Kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, waislamu bado wanazo sababu za kuzuia wanawake kwenda kuzika?

Kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, waislamu bado wanazo sababu za kuzuia wanawake kwenda kuzika?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Nilikuwa naangalia hii video niliyotumiwa na rafiki ya mmoja.


Kwenye video hii inaonesha tangu mtu anafungwa kwenye sanda mpaka anazikwa.

Nikajiuliza ni kwa nini waislamu wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, ni Muongozo wa dini yao unaotokana na maamrisho ya mwenyezimungu yaliyomo kwenye Quran Tukufu, ama ni tamaduni tu?

Waislamu ulimwengu mzima wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, hicho kinachofanya wanawake kuzuiwa kwenda kuzika, kwa maendeleo haya ya teknolojia hasa ya mawasiliano, wanawake hawawezi kukiona?

Je, picha za video na mitandao ya kijamii haiwezi kumfanya mwanamke wa Kiislamu kujua nini huwa kinafanyika kwenye maziko ya Kiislamu?
 
Cha kushangaza Hao hao wanaokatazwa kwenye dini yao,
Akifariki jirani Mkristo wana hudhuria kwa kufuata taratibu zote za kikristo,ikiwemo kumtazama Marehemu kwa mara ya mwisho(kuaga mwili wa marehem)
Na kuhudhuria makaburini wkt wa mazishi.
 
Nilikuwa naangalia hii video niliyotumiwa na rafiki ya mmoja.


Kwenye video hii inaonesha tangu mtu anafungwa kwenye sanda mpaka anazikwa.

Nikajiuliza ni kwa nini waislamu wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, ni Muongozo wa dini yao unaotokana na maamrisho ya mwenyezimungu yaliyomo kwenye Quran Tukufu, ama ni tamaduni tu?

Waislamu ulimwengu mzima wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, hicho kinachofanya wanawake kuzuiwa kwenda kuzika, kwa maendeleo haya ya teknolojia hasa ya mawasiliano, wanawake hawawezi kukiona?

Je, picha za video na mitandao ya kijamii haiwezi kumfanya mwanamke wa Kiislamu kujua nini huwa kinafanyika kwenye maziko ya Kiislamu?
Hakuna dini inayoenda na wakati.
Unachouliza ni kwamba mpaka sasa bado uislamu hauoni haja ya kuingiza mambo ya kipagani yaani yakikafili (mambo ya kisasa)kwenye dini
 
Hakuna dini inayoenda na wakati.
Unachouliza ni kwamba mpaka sasa bado uislamu hauoni haja ya kuingiza mambo ya kipagani yaani yakikafili (mambo ya kisasa)kwenye dini
Hapo ndiyo ujenge hoja Sasa. Mimi nataka kuongeza ufahamu wangu kuhusu jambo hili na siyo kuanzisha mabishano.

1gb naye kaongezea jambo hapo kwenye bandiko lake msome.
 
Dini zina masharti ya kihayawani sana na watu wala hawataki kujiuliza wanayaamini tu hata kama hayana maana yoyote.

Unajiuliza kwamba mwanamke akiona maziko Mungu anateseka na nini ama anaumia wapi ama, ama mwanamke akiona maziko atamzuia marehemu kwenda akhera?

Ni mambo ambayo hata common sense tu inakataa lakini unaambiwa ni maelekezo ya Mungu, unajiuliza huyo Mungu wakati anatoa hayo maagizo alikua amechanganyikiwa ama dish limeyumba ama ni nini shida?

Dini ni ulevi mbaya sana.
 
Je, ni Muongozo wa dini yao unaotokana na maamrisho ya mwenyezimungu yaliyomo kwenye Quran Tukufu,
Nimegundua kuwa wewe huna lengo la kujifunza. Nyuzi zako za zamani nilikuwa nadhani unataka kujifunza, lakini nimegundua hutaki kujifunza. Ulishawahi kuanzisha uzi (upo Jukwaa la Dini) ukauliza kuhusu Sunnah na ukajibiwa. Ila sijui why unauliza swali kama hili tena.



