Kuuliza si ujinga, Tanzania tuna Amiri Jeshi wakuu wangapi? Je Chalamira ana mamlaka Kwa Majeshi ya ulinzi na usalama?

...Mkuu wa Mkoa angekuwa na Busara kweli, angeweza TU Siku nyingine ya Kufanya Usafi Kabla au Baada ya Tar 24, Kwa Vile CHADEMA waliisha itangaza Siku hiyo kuwa ya Kufanya Maandamano Yao ya AMANI !
Kulikuwa hakuna haja ya Mwanasiasa mmoja kuwa KICHWAMAJI...[emoji35][emoji35]

Sent from my TECNO BD4j using JamiiForums mobile app
 
Kama jeshi ndilo limempa taarifa Chalamila mipango yake ya usafi, naye kafanya kutangaza, hapo utasema je?
Mhhh kwani jeshi halina msemaji wake hadi wa mtumie Chalamila

Mbona wakati wanatangaza msako wa sare za jeshi hawakumtuia yeye [emoji848][emoji848][emoji848]
 
Chalamila yupo sawa mbona, waingie tu mtaani wakusanye makopo na kufagia Barabara....yeye mwenyewe anajua Fika hawana kazi yeyote!
 
Chalamira = Chalamila.

Shuleni huwa mnaenda kusomea ujinga?

Sasa Elimu ya mtu inahusikaje hapo? Mbona mnakua na ubazazi sana watu wa humu?

Mkosoe mtu akikosea muundo wa sentensi au akikosea kuumba herufi katika msamiati ila sio jina la mtu. Kwenye majina hapo wengi hua tunakosea hasa majina yetu ya kibantu haya ni mvurugano mtupu.
 
Dr nchi yetu ina watu wa ajabu sana! Yaani mwenyeikiti wa kamati ya ulinzi na usalama anahusika na jeshi!!!

Watu hawaelewi kwamba Jeshi lina ' independent admin structure' hata Waziri ana limited power katika Jeshi.

Kwa upande mwingine Jeshi 'limeruhusu' hali ya utata kwa kushirikia katika shughuli zinazohusiana na siasa.

Wapinzani wanapokuwa na maandamano jeshi linafanya '' usafi'' , watu wanajua na wanaona jeshi linavyoingia katika siasa za mitaani. Wasi wasi ni kwamba jeshi ni watu na wanahisia ziwe!
 
Jeshi ni taasisi ilio chini uongozi wa kiraia.
CDF hawezi kuanzisha mashambulio au vita ila kwa amri ya amiri jeshi mkuu ambae ni raia.


Sent from my BLA-L29 using JamiiForums mobile app
 
Jinga hilo, lipuuze tu.
 
Kwa kauli ile hata kama katumwa lakini haikupaswa kutolewa na RC ikiwa anazungumzia Vyombo vikubwa kama Jeshi na majeshi yoote.

Jeshi la Tanzania kwa makundi yake yoote yana

1. Mipaka yake
2. Heshima yake
3. Kazi zake

Kauli ya RC inaweza pia kubackfire.
 
Kama jeshi ndilo limempa taarifa Chalamila mipango yake ya usafi, naye kafanya kutangaza, hapo utasema je?
Jeshi lina msemaje wake wa Kijeshi na humtumia pale linapotaka kutoa taarifa yoyote kwa Umma.
 
Tatizo linakuja kwenye mgao wa V8 wanajeshi wa Top rank nao wanapata, usitegemee liwe Jeshi la wananchi.

Mpaka kizazi cha wanajeshi wenye Kadi za CCM wote wafe Kwanza ndio tutakuwa na Jeshi la wananchi na siyo branch of CCM, kina Kinana bado wapo hai.
 
Nadhni hili ni tatizo kama lipo
 
JK siku zake za mwisho madarakani alisema atakuja rais ambaye ataiweka pembeni katiba, hivi sasa nchi inaendeshwa kifamilia kama tulivyoona Zanzibar na amiri jeshi wao mkuu huku mama akiwa mgeni! Na huyu wa Dar naye anao uhuru wa kuliamuru jeshi.
 
Kuwa makini na wewe, hilo ni jina halihusiani na kiswahili hivyo hakuna shule yoyote duniani inayofundisha jinsi ya kuandika majina kwa usahihi, mimi nikijiita Uhulu sitakubali ukiniita Uhuru.
Haka Kato kanasumbuliwa na barehe.
 
Nataka siku hiyo nikaone Wanajeshi wanavyokata viuno kufagia na kuokota used condoms mtaani.Yaani jeshi letu Kwa heshima limehit rock bottom.
 
Kuwa makini na wewe, hilo ni jina halihusiani na kiswahili hivyo hakuna shule yoyote duniani inayofundisha jinsi ya kuandika majina kwa usahihi, mimi nikijiita Uhulu sitakubali ukiniita Uhuru.
Safi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…