Kutotambua Matokeo ni Kutomtambua Rais, Serikali na Bunge. Rais Akiishaapishwa ni Rais! Tutaendelea kuruhusu hali hii Mpaka Lini?

Kama kweli anauhakika anataka kulekebisha basi afute matokeo aitishe uchaguzi mpya sio kupamba kitu ambacho hakipo
 
Tutaendelea kuruhusu hadi serikali haramu itakabobadili mtizamo

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
 
Ujinga upi kaka,uo uchaguzi ambao matojeo yanatanfazwa na mkurufebzi,mkurugenzi aliteuluwa na uyo uyo anaegombea,mengibe yanaranfazwa na m/kiti wa tume nae mreule wa anae gombea, kabla ya ujibfa wa chadema nafikirii ungehoji uo ujinga kwanza alafu ndo tuhe kwebye ujinga wa chadema unless other wise umeuliza kiccm zaidiii
 
Wanafanya kama Mandela na makaburu
 
Paskali, wewe ni mwelewa. Usijitoe ufahamu. Hicho unachokiita 'ujinga' kinapangwa na CCM na kutekelezwa na Tume yake ya Uchaguzi. Kukataa kutambua Matokeo ni matunda ya CCM kuteua Wajumbe wote wa Tume ya Uchaguzi.
Wewe Paskali unalijua hili fika.
Najiuliza, umepatwa na nini mpaka ukalaumu matokeo badala ya kisababishi?
Najua unafahamu kuwa Awamu ya 6 haipendi nidhamu ya woga.
 
Paskali, kwa nyongeza tu, nataka nikubaliane na wewe juu ya 'ujinga' kuhusu kutotambua matokeo.
Ujinga ni kitendo kinachotendwa na mtu mjinga.
Sasa hapa tujiulize, wewe na mimi, mjinga ni nani katika hill la kupiga kura?
Mimi naona MJINGA ni wewe Paskali, na mimi 'fundimchundo' na Watanzania wote, ambao tunakubali kutumia muda wetu kwenda kushiriki kwenye zoezi ambalo mwisho wa siku, kura zetu, ambazo ndizo kielelezo cha utashi wetu, hazithaminiwi.
Hypothetically, watu wote tukiamua kukaa nyumbani siku ya kupiga kura, asitokee hata mmoja kwenda kwenye vituo vya kupiga kura, hawa Wezi wa dhamira zetu, wezi wa utashi wetu, wezi wa kura zetu, watalazimika kukubali Uchaguzi huru na wa haki.
Hypothetically.
Kwa sababu mpo Wafia-CCM mtakaowasaliti Watanzania na kwenda kwenye Vituo vya Kupiga Kura kubariki UJINGA unaotengenezwa na Chama cha Mapinduzi, ujinga huu utaendelea kuwepo mpaka siku Watanzania watakaposema, "sasa imetosha", au siku Jumuia ya Kimataifa itakapoweka mguu chini na kuilazimisha CCM kuachia kuimiliki Tume ya Uchaguzi ili tupate Tume Huru ya Uchaguzi.
Nawasilisha.
fundimchundo.
(Paskali, nimekuiga umaliziaji)
 
Kuna Watu unaweza kuwajibu kwa hoja ila sio Pascal, ambaye unajua kabisa kuwa ana maslahi binafsi, anataka madaraka/cheo huko CCM. Mtu kama huyu unatakiwa umjibu yeye kama yeye maana anakua Hana hoja Bali njaa
Kama Paschal angekuwa chaguo la CCM ajue angesaidiwa kuiba kura ili awe mbunge lakini kula za maoni hazikutosha akapata kura moja.Sijui kwanini anaendelea kutoa povu Kwa wezi wa kula Wala wenyewe hawana habari naye.Zimepita teuzi nyingi lakini si GPM au Chifu agaya amemkumbuka. Andika makala ya kutuaminisha umuhimu wa wizi wa kura katika chaguzi za Tanzania.Vinginevyo Pascal unatwanga maji kwenye kinu
 
Dadeeeeki umepiga mule mule
 
Update
Hatimaye Chadema wameacha kushupaza shingo na wamekubali matokeo!, kwa kuufuata ushauri wa bandiko hili CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Nimepokea taarifa, hii kutokea twitwani Kisha nikasoma na bandiko hili humu JF Tundu Lissu: CHADEMA tumeanza kupokea Ruzuku

Chadema wameufuata ushauri wa bandiko hili, waneacha ujinga wa kujifanya hawayatambui matokeo ya uchaguzi wa 2020!, sasa wameacha kushupaza shingo, wameyatambua matokeo kimya kimya!, wamewasamehe mashujaa hawa kimya kimya msamaha ambao utatangazwa rasmi siku ya Jumatano tarehe 8 Machi na Mwenyekiti wa Chadema, mbele ya Rais Samia!.

Iliwa kusemwa kuwa hakuna mkate mgumu wowote mbele ya chai!, tayari Chadema imeisha anza kupokea ruzuku hivyo sasa ita survive!. Na ile kesi ya kina Halima Mdee na wale 19 iliyopo mahakamani itafutwa!.

Hongera sana Chadema, for doing the right thing!, mtabarikiwa, viongozi wenu watabarikiwa, chama chenu kitabarikiwa na Tanzania Itabarikiwa!.
Mungu ibariki Chadema
Mungu ibariki CCM kwa kukubali reconciliation
Mungu ibariki Tanzania
Paskali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…