Je, picha za video na mitandao ya kijamii haiwezi kumfanya mwanamke wa Kiislamu kujua nini huwa kinafanyika kwenye maziko ya Kiislamu?
Wanawake kutokwenda kuzika sio kwa sababu walikuwa hawajui/hawajawahi kujua mazishi ya Kiislam. Unafikiri wanawake hawaendi kuzika kwa sababu hawajui mazishi ya Kiislam? Wanawake katika Uislam wanalazimika kuisoma Dini yao kama wanaume. Wanawake wanatakiwa kuisoma Dini yao, hakunaga kauli za "mwanamke hana Dini" katika Uislam. Wanawake pia wanakalifishwa na Shariah za Allah, na kuitekeleza Dini kunahitajika Elimu/kusoma, hivyo nao lazima wasome.

Ila hukmu hutofautiana baina ya wanaume na wanawake katika baadhi ya mambo ya Kishari'ah kwa Hikma ya Allah ambaye kawaumba wanawake na wanaume na anawajua vizuri zaidi. Mfano wote wanapaswa kuswali (wanawake na wanaume) ila kuna hukmu wanatofautiana.

Sio kwamba wanaonewa au kukandamizwa.

Na sio kwamba hawafanyi mambo fulani kwa sababu tu hawajui/hawawezi kujua. Kama unavyotaka kuashiria.

Kukutaarifu tu;
Wanawake wanaosha maiti za wanawake wenzao, bali Mwanamke anaruhusiwa kuiosha maiti ya mumewe, wanawake wanaweza kukafini wanawake wenzao (kuwavika sanda). Wanawake wanaswalia maiti (ya mwanamume au mwanamke), hawaendi tu kuzika makaburini.

Kutokwenda makaburini kuzika isikupe tabu. Kukatazwa wanawake kufanya jambo fulani wala sio ajabu. Hili hata kwa wanaume, kuna mambo wanakatazwa ila wanawake wanaruhusiwa. Mfano ni haramu mwanaume kuvaa dhahabu (hapa duniani) ila ni halali kwa wanawake, ni haramu wanaume kuvaa hariri (hapa duniani) ila ni halal kwa wanawake.

Kuna mambo wanaume wanalazimishwa ila kwa wanawake wamepewa hiari, mfano ni ni LAZIMA mwanaume kuswali Swala ya Ijumaa, ila mwanamke anaweza kuswali Swala ya Ijumaa au akitaka akaswali Dhuhr nyumbani kwake badala ya Swala ya Ijumaa, hiari hiyo hajapewa mwanaume, LAZIMA kwa mwanaume (labda awe na udhuru wa kishari'ah). Ni lazima mwanaume kuswali Swala za Faradhi Msikitini katika Jamaa (isipokuwa anapokuwa na udhuru wa kishari'ah utakaomfanya asiswali Jamaa msikitini) ila sio lazima kwa mwanamke kuswali Jamaa msikitini, ila anaweza kuswali msikitini.



Na mifano mengine mingi.


Hukumu zinaweza kubadilika si kwa jinsia tu, hata mtu mmoja huyo huyo, hukmu katika mambo ya Ibadah zinaweza kubadilika kwake kulingana na hali, mfano; mtu anawajibika kuswali Swala tano za Faradhi, ila anavyoswali akiwa katika hali ya kawaida (mzima na afya) ni tofauti kidogo na atakavyoswali katika hali za dharura kama ugonjwa na safari (kuna tahfifu kapewa), hukmu zinabadilika kulingana na hali yake atakayokuwa nayo na Shari'ah ishaweka bayana katika kila hali.

Uislam sio Dini ya Usawa. Ni Dini ya UADILIFU. Hakuna usawa katika Uislam, kuna Uadilifu.

So usitake kutaka kuleta mambo ya "usawa" yaliyotokana na fikra za watu nje ya Uislam (ambazo ni uongo mtupu na uharibifu).

Tunaridhia Shari'ah kutoka kwa Mola wetu. Na tunasikia na tunatii.

Na Allah ni Mjuzi zaidi.
 
