Kutumika Mbwa kwenye uokoaji Syria na Uturuki

Kutumika Mbwa kwenye uokoaji Syria na Uturuki

Trubarg

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2020
Posts
4,388
Reaction score
7,223
Mbwa bado anaonekana ni kiumbe chenye msaada sana kwa binadamu. Kwa sasa Mbwa anatumia sana kwenye nchi ambazo zimepata majanga ya tetemeko Hivi karibuni yaani Syria na Uturuki.

Najiuliza nchi hizi ni za kiislamu vipi kuruhusu Mbwa atumike wakati kwa uislamu Mbwa ni najisi. Nauliza tu kupata uelewa siyo vita.
 
Unajua unajisi wa mbwa unakuja vipi, au ukoje? Unajua kama ni ruksa kufuga mbwa?

Mbwa mwenyewe hawezi kusemwa ni najisi kwa kutokuwa na dalili ya hilo, isipokuwa mate yake na majimaji ya puani mwake yanachukuliwa ni najisi ki-Shariy’ah ikiwa ni wa kufuga au vinginevyo kwa dalili iliyopatikana kutoka katika Hadiyth. Na kwa hivyo chombo chochote ambacho kitarambwa na mbwa kinapaswa kutwaharishwa kwa kuoshwa mara saba bila kutofautisha ni mbwa gani aliyekiramba, mojawapo kwa mchanga. Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kukitwahirisha chombo kilichorambwa na mbwa kunafanywa kwa kuosha mara saba, mojawapo kwa udongo” [Ahmad, Muslim, Abu Daawuwd na al-Bayhaqiy]

Na ikiwa ataramba chombo chenye chakula kikavu, kile chakula kilichoguswa na mdomo wa mbwa na kilicho pembezoni mwake kinatakiwa kitupwe, ama kilichobaki ni twahara kinaweza kubakishwa. Ama manyoya ya mbwa yakiwa makavu ni twahara. Sehemu iliyo najisi ya mbwa ni ule mdomo wake kwa ajili ya umandemande.

Hivyo, mtu kucheza na mbwa au kumpakata na kumfanya ni kichezeo, si jambo lenye kushauriwa kwa kupatikana uwezekano wa kunuswa au kurambwa nguo yake na maeneo ya kuswalia na sehemu mbalimbali za nyumba yake. Mbwa si kama paka, hivyo si jambo zuri watu kuiga tabia za wasio Waislamu na wao kuanza kufuga mbwa wa vichezeo na kuwafanya kama paka. Muislamu hata akibidi kuwa na mbwa wa ulinzi, anapaswa amweke nje ya nyumba; uani au sehemu ambayo si ndani ya nyumba ili kuepuka kutiliwa najisi vyombo, nguo na sehemu za kufanyia 'ibaadah.
 
Mbwa bado anaonekana ni kiumbe chenye msaada sana kwa binadamu. Kwa sasa Mbwa anatumia sana kwenye nchi ambazo zimepata majanga ya tetemeko Hivi karibuni yaani Syria na Uturuki.
Najiuliza nchi hizi ni za kiislamu vipi kuruhusu Mbwa atumike wakati kwa uislamu Mbwa ni najisi. Nauliza tu kupata uelewa siyo vita.
Mkuu kuna hulka ya watu kuvamia vitu ambavyo wana taarifa zake kwa juu juu tu.
Hebu jihabarishe ni katika mazingira gani mbwa anakuwa najisi.
 
Unajua unajisi wa mbwa unakuja vipi, au ukoje? Unajua kama ni ruksa kufuga mbwa?

Mbwa mwenyewe hawezi kusemwa ni najisi kwa kutokuwa na dalili ya hilo, isipokuwa mate yake na majimaji ya puani mwake yanachukuliwa ni najisi ki-Shariy’ah ikiwa ni wa kufuga au vinginevyo kwa dalili iliyopatikana kutoka katika Hadiyth. Na kwa hivyo chombo chochote ambacho...
Watu hatuna taarifa sahihi ila tunahisi tunazo.

Afadhali umetoa somo
 
Kwa hiyo uko uturuki wanapokwenda kunusa na kulambalamba kuokoa manusura , mji mzima unabidi utawazwe mara saba?, akilamba manusura inabidi naye akatawazwe mara saba?

Baniani mbaya kiatu chake dawa
Halafu mnalaumu waalimu.Kuna binadamu hawajaumba kufundishika.Wao wapo wapo.Bora liende. Akili zao wakiweza kusukuma mavi na za kuwafikisha nyumbani inatosha.
 
Unajua unajisi wa mbwa unakuja vipi, au ukoje? Unajua kama ni ruksa kufuga mbwa...
sheikh wangu mbwa Hana unajisi wowote,si mate Wala maji ya pua,ndiyo maana wwngine hadithi hatuzitaki,zinazua mengi.

QUR'AN 5:4

Wanakuuliza wamehalalishiwa nini?..sema mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri na 'mlichowafundisha WANYAMA kuwinda....'
 
Mbwa bado anaonekana ni kiumbe chenye msaada sana kwa binadamu. Kwa sasa Mbwa anatumia sana kwenye nchi ambazo zimepata majanga ya tetemeko Hivi karibuni yaani Syria na Uturuki.
Najiuliza nchi hizi ni za kiislamu vipi kuruhusu Mbwa atumike wakati kwa uislamu Mbwa ni najisi. Nauliza tu kupata uelewa siyo vita.
QUR'AN 5:4 ibaondoa uwongo wote wa kudai mbwa ni nahisi,huo ni uzushi tu wa watu
 
Halafu mnalaumu waalimu.Kuna binadamu hawajaumba kufundishika.Wao wapo wapo.Bora liende. Akili zao wakiweza kusukuma mavi na za kuwafikisha nyumbani inatosha.
We ni mwalimu kweli ?Mimi nimeuliza maswali kwa wewe mwalimu, au hujaona alama ya kiulizo hapo juu?

Embu jibu swali mwalimu
 
sheikh wangu mbwa Hana unajisi wowote,si mate Wala maji ya pua,ndiyo maana wwngine hadithi hatuzitaki,zinazua mengi
QUR'AN 5:4
Wanakuuliza wamehalalishiwa nini?..sema mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri na 'mlichowafundisha WANYAMA kuwinda....'
Unasema?! hadithi hauzifanyaje? utafahamu vipi maana ya quran na muradi wake kama haukubali maneno ya mtume swala na salaam ziwe juu yake?.
 
Mbwa bado anaonekana ni kiumbe chenye msaada sana kwa binadamu. Kwa sasa Mbwa anatumia sana kwenye nchi ambazo zimepata majanga ya tetemeko Hivi karibuni yaani Syria na Uturuki.
Najiuliza nchi hizi ni za kiislamu vipi kuruhusu Mbwa atumike wakati kwa uislamu Mbwa ni najisi. Nauliza tu kupata uelewa siyo vita.
Mbwa hajakatazwa kufugwa kwa matumizi ya ulinzi uokozi uwindaji mkuu karibu kusoma
 
Unasema?! hadithi hauzifanyaje? utafahamu vipi maana ya quran na muradi wake kama haukubali maneno ya mtume swala na salaam ziwe juu yake?.
Maneno yaliyokusanywa miaka 200 baada ya mtume kufa unakuwa na uhakika gani ni ya mtume!?... Qur'an imesema yenyewe ni nyepesi kueleweka,wewe unadai ngumu kueleweka,unabishana nayo!?
 
Back
Top Bottom