Kuwafukuza uanachama Wanawake mashujaa 19 ni kujipiga risasi mguuni

Kuwafukuza uanachama Wanawake mashujaa 19 ni kujipiga risasi mguuni

Mziki uliowashwa na CCM unachezwa kwa vurugu kubwa na Chadema.
Kuna ngumi zitalika muda simrefu pale Ufipa.
 
Tatizo ni kwamba hata ukiwafukuza, ccm watakingia kifua na wataendelea kuwa bungeni!
Lakini lengo lao la kupata hela za mabeberu,sababu wana bunge lenye wapinzani halitatimia.
Ccm hawana shida na akina Mdee bali wanataka watumike kupata trillion za mabeberu.
 
Lakini lengo lao la kupata hela za mabeberu,sababu wana bunge lenye wapinzani halitatimia.
Ccm hawana shida na akina Mdee bali wanataka watumike kupata trillion za mabeberu.
Kwann lisitimie wakati kambi ya upinzani imeshapatikana ?

Wasipotupa hizo pesa watakuwa wana visa na sisi
 
Lakini lengo lao la kupata hela za mabeberu,sababu wana bunge lenye wapinzani halitatimia.
Ccm hawana shida na akina Mdee bali wanataka watumike kupata trillion za mabeberu.
Hilo lipo wazi mkuu, hata MATAGA wengine humu, leo wanajifanya kumsifu Mdee, mara eti kutetea haki za wanawake, hakuna upendo wala nini, nia yao ni kubomoa chadema na kujijenga wao! Lakini mimi naona fursa hapo hapo ya kujenga chama!
 
Chonde chonde kamati kuu ya CHADEMA, huu mtego utegueni kwa hekima. Kuwafukuza wanawake 19, au 20, ambao Ndio wanawake imara na wenye nguvu zaidi nchini kwa sasa, siyo tu kujipiga risasi mguuni, ni kumpa adui nafasi ya kujilinda na kukushambulia!

Sisiemu wana pandikiza mapandikizi kila leo, wale kina ‘Mamvi’, mzee ‘gusa unuke’, nk! Kwanini tusiwachezee mchezo wao huo huo?! Unapata wapi fursa nyingine kama hii!? Naomba suala la wamama tulimalize, alafu watu kadhaa vichwa kama Mnyika, na Catherine Ruge waunge juhudi mkono, waende jikoni mle, wakatulee mbinu! Kwa nini tutegemee njia moja tu? Huyu adui tunatumia njia hiyo tangu 1995, na tunapigwa?! Ok, Lisu na Lema wamekimbilia uhamishoni, ni mbinu lakini isiwe ya mwisho!

Wacha watutukane, watubeze na kutudharau, lakini mwishoni tuwatoe madarakani! Lengo lao chama kisambaratike na kufa, lakini Sisi tuamue kusambaratika na kuishi!

Kesho tokeni na agenda ya kukivunja vunja chama! Kama kawaida Mwamba Mbowe abebeshwe lawama ya kawaida ya kupenda ruzuku, kuwa ameteua 19 peke ake, alafu wajumbe wengine wakuu wajivue uanachama, waunge juhudi waingie serikalini, ‘kimafia’!! Tufe ili kuishi, sambaratisha chama kiingie kila uwanja wa vita.

Kila tutakapo ingia tueneze u-CHADEMA wetu, kama Wakristo wanavyoeneza Ukristo wao China, chini kwa chini! Tusitake mafanikio ya mda mfupi tu, tujipangeni ‘kimafia’ kwa ajili ya mafanikio ya muda mrefu!

Ni maoni yangu lakini nitaendelea kuunga mkono upinzani kwa hali na mali, hata kama ushauri wangu hautafuatwa!
Chadema ipo ICU mda wowote inafariki ghafra na kupora kwa chadema ni kuwafukuza wa kike 19 a.k.a wanandungai kinyume na hapo chadema inafariki ghafra na kuwa level ya chauma UDP DP TLP NCCR na CUF ya Lipumba
 
Kuwafukuza uanachama ni option mojawapo ila hatarishi sana na bila shaka Chama hakitaopt kufanya hivyo

Huu ndio muda sasa wa akili kutawala hisia na mihemuko. Ni muda wa kuconsider athari za maamuzi yoyote in totality. Madhara ya kuwaacha hawa labda ni kupelekea watu wachache (Mnyika?) kuachia ngazi/kuondoka na hii inaweza kuonekana haina athari kubwa. Itakuwa ni case ya whether kutimua watu 20 au kuwaacha watu watatu or so waondoke🙂

Wakifukuzwa hawa 19/20 (Aida?) most likely watakimbilia mahakamani, Dola itawalinda na wataendelea kula posho nene mpaka June 2025.

Hapo katikati mihemuko ikipungua, wanaweza kusameheana, wakaanza kuchangia chama financially huku wakijipanga na uchaguzi wa 2025

Haya mambo hayahitaji hasira na Siasa ni Sayansi!
Bora wawe wabunge wa mahakamaccm kuliko kukaa na maradhi ya wakke 19 wanandungai ambao wataivua heshima yote ya chadema na kudharaulika Duniani kote
 
Hakuna mkubwa kuiko chama covid 19 waondoke wote
Wanandungai 19 ni Sumu ni corona iliyoingia chadema bora wafukuzwe mapema chadema ipone kinyume na hapo chadema itadharaulika na kuwa chama cha hovyo mno
 
Chuki yako kwa Mbowe inatambulisha upo upande gani, na mpo wengi!
Hakuna chuki kwa mbowe Tambua mbowe anawadharau viongozi wenzake, mfano kaenda kuchukua bilion 3 peke yake CCM kamgawia Salum mwalimu kidogo kawazunguka Lisu na mnyika na sasa yupo nyumbani kwa Kenyata kenya anaficha hizo pesa kwanza ndipo atengeneze mazingira ya kuwahadaa watanzania , chadema ichague moja kudharaulika zaidi au kuheshimika zaidi leo
 
Mbowe na wakike 19 wanandungai lao ni moja wapo after money’ huku akiwinda ruzuku haramu tokea kwao ndiyo maana kawazunguka akina Lisu na mnyika kienyeji kwa njia haramu za kishetani lakini leo anaenda kuumbuliwa endapo hatakuwa na uthubutu wa kuwafukuza hao wanandungai 19 waliojisimika ubunge kienyeji
 
Chadema ipo ICU mda wowote inafariki ghafra na njia pekee ya kuiokoa chadema ni kuwafukuza wa wanandungai 19 tu siyo vinginevyo
 
Sio kweli kwamba kuwafukuza ni kujipiga risasi mguuni, kwani wamekwishapoteza sifa ya kuwa mashujaa.
 
Chadema ipo ICU mda wowote inafariki ghafra na njia pekee ya kuiokoa chadema ni kuwafukuza wa wanandungai 19 tu siyo vinginevyo
Kuwepo au kutokuwepo kwa COVID-19, hakuwezi kuiua chadema! Maneno kama hayo kuhusu Mbowe, wameyaimba sana ccm, naona ni zamu yetu sasa! Tujihadhari tu, kama tukimmaliza Mbowe, tutamuanza Nani?!
 
Back
Top Bottom