Kuwa na followers Wengi Instagram hakuna faida?

Kuwa na followers Wengi Instagram hakuna faida?

Hebu fafanua hapa
Kuna watu wanauza huduma ya "KUZA FOLLOWERS" unamlipa anabost akaunt yako. Followers wanajazana kibao alafu hawana msaada wowote hasa kibiashara. Mana huwaga hewa tu... Mm nlitamani niwe na followers 200k huku nkiwa sijapost kitu hata kimoja huko insta. Nadhani ningevuja rekodi ya dunia
 
Kuna watu wanauza huduma ya "KUZA FOLLOWERS" unamlipa anabost akaunt yako. Followers wanajazana kibao alafu hawana msaada wowote hasa kibiashara. Mana huwaga hewa tu... Mm nlitamani niwe na followers 200k huku nkiwa sijapost kitu hata kimoja huko insta. Nadhani ningevuja rekodi ya dunia
[emoji38][emoji38]
 
Nilikuwa naangalia wasanii wenye followers Wengi nimeshangaa kuona Zuchu kazidiwa followers na wasanii Wengi wa kike lakini wasanii hao Wana "struggle"... kulinganisha na Zuchu ..imenishangaza sana.

Nilifikiri sanaa ya sasa kuwa na followers Wengi ndo kila kitu. Unauza chochote na unapata matangazo Tele...lakini ajabu sana kuna wasanii "Wana struggle Sana" huku Wana followers milioni zaidi ya tano..... tatizo ni nini?

Kingine mbona watu wenye page zenye followers chini ya milioni wengine Wana claim wanaendesha maisha Yao vizuri Tu Kwa kupitia page zao?

Shida ni nini kwa wasanii wenye followers Wengi?

Kuna yeyote anajua hii industry na mbinu zake kuhusu followers??
Engagement ndio mtaji. Ukipeleka tangazo lako kwa watu wa insta usitazame followers utakula za uso.
 
Wasanii wote huigiza maisha hadi siku wakifa ndo ukweli utajulikana.

Kwa watu kama CR7, Messi inajulikana kila Post ya Tangazo ni zaidi ya Tzs 2.2bil

Hawa wa hapa kwetu sana sana ni 50,000 kutangaza Matangazo ya Nguvu za Kiume
Nenda na million 5 yako kwa Diamond akuwekee tangazo lako kwenye page yake. Ukifanikiwa nakuongeza mil 5 nyingine.
 
Alafu ukiwakuta viwanja ni huruma sana...
#code zao tunazo
 
Kuna umaarufu na ushawishi yaani Fame vs Influence, kwenye matangazo inaangaliwa influence. Je, neno lako linaweza kumuaminisha mtu anunue unless anaekupa tangazo anataka biashara yake ijulikane

Kingine ni targeting, hapa wasanii wengi kwenye branding wanakwama sana kwa sababu hawana positioning kabsaaa

Mfano shilole anapata sana endorsements za bidhaa zinazohusiana na mapishi kwa sababu kajitanabaisha kama mpishi. Wasanii wengi hawana hiki kitu

Mimi Mars mdada flani classic and fashionable lakini pia analinda sana reputation yake ndio maana matangazo ya nywele na bidhaa za middle class wengi anapata

Diamond jamaa flani bad boy mwenye pesa, mafanikio na flash life kama mbele, kiufupi anaishi dream life ya vijana wengi inayomfanya kuwa fame na influence

Kingine wengi hawana managers ambao elimu zipo kichwani na kaujanja ka mujini kapo. Mfano Hamisa na Idris wanafanya sana kazi na professionals kama dr. Ulimwengu ndio maana wanapata sana deals

Kuwa na fame ni jambo moja, kuwa na influence ni jambo jingine na kubadili followers kuwa pesa ni jambo jingine
 
Mtu mwenye followers zaidi ya M kulala njaa ni uzembe. Karibu biashara yoyote ukifungua itaenda.
 
Ushaona akaunt ya yule dada mfupi anaitwa TAUSI? ana follower 1m lakini akipost hizo like na comment hazifiki 100. Wananunua booster waleee. Anaonekana ana watu wengi kumbe hewa tu
Hiyo sio sababu hata cr7 ana followers milion miatano 500M anaelekea 600 lakini akipost anapata 10M yaan hata robo ya followers wake hawafiki
 
Hiyo sio sababu hata cr7 ana followers milion miatano 500M anaelekea 600 lakini akipost anapata 10M yaan hata robo ya followers wake hawafiki
We jamaa. TAUSI Hana uwezekano wa kumiliki followers wengi kuliko mkojani.. follower MILIONI. Like na comment chini ya 100.
Unajua kimahesabu hapo ni chini ya 0.00001% pekee walioengage hapo?
 
Back
Top Bottom