Kuwafungia raia yaani kitu kinachoitwa Lockdown ni kuwapa ‘DEATH MULTIPLE CHOICE’

Kuwafungia raia yaani kitu kinachoitwa Lockdown ni kuwapa ‘DEATH MULTIPLE CHOICE’

Mpaka sasa hakuna nchi iliyo na uhakika wa matibabu not to mention means to be used to totally tackle down the epidemic virus, sisi wale tunaitwa shit hole countries, Rwanda, Kenya na hizo nyingine unazozing’ang’ania combined, unategemea nn kipya haswa kutoka kwenye hizo nchi?

Hutaki jifukiza, omba, hutaki omba jifungie ndani.
“We are born to die, why fight to live?” The game.

You are wrong. Be fair to yourself. Unknowingly you've subscribed to the doctrine of your master:

Wa kufa acha wafe hadi tunaowaita mabeberu watakapogundua dawa au chanjo. Sasa hivi mko chini ya mnazi kuokota embe dodo.

Beberu mnayemsubiria atafute tiba au chanjo kibongo bongo kwa mlango wa nyuma mna mnanga ati anawaletea corona kwenye misaada yake. Haya ni Tanzania tu!

Watakaopona bahati yao. Watakaokufa tutaita mpango ya Mungu. Shame on you!

Rwanda, Kenya na Uganda wenzetu hao katika EAC wako vizuri. Wanapigana ndani ya machungu yao and they will prevail.

It should concern you if you like, wenzetu tuliochagua kufanana nao ni hawa hapa chini. Disgrace:

IMG_20200424_182838_396.jpg
 
Huu ni ukweli usiopingika kabisa, approach yetu katika kudeal na majanga, maendeleo na vingine vingi haipaswi kufanana na Ulaya as we are quite so different in terms of many things, almost everything by the way.

Ukiongea na wazungu wenye mtizamo walau chanya juu ya maendeleo ya Afrika watakuambia, kuna mmoja alini-expose kusoma kitabu kinaitwa “Dead Aid”, humo utajua kwanini Afrika tumepewa misaada ya mabilioni ya dola za kigeni lakini mpaka sasa maendeleo hakuna.

Jiwe ni jiwe kweli kweli na kwa hilo nampa kudos from mi heart.
Yeah! We are deadly different,and the difference is--------our ignorance!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na Wolle;

Kwanza niseme kwenye ukweli huwa siko affiliated na chama chochote kile. Katika mijadala ya tahadhari dhidi ya Corona nimefuatilia sana wengi wakisema serikali ya Magufuli inafanya mzaha na kuhatarisha uhai wa watu.

Wanaosema haya hasa ni viongozi wa Vyama Vya Upinzani na wachache wa CCM na zaidi sana wanasema kwamba uhai haulinganishwi na mapato ama uchumi. Ni kweli uhai haulinganishwi na kitu chochote kile lakini siyo kweli kwamba serikali ya Magufuli inacheza na kuhatarisha uhai wa watu kuhusu uchukuaji wa tahadhari dhidi ya janga la Corona.

Wakati naelekea kwenye point yangu tukumbuke pia kuwa Afrika na Ulaya ni mabara mawili tofauti, kitamaduni, kiuchumi na kijiografia. Mifumo ya maisha ya raia wa Ulaya na nchi za Magharibi ni tofauti na yetu Afrika, mifumo ya biashara ya Ulaya ni tofauti na yetu, miundombinu ya Ulaya ni tofauti na yetu. Ukuaji wa Uchumi wa Afrika ni tofauti na ule wa Ulaya.

Hivi uliwahi kujiuliza kwamba ni kwanini Afrika tusiige mbinu walizotumia Ulaya ili tujikwamue kiuchumi tuondokane na umaskini? Viongozi wengi wa Afrika wamejaribu sana kuziiga hawajafanikiwa, unadhani ni kwanini? Kwasababu ile modeli ya uchumi wa ulaya (European economic model) haiwezi kukidhi haja ya bara la Afrika. Sasa kwanini katika kudhibiti Corona tutumie model inayotumiwa na bara la Ulaya? Tuachane na hayo.

