Kuzuia mikutano ya siasa kunaifubaza CCM na kuimarisha Upinzani, ndio maana Uchaguzi Mkuu 2020 ulikuwa mgumu kwa CCM

Naye anataka kusifiwa kama vile alilazimishwa kuwa Rais
 
Kelele za mwoga: "Mshikeni nitamuua".
 
Mzee Mgaya katika ubora wake. Na hapa ndipo tofauti kubwa kati yako na akina Elitwege na mwenzake Etwege huonekana.
 
Uko sahihi sana. Upinzani sio mtu wala chama ni ideology inayoishi mioyoni mwa watu. 1995, chama kikubwa cha upinzani kilikuwa ni NCCR Mageuzi chini ya Mrema. Kikafanyiwa figisu na kudumazwa. Ilipofika 2000 chama chenye nguvu kikawa ni CUF chini ya akina Lipumba, kikatungiwa madai ya ugaidi, kikadumazwa. Ibaibuka Chadema kunako 2010, maisha yanaendelea. Chadema ikidumazwa itaibuka ACT ama UDP na maisha ya upinzani yataendelea kama kawaida. Wanaowaza kuua upinzani wajitafakari sana.
 
Mkutano unaofanyikia mbeya unakuathiri vipi wewe uliepo nanja?
 
 
Kumbe? Lakini si wanaema hakuna mkubwa kuliko chama? Wanashondwaje kuwa outshine hao viongozi wao?
Aah wapi, Magufuli aliwafyatisha mikia mpaka wengine mikia imekuwa vilema hawawezi kuinyoosha tena!
 
Bwashee meza dawa zako dishi limetulia utadhani imeandikwa na wa ufipa πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ kumbe wa lumumba!!! Ngoja sasa uache kunywa dawa zako 🀣🀣🀣
 
Mzee Rukhsa katika kitabu chake amesema kuwa CCM wakati wanajadili na kukubali Ujio wa vyama vingi walikubaliana asiwepo Mgombea binafsi na Kusiwepo uwezekano wa vyama kuungana.
 
Huruma ya Mungu haipimiki maana ni kubwa sana LAKINI hasira ya Mungu haizuiwi na mwanadamu awaye yeyote.

Mungu huwapa wanadamu nafasi ya kujirudi, na kurudia utu wao. Viongozi wa CCM walipewa nafasi hiyo, lakini hawakubadilika kwa lolote. Wakatenda kwa ukaidi, dhuluma, uonevu na upendeleo.

Mungu ameendelea kutoa nafasi kwa hawa walevi wa madaraka. Lakini kiburi kikiendelea, Tanzania inaweza kuendelea kuongozwa na Makamu wa Rais kila baada ya uchaguzi.

Enendeni katika haki. Msipendelee wala kuonea hata mkamfanya Mungu wa haki akwa kinyume chenu.

Watu walimwomba sana Mungu wakati wa awamu ya 5. Maombi yalikuwa ya aina mbalimbali, lakini mengine ilikuwa ya kumwomba Mungu awaondolee mtawala mbaya. Kwa namna gani, hakuna aliyefikiria, maombi ilikuwa kuwaondolea mtawala mbaya. Maombi yao, kwa wakati ufaao, Mungu akatekeleza, tena kwa namna ambayo wengi hawakutarajia. Lakini ni nani mwenye kuhoji hekima ya Mungu?

Watu wa Mungu, wakati wakimshukuru Mungu kwakusikiliza sala zao, japo Mungu kawajibu maombi yao kwa mkono wenye nguvu, wa kuogofya, wasichoke kuendelea kumwomba awainulie kiongozi mwenye hekima, kiongozi mwenye upendo, kiongozi msikivu tena asiye na upendeleo, na pale kiongozi akikengeuka kwa kiburi na jeuri, awanusuru watu wake kwa kumwondoa kwa namna yoyote iwayo.
 
Kama unadhani atatokea kiongozi kupitia ccm atakaewaonea huruma wapinzani umepotoka sana.
 
Tatizo CCM ilishajifiaga hamna Chama nyie, na MaCCM wote mnalijua hilo,
Samia analinda tu teuzi zenu ,hakuna uchumi utajengwa na MaCCM baada ya kushindwa miaka zaidi ya 60. Tusichoshane.
Nafikiri statement sahihi hapa ni WATANZANIA WALISHAJIFIAGA...CCM ni chama cha siasa na lengo lake kuu ni kutawala na Mimi sioni kama wamefeli kwenye lengo Lao Hilo,na wanatawala comfortably, wananchi wako kama chura na Ng'ombe CCM maji anakunywa vizuri tuu...Kwa muktadha huo.. Failure sio CCM..Aliyefeli hapa anajijua sema hataki tuu kujikubali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…