Nilikuwa naangalia hii video niliyotumiwa na rafiki ya mmoja.


Kwenye video hii inaonesha tangu mtu anafungwa kwenye sanda mpaka anazikwa.

Nikajiuliza ni kwa nini waislamu wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, ni Muongozo wa dini yao unaotokana na maamrisho ya mwenyezimungu yaliyomo kwenye Quran Tukufu, ama ni tamaduni tu?

Waislamu ulimwengu mzima wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, hicho kinachofanya wanawake kuzuiwa kwenda kuzika, kwa maendeleo haya ya teknolojia hasa ya mawasiliano, wanawake hawawezi kukiona?

Je, picha za video na mitandao ya kijamii haiwezi kumfanya mwanamke wa Kiislamu kujua nini huwa kinafanyika kwenye maziko ya Kiislamu?
Nani kakumbi elimu ya kuandaa mwili na kuzika ni siri?

Kila mtu aliyepita madrasa anasoma na kuna maelfu ya vitabu toka enzi za Mtume Salallahu allayhi wasalaam vinafundisha.

Hekima zipo nyingi mno za wanawake kutoingia kwenye kutoenda makaburini kuzika ikiwemo kupunguza drama, vilio ambavyo havisaidii lolote zaidi ya kuslow down mazishi.

Mazishi kwetu ni jambo lenye uzito na tumeelekezwa kulifanya kwa uharaka.
 
Dini iko mbele ya mda.hiyo technology inahusika vipi na sheria hizo?
 
Cha kushangaza Hao hao wanaokatazwa kwenye dini yao,
Akifariki jirani Mkristo wana hudhuria kwa kufuata taratibu zote za kikristo,ikiwemo kumtazama Marehemu kwa mara ya mwisho(kuaga mwili wa marehem)
Na kuhudhuria makaburini wkt wa mazishi.
Hii ndio maana ya kuheshimiana sio kitu cha kushangaa , ukiwa Roma utafanya ya Roma, ukiwa Saudia utafanya ya Saudia
 
Nilikuwa naangalia hii video niliyotumiwa na rafiki ya mmoja.


Kwenye video hii inaonesha tangu mtu anafungwa kwenye sanda mpaka anazikwa.

Nikajiuliza ni kwa nini waislamu wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, ni Muongozo wa dini yao unaotokana na maamrisho ya mwenyezimungu yaliyomo kwenye Quran Tukufu, ama ni tamaduni tu?

Waislamu ulimwengu mzima wanazuia wanawake kwenda kuzika. Je, hicho kinachofanya wanawake kuzuiwa kwenda kuzika, kwa maendeleo haya ya teknolojia hasa ya mawasiliano, wanawake hawawezi kukiona?

Je, picha za video na mitandao ya kijamii haiwezi kumfanya mwanamke wa Kiislamu kujua nini huwa kinafanyika kwenye maziko ya Kiislamu?
Ni ukulele na ujinga. Kuna kitu kigumu duniani kama kujifungua ?
 
Ndugu yangu Baljurashi unanisingizia. Sina lengo lingine ila kujifunza.

Pia Mimi huwa nauliza maswali ambayo wengine wanaona ni "taboo" kuuliza.

Sina nia ya kutaka usawa kwenye dini isiyo yangu bali nahusika nayo. Leo nazika ndugu yangu kitovu kimoja ambaye ni Muislamu. Je hapo uislamu haunihusu?

Hizi dini ni wachache wa mjini ambao hatuna mchanganyiko wa hizi dini mbili kwenye familia zetu.

Hata hivyo maelezo yako mareefu hayajajibu swali langu. Jee wanawake kutokwenda kuzika ni maamrisho ya mwenyezi Mungu ama ni mapokeo ya kitamaduni tu?
 
Nimegundua kuwa wewe huna lengo la kujifunza. Nyuzi zako za zamani nilikuwa nadhani unataka kujifunza, lakini nimegundua hutaki kujifunza. Ulishawahi kuanzisha uzi (upo Jukwaa la Dini) ukauliza kuhusu Sunnah na ukajibiwa. Ila sijui why unauliza swali kama hili tena.




