalam sana wa mambo ya madawa haya kizungu na alitupatia maji ambayo anasema ni kemikali sumu na inaweza kumzimisha mtu. Alitwambia ni nitrous oxide kwahyo hata sisi tuwe nayo makini. Tulianza kuwawinda haswa huko huko Mererani kwenye nyumba za wageni na 🍺🍻. Mara nyingi hawa wakishapiga mishondo wanakuwa na wapambe saivi ndio chawa ila kipindi hicho ni wapambe.

Nakumbuka aliingia Ima akiwa na wapambe wake akamwita meneja wa bar na kumpa hela acheze wimbo mmoja tu aliuchagua mpaka achoke. Kutokana na watoto wale wakichaga nimekaa nao pale wanaita jamaa alituma wapambe wake waje na sisi tulikuwa 5 jumla wanaume 3 na warembo 2. Hivo sisi hatukubana nao wakasema hawana hela hawa miyeyusho hivyo wakatuhama nakuhamia meza kuu ya hela.

Hapo tuliona mambo yanaenda kama tulivyopanga. Sisi tuliondoka na kwenda eneo letu kutulia tukisubiri ishara.

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.
Katika misheni za ujangiri hajakutana na kina master huko a.k.a Umughaka ???
 
Kama uliyaweza maisha ya kigoma-kasulu-kibondo basi wew ni kiboko popote unaishi

Mkeo umemchalanga na mapanga lakin wewe unaenda kula vya wenzio

Matukio yote hayo lakin polisi hukuwah kulala,ulikuwa na nyota ya ajabu sana
Hii stori imenifunza kuwa WABAYA HUTENGENEZWA.
Jamii ikichukua jukumu lake katika malezi huenda tukapata kizazi bora na kinyume chake ni kweli
 
Sehemu ya 12
Niliondoka nakurudi mwanga kisha kurudi Tabora. Baada ya kufika Tabora nilimkuta mwanamke wangu na mwanaume mwingine geto kwangu, hasira zilinipanda sana ila kila nikipiga hesabu niwafanye nini naona haiji kabisa na nguvu nilikosa. Ilibidi niondoke na kwenda mMwinyi Mchichani maeneo ya bar [emoji481] kupiga vyombo kidogo. Kule nilipata dokezo juu ya vifo vya kina Kinehe na Mpoladuhu. Ila Madelagawisa yeye alikuwa korokoroni hivyo nikaona kukaa hapa Tabora ni msala tayari.

Nikarudi home mida ikiwa imeenda, kufika bado namkuta msela hajaondoka ilibidi nipambane nae sasa kiume na mwanamke akanipigia kelele za mwizi! Saa hiyo tungi na mimi zipo kichwani, watu wakaja full shangwe wakijua ni mwizi kweli ila bahati nzuri na pona yangu majirani ndio walikuwa wa kwanza kufika na wenyewe kutaka kujua kulikoni?
Mimi nikasema huyo ni mke wangu na nimemfumania, mwanamke naye anasema mimi siyo mumewe ila nilikuwa mpenzi na tulishaachana sasa nimekuja kumvunjia ndoa yako.

Kutokana na pombe watu wakanisihi niondoke na niwe mstaarabu kesho pakikucha basi nirudi nikiwa timamu. Kwangu niliona hapakuchi kabisa nikaondoka na kurudi Mwinyi nilila huko kwa tungi mpaka majogoo. Mida ya saa nne nilienda Kiyungi kuvuta bangi kidogo ili akili ikae sawa, na kweli ilikaa sawa nikaenda geto Isevya nikatulia zangu kimya kwa muda wa wiki nzima nawaza na kuwazua.

Usiku wa saa mbili nilitoka na kwenda kwa mwanamke, bahati nzuri nilimkuta nikamuuliza tena mara ya mwisho mimi ni mwizi na siyo mumeo? Akanijibu usinisumbue huku akifyonza kurudi ndani na mimi sikuchukua raundi nilimlima na panga upande wa kushoto kichogoni kwenda kwenye sikio alipiga kelele nikamwongeza lingine akiwa tayari yuko chini ni kama naua nyoka. Kisha nikakimbia usiku huo huo na kuelekea mpaka Usule. Nilikaa huko mpaka kunapambazuka, nikarudi Mwinyi kesho yake pale pale bar nikaambiwa natafutwa kama shilingi kwa kumjeruhi mwanamke na mapanga. Sikujali sana nikaanza kuunga unga magari mpaka nikafika Sikonge. Nililala usiku mmoja hapo Sikonge likapita doria kali sana kwenye nyumba za wageni ila hawakunibaini.

Kutoka nilienda mpaka Chunya kisha nikaingia Mbeya Mjini. Nililala Mbeya siku moja alfajiri na mapema kulivyokucha nikaingia stendi bahati nzuri nikakutana na jamaa mmoja wa kitambo kidogo huko Arusha. Tukapiga story sana mi nikamwambia sasa hivi nafanya biashara ya karanga kutoka Malawi kuja Tanzania. Na yeye akaniambia sasa hivi ana miaka 2 Mbeya anafanya kazi kubadili hela na kijiwe chao kikuu ni Tunduma. Nikampa hongera na kumuuliza unaelekea Tunduma sio? Akasema bado kuna hela anasikilizia basi na mimi nikamwambia tutafte eneo tukae tunywe kidogo maana tumekutana ugenini basi muhimu kukumbukana.

Nakweli bila hiyana alikubali na kwasababu yeye ni mwenyeji zaidi yangu basi tulienda location kujipongeza.

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho
Wanawake wa kinyamwezi ni hatari kwa afya yako
 
Yeah yeah ....
Here we gou ..
Iz lk story about NYOKAA, TUMBONII ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC ETC
enzi hizo our native land Arusha ikiwa On firE.











but mwendelezo plzz ..
 
Hivi ni kwanini hii sehemu inaua sana, kuna mteremko au njia nyembamba?

Nafikiri nimepita njia hiyo kutokea Arusha kwenda Mererani lkn ramani imenitoka sina kumbukumbu na mwonekano wa eneo hilo
Daraja la Nduruma lilikuwa likiua sana wakati barabara ilikuwa finyu.

Pia ndiko mteremko mkali unaishia ujitokea Arusha mjini.
Huo mteremko ni mkali magari yakifeli breki hasa magari makubwa huleta madhara.
Kwasasa barabara ni mbili na daraja limejengwa vizuri sana ni ngumu gari kuangukia mtoni
 
Daraja la Nduruma lilikuwa likiua sana wakati barabara ilikuwa finyu.

Pia ndiko mteremko mkali unaishia ujitokea Arusha mjini.
Huo mteremko ni mkali magari yakifeli breki hasa magari makubwa huleta madhara.
Kwasasa barabara ni mbili na daraja limejengwa vizuri sana ni ngumu gari kuangukia mtoni
OK, kumbe ni barabara kuu ya Moshi - Arusha!

Ahsante
 
Back
Top Bottom