Kuweni makini na mchanga wa kaburini

Duuh
 
Wewe nawe unaleta hadithi za kale tena. Shule muhimu sana.
 
Hakuna wachawi au uchawi. Acha utapeli
 
HII KITU ILITOKEA KTK FAMILIA YETU MZEE ALIJENGA NYUMBA MIAKA YA 2000's, SASA ILE NYUMBA ILIKUWA INACHANGAMOTO YA DADA ZANGU KUUMWA UMWA OVYO OVYO, MARA MAPEPO, MNALALA MNASIKIA VITU VIZITO VINATEMBE NDANI YA GYPSUM BOARD, NDOTO MBAYA MBAYA TUPU ILA TUKISAFIRI KWENDA KUWATEMBELEA NDUGU ILIKUWA SHWARI, KIMBEMBE KINAKUWA PALE TUWAPO NDANI YA ILE NYUMBA.

ilipofika miaka ya 2015 tukaona labda ili eneo kuna jambo lisilo la kawaida na nyumba aliijenga mzee mwaka 2000. mim binafsi nikaanza kufuatilia historia ya ile plot na mmiliki aliyetutangulia kabla yetu.

laah haulaa kumbe kile kingongwe bado kilikuwa hai alihamia wilaya ingine few miles away,. nikampeleleza kiasi na vihongo vya sukari na mchele mwishowe akanambia ukwel wa ile plot na kile kilichopo pale chini kumbe ndio ilikuwa chanzo cha taabu yote pale.

mzee akanunua plot ingine akajenga akahama nowdays hakuna matatizo tena tu shwari kabisa, ile nyumba bado ipo hatujaweka mtu wasije wakasema tulikuwa wachawi tumeacha tunguli ndani.
 
Hi ngozi nyeusi Inashida sana wenzetu Wazungu wanaendelea kurusha drones na kugundua 5G sisi bado tunahangaika na mchanga wa makaburini na njiapanda dume na jike
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nitafuteni mimi kwa wakati wenu ili nipate kuondoa hivyo vitu vibaya katika hiyo nyumba muliyo hama.
 
Wakati KONOIKE wanahamisha makaburi ya Sabasaba Mbagala tulichukuwa kifusi cha makaburi tukajengea makwetu na tuko salama usalmin.

Kule Tarime tunalima juu ya makaburi (tena bangi nk) na kuvuna na tuko salama usalmin.

Tulihamisha udongo wa kaburi la marehemu toka Mombasa kuja kumzika upya Tz na tuko salama usalmin.

Wachagga wanaongoza kwa kuhamisha madongo ya makaburi na ndiyo matajiri wakubwa badala yake Wakwere ndiyo wanaongoza kwa vichaa JMT, Wachagga wako salama usalmin.

Shule ya Msingi Muhimbili na Msikiti wa Ijumaa wa kumbukumbu ya Sheikh Jumbe Muhammad Tambaza vimejengwa kwenye sehemu za makaburi ya Muhimbili na wanafunzi na waumin wa Msikiti wako salama usalmin.

Clock Tower Dsm kwy mitaa ya Samora, India na Mosque kuna kaburi la karne 3 la Sharif Abdul Shakhul Salim Latas aliyekufa kabla ya Said Majid wa Oman; limefanyika mkeka wa watu kupumzikia na wafagizi wa Jiji la Ilala wanafagia dongo lake na Watunza bustani ile wanalima dongo lake na kubeba kwenye matoroli na kuondoka nayo lakini wako salama usalmin.

Mission-town wa Samora ndiko wanakonywea kahawa, kusoma magazeti na mijadala ya Dar Derby lakini wako salama usalmin.

Waliosoma Archaeology au Archeology wamefukua makaburi ya binadamu na viumbe vingine na wako vizuri tu hadi kesho. Wanachimba kukusanya Artifacts, Biofacts, Ecofacts nk.

Kwenye Makumbusho ya Taifa watu wanaishi na mafuvu ya akina Kabaka, Mangi Meli, Mangi Meza, Mkwawa, Zinjanthropus, Dryopithecus, Ramapithecus, Australopithecus, Homo Erectus, Homo Sapien (Neanderthalensis), Homo Sapien Sapien na wako vizuri tu hadi kesho.

Waliogundua mafuta waliyatoa kwenye mabaki ya viumbe hai vilivyozama chini ya ardhi mamilioni ya miaka na vizazi vyao viko vizuri tu hadi kesho. Bila kufukua mabaki hayo leo magari yangekuwepo? Nishati ya kuendeshea magari, meli, ndege, treni, mitambo ingetoka wapi?

Waliogundua madini walifukua makaburi. Wanaojenga maghorofa wanafukua mabaki ya viumbe, wanaosoma udaktari wanacheza na maiti, wanaokusanya forensic evidence kugundua wahalifu wanafukua makaburi.

Dodoma kuna Maabara ya Wizara za Ardhi na Kilimo iliyobeba sampuli za dongo zote za JMT kwa ajili ya kutambua maeneo mazuri ya kilimo. Nao watafiti wa sayansi ya udongo walifukua ardhi.

Israel walifukua makaburi ya Manabii na Mitume na waliofanya hivyo vizazi vyao havijapata laana wala uzezeta. Mafuvu hayo yanaiingizia nchi fedha za kigeni kuchangia bajeti.

