Kuwatumia vibaya Diamond na Ali Kiba kwenye siasa za Simba na Yanga ''kutaua" soka la Tanzania

Kuwatumia vibaya Diamond na Ali Kiba kwenye siasa za Simba na Yanga ''kutaua" soka la Tanzania

Haikuwa promotion mkuu. Watu walikuwa wanaambiwa tu wiki ijayo kuna mechi ya Simba na Yanga. Hakukuwaga na blah blah blah sijui Msanii fulani atakuwepo etc
Ndo promotion yenyewe hiyo mkuu, watu wakishaambiwa kuna mechi siku fulani ni nini hicho kama si promo!?
 
Inajulikana tangu enzi za Pontyo wa Pilato kwamba shabiki wa Yanga hawezi kuwa shabiki wa Simba and vice versa.
Sio tu hivyo bali hadi kwenye kutakiana mafanikio na kuombeana njaa ndani ya uwanja.

Shabiki wa Simba hawezi kufurahia mafanikio ya ndani ya uwanja ya Yanga hata itokee nini.

Miaka ya nyuma wazee wetu walikuwa wanachukia hadi rangi za timu pinzani.


Mfano Mwameja Mohamed Mwameja ( jina lake haitwi Mohamed Mwameja ila anaitwa Mwameja Mohamed Mwameja) anasimulia.

Baba angu ni shabiki wa Yanga lia lia kama tu ilivyo kwa mzee wangu mzee Hussein Daima( Baba mzazi wa Mohamed Hussein Machinga kule Mtwara)

Familia yetu inajulikana ni familia ya wanayanga watupu. Kuna kipindi nikiwa Simba Sport niliwahi kuhisiwa Nina mapenzi na Yanga hadi kutengwa kambini Zanzibar mwaka 92 baada ya mimi kusaini Yanga na Ken Mkapa na Kipese kusaini Simba. Sekeseke lilikuwa kubwa sana hadi Mzee Mwinyi akaingilia kati na kutumia busara ya kiutu uzima ambapo alisema Mimi nibaki Simba na Ken Mkapa abaki Yanga.

Sakata hilo lilikoleza uvumi kwamba Mimi Yanga. Kabla mzee Mwinyi hajaingilia kati kuna watu walitumwa kuja kunimwagia tindikali ila Mwenyezi Mungu alininusuru watu hao hawakunidhuru.

Maneno ya chinichini yalikuwa kwamba Mimi Mwameja Nina mapenzi na Yanga ila Simba nipo kikazi tu.

Sasa pale kwetu Tanga Mwakidila kulikuwa na mzee rafiki yake baba shabiki wa Simba lia lia.

Kuna siku huyu mzee alikuja nyumbani sasa akasikia kiu akanituma nimletee maji ya kunywa.

Pale nyumbani kwetu ilikuwa karibu kila.kitu ni kijani na njano hadi vikombe.

Nikachukua maji kwenye kikombe cha rangi ya njano nikampelekea yule Mzee. Mzee alifura kwa hasira. Pamoja na kwamba alikuwa na kiu lakini alinimwagia yale maji yote.

" umekosa adabu wewe mtoto unaweza vipi kuthubutu kunipa maji kwenye kikombe cha rangi cha njano"


Hivyo ndivyo ilivyo kuwa.

Back 2 Diamond na Ali Kiba.

Diamond anajulikana ni shabiki wa Simba, lakini ghafla tukasikia sijui amekuwa shabiki wa Yanga. Sijui kapewa hela sijui kashawishiwa na Hajj blah blah blah.

Juzi tena tukashuhudia kituko cha karne. Ali Kiba ambae anajulikana kama shabiki wa Yanga eti kahamia Simba kafanya na wimbo kabisa.

Kwenye interview anasema hawezi kushabiki timu ambayo imemtenga(kumtenga vipi? Kutompa show? Kumpa show Diamond? ama? )

If the answer is Yes how deep was ur bond with Young Africans for you to live the team just like that? (Wewe sio mchezaji wala muajiriwa. Ur just a mere fan)


MADHARA YAKE: Itawafanya vijana wadogo na watakao zaliwa baadae waone kumbe mtu kuhama Yanga kwenda Simba ni jambo la kawaida tu.

Ukitangukia stage hii, Itaua ushabiki na unazi wa Simba na Yanga ambao ndio roho ya mpira wa Tanzania.

Mpira utapoteza mvuto. Vijana watajihusisha na .mpira kwa ajili ya kubeti tu.


ATHARI ZIMEANZA KUONEKANA.

