Kuvaa saa enzi hizi za dijitali ni mbwembwe au usharobaro?

Kuvaa saa enzi hizi za dijitali ni mbwembwe au usharobaro?

Hebu nambie rafiki, mtu anakupigia simu na katikati ya mazungumzo anakuuliza 'ni saa ngapi sasa hivi ili tuone muda mzuri wa kukutana'? Unafanyaje? Tuseme, simu yako imepotea / imeharibika au imeishiwa moto, unafanyaje?Chukulia una simu ya screen touch, ambayo ili ifanye kazi, unahitaji kuianzisha; na muda wa kuianzisha ni mrefu na wa usumbufu kuliko ule wa kuangalia saa. Je huoni kama hali hii hiyo ni upotezaji wa muda?
Aidha, saa ni mwajiri mkubwa sana kuanzia viwanda vyenyewe, wauzaji na wale wanaozitengeneza zinapoharibika (repairers). Je, hawa waajiriwa wote wataenda wapi iwapo watu wataacha kuvaa saa kwa kujifanya kwamba wao ni wa kisasa na wale wenye kuzivaa ni washamba?
Kila kitu kina nafasi yake katika maisha. Wala si haki kusema uvaaji saa ni ushamba (nami ni mvaa saa mkongwe)! Aidha kuna saa ambazo, kuzinunua, kunahitaji mahesabu makali!
Jitafakari!
 
View attachment 189231
Mimi nashindwa kuelewa kabisa watu (hasa wanaume) wanaovaa saa enzi hizi za dijitali kama wanafanya hivyo kwa makusudi au ni mbwembwe tu. Kwanini nasema hivyo? Siku hizi yapata 98% ya watanzania wote wanamiliki simu na kwenye simu kuna saa.

Utamkuta mwanamume sharobaro anamiliki simu 3 kwa mpigo na wakati huo huo katupia bonge ya saa kiganjani mwake. Kuvaa saa kwa wanawake inaleta maana kidogo kwa kuwa inachukua nafsi ya bangili &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; ni pambo la kike.

Sikumbuki mara ya mwisho kuvaa saa na sitegemei kuivaa tena labda nikiwa kwenye chumba cha mtihani nitaibeba na kwenda nayo na baada ya kumaliza kupiga paper nitampa demu wangu avae kama bangili. Uvaaji wa saa enzi hizi unawafaa zaidi wanafunzi wa shule za msingi kwa kuwa wengi wao hawamiliki simu. Tujifunze kuishi kulingana na wakati.

:israel:
======

Mada hii ni moja kati ya zilizojumuishwa kwenye kipindi cha Jamii Leo katika chaneli yetu ya YouTube. Kuona habari nyingine zaidi, tazama video hii hapa chini:




Hao wenyewe waliopiga hatua kidigitali nchi kama USA wanavaa saa tena za gharama sembuse sie...
images
 
Kuna vitu ambavyo VINAKUONGEZEA MUONEKANO MZR...mfano SAA...MKANDA..VIATU....haya maeneo muhimu sana tu ktk utanashati.... huwezi kujuwa umuhimu wa SAA...kama sio MTANASHATI...labda mwenzetu ni wale WANAOVAA CHUPI KWA KUINUSA KWANZA...ndy ajuwe kama ni CHAFU...siwezi kukulaumu mkuu
 
Kuna vitu ambavyo VINAKUONGEZEA MUONEKANO MZR...mfano SAA...MKANDA..VIATU....haya maeneo muhimu sana tu ktk utanashati.... huwezi kujuwa umuhimu wa SAA...kama sio MTANASHATI...labda mwenzetu ni wale WANAOVAA CHUPI KWA KUINUSA KWANZA...ndy ajuwe kama ni CHAFU...siwezi kukulaumu mkuu
Mkuu nakubaliana nawe kwamba kuvaa saa ni sawa na kuvaa vazi la urembo kama hereni, bangili au skafu...haitofautiani na mwanamke anayevaa mkoba kama urembo ghairi ya kuhifadhia vitu. Ni kweli kuwa katika karne hii kuvaa saa kwa lengo la kutunzia muda ni kujibebesha mzigo usiokuwa na sababu.
 
Mkuu nakubaliana nawe kwamba kuvaa saa ni sawa na kuvaa vazi la urmbo kama hereni, bangili au skafu...haitofautiani ] na mwanamke anayevaa mkoba kama urembo ghairi ya kuhifadhia vitu. Ni kweli kuwa katika karne hii kuvaa saa kwa lengo la kutunzia muda ni kujibebesha mzigo usiokuwa na sababu.
Kwako ndy unaona kuvaa saa ndy unaona ni kujibebesha MZIGO.. KWAHIYO unataka kusema wewe hata chupi huvai?sababu NJE umevaa SURUALI?sasa CHUPI ya nn wakati SURUALI TU inatosha?huoni pia ni MZIGO?
 