Hapa tujipime wenyewe kwa nchi yetu ya Tanzania tuachane na bara la Afrika. Uchumi wa Watanzania wengi hasa kwenye miji na majiji makubwa ni ule wa 'hand to mouth,' kabla hata ya lockdown yaani hali ikiwa kawaida tu watu wana-starve! Je vipi wakiwa locked down? Haijalishi nusu karantini au karantini nzima (Patial or total lockdown), watu watahangaika sana. Ndiyo maana nasema Kuwafungia raia kwa kitu kinachoitwa 'Lockdown' ni kuwapa ‘DEATH MULTIPLE CHOICE’ Yaani mtu atachagua;

A) Akae ndani kuepuka corona afe kwa njaa au

B) Atoke aende kwenye shughuli za kumpa mkate aepuka njaa afe kwa corona.

Huku nafasi kubwa ya kifo ikiwa kwenye lockdown kuliko wangeachwa wafanye shughuli huku wakichukua tahadhari, kwasababu kumbuka kwenye lockdown raia watapambana na njaa pamoja na polisi ama vyombo vya ulinzi na usalama kwa ujumla. Hapa naungana na Mh. Rais Dr. Magufuli. Na hapa naongezea kuwa lockdown itaua zaidi kuliko Corona yenyewe.

Denis Waitley, mwandishi wa vitabu na mwanasaikolojia aliwahi kusema, “Life is inherently risky. There is only one big risk you should avoid at all costs, and that is the risk of doing nothing.”
Kwa tafsiri ya kawaida kabisa akimaanisha kwamba, “Maisha ni hatari kwa asili. Kuna hatari moja tu ambayo unapaswa kuepukana nayo kwa gharama zote, nayo ni hatari ya kutofanya chochote."

Fikiria Tume-lockdown Dar es Salaam, hapo tutakuwa tunapoteza watu kwa corona na kwa njaa huku uchumi na mapato vikiwa vimesimama. Kuacha watu waendelee na shughuli huku wakichukua tahadhari ni jambo la busara zaidi kuliko kukaa ndani watu wakiwa hawafanyi chochote wakisikiliza habari za corona.

Kumbuka namna ya kurudisha uchumi uliopotea Ulaya ni rahisi zaidi kuliko kurudisha kurudisha uchumi uliopotea Afrika (hasa Tanzania)

Mwisho kabisa nampa Rais Magufuli alama ya “A” kwa kufaulu mtihani ambao somo lake niliwahi kufundishwa na mwalimu wangu wa chuo kwenye kipengele kimoja kinaitwa ‘Professional Dilemma’. Walio wengi wameshindwa kufaulu changamoto hii, wamechanganyikiwa, mara walaumu uchumi kuyumba mara walaumu kutoku-lockdown.

Nakutakia kazi njema, endelea kufanya kazi huku ukijilinda wewe na uwapendao.

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA
Hauna mawazo mapya juu ya namna serikali inaweza kupambana na ugonjwa wa corona zaidi ya c&p? hauko productive mkuu,,,
Mh rais anatakiwa kushauriwa ili atoe maamuzi mazuri.
Unaweza mchoma corona mwilini mwako kwa mvuke wenye 100 C bila wewe kudhurika? hii nayo unaipa A?
Hujawai fikiria namna yoyote ya kupunguza misongamano mijini ili kupunguza kasi ya maambukizi?

Sina chama na sitakuja kuwa na chama.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe ndiyo maana Uganda vifo vimekua vingi sana!

Nadhani kwa wanavyojua wao hata Rwanda vifo vimekuwa vingi sana na vinaongezeka kwa kasi sana kila uchao.

Hao ndiyo werevu wetu na eti wamejizatiti vilivyo vichwani mwao kufungua vinywa vyao mbele za wengine bila hoja wala ushahidi.

Idiots!

Kweli ujinga ni zigo la miiba!
 
Kweli aisee kama hadi leo tunasota kwa hasara ya vita ya Kagera ni kweli kuinua uchumi Africa ni kazi ngumu
 
Mkuu bandiko lako linakosa usahihi kabisa. Uganda, Rwanda, Kenya ni Afrika wala si ulaya au marekani kama unavyojaribu kujidanganya. Baadhi wamekwenda total lockdown na partial lockdown. Wengine ni masikini kuliko hata sisi. Wako vizuri na wanasonga mbele.

