Kuuziwa chakula bei juu kwa Wasafiri ni kero kubwa

Kuuziwa chakula bei juu kwa Wasafiri ni kero kubwa

luangalila

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2014
Posts
6,346
Reaction score
6,928
Hili janga ni kama limerejea tena kwa speed ya kasi mnooo fikiria unapokuwa safarini sahani ya wali maharage unanunu kwa 4000, wali nyama. 5000, kuku robo ni 10,000, Chaji ya rangi 1000.

Kuwa msafiri sio kuwa kosa la kulanguliwa vitu bei juu au ndio kusema na wao wameathiriwa na vita vya Ukraine?
 
Hili jambo nadhani ni very challenging kuliko tunavyoliona.

Kuna mdahalo ITV waliitisha kati ya TABOA, Madereva, Abiria, na chama cha watetezi wa abiria kuhusu gharama za vyakula njiani.

Changamoto zilikuwa kama ifuatavyo,

* Abiria wenyewe hawakuwa wanaafikiana,abiria wengine walikuwa wanataka hoteli za hadhi na wako tayari kulipia, na abiria wengine walikuwa wanapendekeza gari lisimame kwenye hoteli za hadhi ya chini. Swali likawa ni Je, basi lisimame mara mbili kukidhi matakwa ya abiria wote? Abiria nwengine hawakuridhia kwa kuona ni upotezaji wa muda.

*Madereva wao wakasema wanatafuta hoteli ambayo kimsingi ipo katikati ya safari, ambapo kiuhalisia ni interior sana na hoteli ni chache. Wakaja na hoja kwamba, huwezi kumtoa abiria katika route ya Dar- Babati alafu ukamshusha akale kibaha mjini kwenye mahoteli mengi kwa sababu ya bei.

*Madereva wakaja na hoja nyingine yenye mgogoro kuhusu CHOO. Wakasema serikali inataka abiria wakashushwe sehemu sahihi za kujisaidia, na mara nyingi hizo sehemu unakuta ni za kulipia na abiria hawataki kabisa gharama, kwa hiyo wanachofanya ni kutumia tu busara kutokana na mazingira ili wananchi wajisaidie majoring bila kuwatesa.
 
Mbona hili jambo kila siku linajadiliwa humu, mwisho juzi thread kama hii ilikuwemo humu.

Suluhisho ni moja tu, beba kiporo chako cha ubwabwa na ndondo usafiri nacho kama ukiona humudu gharama za chakula humo barabarani. Uzuri ni kwamba hushurtishwi kununua hicho chakula ni hiari yako.
 
Zile hoteli mara nyingi zipo Pori , customer ni hao hao wasafiri , na wako limited , operation cost ni kubwa , ili kucover situation inabd bei iwe kubwa mkuu , mana maharage ya kilala, yanachacha wanamwaga , imagine umeyauza Kwa bukubuku
 
Shida ya wabongo tunapenda sana kula safarini, safari fupi tu ya Dar -Moshi/Dodoma/Iringa mtu anataka ale nyama choma kuku/mbuzi.! Wakati unaweza kukausha tu ukafika kwako ukapika ugali maharage ukashiba bila gharama
 
Hili jambo nadhani ni very challenging kuliko tunavyoliona.

Kuna mdahalo ITV waliitisha kati ya TABOA, Madereva, Abiria, na chama cha watetezi wa abiria kuhusu gharama za vyakula njiani.

Changamoto zilikuwa kama ifuatavyo,

* Abiria wenyewe hawakuwa wanaafikiana,abiria wengine walikuwa wanataka hoteli za hadhi na wako tayari kulipia, na abiria wengine walikuwa wanapendekeza gari lisimame kwenye hoteli za hadhi ya chini. Swali likawa ni Je, basi lisimame mara mbili kukidhi matakwa ya abiria wote? Abiria nwengine hawakuridhia kwa kuona ni upotezaji wa muda.
sijawai ona hotel ya hadhi ya juu barabara zote za mkoa ambapo magari husimama kwa ajili ya vyakula ni upigaji tu wa madereva ili wapewe msosi wa bure
 
Shida ya wabongo tunapenda sana kula safarini, safari fupi tu ya Dar -Moshi/Dodoma/Iringa mtu anataka ale nyama choma kuku/mbuzi.! Wakati unaweza kukausha tu ukafika kwako ukapika ugali maharage ukashiba bila gharama
Kabisa.
Unakuta mtu ilimradi tu yupo safarini basi gari likianza tu anaanza kutafuna vyakula, muda ambao angekuwa nyumbani pengine bado amelala au yupo shambani [kazini] bila kula chochote.
 
Hili suala juzi kati lililetwa humu ikawa nongwa.
Jana nmepanda basi kuna mwamba alipandia singida, nafkiri ni mkulima. Kwanza kakosa siti, akakaa kwenye korido,. After that akatoa kisu af akafungua mfuko aliokua nao. Ndani kulikua na tikiti.

Jamaa akaanza kuenjoy tunda. Anakata tikiti anakula na anaangalia movue kiulaini sana. Nkajifunza kitu. Next time na mimi ntapanda na mtungi mdogo wa gesi ili kukwepa gharama.
 
Hili janga ni kama limerejea tena kwa speed ya kasi mnooo fikiria unapokuwa safarini sahani ya wali maharage unanunu kwa 4000, wali nyama. 5000, kuku robo ni 10,000, Chaji ya rangi 1000.

Kuwa msafiri sio kuwa kosa la kulanguliwa vitu bei juu au ndio kusema na wao wameathiriwa na vita vya Ukraine?
Tatizo siyo bei bali ni ubora wa huduma na vyakula vyenyewe ni za kishenzi sana
 
Hili jambo nadhani ni very challenging kuliko tunavyoliona.

Kuna mdahalo ITV waliitisha kati ya TABOA, Madereva, Abiria, na chama cha watetezi wa abiria kuhusu gharama za vyakula njiani.

Changamoto zilikuwa kama ifuatavyo,

* Abiria wenyewe hawakuwa wanaafikiana,abiria wengine walikuwa wanataka hoteli za hadhi na wako tayari kulipia, na abiria wengine walikuwa wanapendekeza gari lisimame kwenye hoteli za hadhi ya chini. Swali likawa ni Je, basi lisimame mara mbili kukidhi matakwa ya abiria wote? Abiria nwengine hawakuridhia kwa kuona ni upotezaji wa muda.

*Madereva wao wakasema wanatafuta hoteli ambayo kimsingi ipo katikati ya safari, ambapo kiuhalisia ni interior sana na hoteli ni chache. Wakaja na hoja kwamba, huwezi kumtoa abiria katika route ya Dar- Babati alafu ukamshusha akale kibaha mjini kwenye mahoteli mengi kwa sababu ya bei.

*Madereva wakaja na hoja nyingine yenye mgogoro kuhusu CHOO. Wakasema serikali inataka abiria wakashushwe sehemu sahihi za kujisaidia, na mara nyingi hizo sehemu unakuta ni za kulipia na abiria hawataki kabisa gharama, kwa hiyo wanachofanya ni kutumia tu busara kutokana na mazingira ili wananchi wajisaidie majoring bila kuwatesa.
Ni ngumu sana kumridhisha kila mtu kwenye hili jambo
 
Back
Top Bottom