Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 7,207
- 17,674
Habari wana jamvi.
Mwaka jana baada ya timu ya Arsenal kufanya vibaya kwenye ligu kuu ,mashabiki wake kote duniani walipaza na kumzomea kocha mkuu Wenger aondoke ili kupisha mabadiliko ya kiungozi kwenye timu hiyo.
Kocha Wenger aliwapuuza sana mashabiki hao lakini mwisho wa siku aliamua kusikiliza kilio chao na kuamua kuondoka kwa kukubali ukweli kwamba timu inapofanya vibaya wakulaumiwa ni kocha na ni lazima hutimuliwa.
Nimetolea mfano wa timu ya Arsenal kwa kulinganisha na ufanyaji vibaya wa chama kikuu cha upinzani nchini Chadema.
Chadema toka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 imepoteza mvuto kwa wananchi ! Madiwani na wabunge wa chadema wanajivua nyasifa zao ndani ya chama hicho na kuomba kupokelewa ccm.! Yote haya yanatokea kocha akiwa Mbowe.
Kwa hali ilivyo sasa ndani ya chama hicho hamna namna ambayo Mbowe atazuia anguko la chadema nchini.
Ili kuruhusu mabadiliko na morali mpya ndani ya chadema ni lazima kocha Mbowe azomewe na kufukuzwa kama kocha Arsene Wenger wa Arsenal.
Hoja ya kwamba Mbowe akiondoka chadema itaangukia mikononi mwa wasaliti haina mashiko mbele ya wapenda mabadiliko.
Hata akina Lipumba , Mbatia , Cheyo , Mrema walikuwa wanasema hivi hivi eti wakiondoka chama kitakaliwa na wasaliti . Kiko wapi sasa?
#Mbowe must Go
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwaka jana baada ya timu ya Arsenal kufanya vibaya kwenye ligu kuu ,mashabiki wake kote duniani walipaza na kumzomea kocha mkuu Wenger aondoke ili kupisha mabadiliko ya kiungozi kwenye timu hiyo.
Kocha Wenger aliwapuuza sana mashabiki hao lakini mwisho wa siku aliamua kusikiliza kilio chao na kuamua kuondoka kwa kukubali ukweli kwamba timu inapofanya vibaya wakulaumiwa ni kocha na ni lazima hutimuliwa.
Nimetolea mfano wa timu ya Arsenal kwa kulinganisha na ufanyaji vibaya wa chama kikuu cha upinzani nchini Chadema.
Chadema toka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 imepoteza mvuto kwa wananchi ! Madiwani na wabunge wa chadema wanajivua nyasifa zao ndani ya chama hicho na kuomba kupokelewa ccm.! Yote haya yanatokea kocha akiwa Mbowe.
Kwa hali ilivyo sasa ndani ya chama hicho hamna namna ambayo Mbowe atazuia anguko la chadema nchini.
Ili kuruhusu mabadiliko na morali mpya ndani ya chadema ni lazima kocha Mbowe azomewe na kufukuzwa kama kocha Arsene Wenger wa Arsenal.
Hoja ya kwamba Mbowe akiondoka chadema itaangukia mikononi mwa wasaliti haina mashiko mbele ya wapenda mabadiliko.
Hata akina Lipumba , Mbatia , Cheyo , Mrema walikuwa wanasema hivi hivi eti wakiondoka chama kitakaliwa na wasaliti . Kiko wapi sasa?
#Mbowe must Go
Sent using Jamii Forums mobile app