Wanawake kutokwenda kuzika sio kwa sababu walikuwa hawajui/hawajawahi kujua mazishi ya Kiislam. Unafikiri wanawake hawaendi kuzika kwa sababu hawajui mazishi ya Kiislam? Wanawake katika Uislam wanalazimika kuisoma Dini yao kama wanaume. Wanawake wanatakiwa kuisoma Dini yao, hakunaga kauli za "mwanamke hana Dini" katika Uislam. Wanawake pia wanakalifishwa na Shariah za Allah, na kuitekeleza Dini kunahitajika Elimu/kusoma, hivyo nao lazima wasome.

Ila hukmu hutofautiana baina ya wanaume na wanawake katika baadhi ya mambo ya Kishari'ah kwa Hikma ya Allah ambaye kawaumba wanawake na wanaume na anawajua vizuri zaidi. Mfano wote wanapaswa kuswali (wanawake na wanaume) ila kuna hukmu wanatofautiana.

Sio kwamba wanaonewa au kukandamizwa.

Na sio kwamba hawafanyi mambo fulani kwa sababu tu hawajui/hawawezi kujua. Kama unavyotaka kuashiria.

Kukutaarifu tu;
Wanawake wanaosha maiti za wanawake wenzao, bali Mwanamke anaruhusiwa kuiosha maiti ya mumewe, wanawake wanaweza kukafini wanawake wenzao (kuwavika sanda). Wanawake wanaswalia maiti (ya mwanamume au mwanamke), hawaendi tu kuzika makaburini.

Kutokwenda makaburini kuzika isikupe tabu. Kukatazwa wanawake kufanya jambo fulani wala sio ajabu. Hili hata kwa wanaume, kuna mambo wanakatazwa ila wanawake wanaruhusiwa. Mfano ni haramu mwanaume kuvaa dhahabu (hapa duniani) ila ni halali kwa wanawake, ni haramu wanaume kuvaa hariri (hapa duniani) ila ni halal kwa wanawake.

Kuna mambo wanaume wanalazimishwa ila kwa wanawake wamepewa hiari, mfano ni ni LAZIMA mwanaume kuswali Swala ya Ijumaa, ila mwanamke anaweza kuswali Swala ya Ijumaa au akitaka akaswali Dhuhr nyumbani kwake badala ya Swala ya Ijumaa, hiari hiyo hajapewa mwanaume, LAZIMA kwa mwanaume (labda awe na udhuru wa kishari'ah). Ni lazima mwanaume kuswali Swala za Faradhi Msikitini katika Jamaa (isipokuwa anapokuwa na udhuru wa kishari'ah utakaomfanya asiswali Jamaa msikitini) ila sio lazima kwa mwanamke kuswali Jamaa msikitini, ila anaweza kuswali msikitini.



Na mifano mengine mingi.


Hukumu zinaweza kubadilika si kwa jinsia tu, hata mtu mmoja huyo huyo, hukmu katika mambo ya Ibadah zinaweza kubadilika kwake kulingana na hali, mfano; mtu anawajibika kuswali Swala tano za Faradhi, ila anavyoswali akiwa katika hali ya kawaida (mzima na afya) ni tofauti kidogo na atakavyoswali katika hali za dharura kama ugonjwa na safari (kuna tahfifu kapewa), hukmu zinabadilika kulingana na hali yake atakayokuwa nayo na Shari'ah ishaweka bayana katika kila hali.

Uislam sio Dini ya Usawa. Ni Dini ya UADILIFU. Hakuna usawa katika Uislam, kuna Uadilifu.

So usitake kutaka kuleta mambo ya "usawa" yaliyotokana na fikra za watu nje ya Uislam (ambazo ni uongo mtupu na uharibifu).

Tunaridhia Shari'ah kutoka kwa Mola wetu. Na tunasikia na tunatii.

Na Allah ni Mjuzi zaidi.
Umejitahidi kuchambua kiungwana sana mkuu.
 
Back
Top Bottom