Hivi kweli leo hii timu kongwe nchini kama Yanga na Simba haziwezi kujaza uwanja wa Mkapa mpaka ipigwe promo?

Mpaka watu wahamasishwe?

Miaka ya tisini hakukuwq na instagram wala Facebook wala twitter wala tiktok wala akukuwaga sijui na promo lakini viwanja vilikuwa vinajaa mapema tena kwenye mechi ambayo Yanga au Simba wanacheza na timu ya kawaida achilia mbali mechi ya Simba na Yanga au ya kimataifa.


Hivi kweli timu kongwe kama Simba ambayo ina mamilioni ya mashabiki Tanzania inastahili kweli kujitapa kuujaza uwanja wa mkapa? Kweli? Seriously kabisa? Ndio tumefikia hapo?

Uwanja ambao Mwamposa mtu mmoja aliujaza ukatapikq hadi nje.


Kwa kujivunia kujaza uwanja tumerudi nyuma kwa miaka sabini . Kwa ukubwa wa Yanga na Simba zinapaswa kuwa zimeshavuka hiyo stage ya kutamba kujaza uwanja..

Timu kama Azam au Tabora United zingejisifu kujaza uwanja ingeweza kueleweka lakini sio kwa Simba na Yanga.


TUNAPOELEKEA : kama huu upuuzi wa kuwaingiza wasanii kwenye siasa za Simba na Yanga asipokemewa tunapoelekea itakuwa ili Simba na Yanga zijaze inabidi mashabiki walipiwe tiketi kuingia uwanja ni, wachukuliwe kwenye magari kutoka matawinj kwao, wapelekwe na pombe au pilau za bure..
Tunakoelekea itabidi tuwaombe CCM tekiniki za kujaza uwanja Kwa kusomba watu kwenye malori
 
Haikuwa promotion mkuu. Watu walikuwa wanaambiwa tu wiki ijayo kuna mechi ya Simba na Yanga. Hakukuwaga na blah blah blah sijui Msanii fulani atakuwepo etc
Sasa unataka tuishi kama zamani? Hata huko ulaya kukiwa na big match huwa inapigwa promo kupita maelezo. Msilazimishe kila jambo la zamani lionekane bora kuliko la sasa, kwanza zamani watu walikuwa wanalazimika kwenda uwanjani kwasababu mpira ulikuwa hauoneshwi kwenye luninga na hata ikibahatika unaoneshwa ilikuwa hovyo sana.

Tofauti na sasa, mpira unaoneshwa live na kwa ubora kabisa lkn maelfu bado wanaenda uwanjani licha ya maisha ya sasa kuwa na changamoto nyingi kuliko zamani.
 
Kizazi hiki kinawaza hela na kubet kuliko mahaba ya dhati ya timu zao.


Leo hii Yanga ikicheza ikashinda mashabiki wa Simba wanafurahi maana mikeka imetiki and viceversa is true.

LIKUD mzee mwenzangu wahenga walisema kila zama na kitabu chake, hivyo zama za sasa hazitaki tuishi kwa misingi ya 1970's bali tuishi kwa misingi ya 2020's
 
Kizazi hiki kinawaza hela na kubet kuliko mahaba ya dhati ya timu zao.


Leo hii Yanga ikicheza ikashinda mashabiki wa Simba wanafurahi maana mikeka imetiki and viceversa is true.

LIKUD mzee mwenzangu wahenga walisema kila zama na kitabu chake, hivyo zama za sasa hazitaki tuishi kwa misingi ya 1970's bali tuishi kwa misingi ya 2020's
Sahihi kabisa mkuu
 
  • Thanks
Reactions: K11
Miaka ya tisini kulikua na uwanja unaobeba watu elf sitini?
Elfu 40 shamba la.bibi. elfu 40 com kirumba. Elfu 30 sokoine. Elfu 25 Sheikh Amri Abeid Arusha . Elfu 25 mkwakwanj Tanga. Elfu 30 Ali Hassan Mwinyi Tabora. Elfu 30 uwanja wa Amani Znz. To mention but a few
 
Kadri miaka inavyozidi kwenda Tasnia ya Michezo na Burudani hapa Bongo inazidi kukosa wapenzi mashabiki.
 
Mapato yalikuwa sh ngp [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kama ulitaka kuzungumzia mapato ungefanya hivyo ila mada iliyopo na majibu yako yalikuwa idadi ya watazamaji
 
Naunga mkono hoja ni ushamba kuwatumia wasanii wa muziki au tasnia nyingine kama kigezo cha timu hizi kukubalika.

