Kwa akili ya kawaida mtu hawezi kubinafsisha Bandari zote nchi nzima! Waziri alilishwa nini?

Trable

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2023
Posts
1,781
Reaction score
3,288
Mtu umeenda kutafuta wawekezaji, mwekezaji anakwambia, ninataka unipe Bandari, na unipe Bandari zote mpaka za kwenye maziwa na kama zipo za mito nazo nipe ili sasa tufunge mkataba.

Tena haitoshi, anakwambia umpe Bandari hizo kwa maisha yote ya uhai wa Bandari hizo! Hujiulizi tu kwamba huyu mwekezaji hafai hata kusilizwa?

Hata kama alikuwa kakupa na chakula kitaamu kiasi cha kuzidi ulichowahi kula, hapo hapo tayari utaanza kukiona ni kichungu, hata hilo hakuna? Waziri wetu, anapaswa ahojiwe!

Hawa warabu walimlisha nini? Dawa au uganga gani walitumia kumpa Waziri wetu mpaka kajikuta anakubaliana na huo upuuzi?

Mbona haiwezekani jamani!
 
Wacha mama afanye yake aisee watanzania wezi sana

USSR

Sent from my TECNO B1c using JamiiForums mobile app
 
Inauma inabdi tuzoee tu yana mwisho haya
 
Huyo waziri ajiuzulu. Anasubiri nini?
 
Walipo ingia madarakani kulikuwa na yale maono ya nchi hii ni dona kantiri, Dp wanaenda kwa haraka sana kulifanikisha hilo. Na kwa vile haioneshwi ni jinsi gani Dp wananufaika, basi mgawo wa JMT unaweza ukawa ni mkubwa saaaaanaaa.
Acha basi mkuu!

Mkataba ukiwa mbovu, kila kitu ni kibovu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…