Kuna Mtu alishazoea kuvaa yaani asipo vaa anajiona kuna kitu amekosa mwilini mwake
 
Mkuu saa inavaliwa kwa malengo mawili, kuonyesha majira, vilevile kupendeza, kama ilivyo nguo, kusitiri mwili na kupendeza vilevile.
Mimi ni addict wa kuvaa saa, nikiisahau nitaomba ruhusa kazini niirudie.

Mimi pia nina saa nyingi mno ndio ugonjwa wangu. Nikisahau kuvaa saa narudi kuvaa ni kama sijavaa viatu
 
Ukiwa japan na kumuuliza mtu saa ngap? Atakushangaa sana,coz japan kila mtu anavaa sana coz wanaenda sana na muda na wako biz sana,mm lazima niwe na saa mda wote,naweza kusaa simu lakin saa lazima niwe nayo
 
simu ni kila kitu. stopwoch. rimainda. aram cloku nk tena hata kama umeizima inaweza kukuamsha. mnao sema pambo nawaunga mkono. mimi naona mzigo tu
Acha kuwa na akili fupi iviupo katika mkutano, presentation,au kwenye kikao utatoa simu na kuiwasha, not serious saa ni saa na simu ni simu, acha ubashit
 
View attachment 189231
Mimi nashindwa kuelewa kabisa watu (hasa wanaume) wanaovaa saa enzi hizi za dijitali kama wanafanya hivyo kwa makusudi au ni mbwembwe tu. Kwanini nasema hivyo? Siku hizi yapata 98% ya watanzania wote wanamiliki simu na kwenye simu kuna saa.

Utamkuta mwanamume sharobaro anamiliki simu 3 kwa mpigo na wakati huo huo katupia bonge ya saa kiganjani mwake. Kuvaa saa kwa wanawake inaleta maana kidogo kwa kuwa inachukua nafsi ya bangili &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; ni pambo la kike.

Sikumbuki mara ya mwisho kuvaa saa na sitegemei kuivaa tena labda nikiwa kwenye chumba cha mtihani nitaibeba na kwenda nayo na baada ya kumaliza kupiga paper nitampa demu wangu avae kama bangili. Uvaaji wa saa enzi hizi unawafaa zaidi wanafunzi wa shule za msingi kwa kuwa wengi wao hawamiliki simu. Tujifunze kuishi kulingana na wakati.

:israel:
======

Mada hii ni moja kati ya zilizojumuishwa kwenye kipindi cha Jamii Leo katika chaneli yetu ya YouTube. Kuona habari nyingine zaidi, tazama video hii hapa chini:

Ndugu tangu, saa ya mkononi haina mbadala.

Saa ya mkononi haiwezi linganishwa na bangili mkuu.

Binafsi mi dipendi kudharau mtazamo wako huo maana wapo kama wewe ambao watakuja na mawazo kama ya kwako, hao watapinga kuvaa mkanda wakati suruhali haipwai, kuvaa soksi, na hats kuvaa chupi wakati una bukta.

Labda nikupatie tu uelewa kidogo katika tasnia ya mavazi na utanashati.

Utaonekana mtu wa ajabu sana kama unatoa simu mfukoni kwa ajili ya kuangaliaumajira

Fahamu kuwa saa inakwongezea hadhi katika mwonekano wako.

Simu ni kwa ajili ya mawasiliano na saa ni kwa ajili ya majira.

We we unataka kutuaminisha kwamba zama hizi hakuna haja ya kununua kalenda kwa sababu kalenda ipo kwenye simu, siku nyingine utakuja na mada kuwa hakuna haja ya kununua radio, diary, TV, wala komputer kwasababu vyote hivyo vipo kwenye simiu.

Binafsi Mimi huwa sitoki ndani mpaka nipigilie mkonono msaa wangu wa Rollex.

Saa ni kigezo cha usmati na kujali, kujiamini.
 
Duh haya bhana!
Na hata unapokuwa unafanya "presentation" ofisini kwako au mahali popote ambapo ni "official" mbele za watu, toa simu yako/zako uangalie muda!

Acha kuwa na akili fupi iviupo katika mkutano, presentation,au kwenye kikao utatoa simu na kuiwasha, not serious saa ni saa na simu ni simu, acha ubashit

Take into account that kwenye maofisi mengi na presentation rooms huwa kunakuwa na saa ya ukutani.
 
Ni sawa na wale wanaotoa Ipad sijui nn kanisani na kutukia Biblia zilizokuwa Installed...Huu ni utovu wa nidhamu na sii uungwana....
Sasa nawe tena umeleta mada nyingine. Kwani kuna kosa gani kwa wewe unayesoma makaratasi na huyu anaesoma soft copy?
Utovu wa nidhamu upo wapi hapo ndgu yangu?
 
Back
Top Bottom