Kuweni wakweli tu. Sura zenu mbaya ndiyo maana hampost picha zenu mitandaoni

Kuweni wakweli tu. Sura zenu mbaya ndiyo maana hampost picha zenu mitandaoni

Ubaya au uzuri unaupimaje?

Kwa kuangalia tu ?

Kila mtu atakuwa na namna yake na sio hiyo yako utake iwe Kwa kila mtu!
Mkuu ubaya wa muonekano unapimwa kwa macho tu. Kama sura imekaa utadhani unajisaidia haja kubwa wewe ni mbaya.

Kama tumbo na makalio havijitofautishi wewe ni mbaya.

Kama meno yako mbalimbali kama uma wewe ni mbaya
 
Nashindwa kuelewa , hivi baada ya kuposti picha yako ni faida gani unapata? Au kuna kiasi cha pesa mnakipata kupitia hiyo mitandao?

Ukute tunapishana na pesa kumbe wengine mnapata baada ya kubinua makalio yenu.
 
Ukweli ndo uo kinacho fuata apo ni hekima busara na utu iwapo kama utamkosoa mtu maanayake unamkosoa alie muumba. Kwa mfano chukulia umepita eneo flan ukakuta nyumba imejengwa inamuonekano mbaya na huyo mjengaji yupo eneo ilo ukakosoa juu ya mwonekano wa iyo nyumba mjengaji akakusikia juu ya kejeli yako nan ataumia kat ya nyumba na mjengaj juu ya ukosoaji wako?
 
Hakudaga mtu mwenye sura mbaya!

Usikosoe uumbaji wa Mungu.

Hakuna alojiumba kila mtu kajikuta yupo alivyo.

Kumekucha mkuu naona unamchallenge mtoa maada hadharani, anamaanisha muonekano na swagga au haujaelewa
 
Utakuta Wewe unatumia lakini unajipiga filters za kufa mtu hata Kaka yako akionyeshwa picha yako anashindwa kukutambua nyumbani una rangi ya nyama choma kwenye mtandao una rangi ya kuku wa kukaanga
 
Utakuta Wewe unatumia lakini unajipiga filters za kufa mtu hata Kaka yako akionyeshwa picha yako anashindwa kukutambua nyumbani una rangi ya nyama choma kwenye mtandao una rangi ya kuku wa kukaanga
Kwa upande mm kabla hata sijanawa uso napiga picha na kujiweka mitandaoni. Mungu kanijalia muonekano bora
 
Mimi facebook nina miaka 8 sijapost picha, tangu nasoma chuo huko.
Naonaga kupost ni kama kuweka maisha yangu public kitu ambacho sitaki.

Anayesema hatupost kwa sababu ya sura zetu mbovu, sasa si tungepost hata gari au nyumba tu!
Sema ni hobi ya mtu.
 
Mimi ni mwanaume na kinachosababisha nisiweke dp na nisipost picha yangu mtandaoni ni nna sura fulani hivi ya mviringo yaani nikipost warembo watakoment sana Na wengine kuja inbox kujisemesha

Nna kama miaka kumi hivi sijapost picha mtandaoni Facebook nimeacha picha moja tu Na sijaiweka dp - dp nimeweka white tu yaani walpepa Na whatsapp hivyo hivyo natumia instagram ila ni private na nna watu ninao wajua tu

Mwanzo sikugunduaga kama najichoresha mtandaoni maana ilipelekea mpaka kufananishwa na wakike- nikaona dawa hapa kutokupost tu

Videm vinapenda sana wanaume wenye sura nzuri na ukijua unawavimbia wasikuingie kirahisi
 
Kwenye Sura Mbaya nakataa,
Ila sababu zinaweza kuwa Kati ya hizi;
1. Kuigopa Criticism, tuseme kutokujiamini.
Watu wengine huogopa kupost picha au maudhui mtandaoni Kwa kuogopa Maoni ya Watu wengine. Kuogopa kukosolewa aidha kimaumbile au kimavazi au kivyovyote.

Wapo wenye Sura Mbaya na wanapost picha zao mitandaoni. Na wapo wanaoandika vitu vya kijinga na kupost mitandaoni. Hapo ishu ni kiwango cha kujiamini.
Pia wapo Watu wenye sura nzuri wanaogopa kupost mitandaoni picha zao Kwa sababu hawajiamini, na wapo Watu wenye Akili na msawazo Chanya lakini hawajiamini kuyatoa public.

2. Hobby
Wengine sio hobby Yao kupost picha zao mitandaoni au mawazo Yao mitandaoni.
Hapo kuna makundi mawili, wapo ambao huweka picha za maua, majengo, magari, au Watu mashuhuri,
Kundi hili ni lile ambalo likiingia mtandaoni linaingia Kwa ajili ya ku-refresh au kujifunza.
 
Back
Top Bottom