Ugonjwa umedhibitiwa na hakuna aliye kufa njaa.

Acheni kufanyia siasa Jambo hili ambalo liko wazi mno. Hivi tafsiri zenu mnazipatia wapi? Mbona yameelezwa sana haya mkuu?

Hoja za wanaoona lockdown haifai ni zipi? Tuelimishane - JamiiForums

Hizi njaa mnazoimba kila siku mnaziota tokea wapi?

View attachment 1429029
Covid isipoisha je?.
 
Unafanya mzahaa! Huu ugonjwa ukitupiga kama ulivyopiga Italy halafu tukafanya huo mzahaa unaosimulia hapo juu ndani ya wiki moja nusu ya population ya nchi inaisha!
 
Kuna ushahidi wowote wa takwimu kwamba Nchi za Afrika mashariki zilizofanya lockdown zimepunguza maambukizi kwa asilimia ngapi na sisi ambao hatujafanya lockdown maambukizi yameongezeka kwa asilimia ngapi dhidi ya wenzetu? kwa kuangalia tu madhara ya lockdown waliyoyapata hao unaowasema ni makubwa sana vikiwemo vifo sisi hicho kitu kwetu hakipo. Msipende kuiga na kukosoa masuala ya msingi kama haya, acheni!
Wenzetu wasingekuwa na lockdown, ungekuta sasa wako kwenye malaki wanaelekea kwenye millions of cases and deaths! Nawashangaa sana mnaosema eti Mbona lockdown haijawasaidia! Tumieni akili! Hili gonjwa mtatafutana. Haya!
 
Covid isipoisha je?.

Mkuu hii ni sayansi siyo ramli. Ugonjwa utakwisha na ndani ya muda si mrefu.

Lockdown inasaidia kuwapata wote walioambukizwa na kuwatenga kwa hatua stahiki. Huu ni ugonjwa wa siku 14 tu.

Kadri maambukizi yalivyo mengi kabla ya lockdown ndivyo zoezi la kuwapata wote litakavyo hitaji muda zaidi.

Logically lockdown inatumika kuweza kuidhibiti kasi ya maambukizi. Baada ya hapo shughuli zinarejea katika hali yake ya kawaida na tahadhari zaidi ikiwapo.

Kumbuka serikali ingeitikia mapema kabla ya ugonjwa:

1. Kuzuia ndege na wageni toka nchi zenye maambukizi
2. Kuweka quarantine wageni kwa siku 14

Ugonjwa usingeingia nchini au ungedhibitiwa mapema kama ilivyokuwa kwa case ya Uganda.

Lockdown itatufanya tusafishe ndani kisha sasa tunaporejea hali ya kawaida tu implement hayo hapo juu kuzuia ugonjwa usiingie tena. Huko ndiko ambako Rwanda na Uganda wanaelekea sasa:

Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine? - JamiiForums
 
Mkuu hii ni sayansi siyo ramli. Ugonjwa utakwisha na ndani ya muda si mrefu.

Lockdown inasaidia kuwapata wote walioambukizwa na kuwatenga kwa hatua stahiki. Huu ni ugonjwa wa siku 14 tu.

Kadri maambukizi yalivyo mengi kabla ya lockdown ndivyo zoezi la kuwapata wote litakavyo hitaji muda zaidi.

Logically lockdown inatumika kuweza kuidhibiti kasi ya maambukizi. Baada ya hapo shughuli zinarejea katika hali yake ya kawaida na tahadhari zaidi ikiwapo.

Kumbuka serikali ingeitikia mapema kabla ya ugonjwa:

1. Kuzuia ndege na wageni toka nchi zenye maambukizi
2. Kuweka quarantine wageni kwa siku 14

Ugonjwa usingeingia nchini au ungedhibitiwa mapema kama ilivyokuwa kwa case ya Uganda.

