Kutokutunzwa kwa kumbukumbu za nchi ndiko kunakosababisha Magufuli aonekane Shujaa kuliko wenziwe

Kutokutunzwa kwa kumbukumbu za nchi ndiko kunakosababisha Magufuli aonekane Shujaa kuliko wenziwe

Kwa ukabaji wa pesa wa Magufuli ikiwemo na tozo angefanya makubwa sana nchi hii. Angelipeleka taifa katika levels ambazo hatukuwahi dhani ingetokea in 10 years of his regime
Imagine JPM alipora ushuru wa majengo wa halmashauri, alizuia safari za nje, alikataa kuajiri n.k ila Bado miradi alikua anakopa!! Sasa JK alikusanya less than 900 B kwa mwezi ila amefanya miradi mikubwa sasa jiulize naye angekataa kuajiri na angezuia safari za nje angefanya mangapi zaidi?

Kingine Samia anakopa sana sababu JPM alianzisha miradi mingi kwa mkupuo mfano SGR, Bwawa la Umeme Rufiji, hayo ni matrillion Sasa bila kukopa atayamaliza vipi? Mbaya zaidi akiyatelekeza mtasema ameshindwa nchi!!

JPM was overrated
 
Ikifika kwa JK ufisadi hamuuoni, ukwepaji kodi, wafanyakazi kutowajibishwa na kudharau wananchi na katiba pamoja na madawa ya kulevya yalivyoua vijana.

Mnaona kajenga miradi tu au sio na kuachia hela ya madawa kutapakaa mitaani huku huduma za kijamii zikiwa hoi bila usimamizi. Na hakuna kitu kinaacha kumbukumbu mbaya kama maumivu ya halaiki in favor of the elites. Magufuli alitufumbua macho kwamba tawala iliopita ilikuwa inatufanya sisi ng'ombe huku wao wakijineemesha na kufisadi hela za miradi tu.
Hoja ya nyie team JPM ni Miradi Miradi Miradi kwamba hawezi sahaulika sababu ya miradi kibao aliofanya na ndio maana tunafanya comparison na JK kwenye miundombinu.

Ila linapokuja suala la ufisadi awamu zote tu za CCM ni mafisadi Hilo halina ubishi. So unless mtumie metrics zingine ila kwenye miradi he's bar average when compared to JK.
 
Mzee acha kuwa muongo Moja ya skendo ilifikia muda mizengo pinda aliingilia kati jpm alikuwa tayar kuachia uwazir kisa ni kubomoa hayo majengo ikiwemo ya Tanesco Kikwete alikuwa hatak majengo Yale yamobolewe kupisha upanuzi wa barabara
Allen Kilewella yupo sahihi mchakato wa hyo interchange ulianza kipindi Cha JK kupitia mradi mkubwa wa DMDP chini ya kipengele Cha de-congestion dar es salaam kwenye Mpango wa taifa wa miaka 5. So kuanzia mwendokasi phase 1 and 2, sijui upanuzi wa Barabara n.k lilikua zao la JK. Tatizo mnachanganya actual ujenzi na pesa kutolewa!!

Barabara ingejengwa tu hapo ubungo with or without kubomolewa TANESCO!!
 
Unamlinganisha mtu aliyejenga viwanda nchi nzima vikaja kuuzwa na Mkapa, na huyu mnayetaja kwa mambo ya daraja na miradi ambayo hakuna alioacha umekamilika na sasa inakamilishwa na Samia Suluhu.
Shida kubwa ni kunarrow tatizo badala ya kulitazama kwa ukubwa wake, mfumo aliouasisi mwalimu ndio ulizalisha viongozi aina ya Magufuli, rejea nyuma huko utakuta changamoto za kimaadili kwa mwalimu kama kiongozi ' sikupi kisa cha yona kazi Bure au changamoto ya Mwl na Osca kambona lakini itoshe tu kueleweka kwamba CCM imetufanya kuwa dhaifu sana Kama Taifa na hili ni kutokana na kule mwalimu kushindwa kumudu kuongoza nchi tangu awali kutokana na udhaifu wake wa kimaadili kama kiongozi. The bottom line
 
Mradi Gani mkubwa kuliko wote?
JK pekee tu UDOM, Mloganzila, Terminal 3 Airport ya DSM, Bomba la Gesi, Kinyerezi 1 and 2, Mwendokasi, mradi wa kuhamisha Maji ya ziwa Victoria kwenda kati ya nchi, Taasisi ya moyo JKCI, Shule za kata, Lami nchi nzima, Madaraja kama Kigamboni na malagarasi duh hizo za haraka haraka kichwani!!

Hayo angefanya JPM mngemjengea Sanamu!! Mind you JK alifanya hayo yote makusanyo yakiwa chini ya billion 800 kwa mwezi, kukiwa na wafanyakazi hewa na ufisadi wa kutisha!! Imagine Sasa angekua na makusanyo kama ya JPM ya almost trillion 2 kwa mwezi!!!
Ongeza na kiwanda cha Dangote...
 
Magufuli kama McKenzie Kwa kweli
Huwaambii kitu wafuasi wake...
Akitokea mtu akasema wafuasi wa Magufuli wasile chakula mwaka mzima ili afufuke ...mbona tutabaki mdomo wazi...
Hahahahaaaaa
 
Back
Top Bottom