Kuweni makini na wauza vifurushi wa mitandaoni

Kuweni makini na wauza vifurushi wa mitandaoni

KAGAMEE

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2013
Posts
4,457
Reaction score
5,454
Nikiri nimechagua kuibiwa kibwege kabisa. Niliona mtu mmoja anayetangazwa na KIGOGO2014 huko Instagram kuwa anauza bando kwa bei nafuu. Nikamfata inbox kuomba kujua zaidi kuhusu hiyo huduma. Akanieleza huduma ni ya uhakika kabisa, nikaangalia kwenye comment zake sikuona comment yeyote mteja akilalamika kutapeliwa.

Nikaamua kuchagua kifurushi cha bei ya chini kabisa cha 13,000 nitest nione yaliyomo kama yamo. Nikatuma hela kwa namba elekezwa, nikampigia akasema ameipata fedha na soon nitaona SMS ya kifurushi. Baada ya masaa manne, nikapiga simu tena, akasema subiri kidogo. Baadaye nikawa napiga simu, hapokei.

Toka juzi mpaka leo hakuna kifurushi wala nini. Nimecheka sana.

Wengine, naomba msiingie kwenye huo mtego tafadhali.
 
haina haja ya kuwashitua. acha wapigwe hongera kwa kupigwa hiy pesa
 
Kwani Menu ya mtamdao husika huijui? Hapo ulitaka kuiba matokeo yake umeibiwa wewe!
 
sema asilimia kubwa wengi ni matapeli ila wachache sio, mm kuna mdada ndy ananiungiaga gb 25 vifurushi vya CUG (halotel) na sijawah onana nae kuna jamaa yang alini link nae tu almost miez 9 sahz nafanya nae hii kazi
Screenshot_20240608-231339_Truecaller.jpg
 
Umekutana na kitu kizito ila waunga vifurushi og wapo, me ninae mmoja ukitaka vifurushi vya tigo au halotel anakuunga kwanza kisha ndio unamlipa. Nimeshafanya nae kazi karibia mwaka sasa.
 
Kwanza hakuna KIGOGO wa Instagram, Facebook ,Wala telegram. Wote ni magumashi wanatumia jina. KIGOGO og huwa yupo twita na Sasa haandiki tena habari za udaku anajiita KIGOGO MEDIA
 
Back
Top Bottom