Lockdown itatufanya tusafishe ndani kisha sasa tunaporejea hali ya kawaida tu implement hayo hapo juu kuzuia ugonjwa usiingie tena. Huko ndiko ambako Rwanda na Uganda wanaelekea sasa:

Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine? - JamiiForums
New infections mtazipunguza tu na sio kuzizuia
Its all over the world
Naona Mh kaona arisk watakaokufa wafee tu ila wengi watabaki
 
Labda nikwambie kitu.mimi sipo ccm siku zote ni mpinzani.
Ila mimi sio mpinzani FUATA MKUMBO NINA AKILI ZANGU TIMAMU..
siwezi kupigia kelele lock down ambayo hainisaidii kitu.wakati kazi zangu ni za kutoka nje.
Niliwahi kukuuliza UNAFANYA KAZI GANI AMBAYO ITAKUFANYA HUMUDU MAKALI YA LOCKDOWN DOWN.
Mpaka unakufa hautakuja kunijibu
Wewe unawasikia wakililia Lumumba?

Tunaowasikia sisi wako huku:



Sent using Jamii Forums mobile app
 
New infections mtazipunguza tu na sio kuzizuia
Its all over the world
Naona Mh kaona arisk watakaokufa wafee tu ila wengi watabaki

Mkuu si kaona kuwa watakaokufa wafe tu wengi watabaki kwani yeye siyo nabii kuwa na uhakika na hilo.

Nadhani kaona wa kufa wafe hadi beberu (anayem-beza kibongo bongo kwa mlango wa nyuma) atakapogundua dawa au chanjo. Atakaye kuwa hai kipindi hicho bahati yake atakaye kufa iwe ni mipango ya Mungu.

Sikiliza madaktari wa wataalamu wengine wa afya - hakuna wanayekubaliana naye kwenye hilo.

Baada ya kuudhibiti na kuisafisha nchi na ugonjwa huu, kwa wananchi panapo nia utazuiliwa kabisa usiwafikie, kama ambavyo ungezuilika kabla ya ugonjwa kuingia kama nia ingalikuwapo. Angalia case ya sasa China, Uganda, Rwanda, South Korea nk.
 
Labda nikwambie kitu.mimi sipo ccm siku zote ni mpinzani.
Ila mimi sio mpinzani FUATA MKUMBO NINA AKILI ZANGU TIMAMU..
siwezi kupigia kelele lock down ambayo hainisaidii kitu.wakati kazi zangu ni za kutoka nje.
Niliwahi kukuuliza UNAFANYA KAZI GANI AMBAYO ITAKUFANYA HUMUDU MAKALI YA LOCKDOWN DOWN.
Mpaka unakufa hautakuja kunijibu

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa mawazo yako unadhani nani ana kazi za kubaki ndani? Pana ugonjwa unaosambaa kwa kasi unauwa 5% - 10% ya walioambukizwa. Nadhani ya ugonjwa huu yataonekana zaidi maambukizi yakiwa mengi (yaani likichanganya).

Usipoelewa:

1. Ugonjwa huu siyo siasa. Unapoanza kueleza u CCM au upinzani ujue umeshapotea na unachoongelea siyo Corona tena.

2. Vita zozote kama ilivyo hii inataka sacrifice (kujitoa). Huwezi kupata kote. Pana uchumi na maisha. Lazima kuchagua moja. Hakuna anayesema hakuna athari kwenye uchumi. Hilo hata mtoto mdogo ambaye leo shule haendi kwa sababu vya Corona anajua.

3. Utamudu vipi makali ya lockdown? Hili limeelezewa sana. Kwa mara nyingine nakupa tena hapa:

IMG_20200424_181650_106.jpg


4. Muhimu kutambua Corona ni vita vya taifa si vita vya mtu mmoja mmoja. Ondoa ubinafsi. Usiseme utamudu vipi sema tutamudu vipi? Sote kabisa kwa umoja wetu.

5. Kwa vile hii ni vita vya pamoja nadhani unaona sasa shughuli yangu, yako na yule si suala tena (yaani ni irrelevant).

Kunywa maji mengi usome kuelewa mjinga utakuwa wewe hadi lini mkuu.

Badilika!
 
Mkuu kwanini tunakomalia sana marekani?

Kwa nini siyo Rwanda, Uganda, Kenya wala South Africa?

Au labda mkuu huu ugonjwa utaondoka je hapa kwetu? Si unajua kuutokomeza ni mpaka kila mwathirika apatikane mmoja mmoja kutoka kokote kule aliko nchini?