Shabiki wa ukweli hahami hata siku moja. Mimi nimekuwa shabiki wa Arsenal licha ya kuwa Arsenal imekuwa ikifanya vibaya kwenye EPL kwa miaka ishirini sasa sijawahi kufikiria kuhama na hiyo ni timu ya ughaibuni ambako sijawahi kufika sembuse timu ya hapa nyumbani.

Eti Diamond anasema amehama Simba kumfuata Haji Manara,huu ni ujinga kabisa.
SAGAI,
Nadhani tuangalie mienendo ya wanamuziki wetu na jinsi wanavyojipatia kipato kupitia umaarufu na umaarufu huo wanaupataje?
Mara nyingi umaarufu wa wanamuziki wa nchi hii unapatikana kutokana na mabifu.

Hadija Kopa Vs Nasma Khamis.
Msondo Vs Sikinde
Vijana Jazz Vs Bima Lee
TOT Plus Vs Twanga Pepeta
Ali Kiba Vs Diamond
Nk nk nk.

Ukiangalia vizuri ni kama Diamond kafuata upepo wa mafanikio ya Yanga ya miaka 2 hii ili kutengeneza fedha, lakini akaegemea kwenye bifu la Manara na Barbara (Simba) ili apate mapokezi Makubwa toka Yanga akijua baada ya tukio lile atazoa subscribers wengi toka mashabiki wa Yanga na akaunti itatuna. Yaani mashabiki wake wa siku zote ukiunganisha na wapya wa kutoka Yanga watakaofuata mkubwa, kipato hakitakuwa haba. Na naamini alifanikiwa.

Baada ya kuona hivyo Kiba naye akatafuta Nitoke vipi ili apokelewe Simba. Kama zali tamasha la Simba ambalo miaka ya nyuma lilifana Kwa kutumia mafanikio ya uwanjani ya msimu husika mwaka huu kigezo hicho kikakosekana kikabaki kigezo cha Utambulisho wa Wachezaji pekee. Ndipo Kwa ubunifu mkubwa Ahmed Ally akaibuka na Kibegi. Kibegi kikawa Kibegi na tena kikatengenezewa Version. Kikawa na version I, II na III ambayo Kiba aliibuliwa from no where. Kwa vile ni Msanii akaibuka na Wimbo àmbao ulipambwa Sana na Wanasimba ili kunogesha tukio wengine wakidiriki kusema ndio wimbo Bora wa Simba hivyo ufanywe wimbo rasmi wa timu (Team anthem). Lakini ukisikiliza wimbo wenyewe na rithym ya kawaida ya Simba Simba vinakwenda tofauti. Hata baadhi ya maneno yaliyomo kama vile Simba ndiyo timu No.1 Afrika hayaakisi uhalisia.

Kwa maoni yangu nakubaliana na wewe kwamba kuhamisha muziki bila tahadhari na kuupeleka kwenye soka letu kutakuwa na athari chanya na hasi na ni dhahiri hasi itazidi chanya.
Ukiangalia kwenye siasa kama uwanja wa kufanya siasa Tanzania ungekuwa level, hawa wanamuziki usinhewaona wote wakiwa CCM. Huko wamekwenda kulinda vitumbua vyao wakihofiwa kupigwa rungu na serikali wakionekana upande wa pili au kuwa neutral. Utakumbuka Diamond alitaka kulinda hadhi yake Kwa kubaki neutral kisiasa akapelekewa TRA na akaangushiwa bill ya Kodi bil.4?

Nimalizie Kwa kusema viongozi wenyewe wa timu wanapaswa kuchukua tahadhari za makusudi kulinda Kwa wivu hadhi ya soka isitekwe na kitu kitakachofubaza radha yake.
 
Hiyo miaka ya 90 unayosema Simba na Yanga zilikuwa zinajaza uwanja kulikuwa na uwanja wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000?

Unasifia kujaza uwanja wa watu 8k!!??? Tukubali tukatae ila ukweli ni kuwa kizazi hiki kimeuheshimisha mpira wa bongo, hizo nyingine zitabaki kuwa ngojera tu.
Unapobisha uwe na takwimu siyo kumpinga Mtu ionekane wewe wa kisasa wakati yeye ni wa zamani na Wa kisasa pia maana nyakati zote mbili alikuwepo. Una Taarifa Mechi ya Simba Vs Pamba ilikuwa inajaza uwanja wa CCM Kirumba bila promo na watu wengi wanabaki nje kama walioko ndani? Je, uwanja wa Kirumba u achukua watu 8000 kama ulivyosema? Unajua mwaka 1990 Tanzania ilikuwa na watu wangapi na Sasa inao wangapi?
 
Back
Top Bottom