Pre GE2025 Kuuawa kwa Mzee Ali Kibao hakutafifisha jitihada za CHADEMA kuikomboa nchi

Pre GE2025 Kuuawa kwa Mzee Ali Kibao hakutafifisha jitihada za CHADEMA kuikomboa nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Hili liwe angalizo kwa Watekaji na Wauaji na Viongozi wa Nchi ya Tanzania Wanaowatuma kuteka na kuua, Kwamba CHADEMA haitavunjika Moyo kutokana na Mauaji ya Mohamed Kibao, hizi mbinu za vitisho kwenye zama za sasa ni mbinu zilizopitwa na Wakati.

Mzee Kibao alipokuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga hakuna aliyemgusa, kumtisha wala kumteka, Kuhamia CHADEMA tu limekuwa kosa la hukumu ya Kifo!

Hizi siasa za kishamba zinazoletwa na viongozi wa sasa wakiongozwa na Samia Suluhu Hassan, hazina tija yeyote kwenye Nchi na wala hazitoikatisha tamaa CHADEMA, zaidi sana zinaidhalilisha Nchi kwenye Jumuiya ya Kimataifa.

Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Bali Ifahamike Kwamba Chadema itaendelea kuhakikisha Nchi na Wananchi wanakombolewa, hii ni kwa sababu Hakuna mahali popote kwenye Dunia hii ambako Shetani aliwahi kumshinda Mungu

Hata wewe Mwanaccm hupaswi kufurahia jambo hili, hii ni kwa vile Shetani hajawahi kuwa na Rafiki, akichoka kushughulika na Chadema atashughulikia Wanaccm Wenzake, Mifano ni Mingi Mno, Nape Nnauye, Edward Lowassa na Phillipo Mangula iwe sehemu ya Mafunzo kwenu.
Jinga tu nyie
 
Haya mambo ya kuuana sio issue kabisa. Serikali ilichukulie hili swala kwa uzito sana maana hii chuki inayo pandikizwa ni mbaya sana inaweza kudumu kwa vizazi kazaa mbeleni.
Na kama ni watu wa serikali wana husika wajue madaraka sio kitu cha kudumu wasitengeneze mazingira mabaya kwa vizazi vyao vijavyo.
Kila mtu ana haki ya kuishi mpaka pale mwenyezi Mungu atakapo mhitaji
 
Mzee Kibao alipokuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga hakuna aliyemgusa, kumtisha wala kumteka, Kuhamia CHADEMA tu limekuwa kosa la hukumu ya Kifo!
Kuna mengi zaidi ya kutambua katika tukio hili.
Kwanza, huyu anatumika kama mfano kwa aina fulani ya watu ambao hawatakiwi kuwa ndani ya CHADEMA. Huo ni ujumbe tosha kwao.

Inawezekana sasa kuanza kujenga nadharia ya aina fulani kuhusu kinacho endelea nchini. Kuna kundi linalomshikiria mama na kuhakikisha atabaki madarakani kwa manufaa ya kundi hilo maalum. Kwa sasa sitataja sifa kuu ya kundi hili; lakini viashiria vya wazi vipo na vinaanza kujitokeza waziwazi. Pengine kufikia kwenye kampeni za uchaguzi mkuu, kundi hili litakuwa lime jibainisha zaidi kuliko ilivyo sasa.

Ule mgawanyiko tulio dhani tulisha vuka ngazi hiyo salama, inawezekana sana wakati huu ndio ukawa tatizo kubwa kwa Tanzania.
Hizi siasa za kishamba zinazoletwa na viongozi wa sasa wakiongozwa na Samia Suluhu Hassan, hazina tija yeyote kwenye Nchi na wala hazitoikatisha tamaa CHADEMA, zaidi sana zinaidhalilisha Nchi kwenye Jumuiya ya Kimataifa.
Huyu mwanamke alisha jitambulisha toka zamani kuhusu mambo haya, lakini watu hawakujuwa tu na kujifanya kupuuza. Sasa watamwona alivyo kiuhalisia wake.

Kawapanga watu wake sehemu zote husika huku watu wakipuuza upangaji wake huo. Sasa kazi ndio imeanza.
 
Nape Nnauye alipotekwa alikuja kwetu kutulilia, tunaamini na wewe siku yako ikifika utakuja
Punguani.baada ya msiba nawaangalia chadema wanawasha magari yao ya kifahar wanaondoka.
Nikaangalia na wanaFamilia nikasikitika sana
 
Ndivyo akili madhubuti iliyojaa utu na ubinadamu inanifanya niwe na tafakari ya namna hio, kama una maswali tukutane kwenye comments.

Chief Wadiz
 
Back
Top Bottom