Pre GE2025 Kuuawa kwa Mzee Ali Kibao hakutafifisha jitihada za CHADEMA kuikomboa nchi

Pre GE2025 Kuuawa kwa Mzee Ali Kibao hakutafifisha jitihada za CHADEMA kuikomboa nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Screenshot_2024-09-08-10-48-20-1.png

Hili liwe angalizo kwa Watekaji na Wauaji na Viongozi wa Nchi ya Tanzania Wanaowatuma kuteka na kuua, Kwamba CHADEMA haitavunjika Moyo kutokana na Mauaji ya Mohamed Kibao, hizi mbinu za vitisho kwenye zama za sasa ni mbinu zilizopitwa na Wakati.

Mzee Kibao alipokuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga hakuna aliyemgusa, kumtisha wala kumteka, Kuhamia CHADEMA tu limekuwa kosa la hukumu ya Kifo!

Hizi siasa za kishamba zinazoletwa na viongozi wa sasa wakiongozwa na Samia Suluhu Hassan, hazina tija yeyote kwenye Nchi na wala hazitoikatisha tamaa CHADEMA, zaidi sana zinaidhalilisha Nchi kwenye Jumuiya ya Kimataifa.

Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Bali Ifahamike Kwamba Chadema itaendelea kuhakikisha Nchi na Wananchi wanakombolewa, hii ni kwa sababu Hakuna mahali popote kwenye Dunia hii ambako Shetani aliwahi kumshinda Mungu

Hata wewe Mwanaccm hupaswi kufurahia jambo hili, hii ni kwa vile Shetani hajawahi kuwa na Rafiki, akichoka kushughulika na Chadema atashughulikia Wanaccm Wenzake, Mifano ni Mingi Mno, Nape Nnauye, Edward Lowassa na Phillipo Mangula iwe sehemu ya Mafunzo kwenu.
 
Wapumbavu wakubwa nyie CHADEMA endeleeni kubwata badala yakuchukua Kali

Mzee kafariki bila hatia na kwann hamkumtangaza kuwa kahamia kwenu kutoka ccm


Mnyika aliulizwa na waandishi wa habari kuwa huyu mzee ni nani akajibu kihuni huni tu ..mkomeshwe kabisa
Huyu hakuja Chadema Juzi, halafu wanaohamia Chadema ni wengi mno, si rahisi kuwatangaza wote hadharani
 
Falsafa ya dini badala yakuja kuhakikisha kwamba yalio andikwa yana uhakika nawatu wapate hofu zaidi sasa kwabahati mbaya zaidi ndio imekuja kuwasanua watu kua moto mkali sana wakuchoma naulio jaa majoka makubwa
HAUPO👈
achilia mbali kusifu,kula kunywa na nakila starehe lakini watu wamepuuza kabisa ahadi hii.
nawaza kikundi,au watu flani wenye imani thabiti tena wakiwa na akili timamu juu ya mungu muumba hawawezi kufanya kitendo kibaya mnooo.
huwezi kuuwa watu kama unauhakika kabisa kesho kuna
MOTO👈
😭😭😭😭😭
 
Hakuna mtu Muoga kama Mtanzania, hata mimi ni muoga sana 🤣



Labda Chadema muelekeze nguvu siasa zenu kuelekea kwenye majeshi na muungwe mkono na vyombo vya ulinzi na usalama (polisi, usalama, jeshi)
Jeshi likiungana na likitaka kuwaweka chadema madarakani ni kitendo cha sekunde chache tu 🤣🤣


Akina sisi ni waoga tuko bize na mipira, miziki, mapenzi na misambwanda 🤣


OVA
 
Acheni wehu nyie mnashindwa kujikomboa wenyewe mtakomboa nchi?? Nchi haiwezi kukombolewa Kwa maridhiano na siasa za kwenye Keyboard... Mnaboa bwanaa
haya ungeandika kuelekea kwa walioshika nchi
 
Hakuna mtu Muoga kama Mtanzania, hata mimi ni muoga sana 🤣



Labda Chadema muelekeze nguvu siasa zenu kuelekea kwenye majeshi na muungwe mkono na vyombo vya ulinzi na usalama (polisi, usalama, jeshi)
Jeshi likiungana na likitaka kuwaweka chadema madarakani ni kitendo cha sekunde chache tu 🤣🤣


Akina sisi ni waoga tuko bize na mipira, miziki, mapenzi na misambwanda 🤣


OVA
Ingekuwa Kenya vipi?
 
View attachment 3090100

Hili liwe angalizo kwa Watekaji na Wauaji na Viongozi wa Nchi ya Tanzania Wanaowatuma kuteka na kuua, Kwamba Chadema haitavunjika Moyo kutokana na Mauaji ya Mohamed Kibao, hizi mbinu za vitisho kwenye zama za sasa ni mbinu zilizopitwa na Wakati.

Mzee Kibao alipokuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga hakuna aliyemgusa, kumtisha wala kumteka, Kuhamia Chadema tu limekuwa kosa la hukumu ya Kifo, Hizi siasa za kishamba zinazoletwa na viongozi wa sasa wakiongozwa na Samia Suluhu Hassan, hazina tija yeyote kwenye Nchi na wala hazitoikatisha Tamaa CHADEMA, zaidi sana zinaidhalilisha Nchi kwenye Jumuiya ya Kimataifa

Bali Ifahamike Kwamba Chadema itaendelea kuhakikisha Nchi na Wananchi wanakombolewa, hii ni kwa sababu Hakuna mahali popote kwenye Dunia hii ambako Shetani aliwahi kumshinda Mungu

Hata wewe Mwanaccm hupaswi kufurahia jambo hili, hii ni kwa vile Shetani hajawahi kuwa na Rafiki, akichoka kushughulika na Chadema atashughulikia Wanaccm Wenzake, Mifano ni Mingi Mno, Nape Nnauye, Edward Lowassa na Phillipo Mangula iwe sehemu ya Mafunzo kwenu .
Ukiunganisha Kauli za makada wa ccm
Sidhani kama polis wamo.

Rejea DC longido akiwa mwanachama wa ccm, nape na yule askari aliyesema nasisi tumo
 
Inasikitisha sana.lakini sometimes kupambania wajinga tuitwao waTanzania ni ujinga na wenyewe..bora ubaki na uhai wako ukacheke na wajukuu..ona sasa mzee wa watu walichomfanyia.Dah!
Kosa lake ni nn kua mlengawa wa kushoto mie nasemaga katiba ibadilishwe kibaki chama kimoja km uchinani tuone hayo maendeleo km uchina manake ndo mawazo ya wanaccm
 
Ingekuwa Kenya vipi?
Wakenya ni watata. Ila Tanzania sisi ni waoga mno, hata mimi ni muoga sana 🤣🤣.


Chadema waelekeze nguvu ili waungwe mkono na wanajeshi. Sisi raia tutaongea mitaani na mitandaoni kwenye comments.
 
Back
Top Bottom