Mkuu nini mbadala?

Kwa nini mstakabala huu wanaotumia Rwanda na Uganda ni mwiba kwetu? Tatizo liko wapi?

View attachment 1429085
Inatosha kukwambia kwamba Tanzania bila "lockdown (partial/total)" au "Curfew" itashinda vita dhidi ya COVID-19, upende usipende.

Baada ya ushindi, Tanzania itakuwa imara katika nyanja zote za maendeleo kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiteknolojia. Kwa mfano:-
1) Kijamii: watu watakuwa wamebadili tabia za kiafya kutoka nyakati za giza za kutokujali usafi wa miili yao na mazingira.
2) Kisiasa: mshikamano bila kujali itikadi zao.
3) Kiuchumi: kuzingatia kanuni mhimu za uchumi hususani matumizi mazuri ya rasimali watu na vitu.
4) Kiteknolojia: uvumbuzi wa zana za uzalishaji mali, pale ambao bidhaa mhimu zinazalishwa hapa nchini badala ya kutegemea kuagizwa kutoka nchi za nje kulikofungwa mipaka.

Ni kweli kutahitajika nguvu za ziada ili kila mwananchi azingatie ushauri wa kitaalamu kujikinga dhidi ya maambukizi ya COVID-19. LAKINI, mwisho wa siku faida ni kubwa kuliko hasara, kama zilivyotajwa hapo juu.

TANZANIA bila korona inawezekana kama kila mwananchi atatimiza wajibu wake wa kuthamini uhai wake na wa mtu mwingine bila kujali siasa, dini, rangi, elimu, hali ya maisha nk

Niwatakie Waislam mfungo mwema na salama.
 
Umeuliza kupata majibu? Au kujikoki kufikia conclusion unayotaka?

Mind you the two are different. Ila kama unataka ushahidi mmoja huu hapa:



Kama unataka zaidi tutakupa.
Uganda wana uzoefu wa muda mrefu wa kupambana na majanga (km ukatili wakati wa utawala wa Amini) ikiwemo magonjwa yanayoambukiza (km ebola). Sikiliza hiyo "video clip" uliyoweka kwa umakini.

Kenya na Rwanda, ni nchi ambazo ziko kwenye "total/partial lockdown" kiwango cha maambukizi ni kikubwa kuliko Tanzania na Burundi ambako wananchi wanaendelea na shughuli zao kwa kuzingatia tabia sahihi za kiafya.
 
Inatosha kukwambia kwamba Tanzania bila "lockdown (partial/total)" au "Curfew" itashinda vita dhidi ya COVID-19, upende usipende.

Baada ya ushindi, Tanzania itakuwa imara katika nyanja zote za maendeleo kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiteknolojia. Kwa mfano:-
1) Kijamii: watu watakuwa wamebadili tabia za kiafya kutoka nyakati za giza za kutokujali usafi wa miili yao na mazingira.
2) Kisiasa: mshikamano bila kujali itikadi zao.
3) Kiuchumi: kuzingatia kanuni mhimu za uchumi hususani matumizi mazuri ya rasimali watu na vitu.
4) Kiteknolojia: uvumbuzi wa zana za uzalishaji mali, pale ambao bidhaa mhimu zinazalishwa hapa nchini badala ya kutegemea kuagizwa kutoka nchi za nje kulikofungwa mipaka.

Ni kweli kutahitajika nguvu za ziada ili kila mwananchi azingatie ushauri wa kitaalamu kujikinga dhidi ya maambukizi ya COVID-19. LAKINI, mwisho wa siku faida ni kubwa kuliko hasara, kama zilivyotajwa hapo juu.

TANZANIA bila korona inawezekana kama kila mwananchi atatimiza wajibu wake wa kuthamini uhai wake na wa mtu mwingine bila kujali siasa, dini, rangi, elimu, hali ya maisha nk

Niwatakie Waislam mfungo mwema na salama.

Mkuu umeandika mengi zaidi kwenye faida ikiwa ugonjwa umeondoka. Yaani umeongelea mno ubora wa peponi baada ya kufika badala ya kujikita kwenye namna ya kufika kwanza.

"Inatosha kukwambia kwamba Tanzania bila "lockdown (partial/total)" au "Curfew" itashinda vita dhidi ya COVID-19, upende usipende."

