Uchaguzi 2020 Kutokuwasiliana kwa viongozi wakuu wa ACT-Wazalendo na CHADEMA kumewapa mwanya CCM kufanya watakavyo

Uchaguzi 2020 Kutokuwasiliana kwa viongozi wakuu wa ACT-Wazalendo na CHADEMA kumewapa mwanya CCM kufanya watakavyo

Nawaagiza Mbowe Lisu . Zitto, Membe wakutane Mara moja tunataka wabunge wengi na madiwani wengi. Huwezi kupata kura za uraisi ikiwa wagombea 500 qamekatwa. Nani atatia chachu ya kampeni,. Nani atalinda kura zako.

Naagiza viongozi CDM , ACT toeni siku moja ya kufuatilia kinachoendelea huko Dodoma. Nendeni tarehe Tisa niwaambie tupo DODOMA tumeahirisha kampeni kuchukua matokeo.

Msiache tume ijiamulie
 
Hakuna mpinzani atashinda Watanzania wamewakataa nyie vibaraka wa mabeberu Sexless,
Mabeberu yako chato yanavuta bangi. Si muwafukuze mabalozi mabeberu na nyinyi mabalozi wenu muwarudishe , unajamba bure kama vile Askofu Gwajima ulimpa mlo
 
unawaagiza wewe kama nani?
mwaka huu wafuasi mnatoa,maagizo,maelekezo na ushauri kwa saana tu,hiyo ni dalili kwamba mambo sio mazuri
usilojua ni kwamba lissu hakua chaguo la mbowe,kwa sababu lissu amesunda pesa yake yote aliochabgiwa na mabeberu kaificha ubeleshi,Nyalandu alikua tayari kutoa hela yote lakin wajumbe wakamfyeka
chadema haina pesa ya kampeni na Mbowe hataki kuingia mfukoni kwa sababu anajua watashindwa tu
 
Mhe. Mbowe na Mhe. Zitto kwa kweli mnatakiwa muende NEC kwa ustaarabu kufuatilia hatima ya mapingamizi. Msiwaachie wagombea mzigo huu.
 
Aliwatetea Mabeberu yatuibie madini yetu yeye akilipwa

Rais Magufuli akatutea kwenye madini tukapata haki yetu

Kiufupi lissu ni msaliti wa Nchi angekuwa raia wa USA au Russia asingekuwepo uraiani
Nenda kasome mkataba na Barick ndio utapata akili. Achana na mambo ya kufafanuliwa na Polepole
 
Kutokuwasiliana kwa viongozi wakuu wa ACT Wazalendo na CHADEMA kumewapa mwanya CCM kufanya watakavyo. Suala la mapingamizi ni suala nyeti hivyo linahitaji nguvu kubwa.

Kipindi Cha Korona mbowe alichachamaa Kila siku mfululizo na speech zake zilipatikana kirahisi kwenye social media. Iweje leo amekaa kimya . Iweje wagombea waende tume peke yao badala ya kwenda na viongozi wao.

Inawezekanaje kupata muda wa kuridhiana na TBC mkashindwa kupata muda wa kuweka presha kubwa kwa tume. Au Mbowe na Chadema mmekubali udhalimu huu wa kuengua wagombea?

Kazhia hii sio ya kushughulikiwa na chama kimoja. Zitto Mbowe ondoeni tofauti zenu kwa maslahi ya upinzani demokrasia na utu ustaarabu na maendeleo ya taifa.

Nawaagiza Mbowe Seif Lisu, Zitto kaeni pamoja itisheni mkutano na media. Pelekeni malalamiko yenu balozi na jumuiya za kimataifa . Toeni siku moja msifanye kampeni nendeni DODOMA kuwasilisha uhitaji wa majibu ya rufaa .

Mbowe kama mwenyekiti hukupaswa kugombea ubunge . Kugombea kwako kunaathiri sana mikakati na utekelezaji wa kampeni. Next time achia Jimbo Kama Mnyika.
Usiwe na wasiwasi utaona mambo.
 
Back
Top Bottom