Kuuliza si ujinga: Tunapokopa kama Taifa, dhamana yetu huwa ni nini?

Kuuliza si ujinga: Tunapokopa kama Taifa, dhamana yetu huwa ni nini?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Takribani mikopo yote inayotolewa kwa watu binafsi, taasisi au nchi huwa na masharti. Pamoja na kwamba masharti hayo kukubaliwa na pande zote za mkopo husika (Mkopeshaji na Mkopaji), masharti hayo huandaliwa na Mkopeshaji kwa ajili ya kulinda maslahi yake-urejeshwaji wa mkopo pamoja na faida.

Kati ya masharti ya mkopo ambayo yasioepukika ni kuhusiana na dhamana ya mkopo (security/securities). Hapa Mkopaji huweka rehani mali yake fulani kama dhamana au hakikisho la kulipwa kwa mkopo. Pale ambapo Mkopaji anaposhindwa kulipa mkopo huo, Mkopeshwaji hushughulika na dhamana hiyo kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kuiuza.

Dhamana za mikopo ni vitu kama ardhi, mishahara, magari, mitambo, hisa na kadhalika. Hizi zimekuwa za kawaida na maarufu kwenye mikopo itolewayo na taasisi za kifedha kwa watu binafsi, taasisi na kadhalika. Kwa ngazi za kinchi (pale ambapo nchi moja inaikopesha nchi nyingine) dhamana ya nchi mkopaji huwa ni nini hasa? Najua masharti mengineyo kama muda wa kulipa huwepo pia.

Mfano, Tanzania inapokopa kutoka mfano Benki ya Dunia au nchi nyingine, dhamana ya mkopo husika huwa ni nini?
 
Takribani mikopo yote inayotolewa kwa watu binafsi, taasisi au nchi huwa na masharti. Pamoja na kwamba masharti hayo kukubaliwa na pande zote za mkopo husika (Mkopeshaji na Mkopaji), masharti hayo huandaliwa na Mkopeshaji kwa ajili ya kulinda maslahi yake-urejeshwaji wa mkopo pamoja na faida.

Kati ya masharti ya mkopo ambayo yasioepukika ni kuhusiana na dhamana ya mkopo (security/securities). Hapa Mkopaji huweka rehani mali yake fulani kama dhamana au hakikisho la kulipwa kwa mkopo. Pale ambapo Mkopaji anaposhindwa kulipa mkopo huo, Mkopeshwaji hushughulika na dhamana hiyo kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kuiuza.

Dhamana za mikopo ni vitu kama ardhi, mishahara, magari, mitambo, hisa na kadhalika. Hizi zimekuwa za kawaida na maarufu kwenye mikopo itolewayo na taasisi za kifedha kwa watu binafsi, taasisi na kadhalika. Kwa ngazi za kinchi (pale ambapo nchi moja inaikopesha nchi nyingine) dhamana ya nchi mkopaji huwa ni nini hasa? Najua masharti mengineyo kama muda wa kulipa huwepo pia.

Mfano, Tanzania inapokopa kutoka mfano Benki ya Dunia au nchi nyingine, dhamana ya mkopo husika huwa ni nini?
Mkopo wa korea ni wa miaka 40.
Sasa walipaji wazazi wao wenyewe hawajazaliwa, yaani 2070 ndio tutalipa.
 
Dhamana ya mkopo huwa ni Tanzania yenyewe, unapozungumzia Tanzania yenyewe maana yake unazungumzia nchi yenye rasirimali na asset mbalimbali yakiwemo majengo ya ubalozi, mashirika ya umma na mali zake, shares kwenye makampuni mbalimbali, rasirimali kama madini, mafuta na gas.

Anapotia saini Rais maana yake Taifa ndio limekopa kwa dhamana ya hivyo nilivyoandika juu, japo ipo mikopo mingine yenye masharti mengine tofauti na hiyo, mfano unakopa ijengwe reli wairun wenyewe kwa muda fulani warudishe hela zao na faida then wanakuachia.
 
Zote au huwa zinatajwa mahsusi?
Sio rahisi kutaja mahususi kwa sababu mambo ya taifa ni rahisi sana kubadilika, ukiweka mahususi ni mbuga fulani ya wanyama halafu baada ya mwaka hiyo mbuga ikageuzwa makazi ya watu au kituo cha kuzalisha umeme ina maana mkopeshaji utapoteza, mara nyingi huwa ni blank cheque tu.
 
Takribani mikopo yote inayotolewa kwa watu binafsi, taasisi au nchi huwa na masharti. Pamoja na kwamba masharti hayo kukubaliwa na pande zote za mkopo husika (Mkopeshaji na Mkopaji), masharti hayo huandaliwa na Mkopeshaji kwa ajili ya kulinda maslahi yake-urejeshwaji wa mkopo pamoja na faida.

Kati ya masharti ya mkopo ambayo yasioepukika ni kuhusiana na dhamana ya mkopo (security/securities). Hapa Mkopaji huweka rehani mali yake fulani kama dhamana au hakikisho la kulipwa kwa mkopo. Pale ambapo Mkopaji anaposhindwa kulipa mkopo huo, Mkopeshwaji hushughulika na dhamana hiyo kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kuiuza.

Dhamana za mikopo ni vitu kama ardhi, mishahara, magari, mitambo, hisa na kadhalika. Hizi zimekuwa za kawaida na maarufu kwenye mikopo itolewayo na taasisi za kifedha kwa watu binafsi, taasisi na kadhalika. Kwa ngazi za kinchi (pale ambapo nchi moja inaikopesha nchi nyingine) dhamana ya nchi mkopaji huwa ni nini hasa? Najua masharti mengineyo kama muda wa kulipa huwepo pia.

Mfano, Tanzania inapokopa kutoka mfano Benki ya Dunia au nchi nyingine, dhamana ya mkopo husika huwa ni nini?
Wananchi wa Tanganyika.
 
Sio rahisi kutaja mahususi kwa sababu mambo ya taifa ni rahisi sana kubadilika, ukiweka mahususi ni mbuga fulani ya wanyama halafu baada ya mwaka hiyo mbuga ikageuzwa makazi ya watu au kituo cha kuzalisha umeme ina mkopeshaji utapoteza, mara nyingi huwa ni blank cheque tu.
Nimekuelewa Mkuu
 
Hakuna dhamana, Zaidi, mikopo hii inakubana kununua baadhi ya products sehemu flani kama regulations tu ya kawaida, ila mkopo wa taifa haupo kama wa mtu binafsi, usichanganyikiwe na story za vijiweni, maswala yakutoa vitu yalikua enzi za kina chief mkwawa huko au mangi meri, baada ya serikali kujiunda, hamna hizo harakati.
Mfano mdogo ni internal debts za watu binafsi na serikali. Unajenga shule ya kata, unanunua viti unapojua wewe kwa bei chee. Ila pale unaonyesha pesa ya reja reja na unalipwa.
 
Kwa taifa masikini dhamana huwa ni rasilimali zake na mali zake nyingine mbalimbali kama ndege, majengo n.k
Kwa mataifa tajiri ukopaji wake huwa ni kwa kuuza Treasury bonds and bills, hapo mkopeshaji inakuwa kama unavyonunua hisa za kampuni Ltd, hapo hata hilo taifa likishindwa kulipa huwa hakuna chochote cha kukufudia. Inakubidi uombee tu hilo taifa liwepo siku zote na wasivurugane kwa vita au machufuko ili uendelee kulipwa.
 
Back
Top Bottom