Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 3,092
- 5,386
Nafikiri katika technologia ambayo inatakiwa ifanyiwe maboresho ya haraka (kama bado) ni taa za barabarani kwa matumizi ya Highway kwani kwa sasa naona kama hazina manufaa stahiki.
Najaribu kufikiria kwa akili ya kawaida tu, kuruhusu Barabara kuu itumike pengine kwa masaa 6 hadi 10 hivi kati ya masaa 24 na unakuta kuna wakati njia moja haina kabisa magari ila taa inalazimisha magari kusubiri.
Kwa kuwa bado tuna maeneo makubwa, nafikiri ipo haja ya kufikiria kutumia round about kuliko taa za barabarani ikiwa ni Pamoja na kujumuisha vivuko vya watembea kwa miguu kwa maeneo yenye watu wengi
Nakumbuka Barabara ya Morogoro iliyojengwa na Wajapani miaka hiyo; walipo fika eneo la Msamvu moja ya muunganiko wa Barabara ambao ni busy Tanzania kwa kupitisha MALORI na mabasi, waliamua kuweka round about kubwa na kumaliza kabisa msongamano wa magari eneo hilo; Pale Chalinze pia walifanya hivyo hivyo. Kuna uwezekano walitambua madhaifu ya technology ya taa......
Tofauti na round about, nafikiri ipo haja ya kufikiria technologia ya taa za barabarani zenye sensor ya kuweza kuwasha tu barabara yenye magari na pengine kuwasiliana na taa inayofuata ili gari likiruhusiwa, liende moja kwa moja na sio kusimamishwa na taa nyingine pengine ndani ya kilometa mbili....
Najaribu kufikiria kwa akili ya kawaida tu, kuruhusu Barabara kuu itumike pengine kwa masaa 6 hadi 10 hivi kati ya masaa 24 na unakuta kuna wakati njia moja haina kabisa magari ila taa inalazimisha magari kusubiri.
Kwa kuwa bado tuna maeneo makubwa, nafikiri ipo haja ya kufikiria kutumia round about kuliko taa za barabarani ikiwa ni Pamoja na kujumuisha vivuko vya watembea kwa miguu kwa maeneo yenye watu wengi
Nakumbuka Barabara ya Morogoro iliyojengwa na Wajapani miaka hiyo; walipo fika eneo la Msamvu moja ya muunganiko wa Barabara ambao ni busy Tanzania kwa kupitisha MALORI na mabasi, waliamua kuweka round about kubwa na kumaliza kabisa msongamano wa magari eneo hilo; Pale Chalinze pia walifanya hivyo hivyo. Kuna uwezekano walitambua madhaifu ya technology ya taa......
Tofauti na round about, nafikiri ipo haja ya kufikiria technologia ya taa za barabarani zenye sensor ya kuweza kuwasha tu barabara yenye magari na pengine kuwasiliana na taa inayofuata ili gari likiruhusiwa, liende moja kwa moja na sio kusimamishwa na taa nyingine pengine ndani ya kilometa mbili....