Ni jambo la kheri sana kuishinda Corona kwa namna yoyote ile. Ila tutaishinda vipi tupe mkakati au mikakati mkuu.

Mikakati iko wapi?

Utajiri na kheri ya baadaye bila kujali hatari ambayo hujaivuka kitabu cha "Lila na Fila Havitengamani" kinatambua mada muhimu yenye kufanana na hali yetu leo: "Tamaa mbele, Mauti nyuma".
 
Uganda wana uzoefu wa muda mrefu wa kupambana na majanga (km ukatili wakati wa utawala wa Amini) ikiwemo magonjwa yanayoambukiza (km ebola). Sikiliza hiyo "video clip" uliyoweka kwa umakini.

Kenya na Rwanda, ni nchi ambazo ziko kwenye "total/partial lockdown" kiwango cha maambukizi ni kikubwa kuliko Tanzania na Burundi ambako wananchi wanaendelea na shughuli zao kwa kuzingatia tabia sahihi za kiafya.

Isije kuwa unayo sikiliza siyo hii tunayoisikiliza wengine?

Acheni siasa. Waachieni wataalamu wa afya washauri kitaalamu hatua za kuchukua:

1. Uganda na Rwanda hawana vifo vya Corona.
2. Uganda na Rwanda wana wagonjwa wachache wa Corona kuliko sisi..
3. Uganda na Rwanda maambukizi yamepungua mno na wanaelekea kulegeza hizi lockdowns kwenda kwenye maisha ya kawaida.

Hawa wanaelekea kwenye hiyo prosperity uliyotumia muda mwingi kuielezea. Hawa jamaa watatupita katika yote hayo ya prosperity.

Sisi tusipoangalia wakati tukiwa tunahangaika na huu ugonjwa wenzetu watakuwa kwenye real mavuno.
 
Isije kuwa unayo sikiliza siyo hii tunayoisikiliza wengine?

Acheni siasa. Waachieni wataalamu wa afya washauri kitaalamu hatua za kuchukua:

1. Uganda na Rwanda hawana vifo vya Corona.
2. Uganda na Rwanda wana wagonjwa wachache wa Corona kuliko sisi..
3. Uganda na Rwanda maambukizi yamepungua mno na wanaelekea kulegeza hizi lockdowns kwenda kwenye maisha ya kawaida.

Hawa wanaelekea kwenye hiyo prosperity uliyotumia muda mwingi kuielezea. Hawa jamaa watatupita katika yote hayo ya prosperity.

Sisi tusipoangalia wakati tukiwa tunahangaika na huu ugonjwa wenzetu watakuwa kwenye real mavuno.
Hali halisi kwa leo ni kama ifuatavyo:
Screenshot_20200425-134606_Samsung Internet.jpg
Screenshot_20200425-134726_Samsung Internet.jpg
Screenshot_20200425-134650_Samsung Internet.jpg
 
Mkuu umeandika mengi zaidi kwenye faida ikiwa ugonjwa umeondoka. Yaani umeongelea mno ubora wa peponi baada ya kufika badala ya kujikita kwenye namna ya kufika kwanza.

"Inatosha kukwambia kwamba Tanzania bila "lockdown (partial/total)" au "Curfew" itashinda vita dhidi ya COVID-19, upende usipende."

Ni jambo la kheri sana kuishinda Corona kwa namna yoyote ile. Ila tutaishinda vipi tupe mkakati au mikakati mkuu.

Mikakati iko wapi?

Utajiri na kheri ya baadaye bila kujali hatari ambayo hujaivuka kitabu cha "Lila na Fila Havitengamani" kinatambua mada muhimu yenye kufanana na hali yetu leo: "Tamaa mbele, Mauti nyuma".
Umeisoma au umepita tu kwa kuwa tayari una maoni hasi. Katika bandiko langu hilo, na michango yangu humu JF, kuhusu gonjwa hili, nimeandika: TANZANIA bila korona inawezekana kama kila mwananchi atatimiza wajibu wake wa kuthamini uhai wake na wa mtu mwingine bila kujali siasa, dini, rangi, elimu, hali ya maisha nk
 
Back
Top Bottom