Watu walikuwa wanavamia usiku kuchukuwa dongo kwy kaburi la Maalim Seif Sharif Hamad hadi lilipofanywa lindo maalum la FFU na hatujasikia wamekufa au kuwa mazezeta.

MziziMkavu kajipange upya namna ya kutapeli watu.

Mhu.9:5
kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.

MziziMkavu unataka kuwapiga ela wajinga ambao ndiyo wengi duniani.

Kama uganga ni ukweli kwanini waganga msiende kuiba ela ($ na €) Benki Kuu mkawa matajiri kama Dangote?

Kama uganga ni ukweli kwanini msiwafufue Nyerere na watakatifu Mitume na Manabii waje kuisahihisha dunia? Hususan Afrika?

Kama uganga ni ukweli kwanini msijenge misonge ya nyasi ya kuagulia pembeni mwa mahospitali (kama famasi zilivyo) ili wagonjwa wakishuka kwenye magari wachague pa kwenda kama ni hospitali au kwenye misonge? Kwanini mnaagua mafichoni?

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
OHHHH AFRICA.
UMASIKINI HUU............

HAKUNA UMASIKINI MBAYA ZAIDI KAMA UMASIKINI WA FIKRA.

UMASIKINI WA FIKRA NI MBAYA MNO.
NI MBAYA ZAIDI YA BIASHARA YA UTUMWA.

MZIZI MKAVU FICHA UJINGA
 


Nimegundua ni Biashara.

WAJINGA NDIO WALIWAO.

ANALETA BIASHARA KAMA HIZI MBELE YA WEREVU ANAHARIBU KABISA BIASHARA ZAKE.


WAFU HAWAJUI MENO LOLOTE.
 
Hi ngozi nyeusi Inashida sana wenzetu Wazungu wanaendelea kurusha drones na kugundua 5G sisi bado tunahangaika na mchanga wa makaburini na njiapanda dume na jike
Wazungu wanajua yote hayo tena na mengine mengi ambayo wew huyajui kwa sababu wao hawaweki mipaka ya elimu kama unavyotaka wew ila wanatuwekea mipaka sisi ili tusijue Siri za dunia hii

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Unajaribu kusema nini? Maana Tanzania ilikua ni eneo la Makaburi ndiyo maana mabaki ya mtu wa kale yaligundulika huku.
 



1. Ujinga mkubwa sana huu, moja siamini kabisa katika huu ushirikina, 100% ni ulofa.

2. Hawa wajinga wanofanya huu ujinga, uwa wanapewa maelekezo na watu wao, waganga mara nyingi.

Sasa sijui unawaje kufikiri kwamba hawana maelezo specific namna ya ku execute zoezi lao.
 


Wewe ni mshirikina uliyekubuhu.
 
Waliosoma Archaeology au Archeology wamefukua makaburi ya binadamu na viumbe vingine na wako vizuri tu hadi kesho. Wanachimba kukusanya Artifacts, Biofacts, Ecofacts nk.

Kwenye Makumbusho ya Taifa watu wanaishi na mafuvu ya akina Kabaka, Mangi Meli, Mangi Meza, Mkwawa, Zinjanthropus, Dryopithecus, Ramapithecus, Australopithecus, Homo Erectus, Homo Sapien (Neanderthalensis), Homo Sapien Sapien na wako vizuri tu hadi kesho.

Waliogundua mafuta waliyatoa kwenye mabaki ya viumbe hai vilivyozama chini ya ardhi mamilioni ya miaka na vizazi vyao viko vizuri tu hadi kesho. Bila kufukua mabaki hayo leo magari yangekuwepo? Nishati ya kuendeshea magari, meli, ndege, treni, mitambo ingetoka wapi?

Waliogundua madini walifukua makaburi. Wanaojenga maghorofa wanafukua mabaki ya viumbe, wanaosoma udaktari wanacheza na maiti, wanaokusanya forensic evidence kugundua wahalifu wanafukua makaburi.

Dodoma kuna Maabara ya Wizara za Ardhi na Kilimo iliyobeba sampuli za dongo zote za JMT kwa ajili ya kutambua maeneo mazuri ya kilimo. Nao watafiti wa sayansi ya udongo walifukua ardhi.

Israel walifukua makaburi ya Manabii na Mitume na waliofanya hivyo vizazi vyao havijapata laana wala uzezeta. Mafuvu hayo yanaiingizia nchi fedha za kigeni kuchangia bajeti.

Watu walikuwa wanavamia usiku kuchukuwa dongo kwy kaburi la Maalim Seif Sharif Hamad hadi lilipofanywa lindo maalum la FFU na hatujasikia wamekufa au kuwa mazezeta.

MziziMkavu kajipange upya namna ya kutapeli watu.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Kisha lete andiko kuhusu swala la matumizi ya “Maji ya Maiti” kwa namna nzuri Kama uliwasilosha matumizi ya mchanga wa kaburi.
 
Kataa uchawo kwa jina la Yesu.Hapa tunafundishwa uchawi na ushirikina si vinginevyo.Hii Ni elimu ya kuzimu.



Awareness is empowering,

Wacha tujifunze tujue uharibifu unavyofanyika ili tujipange namna nzuri ya kuombea na kufungua watu.

Madaktari huanza kwa kusomea ugonjwa unavyojitokeza kisha namna ya kuutibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…